Wahandisi wa Kitanzania ujenzi wa bwawa la Stiegler's Gorge!

MTENDAHAKI

JF-Expert Member
Mar 3, 2011
4,013
1,443
Nimepata fursa ya kuandika haya Muda huu!

Nimekusikia Mh. JPM ukitangaza nia ya kujenga bwawa hilo kubwa la umeme. Kwakweli hilo ni jambo jema sana, na kwa namna ninavyokufahamu ukishatamka jambo kinachofata ni utekelezaji! Nataka nikuhakikishie kwamba wahandisi wa kitanzania hawajashindwa kusanifu na kujenga bwawa hilo!Kilichokosekana ni nia ya dhati ya kuwekeza kwenye mradi huo kutoka serikali zilizopita!

Nina hakika katika watumishi wa umma wa kitanzania (wahandisi wa ujenzi (civil), maji na umwagiliaji (hydology and irrigation), umeme (electrical), mitambo(mechanical), mazingira (environment), computer and all other fields including social scientists)! walioko serikalini na sekta binafsi wanaweza kutimiza azma hiyo kwa haraka na muda mfupi wakipewa fursa!

Ni jambo zuri kujifunza kwa waliotangulia (Ethiopia) lakini ni jambo kubwa zaidi watanzania wakifanya maana watatakiwa kufanya na sehemu zingine ambazo zina fursa hii! Faida nyingine ni gharama itakuwa nafuu zaidi wakitumika watanzania na hasa watumishi wa umma (kwa sababu wanalipwa mishahara hivyo wanahitaji uwezeshaji wa kawaida tu) kama ambavyo wamekuwa wakitekeleza miradi mingine mfano barabara, madaraja, mabwawa ya maji na miundombinu mingine!

Kwa namna ulivyo na nia ya dhati, watumishi hawa wa umma hawatakuangusha kamwe. Unapokuja ugeni kutoka Ethiopia tafadhali mawaziri wa Maji, Nishati, Mazingira, kilimo na wengineo wawe wameunda team ya wataalamu wa kuambatana na ugeni huo. Hawa wale kiapo cha utii na uadilifu kama wajumbe wa tume ulizounda na waonyeshe kujiamini na kuwa na uhakika wa kutekeleza hiyo kazi kwa muda mfupi kwa kadri inavyowezekana! Ni lazima wapewe muda maalum wa kukamilisha kazi zote za usanifu wa awali na wa kina ikiwa ni pamoja na kutengeneza michoro yote ya mradi na ujenzi.Ninaamini hii ndiyo namna bora ya kukabili jambo hili!

Bwawa hili sio tu kwamba litasaidia kuzalisha umeme wa kutosha na wa gharama nufuu bali pia litainua sana kilimo cha umwagiliaji (downstream)kwa kutumia maji ambayo yataachiwa kutoka kwenye turbines!Ndio maana ni muhimu sana bwawa likaambata na miundo mbinu ya kupeleka maji mashambani na majumbani mwa watu! Bila shaka kwa pamoja tutafika!

Hapa kazi tu!
Mtendahaki

UPDATES
Nimekuelewa na Tunakushukuru Mr President kwa kuwaamini wataalamu wazalendo.
Wahandisi wa kitanzania msituangushe na wataalamu wengine mtakaokuwa kwenye timu mmepewa fursa ya kuonyesha kwamba pakiwa na political will nyie ni bora kama Marekani, UK, Brazil, China etc. Political will imeonyeshwa na Mh. Rais na sisi tukaonyeshe utaalamu wetu kwa kusanifu na kujenga bwawa bora kabisa kwa gharama ndogo kabisa. Naamini mnaweza!Msisite kutafuta ushauri mnapokwama hasa kwa wataalamu wa mabwawa na umeme walioko vyuo vikuu vya Tanzania (UDSM (CoET), SUA(DEST), MUST (IST-DCE), etc). Wasalaam
 
IMG_0636.JPG
r

stiegler_s_gorg_c9am_tanzania.jpg

stiegler's gorge tanzania - Google-Suche:
 
Tatizo Injinia wakibongo wengi ni Copy and Paste likija suala la Designing...
Ila Magufuli anaeeza wafikiria katika ufalme wa Bwala la St. GEORGE
In general huu mradi ulikwama kwa sababu za kimazingira zaidi, na si kiuchumi wala siasa. Kuna ripoti nilisoma mahali kwamba financiers wa Kizungu waligoma kwa sababu mradi ulikuwa unapunguza kiwango cha maji kwa watumiaji wa chini (downstream users) ambao wako hasa wilayani Rufiji.
 
dam_construction_of_bui.jpg

SWAGA ZA TOKA 2014
In May 2012, RUBADA signed a Memorandum of Understanding (MoU) with a Brazilian firm, Odebrecht International, a reputable dam construction company in the world toward the implementation of a huge Stiegler’s Gorge Power Project.

The signing of the MoU allowed the Brazilian company to start reviewing results of a feasibility study conducted earlier by a Norwegian company, NORCONSULT in 1980 on a similar project that had since been shelved. The whole of the Rufiji Basin has the potential to produce 4,000 MW.

Odebrecht Company Limited has a track record of sucessfully undertaking major hydropower projects in the world. It was involved in the construction of the world’s second largest hydroelectric power plant in Brazil with the capacity of 14,000 MW. Its portfolio includes more than 58,500 MW in construction works and services in the power sector.

Brazil is reputed to have transformed her economy in the past 30 years from a low income country to a middle economy today. More than 85 per cent of the country’s power comes from hydro sources.

Tanzania due to harness more hydroelectric power potential
 
In general huu mradi ulikwama kwa sababu za kimazingira zaidi, na si kiuchumi wala siasa. Kuna ripoti nilisoma mahali kwamba financiers wa Kizungu waligoma kwa sababu mradi ulikuwa unapunguza kiwango cha maji kwa watumiaji wa chini (downstream users) ambao wako hasa wilayani Rufiji.
Yaani utege bwawa halafu upunguze uwepo wa maji?!Zilikuwa swaga za ki-IPTL ili tuendelee kukamuliwa kwenye umeme wa mafuta mazito toka DOWANS and the likes!Wakati ule hata ripoti za wataalamu zilikuwa zinachakachuliwa kirahisi mno! Kwa sasa asilimia kubwa maji yanaishia baharini badala ya kunufaisha wakulima
 
Nimepata fursa ya kuandika haya Muda huu!
Nimekusikia Mh. JPM ukitangaza nia ya kujenga bwawa hilo kubwa la umeme. Kwakweli hilo ni jambo jema sana, na kwa namna ninavyokufahamu ukishatamka jambo kinachofata ni utekelezaji! Nataka nikuhakikishie kwamba wahandisi wa kitanzania hawajashindwa kusanifu na kujenga bwawa hilo!Kilichokosekana ni nia ya dhati ya kuwekeza kwenye mradi huo kutoka serikali zilizopita!
Nina hakika katika watumishi wa umma wa kitanzania (wahandisi wa ujenzi (civil), maji na umwagiliaji (hydology and irrigation), umeme (electrical), mitambo(mechanical), mazingira (environment), computer and all other fields including social scientists)! walioko serikalini na sekta binafsi wanaweza kutimiza azma hiyo kwa haraka na muda mfupi wakipewa fursa!
Ni jambo zuri kujifunza kwa waliotangulia (Ethiopia) lakini ni jambo kubwa zaidi watanzania wakifanya maana watatakiwa kufanya na sehemu zingine ambazo zina fursa hii! Faida nyingine ni gharama itakuwa nafuu zaidi wakitumika watanzania na hasa watumishi wa umma (kwa sababu wanalipwa mishahara hivyo wanahitaji uwezeshaji wa kawaida tu) kama ambavyo wamekuwa wakitekeleza miradi mingine mfano barabara, madaraja, mabwawa ya maji na miundombinu mingine!
Kwa namna ulivyo na nia ya dhati, watumishi hawa wa umma hawatakuangusha kamwe. Unapokuja ugeni kutoka Ethiopia tafadhali mawaziri wa Maji, Nishati, Mazingira, kilimo na wengineo wawe wameunda team ya wataalamu wa kuambatana na ugeni huo. Hawa wale kiapo cha utii na uadilifu kama wajumbe wa tume ulizounda na waonyeshe kujiamini na kuwa na uhakika wa kutekeleza hiyo kazi kwa muda mfupi kwa kadri inavyowezekana! Ni lazima wapewe muda maalum wa kukamilisha kazi zote za usanifu wa awali na wa kina ikiwa ni pamoja na kutengeneza michoro yote ya mradi na ujenzi.Ninaamini hii ndiyo namna bora ya kukabili jambo hili!
Bwawa hili sio tu kwamba litasaidia kuzalisha umeme wa kutosha na wa gharama nufuu bali pia litainua sana kilimo cha umwagiliaji (downstream)kwa kutumia maji ambayo yataachiwa kutoka kwenye turbines!Ndio maana ni muhimu sana bwawa likaambata na miundo mbinu ya kupeleka maji mashambani na majumbani mwa watu! Bila shaka kwa pamoja tutafika!
Hapa kazi tu!
Mtendahaki
Weka na adhabu ambayo mtastahili iwapo ujenzi utakuwa chini ya kiwango ili tusije kulaumiana baadaye,maana hofu kubwa ni wapiga dili,hawa ndio wametufikisha hapa na kutufanya tusiaminiane.
 
Yaani utege bwawa halafu upunguze uwepo wa maji?!Zilikuwa swaga za ki-IPTL ili tuendelee kukamuliwa kwenye umeme wa mafuta mazito toka DOWANS and the likes!Wakati ule hata ripoti za wataalamu zilikuwa zinachakachuliwa kirahisi mno! Kwa sasa asilimia kubwa maji yanaishia baharini badala ya kunufaisha wakulima
Mkuu kwani hujajua principles za hydropower? Ukishajenga bwawa, una control maji yanayotoka katika bwawa kuelekea downstream, baada ya kuzalisha umeme. Kwa hiyo flow inayoingia haiwezi kuwa sawa na ile inayotoka. Hope tuko ukurasa mmoja!
 
Weka na adhabu ambayo mtastahili iwapo ujenzi utakuwa chini ya kiwango ili tusije kulaumiana baadaye,maana hofu kubwa ni wapiga dili,hawa ndio wametufikisha hapa na kutufanya tusiaminiane.
Ndio maana kuna haja ya viapo
 
Mkuu kwani hujajua principles za hydropower? Ukishajenga bwawa, una control maji yanayotoka katika bwawa kuelekea downstream, baada ya kuzalisha umeme. Kwa hiyo flow inayoingia haiwezi kuwa sawa na ile inayotoka. Hope tuko ukurasa mmoja!
Nakuelewa, but always you can allow the minimum flows for ecological and human need
 
In general huu mradi ulikwama kwa sababu za kimazingira zaidi, na si kiuchumi wala siasa. Kuna ripoti nilisoma mahali kwamba financiers wa Kizungu waligoma kwa sababu mradi ulikuwa unapunguza kiwango cha maji kwa watumiaji wa chini (downstream users) ambao wako hasa wilayani Rufiji.

Mkuu umesahau suala nyeti la bianuwai ya Wanyama na mimea (gene pool) ktk pori la Selous. Nina uhakika wataalamu wetu wa ndani watakuja na mipango mizuri ya jinsi ya kuepusha athari juu wanyama na mimea na hatimae mradi utajengwa. Then we can become the African power giant. Wanaharakati wa mazingira watatushambulia lkn faida ni maradufu kulikoni hasara
 
Mkuu umesahau suala nyeti la bianuwai ya Wanyama na mimea (gene pool) ktk pori la Selous. Nina uhakika wataalamu wetu wa ndani watakuja na mipango mizuri ya jinsi ya kuepusha athari juu wanyama na mimea na hatimae mradi utajengwa. Then we can become the African power giant. Wanaharakati wa mazingira watatushambulia lkn faida ni maradufu kulikoni hasara
Usanifu wa bwawa huzingatia yote hayo, ndio maana kihansi kulijengwa
 
Tatizo Injinia wakibongo wengi ni Copy and Paste likija suala la Designing...
Ila Magufuli anaeeza wafikiria katika ufalme wa Bwala la St. GEORGE

Mimi ni mzalendo sana ila nawajua hawa. Hamna kitu. Tutapoteza pesa tukiwaamini hawa. Hebu nipe mfano wa bwawa walilojenga hao wahandisi wa kitanzania? Hatuwezi kufanya majaribio kwa pesa za umma. Wasubiri tuwe matajiri ndipo tuwape hizo fursa za kujaribu na kukosea.
 
Sio lazima wawe wanataaluma hata wanafunzi wao wanaweza kufanya vzr kabisa


Experience matter, utapata wapi mbongo mwenye experience ya dams design and construction nchi hii bila kugusa wanataaluma ambao wanafanya kazi ndani na nje, hata kama wapo ni wachache sana na ni nani anawajua. Kazi zenyewe zinatokea mara moja kwa miaka 20 labda.
 
Back
Top Bottom