Ujenzi wa Barabara ya Kilombero mkandarasi anaidai Serikali?

Dorcas21

Member
Dec 7, 2021
16
65
UJENZI WA BARABARA KILOMBERO MKANDARASI ANAIDAI SERIKALI?

Mheshimiwa Rais, wilayani Kilombero, mkoani Morogoro, miradi mingi ya kimaendeleo ambayo inatumia fedha za umma haikamiliki kwa wakati. Iko mingi sana lakini kilio hasa ni huu mradi wa ujenzi wa barabara ya kiwango cha lami, ya urefu wa kilomita 66.9 tu, Kidatu-Ifakara.

Tangu tarehe 04/05/2018 aliyekuwa Rais wa Tanzania, Hayati John Pombe Magufuli, aweke jiwe la msingi(azindue ujenzi) huku serikali ikisema ingekamilika mwaka 2020 ajabu hadi leo 2022 mkandarasi bado yuko kujenga tu! Mkwamo uko wapi?

Ujenzi wa hii barabara hadi kukamilika kwake itagharimu kiasi cha shilingi za kitanzania bilioni 104.914 ambazo ni ufadhili wa Umoja wa Ulaya(EU) iliyotoa asilimia 49.15 ya gharama ya ujenzi huu, Uingereza(UK) 40.13%, USAID 10.72%, na gharama iliyobaki italipwa na serikali ya Tanzania.

Hii barabara ni ya muhimu katika kuchochea maendeleo ya kiuchumi katika ukanda wa Kilombero na Ulanga. Ili mtu afike halmashauri ya wilaya ya Malinyi, halmashauri ya wilaya ya Ulanga, na halmashauri ya Mlimba kutoka Morogoro mjini ni lazima apitie barabara hii hadi mjini Ifakara.

Ujenzi umeanza 04/05/2018, leo 2022, mkandarasi bado yuko site tu kujenga! Mheshimiwa Rais, ama mlio karibu na mamlaka ya urais, lifanyieni kazi hili. Mwendo wa kinyonga wa mkandarasi katika kukamilisha huu mradi unatokana na nini?
 
Aisee, hii barabara bado tu haijakamilika Hadi leo?...watu wanaleta utani Sasa kwenye vitu vya msingi.
 
UJENZI WA BARABARA KILOMBERO MKANDARASI ANAIDAI SERIKALI?

Mheshimiwa Rais, wilayani Kilombero, mkoani Morogoro, miradi mingi ya kimaendeleo ambayo inatumia fedha za umma haikamiliki kwa wakati. Iko mingi sana lakini kilio hasa ni huu mradi wa ujenzi wa barabara ya kiwango cha lami, ya urefu wa kilomita 66.9 tu, Kidatu-Ifakara.

Tangu tarehe 04/05/2018 aliyekuwa Rais wa Tanzania, Hayati John Pombe Magufuli, aweke jiwe la msingi(azindue ujenzi) huku serikali ikisema ingekamilika mwaka 2020 ajabu hadi leo 2022 mkandarasi bado yuko kujenga tu! Mkwamo uko wapi?

Ujenzi wa hii barabara hadi kukamilika kwake itagharimu kiasi cha shilingi za kitanzania bilioni 104.914 ambazo ni ufadhili wa Umoja wa Ulaya(EU) iliyotoa asilimia 49.15 ya gharama ya ujenzi huu, Uingereza(UK) 40.13%, USAID 10.72%, na gharama iliyobaki italipwa na serikali ya Tanzania.

Hii barabara ni ya muhimu katika kuchochea maendeleo ya kiuchumi katika ukanda wa Kilombero na Ulanga. Ili mtu afike halmashauri ya wilaya ya Malinyi, halmashauri ya wilaya ya Ulanga, na halmashauri ya Mlimba kutoka Morogoro mjini ni lazima apitie barabara hii hadi mjini Ifakara.

Ujenzi umeanza 04/05/2018, leo 2022, mkandarasi bado yuko site tu kujenga! Mheshimiwa Rais, ama mlio karibu na mamlaka ya urais, lifanyieni kazi hili. Mwendo wa kinyonga wa mkandarasi katika kukamilisha huu mradi unatokana na nini?
Kama mzalendo wa kweli nimeamua kujitwisha huu mzigo wa hili deni. Billion 104 tu iyo si ni dollar million 40 na kitu?
 
Kama mzalendo wa kweli nimeamua kujitwisha huu mzigo wa hili deni. Billion 104 tu iyo si ni dollar million 40 na kitu?
SERIKALI WAONGO,,HAWASEMI KWANINI MRADI UNAKWAMA,PROF MBAWALA TWAMBIE UKWELI TUELEWE
 
Nlipita hiyo njia 2019 kwenda ifakara kama mpaka Leo bado kuna tatizo mahali cyo bure
 
Hii barabara ni ya muhimu katika kuchochea maendeleo ya kiuchumi katika ukanda wa Kilombero na Ulanga. Ili mtu afike halmashauri ya wilaya ya Malinyi, halmashauri ya wilaya ya Ulanga, na halmashauri ya Mlimba kutoka Morogoro mjini ni lazima apitie barabara hii hadi mjini Ifakara.
Sijui kama serikali inatambua kuwa barabara hiyo inaweza kuendelezwa mpaka Mufindi au Njombe ikawa ndiyo njia mbadala siku madaraja ya Iyovyi, Ruaha Mbuyuni na Ruaha Ipogolo yakikatika au siku Kitonga kukichafuka kukawa hakupitiki
 
Tangu tarehe 04/05/2018 aliyekuwa Rais wa Tanzania, Hayati John Pombe Magufuli, aweke jiwe la msingi(azindue ujenzi) huku serikali ikisema ingekamilika mwaka 2020
Labda zilitumika kuchukulia ushindi wa kishindo
 
Ukweli ni kwamba wilaya ya Kilombero na mji wa Ifakara kuna shida sana, achilia mbali kutokukamilika kwa barabara ya Kidatu Ifakara kwa kipindi chote hicho lakini pia wilaya hiyo haina hospitali ya wilaya tangu nchi ipate uhuru, na viongozi wapo wala hawajali hilo.
Kwahiyo wilaya ya Kilombero ni eneo ambalo haliangaliwi sana na viongozi wa juu wa serikali katika maswala yote, uchumi, afya, elima na maendeleo kwa ujumla, limekuwa kama shamba la bibi kwa wajanja wachache kujipigia hela bila kufutiliwa na yoyote.
 
Sijui kama serikali inatambua kuwa barabara hiyo inaweza kuendelezwa mpaka Mufindi au Njombe ikawa ndiyo njia mbadala siku madaraja ya Iyovyi, Ruaha Mbuyuni na Ruaha Ipogolo yakikatika au siku Kitonga kukichafuka kukawa hakupitiki
Kwa hiyo bank ya dunia imeshamaliza kutoa fedha zimeliwa?
 
Kilombero na mji wa Ifakara kuna shida sana, achilia mbali kutokukamilika kwa barabara ya Kidatu Ifakara
Msaada:
Hii miji inanichanganya, Kidatu ni sehemu gani, Kilombero ni wapi, kuna sehemu wanapaita Kilombero lakini ukipita unamkuta DC wa Kilosa anahamasisha chanjo kwa wananchi, ukifika Ifakara unaambiwa wilayani ni Kidatu, ukienda Kidatu unakuta bwawa la umeme na wafanyakazi wa Tanesco tu
 
Umesahau mvua kubwa zilizosomba udongo mpaka Kidatu bwawa likataka kupasuka??
Hiyo barabara bila kuweka miundo mbinu ya kupotosha maji hakuna barabara ya lami, itakayodumu hata msimu mmoja wa maporomoko ya maji!

Halafu wapogoro wachawiiiii, hawataki lami, wangetaka lami dk 0, PM alienda huko once hajarudi, yaani jamaa wameroga KASSIM hajarudi!
 
Msaada:
Hii miji inanichanganya, Kidatu ni sehemu gani, Kilombero ni wapi, kuna sehemu wanapaita Kilombero lakini ukipita unamkuta DC wa Kilosa anahamasisha chanjo kwa wananchi, ukifika Ifakara unaambiwa wilayani ni Kidatu, ukienda Kidatu unakuta bwawa la umeme na wafanyakazi wa Tanesco tu
Watu wa kule wajinga sana, hawafafanui sehemu zao vizuri unaweza kupotea, ila kifupi ni kuwa pale ruaha wenyewe wanapaita k2 ipo upande wa wilaya ya Kilosa, then ukivuka daraja tayari upo k1 ambapo ndio kidatu wilayani kulombero. Kwa hiyo kuna kilombero mbili yaani k1 nak2 moja ipo kilosa nyingine ipo kilombero yaani kidatu. Kinachotenganisha ni ule mto ruaha.
 
Watu wa kule wajinga sana, hawafafanui sehemu zao vizuri unaweza kupotea, ila kifupi ni kuwa pale ruaha wenyewe wanapaita k2 ipo upande wa wilaya ya Kilosa, then ukivuka daraja tayari upo k1 ambapo ndio kidatu wilayani kulombero. Kwa hiyo kuna kilombero mbili yaani k1 nak2 moja ipo kilosa nyingine ipo kilombero yaani kidatu. Kinachotenganisha ni ule mto ruaha.
Nashukuru sana mkuu, sijui kwanini wamefanya vile majina yanavuka mipaka
 
Back
Top Bottom