Ujenzi: Je, hii nyumba ya TAKUKURU Dodoma inafikia thamani tajwa ya Tsh. 143 milioni?

Hyo nyumba Ina design mbayaa!!

Kaka nadhani hii ndo sababu mpaka imepelekea kuonekana cheap, kwa gharama Ni sawa kabisa Ila muonekano wake cheap
Kiukweli designer ndo kawapponza, mengine yote nayakubali, mi nimejenga 100 imeisha Ila nyumba haijaisha. Spanish tiles vyooni tu 3 mil 10
 
Wskati unaendelea na uchunguzi ukumbuke pia ujenzi wa nyumba za kuishi hizi za kwetu ujenzi wake ni tofauti sana na seeikali
Mbona unang'ang'ania ni TOFAUTI ni TOFAUTI muda wote... Kwani hizo za SERIKALI ZINAJENGWA MBINGUNI KWAMBA HATUZIONI? Acha uongo wa kizamani ww.. Hilo JENGO hata kama floor na wall yake wangetumia terrazo bado isingefikia hiyo bei.. hata fittings ziko cheap sana.. angalia ukubwa wa madirisha na milango utaona.. Material ya serikali yananunuliwa na watu hawa ambao kila siku tunakuwa nao ofisni na sisi wenyewe wahasibu ndio tunaandikia voucher hizo.. Acheni utetezi wa ajabu. HILO JENGO haliwezi fika mil 100. Hata uwaweke hao wasimamizi ambao kimsingi wana mshahara ambao ndio moja ya jukumu lao.
 
Mbona unang'ang'ania ni TOFAUTI ni TOFAUTI muda wote... Kwani hizo za SERIKALI ZINAJENGWA MBINGUNI KWAMBA HATUZIONI? Acha uongo wa kizamani ww.. Hilo JENGO hata kama floor na wall yake wangetumia terrazo bado isingefikia hiyo bei.. hata fittings ziko cheap sana.. angalia ukubwa wa madirisha na milango utaona.. Material ya serikali yananunuliwa na watu hawa ambao kila siku tunakuwa nao ofisni na sisi wenyewe wahasibu ndio tunaandikia voucher hizo.. Acheni utetezi wa ajabu. HILO JENGO haliwezi fika mil 100. Hata uwaweke hao wasimamizi ambao kimsingi wana mshahara ambao ndio moja ya jukumu lao.
Nimekusamehe bure kwani una jina linafanana na jina mke wangu
 


Karibuni waumini wa majadiliano katika mjadala huu ambao mh Rais amesema angeweza kujenga nyumba hii kwa mill 43.

Kwa mtazamo wangu, licha ya kutoiona nyumba hii kwa ndani huwezi jenga chini ya million 90 na kama gharama za vifaa, mchanga na cement eneo husika zipo juu kufika mill 100 sioni ajabu kwa upande wangu.

Karibuni mafundi kwa majadiliano.

View attachment 1514090
Inategemea ni taratibu zipi za ujenzi zimetumika kuanzia 10% ya aliyeandaa ramani kulingana eneo la ujenzi, 10% ya aliyeandaa BOQ nk,kuna hostel imejengwa na TASAF hapa kijijini kwa milioni 75 lakini kilichotumika kwenye jengo ni 50milioni,hizo milioni 25 kuna gawio kuanzia kamati ya TASAF ya kijiji,Ofisi ya Afisa Mtendaji wa kijiji,kata Ofisi ya TASAF wilaya hadi ya mkoa.Je huu ulaji wote wa nini na wameweka katika utaratibu.Mwisho zile nyumba ndogo za NHC(National Housing Cooperation) za vyumba 2 na sebule unaambiwa milioni 32 hadi 46 je ni vipi?
 
Kama munashangaa hiyo nyumba Mil 140 JPM angewauliza viongozi wake wa CCM waliotumia Bil 6 kujenga Mnara wa Mapinduzi Zanzibar!
 
Huwezi mkuu, nyumba za serikali hazijengwi na vifaa vya ujenzi vya hovyo hovyo.
Tofali grade one tena za kulaza mara nyingi, ratio ya cement ya hali ya juu na bati gauge 26.
Huwa mnakurupuka mnalinganisha na vibanda vyetu vya mtaani.
Pili huwa kuna bei elekezi ya ujenzi mfano mdogo...
...majengo ya hospitali cost/sqm huwa ni 850,000
...magodauni cost/aqm ni 500,000
Na hapa kuna washauri/consultants lukuki
Mfano.. Quantity surveyors
...architects
....structural Eng
Na kadhalika na hawa wote wanalipwa ghali, hapa bado hujajua finishing ya ndani na SAMANI zake.
Msiwe mnakurupuka bila kuwa na ufahamu sahihi

Huwezi kuzunguka nyumba eti ukapata gharama za ujenzi.
Pitia manunuzi na pitia kitabu cha consultants uone mapendekezo yao katika ujenzi pamoja na samani zilizopo ndani
Watu wanaongea ushabiki tuu,tena unaweza kukuta kwenye hiyo hela hata ya supervision ilikuwa inatoka kwa manati.Ujenzi wa kutumia ratio ya 20 block/50kg cement bags tena vibrated (electrical power).Unakuta mchanga na kokoto zinatoka mbali,gharama za material ya finishing. Hizo gharama huenda zipo sawa ila kwa uoga na kujipendekeza kuna watu watakuja na ripoti kuwa kuna hela imepigwa.
 
Hii nyumba Ni kubwa mno,
Tena inatakiwa kua mil 150+ Kama ukiamua kuitendea haki upande wa material

HEBU TUPIGE HESABU SASA

1. MSINGI
(Kusafisha kiwanja, Kuchimba msingi,KIFUSI, tofali,cement, mchanga, maji,kumwaga jamvi,ufundi,mengineyo)
Almost 10mil imekata.

2. Kuinua kuta
(Tofali, mchanga, maji, ufundi,mengineyo)
Almost 15 mil imekata

3. Kumwaga beam nondo 4 nyumba nzima
(Nondo,kokoto,mbao, misumari, maji,mchanga,cement,ufundi, mengineyo)
Almost 10 mil imekata

4. Kupinga kenchi(KUPAUA)
(Mbao,misumari,binding wire, ufundi,fisha bodi ,mengineyo)
Almost 5mil imekata

5. Kupiga bati (kuezeka)
(Bati geji 28 au 26, misumari, gundi, ufundi, mengineyo)
Almost 15mil imekata

BOMA LIMEISHA, ALMOST 45Mil IMESHAKATA

Finishing

6. Hizo dirisha (alminium+ Gril+rangi+mengineyo) zilizotandazwa apo usichukulie poa.
Kwa haraka haraka Ziko sio chini ya 15 apo@500,000.
Mpaka zinavoonekana apo Almost 8mil imekata

7.Bado milango (frem+Top+vitasa+rangi+ufundi, mengineyo)
Kwa haraka haraka haipungui milango 10 ilo jengo. Each 400,000.
Mpaka inavoonekana apo Almost 5mil imekata

8.Hizo tiles bila shaka Ni first grade (TAASISI),
zimetandazwa sakafuni mpaka ukutani.
Mpaka zinavoonekana (tiles,grout,strips,skating,ufundi,mengineyo) apo Almost 15mil imekata

9.Hujaja gharama ya lipu, (mchanga, cement, ufundi,maji,mengineyo)
almost 10 mil nje ndani imekata

10.skimming ya nyumba nzima nje ndani kwa white cement(Rangi, white cement,ufundi, mengineyo)
Almost 7mil imekata

11. Kupiga BANDARINGI kwa ajili ya gypsum bodi.
(Mbao,misumari,ufundi,mengineyo)
Almost 7mil imekata

12. Kupiga GYPSUM BOARD
(Gypsum bodi,skruu, faiba tepu,ufundi,mengineyo)
Almost 7 mil imekata

13. Kupiga RANGI NYUMBA NZIMA nje ndani
(Rangi,ufundi,mengineyo)
Almost 5 mil imekata

14. MFUMO WA UMEME (wayaringi)
Hapo lazima nyaya SINGLE CORE first grade zimetembea za kutosha, TRONIC switch,socket,m/switch,breaker,cutout, earthrod,conduit,boxes, process za KUOMBA MITA TANESCO,ufundi n.k.
Apo almost 10mil imekata

15. MFUMO WA MAJI
Nazungumzia vyooni,jikoni,bafuni na kwingineko.
(MaSink, tanki, mabomba, ufundi, mengineyo)
Almost 5mil lazima ikate.

16. SHIMO LA CHOO
(Kuchimba,tofali,cement,mchanga,nondo,kokoto, ufundi,waya meshi, mengineyo)
Almost 2mil imekata

FINISHING tu MPAKA HAPO, jumla 81mil IMESHAKATA.

Sasa ukijumlisha
Kujenga boma 45mil + finishing 81mil= jumla 126mil.

Unaweza kuongezea na 10 mil ya kupiga FINAL TOUCHES ili kunogesha zaidi nyumba.

Kama urembo kwenye nguzo, vibaraza mbalimbali, bustani, taa za urembo, mfumo wa CCTV camera, bango, n.k

ALMOST 136MILLION inakamilisha Ilo jengo.


My take:
SIDHANI KAMA Kuna upigaji hapa.
Na Kama upo Basi ni kwa kiwango kidogo Sana.

Tena inaweza kua kwa kwa vitu vidogo vidogoKama kulipana posho, overtime,chakula Cha saiti,usafiri n.k.

Vinaweza kukava icho kiwango kinachopelea (yaani 7million) kufikia icho kiwango halisi walichotaja Cha 143million.

Shukran
You nailed it.
Kuna watu hawajawahi au wanakuwa na mihemko tuu ya kisiasa.Woga utapelekea watu waangushiwe jumba bovu bure,yaani kufanya justification ya matumizi kwenye ujenzi hakuketi shida yoyote.Kuna jengo moja nilishiriki kwenye Project Committee,tena tulikuwa tunafanya renovation/rehabilitation (BoQ_alikuwa karibu 170m).Kwenye uhalisia sasa tumefikia zaidi ya 190m kukamilisha jengo.
Hebu imagine ili ufyatue tofali inakubidi upate mchanga wa aina tofauti tofauti uchanganye (maana kuna maeneo hakuna mchanga unaotakiwa zaidi ya vumbi vumbi).Hiyo gharama hapo jamaa kwenye supervision wamemega na hela yao ya mshahara aisee.
 
Watu wanaongea ushabiki tuu,tena unaweza kukuta kwenye hiyo hela hata ya supervision ilikuwa inatoka kwa manati.Ujenzi wa kutumia ratio ya 20 block/50kg cement bags tena vibrated (electrical power).Unakuta mchanga na kokoto zinatoka mbali,gharama za material ya finishing. Hizo gharama huenda zipo sawa ila kwa uoga na kujipendekeza kuna watu watakuja na ripoti kuwa kuna hela imepigwa.
Tena matirio hayo bado yanapelekwa maavara kupinwa ubora kwa gharama kubwa tu
 
Nyumba za serikali lzm zijengwe kwa ubora sio km nyumba y mtu binafsi. Lzm serikali iwe makini kwa hili tusiingiize siasa kwenye taaluma. Nyumba sio kusimamisha tofali. Tizama finishing ikoje. Tukienda hivi kutaka nyumba iwe 43m zitajengwa nyumba za miaka 5 km kambi za wakimbizi.
 
Hiyo nyumba tuseme kupaua ni milioni 10
Msingi na jamvi milion 10.
Kupandisha tofali juu milion 10
Finishing milion 15
Ziada milini 10.

Jumla milioni 55!

Magu yupo sahihi hapo pana upigaji!

Kwa hiyo hela milioni 143 ilitakiwa zitoke nyumba kama hizo 3

Kama TAKUKURU Mambo yako hivyo,

Je, huko mwingine hali ikoje.

Nyumba tatu (3) zimejengwa,

moja ni hiyo ya ofisi

mbili ziko mitaani za kuishi WAJANJA na familia zao.
 
Hiyo nyumba tuseme kupaua ni milioni 10
Msingi na jamvi milion 10.
Kupandisha tofali juu milion 10
Finishing milion 15
Ziada milini 10.

Jumla milioni 55!

Magu yupo sahihi hapo pana upigaji!

Kwa hiyo hela milioni 143 ilitakiwa zitoke nyumba kama hizo 3
Mheshimiwa Raisi yupo sahihi kabisa, kwa milioni 40 with effective supervision unajenga kama hiyo
Haivuki ml 45
Ukinipa M 143 nakuletea nyumba kama hiyo mbili na vimilioni vichache vinabaki.
Hii nyumba kama ni mimi mpaka hapo haizidi milioni 70
Mimi ukinipa 20 nakujengea.
Iyo kwa ml 143 mmmhh wizi mi sio injinia lakini kwa mtizamo wangu wamepiga hata ujengwe msingi mrefu kiasi gani
Hapana,hiyo nyumba ikijengwa na fundi mzuri tu wa mtaani kwa viwango bora kabisa vya kitaalamu haizidi mil 75,nyie kina architech wapigaji sana.calavati tu za maji ya mvua mnajenga mbili wa mil 40,hamfai nyinyi.

Sent from my SM-A105F using JamiiForums mobile app
Sawa ila hata kama lakini haivuki 15
Million 70 safi kila kitu, tuache unafiki
Milioni 143, zinatoka nyumba kama hizo tatu
Pale layman (mwanasiasa) anapokua injinia tena structural engineer.

Sent from my SM-A515F using JamiiForums mobile app
 
*Tofari 5000×1500= 7, 500, 000Tsh

*kokoto na mchanga=2, 000, 000Tsh

*Nondo 100×25000=2, 500, 000Tsh

*ciement mifuko 200×15000=3, 000, 000Ts

*Mabati 80(Gauge 28)
75×33000= 2, 640, 000 Tsh

* mbao= 3, 100, 000Tsh

*madirisha na milango (complete)=
16, 000, 000Tsh

*Tiles +gypsum+rangi=
7, 000, 000Tsh

*maji(pamoja na masinki ya jikoni, chooni) + umeme= 7, 000, 000Tsh

*maitaji madogo madogo
1, 000, 000Tsh
* ufundi Tsh. 10, 000, 000/=


Jumla Tsh 60, 000, 000/=
Unaongelea nyumba standard ya taasisi ya serikali au banda la kufugia kuku?

Sent from my SM-A515F using JamiiForums mobile app
 
Vinavyochangia majengo ya serikali kuwa na gharama kubwa baadhi ni hizi:-
  • Mshauri - huyu naye analipwa kutokana na ujuzi wake (kampuni)
  • Meneja wa mradi- hii itategemea kama atatoka ndani ya taasisi au nje
  • Mkandarasi- hii ni kampuni iliyoajiri mafundi na vibarua kujenga hilo jengo (Kampuni)
  • Upimaji wa udongo- hii pia ni gharama (Kampuni)
  • Upimaji wa malighafi mf. kokoto,mchanga, mawe n.k
  • Kutumia malighafi zenye ubora wa hali ya juu- hii pia ni gharama
  • Kutumia uwiano unaokubalika- mfano;- kwenye zege, tofali, mchanga na simenti, n.k
 


Karibuni waumini wa majadiliano katika mjadala huu ambao mh Rais amesema angeweza kujenga nyumba hii kwa mill 43.

Kwa mtazamo wangu, licha ya kutoiona nyumba hii kwa ndani huwezi jenga chini ya million 90 na kama gharama za vifaa, mchanga na cement eneo husika zipo juu kufika mill 100 sioni ajabu kwa upande wangu.

Karibuni mafundi kwa majadiliano.

View attachment 1514090

Haiwez kuzidi million 50. Tena hiyo Ni kwa viwango vya juu sana. Hicho mbona ni kibanda cha uani.
 
Back
Top Bottom