Ujasusi - Umoja namba 97

SEHEMU YA 74
DAMIANI MISSIONS( MISHENI ZA DAMIANI )
Upande mwingine , alionekana bwana sam au rich sam akiingia ndan ya jengo la LAPF jengo lililkuwa likipatikana ndani ya eneo la Makumbusho sayansi , bwana huyu mara baada ya kuingia ndani ya jengo hili akiwa na gari yake aina ya Prado, baada ya kupaki moja kwa moja alielekea ndani nya jengo hili .
Ndani ya sekunde kadhaa tu alikuwa ndani ya floor ya kampuni ya KILAC , kampuni iliokuwa ikimilikiwa na bwana kimbona .
Baada ya kufika mapokezi aliruhusiwa moja kwa moja na kwenda kuonana na kimbona kwani alikuwa na miadi naye .
“ karibu sana sam “
“ shukrani ndugu yangu “
“tokea siku ile tuachane hatujaonana Zaidi ya kuwasiliana kwenye simu “
“ ndio ni kweli , na ndio maana nimekuja hapa , japo kuna mambo ambayo nataka kujadiliana na wewe , lakini ni vyema pia tumepata nafasi ya kuonana “
“ jambo gani hilo , nadhani sio jambo dogo “
“ si kubwa sana lakini pia sio dogo sana “
“ nakusikiliza ndugu yangu “
“ ni juu ya mpango zero “
“ mpango zero , kuna shida gani si upo chini ya INNOVA?”
“ ni kweli mpango huu upo chini ya INNOVA , lakini wasimamizi wakuu ni sisi tuliopo ndani ya Tanzania”
“ kuna nini juu ya huo mpango ?”.
“ nilikuwa na kikao na wahandisi wa mpango huu , na ili jambo hili kufanikiwa lazima kuwe na majaribio , na majaribio hayo hayawezi kufanyika tu mahali popote “
“ majaribio hayo ni majaribio gani umeniacha mbali mpaka hapo ?”
“ sijajua kwa kina majaribio hayo ni ya aina gani , ila kampuni inahitaji watu wa majaribio “
“ watu wa majaribio ?”
“ ndio , inahitaj watu wa majaribio , lakini watu hao wanaweza kufariki wakati majarbio hayo yakiendelea “.
“ kwa hapo swala hilo ni gumu kwani hatuwezi kuwapeleka watu katika kifo kwa hiari “.
“ndio maana niko hapa , nadhan mpaka hapo umenielewa “
“kwa hio kipi kifanyike , na ni watu wa aina gani wanahitajika ?”
“ wanasema wanahitaji kwanza vichanga kwa awamu ya kwanza kati ya umri wa miezi sia kuendelea mpaka mwaka mmoja , wanahitaji watoto jumla hamsini “
“ hamsini ?”
Kimbona alijikita akitoa macho , watoto wachanga hamsini ni wengi mno , watatoka wapi watoto hao , hilo ndio swali la kwanza lililoingia kwenye kichwa chake .
“ ni wengi mno , tutawapataje sam ?”
“swali hilo ni zuri kimbona “
“ kuna karatasi kutoka makao makuu ya U-97 imekuja , na imeeleza namna ya kuwapata watoto hao ndani ya Tanzania , lakini karatasi hio lazima isainiwe na Raisi Wa Jamhuri Ya Muungano Wa Tanzania na pale itakapo sainiwa moja kwa moja zoezi hilo litaanza “
“ sasa hio karatasi inaeleza nini jinsi ya kuwapata?”.
“bado sijaisoma , lakini muda si mrefu fomu hio italetwa kwenye kikao kitakachofanyika siku chache zijazo , na hio ni baada ya raisi kusaini na kutia muhuri wa barua hio “
“ raisi atasaini kweli , maana hilo swala la vichanga kufanyiwa majaribio ni gumu mno , maana watapatikana wapi?”
“ linaweza kuwa gumu , lakini lazima asaini kwani na yeye yupo ndani ya umoja , na akikiuka maagizo inamaana anakitafuta kifo , na kwa ninavyomjua henry hawezi kukubali kifo “.
“hapo ni kweli , lakini swala hili hata kwa mimi mwenyewe linanipa ugumu sana , huu mpango unaohitaji vichanga ni mpango gani kwanza ?”.
“hilo siwezi kujua kimbona , na nipo hapa kwasababu katika kikao hicho sisi tunaowakilisha wenzetu lazima tutie na sisi sahihi katika karatasi hio ya mkataba “
“ kutia saini tena “.
“ ndio , na hio ndio kazi niliopewa , kuwashawishi wana umoja wote asitokee hata mmoja wa kupinga jmbo hilo , kwa hio kimbona jiandae kwa siku hio “
“mmi nitasaini “ aliongea kimbona na kumfanya sam atabasamu .
“ nilijua utasaini “
“ hahahaha.. unaonekana kunifahamu vyema “
“ ndio maana sisi ni marafiki “
“ ni kweli “.
*****
Damiani alijikuta akipigwa na butwaa , baada ya kuingia ndani ya chumba hiki , hakikuwa chumba , kwani kilionekana kama maabara Fulani hivi yenye teknolojia ya hali ya juu mno ,, mwonekano wa chumba hiki ulikuwa ni wa kipekee ,uliopendezeshwa na tarakishi zilizokuwa zimpangiliwa kwa mpangilio mzuri huku zikiwa zinawaka , lilikuwa ni jambo la kushangaza mno kwa kijana damiani , kwani hakutegemea kama kuna sehemu ndani ya Tanzania yenye chumba kama hicho, chumba hiki kilikuwa kipo chini kabisa ya ardhi kwani hakukuonekana na dirisha lolote Zaidi ya mwanga flani wa rangi ya blue ( ultravilot light ) uliokuwa ukikimulika chumba hiki .
Lakini kilichomshangaza Zaidi , kulikuwa na roboti lililokalishwa kwenye kiti , likiwa na muonekano flani hivi wa kama sanamu zile za budha , lakini lilikuwa na macho flani yanawaka taa , huku likiwa na uwezo wa kuzungusha kichwa , lilikuwa likitoa sauti lakini midomo haikucheza , lakini cha kushangaza Zaidi ni kwamba roboti hili lilikuwa na uwezo wa kuzikotrol tarakishi zote zilizokuwa ndani ya chumba hiko ( LEGACY ROOM )
“Mister Damiani Rabani you can ask me anything
( Unaweza kuniuliza jambo lolote Damiani Rabani)
“wewe ni nani ?”.(Who are you)
“I am designed to assist you in all plan X missions you can call me Miss Nara
Nimetengenezwa ili kukusaidia kukamilisha misheni zote za mpango X unaweza kuniita Miss Nara )
“Nani aliekutengeneza ?”(Who created you)
“Bruno lamberk “.
“What is all about Plan X missions(Mpango X ni mpango gani?)
“Once you reach your final mission you will be informed , remember this is plan X , all deatails is concealed”(Utafahamu mpaka pale utakapofikia misheni ya mwisho ya mpango x , kwasasa ni mpango usiofahamika , na ndio maana unaitwa mpango x)
“ Why am I chosen to do those missions ?”(Na kwanini nifanye hizo misheni? ).
“Because without doing so , you won`t achieve your goals (Kwasababu pasipo kufanya hivyo hutoweza kukamilisha malengo yako)
“What do you know about my goals”(Unafahamu nini kuhusu malengo yangu?”)
“Taking revenge against peaple who involved with your mother`s death”(Kulipiza kisasi dhidi ya watu waliohusika na kifo cha mama yako).
“How did you know about death of my mother when the one created you died the same day and time wth her.( Wewe umejuaje mama yangu amekufa wakati , aliekutengeneza hajakupa hizo taarifa kwani alifariki siku aliokufa mama yangu ?”)
“I am created to have all informations about you Mister Damiani Rabani, I am the one who was instructing through all your steps Damiani (nimetengenezwa kujua vitu kuhusu wewe Mister Damiani , na mimi ndio niliokuwa nakupa maelekezo muda wote”
“Which instructions?”(Maelekezo gani)
“Ask yourself about that Damiani , To give you the hint: This is all of your calling logs, See if I am wrong”(Jiulize kuhusu hilo Mister Damiani , hizi ni taarifa zako zote siku , saa na sehemu uliopiga simu)
Damiani alijikuta akiangalia zile ‘calling logs’ na alijikuta akijua mtu aliekuwa akiwasiliana nae na kumpa maelekezo ni hili roboti linalojiita NARA.
“Vipi kuhusu mwanaume aliekuwa akinipa maelekezo”
“Those are real people staged to help you to accomplish the missions”( hao ni watu halisi , na wapo kukusaidia kukamilisha misheni zako)
“Can i identify them ??”(Naweza kuwajua ?)
“That is beyond informations available, but you will know them with plan X missions accompishiment” (Lipo nje ya uwezo wangu , lakini utawajua baada ya kumamilisha mpango x)
“How can I work with unknown people?(Nitafanyaje kazi na watu ambazo siwafahamu)
“With my help everything is possible Damiani( inawezekana kwani nipo mimi nitakaekusaidia)
“How about Sabi Mboneche (Vipi kuhusu Sabi mboneche?”)
“He is part of Plan X (sehemu ya mpango x)
“Unajua nini kuhusu Mzalendo ?”
“That info ..is unavallable”( Hio taarifa haipo )
Damiani baada ya kupokea hilo jibu alijikuta akishangaa , kwani alichokuwa akijua ni kwamba mzalendo ulikuwa pia unahusiano na mpango x , kwani kwenye maelezo ya sabi , |Madam wema alimwambia kuwa mpango x unamuunganiko na mzalendo , iweje taarifa muhimu kama hio haikuwepo , alijikuta akishangaa mno , lakini alijiambia huenda kuna sabau ya taarifa hio kutokuwepo hapo ndani.
“When am I to get started with those missions) ( ni wakati gani natakiwa kuanza hizo misheni)
“Within those document your are provided with Bruno, there ninety names in order you have to identify the frst name so as I can help you with killing map(Katika nyaraka ulizopewa na Bruno kuna karatasi moja ina majina tisini unatakiwa kutambua jina la kwanza ili nikupe ramani ya kufanya mauji)
Damiani alijaribu kukumbuka juu ya hii nyaraka , na ni kweli aliikumbuka vyema , kuna nyaraka ilikuwa na majina karibia tisini lakini hakuwahi kuyasoma na leo ndio anakumbuka kuwa majina hayo hakuwahi kuyasoma .
“How about those names”( nini kuhusu hayo majina ?)
“Those are what is missions of plan X , you have to kill those people as they are listed in Ascending order” (Ndio misheni zako ndani ya mpango X , watu walioko kwenye yale majiina wanatakiwa kuuwawa kwa mtiririko wa namba kama ilivyopangiliwa)
“Do you mean I have to kill all those people ?(Unamaanisha misheni yangu ni kuwaua hao watu)
“Yes” (Ndio )
“ And why do I have to kill them ??”(Na kwanini ni wauwe kuna sababu gani?)
“By not doing so you won`t be able to trace people who killed your mother” (pasipo kufanya hivyo huwezi kumpata mtu aliehusika na kifo cha mama yako)
Damiani alijikuta akipagawa mno , hakutaka kabisa kukaa tena ndani ya eneo hilo , kwani akili ilikuwa imetibuka Zaidi , alichojua tu ni kwamba hawezi kubishana na roboti hilo kwani sio mtu kwamba litabadili mawazo na ndio maana alitoka kwanza ili arudi kwake akaangalie yale majina , alitaka kujua kwanza watu hao ni wakina nani kabla ya kufanya maamuzi .
*******
Upande mwingine , suzzane alikuwa ashatoka nyumbani kwa sabi mbneche na sasa alikuwa nyumbani kwake , akiwa ndani ya chumba alichokitenga kwa ajili ya kazi zake za kipelelezi , mbele kabisa ya ukuta kulikuwa na picha za watu kadhaa aliokuwa akiwaaangalia huku akiwa amewawekea alama , na moja ya picha iliokuwa imewekewa alama ilikuwa ni ya damiani huku pembeni ikiwa imezungushiwa baadhi ya picha zingine na moja ya picha hizo kulikuwa na picha ya mwanadada janeth , kulikuwa na picha ya merina , kulikuwa pia na picha ya agent z (zakayo ) ,ya stephano lamberk ,kulikuwa pia na picha ya kimbona huku juu kabisa kulikuwa na picha mbili , ilikuwa moja ni ya mheshimia raisi john bendera onyango , na pembeni yake kulikuwa na picha ya bruno lamberk .
Chini kabisa ukitoka picha zilizokuwa zimemzunguka damiani kulikuwa na duara kubwa lilokuwa na x katikati na jina kwa chini yake ‘MZALENDO’.
Miss k (suzzane) alionekana kutafuta koneksheni iliopo katika picha hizo .
“Stephano lamberk ni damiani , nina uhakika na hili kwa asilimia mia moja , hawa wanaomzunguka damiani nina wasiwasi nao , mahusiano yao huenda sio ya kikazi tu , huenda kuna jambo la ziada , huyu merina anaonekana kufahamiana na zakayo , lakini pia zakayo anaonekana kufahamiani na janeth , janeth ni mtoto wa raisi bendera , najua hili sijamwambia mheshimiwa lakini huu sio muda muafaka wa kumwambia , nataka kwanza nijue anaejiita mzalendo ni nani , je kuna uhusiano wowte kati ya damiani na mzalendo , lakini bado kuna ugumu matukio wakati yanafanyika stephano lamberk hakuwa bado nchini kwa maana hio mzalendo ni mtu mwingine , mtu huyu ni nani ?, kama mtu huyu atakuwa anauhusiano na damiani basi uchunguzi wangu lazima uanzie wakati damiani anatoka nje ya nchi hii , nadhani kupitia hapo nitajua kila kitu … lakini janeth anahusikaje na Mzalendo ,kwanini achome madawa ya kimbona “.
Alifikiria agent huyu wakati huo akiwa amesimama ,alionekana kuwa na hasira kweli kila akiangalia paja lake lilikokuwa linamsumbua , alikumbuka vyema tukio la kupigwa risasi na damiani , alijua kumkamata damiani ni swala rahisi mno kwake kwani mpaka hapo alikuwa akijua damiani alikuwa akijificha kwenye kivuli cha stephano lamberk .
Wakati akifikiria hayo simu yake ilitoa mlio , ulikuwa ni ujumbe mfupi wa maandishi kutoka kwa mtu wake anampatia taarifa kutoka ikulu , na ujumbe huo ulikuwa ukimwambia kuwa kesho kuna watu wanaenda kuonana na raisi lakini moja ya watu hao alikuwa ni bwana stephano lamberk , jambo hilo lilimfurahisha sana kwani alitabasamu.
*****
Huku upande wa ikulu raisi Henry alionekana kuwa katika wakati mgumu mno kimaamuzi , kwani muda mfupi uliopita barua kutoka makao makuu ya U-97 ilimfiikia barua ambayo ilimhitaji kutia sahihi na kufanikisha majaribio ambayo yanahitajika kufanyika chini ya mpango zero .
Kulikuwa na vipengele vya aina mbili ndani ya mkataba huo m, kipengele cha kwanza kilikuwa ni kipengele cha hiari , kipengele hichi kilikuwa kinatoa hiari kwa mwanamke yoyote kubeba ujauzito kwa njia ya kupandikizwa mbegu za kiume . lakini swala hilo lilikuwa halifanyiki bure kwa wale ambao walikuwa wakijitolea, kunakuwa na malipo ya milioni kumi kwa kila mwanadada atakae jitolea .
Kipengele za pili kilikuwa si cha hiari , kipengele hiki kilihitaji watoto wachanga ambao ni mapacha wakufanana kwa ajili ya majaribio , hii ndio sehemu iliokuwa ngumu sana na iliompa Zaidi mawazo mheshimiwa , kwani kipendele hiki kilikuwa kikimtaka atie saini ya kuibiwa kwa siri kwa watoto pacha katika hospitali kuu , yaani kama watoto hao watabainika kupotea uchunguzi wote wa kipolisi usilenge kukamata wahusika , bali ulenge kuwaridhisha wananchi kwamba uchunguzi huo unafanyika.
Swala hili lilikuwa gumu kwake ukizingatia kwamba, watoto hao wanaoenda kufanyiwa majaribio kuna mawili wanaweza wakafariki kwenye mchakato wa majaribio au wakapona.
Alisoma makataba huu, Na kisha hakuwa na sababu ya kuusaini kwa siku hio kwani aliiweka pemben huku akifikiria cha kufanya.
****
Wakati hayo yanaendelea ikulu , upande wa Damiani alikuwa yupo ndani ya nyumba yake maeneo ya Makongo juu, alikuwa ameketi kwenye sofa huku akiangalia karatasi ile iliokuwa ni sehemu za nyaraka alizoacha Bruno.
Alikuwa akiangalia majina ambayo ni wakati mfupi tu kaambiwa kwamba watu waliokuwa kwenye majina hayo wanatakiwa kuuwawa, kwake swala hilolilikuwa ni swala gumu ukizingatia na majina yenyewe.
Moja ya majina yaliomshangaza Zaidi ni uwepo wa jina la waziri mkuu mstaafu , bwana Hamduni , kulikuwa pia na jina la raisi mstaafu bwana Athumani ndalu , kulikuwa na jina la mkuu mstaafu wa polisi , bwana Kizito kabwela , kulikuwa pia na jina la kimbona , kulikuwa na jina la Sam ,Damiani aliangalia majina haya yaliokuwa yamepangiliwa katika mtiririko wa kinamba
“Hawa wanahusikaje na kifo cha mama yangu?” lilikuwa ni swali la kwanza kuingia kwenye kichwa cha kijana huyu.
“Kimbona , kimbona “ Alijikuta akitamka hili jina mara mbili , mara picha ya mama yake kupigwa risasi inaanza kumjia kichwani chake , anakumbuka maneno ya ya Marie wakati akiwa Thailland , anakumbuka moja ya watu waliokuwa wakizitaka nyaraka alizokuwa nazo , mmoja wa alikuwa ni mtu aliejiita Sam .
“Kimbona na Sam “Hawa watu inabidi niwe na taarifa zao.
Damiani aliangalia upya ile karatasi kwa mara nyingine , aliangalia majina hayo yote tisini , na katika majina hayo ni machachee sana alikuwa akiyajua , mengi yalionekana yalikuwa majina ambayo sio ya nchi ya Tanzania , kwani kuna yaliokuwa yakisomeka kwa kifaransa , kuna yaliokuwa yakisomeka kwa kichina , lakini kuna pia yaliokuwa yakisomeka kwa kijerumani .
Jina la juu kabisa ndani ya karatasi hio ambalo kwa maelezo ya NARA ni kwamba hio ndio misheni yake ya kwanza , jina hili lilikuwa likisomeka ‘ Mahmood seid ‘..
******
Ni siku nyingine kabisa , siku ambayo raisi henry alikuwa akitegema kuoanana na wageni ambao amewaalika siku hio ndani ya ikulu yake , wageni hao walikua ni stephano lamberk ambaye rasi Henry alikuwa akimjuua kama mfanya biashara ,Merina sosteness , Zakayo na proffessa Janeth .
Kama sabi alivyokuwa amepewa maagizo na raisi ndivyo alivyofanya , kwani wageni hao mheshimiwa huyo alihitaji kuonana nao kila mtu kwa wakati wao , na ndio maana kila mtu alikuwa na ratiba yake ya kuingia hapo ikulu .
Mtu wa kwanza kuonana na mheshimiwa siku hio alikuwa ni Merina , japo mwanadada huyu alikuwa kwenye mawazo juu ya |Damiani kuhusiana na maneno alio yasikia kwa Janeth , lakini hakuacha kufika ndani ya ikulu kwa ajili ya kutii wito wa mheshimiwa , kwake swala hilo lilikuwa muhimu mno kwani ni swala lililokuwa likizihusisha biashara zake kwa ujumla .
Mtu wa pili kufika alikuwa ni Stephano lamberk, haikuleweka sabi alifanya makusudi, lakini muda ambao merina alikuwa akiingia ikulu ndio muda ambao stephano lamberk alikuwa akiingia ikulu.
Katika sehemu ya kuegesha magari mtu wa kwanza kutoka kwenye gari yake ya kifahali alikuwa ni Stephano lamberk , na wakati anatoka tu na gari ya merina ilifika maeneo hayo na kusimama na akatoka mlimbwende huyo ambae siku hio alikuwa amependeza vyema , merina alijikuta akibung`aa mara baada ya kukutanisha macho yake na macho ya stephano lamberk .
Wakati wanaendelea kushangaa iliingia gari nyngine aina ya roll Royce , gari hii ilikuwa ni ya mtaalamu Patrick , na yeye alishuka kwenye gari yake na hata yeye hakutegemea kuonana na Merina eneo hilo .

INAENDELEA

SEHEMU YA 75
THE FIRST MISSION (MISHENI YA KWANZA)

Patrick alimwangalia merina ,na damiani alimwangalia Patrick huku mrembo Merina akiwa ameyapeleka macho yake kwa Steohanoo lamberk , wakati hayo yakiendelea jasusi mwenye roho yake mbaya Miss K au Suzzane , alikuwa na yeye ndani ya hayo maeneo , haikujulikna alifka muda gani ndani ya eneo hilo la kupaki magari ndani ya ikulu , sehemu ambayo magari pekee yanayo ingia hapo ndipo yanappaki , kwani kulikuwa na ‘parking’ nyingi ndani ya ikulu , kuna sehemu ambayo ilikuwa ikitumika kuegesha magari kwa muda mfupi . lakini kuna maegesho ambayo yalikuwa yakitumika kuegesha magari kwa muda mrefu.
Hivyo eneo walilokuwepo watu hawa , ni eneo linalohusika kuegesha magari kwa muda mfupi ( temporary parking for the guest)..
Mtu wa kwanza kutoka ndani ya eneo hilo alikuwa ni Merina , wakati Merina anatoka hapo ndipo Patrick na yeye alimsogelea Merina .
“Vipi Merina ,uko poa?”Aliuliza Patrick .
“ Niko poa” Lilikuwa ni jibu moja tu kutoka kwa Merina na aliongeza mwendo , hakutaka kuongea kabisa na Patrick , ni kama mtu aliekuwa akimuepuka .
“ Karibu sana Miss Merina “ aliongea katibu muhtasi wa ikulu akimkaribisha Merina na kisha akamkaribisha tena Patrick .
“ Karibu sana stephano lamberk “ Aliongea mwanadada Suzzane huku akinyoosha mkono kumpa Stephano lamberk , na bwana huyu aliuangalia ule mkono na kisha akaachia tabasamu na kisha alimpa mkono pia suzzane , lakini wakati wanapeana mkono Suzzane alifanya tukio ambalo lilimfanya Damiani ashituke.
Alimsogelea Damiani Kwa kujivuta kwake Kama mtu anaetaka kumkumbatia, lakini haikuwa hivyo kwani alimsogelea sikioni.
“Karibu sana Damiani rabani “ Aliongea suzzane , na kwa Damiani wala hakushituka , alitabasamu kisha akamwangalia usoni Suzzane kwa kujitoa kwake na kisha akatabasamu , huku akiangalia paja la Suzzane “
“Asante sana Suzzane “ aliongea Damiani na kisha alimpita Suzzane aliekuwa amesimama huku akionekana kukasirishwa na kitendo cha Damiani kutabasamu , kwani alichokuwa akitaka yeye ni kumuona Damiani kupatwa na mshituko , lakini hakuwa hivyo bali mwanaume alitabasamu na kupita , hapo moja kwa moja Suzzane aliona kabisa Adui yake kashamzidi kete , kwani tabasamu lile lilimaanisha kwamba Damiania amekubali kudhihirika mbele yake na kama ni hivyo basi hakuja hapo ikulu kizembe , yaani atakuwa kajipanga na hilo lilimfanya Suzzane moja kwa moja apatwe na mashaka , n ahata jambo lake alillokuwa amelipania kulifanya kughairisha .
Sabi ndio aliekuwa ameandaa mtiririko mzima wa wageni wa raisi kuonana nae mmoja mmoja kama mheshimiwa alivyokuwa akhitaji , kuonana alikuwa ni Merina.
“ Karibu sana Merina “ aliongea mheshimiwa Henry kwa tabasamu kumpa mkono Merina na kisha alimuonesha nafasi ya kukaa , na wakati huo huo aliingia Patrick na baba yake alimsabahi na kisha alikaa kwenye sofa upande aliokuwa amekaa mrembo Merina .
“Merina na Patrick nimewaita hapa kuongea kama familia , mpaka sasa natambua mahusiano yenu na ni muda mrefu sasa tokea muanzishe mahusiano hivyo nataka kuwaona ninyi wawili mkiona , mnaweza kushangaa kwanini nimewaita tofauti tofauti , sababu ni kwamba nimewaita hapa kama wafanya biashara , na ninajua kila mtu anaendesha biashara zake, hivyo nataka mniambie ni lini mnaoana “ Aliongea mheshimiwa raisi na kumfanya Patrick amwangalie Merina na Merina amwangaliae Patrick …….
Nje nako Janeth na Zakayo ndio walikuwa wanafika.
“ Karibu sana Stephano “ aliongea mheshimiwa na kisha Stephano alikaa kwenye masofa , na huku mheshimiwa na yeye akikaa .
“ Nashukuru sana mheshimiwa “.Aliongea huku akipeana mkono wakati huo na Patrick .
“Nikupe hongera bwana Stephano lamberk kwa kuendelea kufanya vizuri kibishara ndani ya Tanzania , hii ni mara yetu ya pili kuoanana “.
“ Ni kweli muheshimiwa na mimi nashukuru sana kuonana na wewe kwa mara hiii ya pili , ni heshima sana kwangu “.
“Nadhani ushawawi kuonana na Patrick “.
“ Ndio , ni moja ya wanahisa katika kampuni yangu , nilikutana nae kwa muda mfupi sana”.
“Unatarajia lini kufungua kampuni yako Rasmi “.
“ Natarajia kuifungua mapema kabla ya mwaka kuisha , lakini lengo kuu la kampuni tutafanya siku ambayo tutazindua bidhaa yetu ya kwanza “
“ Hongera sana , wewe ni kijana mdogo lakni unaonekana kuwa na ndoto kubwa za kuifkisha kampuni yako mbali , naweza kusema kwamba umerithi mbinu zote za kibiahsra kutoka kwa baba yako “ aliongea bwana Henry huku akitabasamu kama mtu.
“ Nashukuru sana mheshimiwa kwa kuutambua uwezo wangu , na mimi naahidi kufanya kazi kwa bidi ili niweze kulinufaisha taifa hili , hususani katika maswala ya ajira “.
“Ni vyema sana kuskia hivyo , ila kwa siku ya leo nimekuitia mahali hapa kwa jambo moja , nadhani unafahamu na sisi pia tunamiliki kampuni ya maswala ya kiteknolojia , hivyo tumeona jambo hili litakuwa jema kama tutashirikiana kwa ukaribu Zaidi “.
“ Unamaanisha partnership ?”
“ Nadhani mpaka hapo umenielewa , na nataka jambo hilo uongee na Ptrick kwani yeye ndio muhudika mkuu na msimamizi wa kampuni zangu zote “.
“ Mheshmiwa hakuna shaka juu ya jambo hilo tunaweza kukaa chini na kuongea , lakini pia swala hli pia siwezi kulitolea maaamuzi peke yangu kwani kuna wana hisa pia , tukifanya makubaliano ya pamoja tunaweza kuangalia ni kwa namna gani tunaweza kuunganisha nguvu “ Aliongea Stephano na kumfanya mheshimiwa atabasamu , kisha walipeana mikono .
Baada ya mazungumzo ya Stephano kuisha , raisi alizungumza na Janeth bendera , na hakuwa na kubwa Zaidi ya kumpongeza kwa kuwa proffesa wa kwanza mwenye umri mdogo ndani ya taifa la Tanzania .
Baada ya madakika kadhaa mazungumzo yao yaliisha , na ikawa ni zamu ya Zakayo kuonana na mheshimiwa .
“Kuna kazi nataka unifanyie ?”
“kazi gani mheshmiwa ?”
“Kuna jambo ambalo linafanyika pasipo mimi ya kujua na baadhi ya wastaafu waliokuwa ndani ya serikali ya raisi bendera .na moja ya watu hao ni Mstaafu matinde “ Aliongea mheshimiwa na kumfanya Zakayo kidogo ashituke , lakini hakutaka kulidhirisha hilo mbele ya raisi .
“Kazi yako ni kuhakikisha unajua ni kipi kinaendelea , ni mara kwa mara nilikuwa nikipokea ripoti wanafanya vikao vya siri , hivyo hio ndio itakuwa kazi yako , kuhusu malipo kwanzia hapa ninap zungumza utakuwa unapata mshahara kama wafanyakazi wengine ndani ya TISS”
“ Sawa muheshimiwa “.
Henry baada ya kumaliza mazungumzo yake na Zakayo alivuta droo ya mtoto wa meza na kisha alitoa picha , picha hio ilikuwa ikimuonesha Zakayo akiwa na Matinge mstaafu wa kitengo cha usalama wa Taifa , aliingalia kwa sekunde kadhaa na kisha aliirudisha huku akionekana kama ni mwenye kulidhishwa na jambo Fulani .
Wageni wote wa mheshimiwa Henry hawakuondoka, kwani mara baada ya kufanya mazungumzo walialikwa kwa ajili ya chakula cha mchana na familia nzima ya mheshimiwa Henry, jambo ambalo hakuna ambae alikataa.
Kulionekana kama kulikuwa na katafrija kwani kuna pia wageni wengi ambao walialikwa siku hio hapo ikulu , moja ya wageni hao alikuwepo bwana Sam , Kimbona , wastaafu wote waliokuwa ndani ya serikali ya mheshimiwa bendera , akiwemo mstaafu Matinde .
Basi wote walijumuika , huku meza aliokaa Stephano lamberk , alikuwepon Merina , Patrick , Janeth pamoja na Damiani wakati wote huo hafla hio unaendelea ,, hafla mabyo hata kwa Patrick hakuwa akijua ilikuwa inahusu nini , basi waliendelea kunywa na kula lakini wakat wpte huo Merina macho yake yalikuwa kwa Sephano lamberk , jambo ambalo kwa Patrick aliliona , hakuelewa kwanini Merina alikuwa akimwangalia sana Stephano , lakini kuna kitu alikiona kwenye macho ya Merina , kitu ambacho alijiambia lazima akifanyie kazi .
Baada ya madakika kadhaa kupita ndipo mheshimiwa Henry na mke wake wema walismama mbele ya Wageni na hio ni mara baada ya chakula na kutoa shukrani , lakini jambo kubwa lililokuwa likihusu tafrija hio ni pongezi kwa mtoto wake wa kike kumaliza masomo yake ya ngazi ya juu , katika kitivyo cha sheria ‘ Harvard law school ‘ mwanadada huyu aliekuwa akifahamika kwa jina la jane , alikuwa mrembo haswa kama mama yake , lakini licha ya pongezi hizo mheshimiwa aliendelea ..
“Licha ya mwanangu kumaliza salama masomo yake kwa ufaulu mkubwa , lakini pia siku ya leo nataka nimpongeze kwa kupata mchumba , kwangu ni jambo la furaha sana lakini pia uchumba huu ni fursa kwa watanzania kwani mchumba mwenyewe ni mtoto wa Mahmood seid kutoka Dubai kijana wake anaifahamika kwa jina la kareem Mahmood seid .” Aliongea mheshimiwa kwa hali ya furaha mnoo , huku familia nzima ikionekana kufurahia uchumba huo na hata waliokuwepo kwenye tafrija hio walifurahia , na hio yote ni kutokana na wengi kumjua bwana huyu anaefahamika kwa jina la Mahmood seidi , alikuwa ni tajiri mkubwa ndani ya Dubai lakini pia duniani akiwa tajiri namba ishirini akiwa na utajiri wa dollar bilioni 46 .
Watu walimpongeza Zaidi jane kwa kuwa na bahati ya kuolewa na mtoto wa kwanza wa tajiri Mahmood , lakini hayo yakiwa yanaendelea kwa upande wa Damiani mambo yalikuwa ni tofauti kabisa .
Jina la Mahmood ni kama lilikuwa likijirudia rudia kwenye ngoma za masikio yake , moja kwa moja akili yake ilimrejesha katika misheni aliopewa na Bruno misheni ambayo hakuwa akijua ilikuwa inahusu nini , ila alichokuwa akijua ni kwamba ndio misheni ambayo ingempelekea kulipiza kisasi kifo cha mama yake .
Licha ya yote hayo hakujipa uhakika moja kwa moja kama mtu ambae anapaswa kumuua ndio huyo anaetajwa kwa jina la Mahmood , na hilo alipanga kwenda kulifatilia , kwani tokea aangalie majna hayo hakuwahi kufanyia uchunguzi wa jina hata moja kwa yale ambayo hakuwa akiyajua .
Ukweli ni kwamba Damiani alikuwa akimjua vyema Zaidi bwana huyu aliokuwa akijulikana kwa jina la Mahmood , na alimjuua kama mfanya biashara kama wengine walivyokuwa wakimjua , lakini akili yake hapo ndio ilianza kufunguka na kuanza kufikiria kuhusu misheni yake , aliomba jina lile lisiwe linamhusu tajiri huyo .
Licha ya kwamba Jane alichumbiwa , lakini waliomchumbia hawakuwepo nchini , na walikuwa wakitarajiwa kuingia nchini wakati wowote kwa tarehe watakayo ipanga kwa hio siku hio ilikuwa ni utambulisho wa uchumba huo ambao uliambatana na barua .
Partick alijikuta akimfata mdogo wake baada ya utambulisho na kisha kumpa hongera , lakini wakati huo alikuwa ameongozana na Merina .
“Broo ..” aliita Jane na kisha walikumbatiana
“kwanini tusifunge ndoa siku moja , kwani mchumba upo nae na ni mrembo na pia unampenda ?” aliongea Jane
“Ndio kwanza nilitoka kuongea na baba juu ya swala hilo , ila mimi na Merina tutalifikiria hilo , ila ni kupongeze sana Jane kwa kutuletea chuma “ Aliongea Patrick na kumfanya Jane atabasamu .
“ Usichezee Fursa sasa broo .. ushindwe wewe tu “ aliongea kiutani na wote wakacheka .
“ Hongera sana “
“ Asante sana shem wangu “.Alijibu oingezi hio kutoka kwa Merina .
Basi baada ya muda sherehe iliisha na kila mtu alitawanyika , baada ya kutka pale Stephano hakiuelekea moja kwa moja nyumbani kwake bali alienda kwenye Nyumba ya Bruno kwa ajili kuingia kwenye LEGACY ROOM ili kujihakikishia kama kweli mtu ambae anatakiwa kumuua katika misheni yake ya kwanza alikuwa ndio huyo Tajiri mkubwa duniani .
“Welcome back Mister damiani in Legacy room”(karibu sana bwana damiani kwenye chumba cha legacy “
“NARA nataka kumjua Mahmood seid kwenye misheni yangu ya kwanza ni nani?”
“Mahmood Seid is an Emirati billionare, a businessman, the founder of MR Group, an Emirati real estate and retail conglomerate with projects in Asia and Africa, His networth is estimated to be 46B USD ... (Mahmood seid ni tajiri na mfanya biashara kutoka Emirate, Mwenye utajiri wa dola bilioni 46 za kimarekani)
“Kwa hio huyu ndio misheni yangu ya kwanza kuifanya ?”
“Ndio mister Damiani, Una siku kumi na tano kukamilisha misheni hio, kuhusu namna ya kufanya mauaji hayo kila kitu kimepangiliwa “
“unamaanisha nini kuhusu kupangiliwa”
“Mpango wa kukamilisha misheni hio ushapangwa na mtu pekee wa kuukamilisha ni wewe , isku ya jumatano asubuhi utapokea mgeni ambae atakupa ramani nzima ya misheni hio “Aliongea Nara na kumfanya Damiani achanganikiwe Zaidi .
“Ni nani aliendaa mpango huo Nara “
“Bruno lamberk “.
“Anaandaaje misheni wakati amekufa “.
“ Hilo sitambui Mister Damiani “.
Damiani alijikuta akiondoka bila ya kusema jambo lolote , huku akiwa na mawazo mengi , hakuweza kumtafisiri Bruno , swali moja kwake tu ni kwamba anaandaaje mauaji huku akiwa amekufa .
******
“ Patrick nahitaji tuonane tuongee “ ilikuwa nisauti ya merina kutoka kwenye simu , wakati huo anapokea simu Patrick alikuwa anaingia ndani ya nyumba anayoishi suzzane na wakati anaongea na simu alikuwa kwenye gari akiwa sehemu ya maegesho .
“Nimefurahi unataka kuonana na mimi , unaonaje kesho “
“ Sawa , tutaonana peacock hoteli “ Aliongea Merina .
“Okey jioni njema ” Alijibu Patrick , na muda huo ilikuwa ni kama saa moja kasoro za jioni , baada ya kukata simu moja kwa moja alitembea na kuingia ndani ya nyumba hio baada ya kukaribishwa na mlinzi .
“Karibu Patrick “ Aliongea suzzane kwa bashasha akimakribisha .
“Asante Suzzane “
Basi baada ya kukaribishana Suzzane alimkaribisha Mvinyo na kisha walianza kuongea .
“Enhe , nlishangaa leo ulivyonipigia simu ukitaka kuonana na mimi “.
“Ni kweli : Aliongea na kisha akanywa funda moja ya wine kisha akaiweka chini huku akikunja nne na kuendelea: “ Nimekuja hapa kuna jambo moja nataka unisaidie .”
“Jambo gani “
“ Ni kuhusu Damiani rabani “
“ Damiani rabani!”Alionyesha ishara ya mshangao
“Ndio , najua wewe ni moja ya wanausalama na unaweza kunisaidia katika hili , nataka kumjua Damiani rabani ni nani na ana uhusiano gani na Stephano lamberk “.
“ kabla hatujaendelea , nataka kujua dhamira yako kwanza “
“Merina anampenda Damiani rabani “
“Ila yeye hakupendi si ndio , na unadhani akishatoweka Merina hatokuwa na jinsi Zaidi ya kukupenda wewe “
“Asante kwa kunielewa “
“Mimi namjua Damiani “.Aliongea Suzzane kwa kujiamini kabisa .
“Ni nani ?”
“Stephano Lamberk “
“Unamaanisha nini ?”
“ Namaanisha , Stephano lamberk ndio Damiani mwenyewe unayemtafuta na kama huamini hilo unaweza ukamuuliza Merina , na yeye analitambua hilo “ aliongea Suzzane huku akinyanyuka .
“Are you sure Suzzane ?”.
“Unaweza kwenda kujihakikishia mbele ya Merina “
Patrick hakutaki kibaki alitoka na moja kwa moja alielekea nyumbani kwake , huku akiwaza siku ya kesho ndio siku ambayo anakwenda kuonana na Merina , na ndio sku ata
kayo jihakikishia Zaidi , lakini wakati akiwa anawaza hayo , alianza kukumbuka matukio yote yaliotokea ikulu , jinsi Merina alivyokuwa akimwangalia Stephano .., akliona jambo lililozungumzwa na suzzane lina ukweli wake .
ITAENDELEA JUMATANO STAY TUNED

HAYA TUMA HIO 2000 NIKUTUMIE MWENDELEZO MPAKA MWISHO NAMBA NI 0687151346 JINA ISSAI SINGANO HAKA KA OFA KANAISHA SAA NNE YA USIKU UKILIPA NI CHEKI WATSAPP
Mbona namba naambiwa siyo sahihi
 
Bado masaa machache kufika mkuu
Mkuu Kwanza nikupongeze kwa uandishi, maana kuandika tu Ni kipaji tosha kabisa

Pili, nikupongeze Sana kwa mchoro wa hadithi, umejitahidi kuweka madhari halisi hapa nakupa 8/10

Tatu hadithi yenyewe umetumia njia ya masimlizi, nafsi ya Kwanza umoja inadhani ulihitaji Sana kueleza ww binafsi kuliko wahusika, (Sina uhakika Kama umeelewa) na kwa nyakati fuln ukajikuta unamasimlizi marefuuu kiasi ambacho unaporudi kwenye hadithi yenyewe unachanganya, mfano kunawakati ulichanganya Kati ya suzani na zakayo Kama sikosei, na kunakipindi pia unachanganya na kumuita merina Ni mtoto wa mke wa raisi, na hii Ni kwa kuwa unasimlia zaidi.. kwenye simliz mpka Sasa nakupa 7/10

Kwenye washiriki asee umejitahidi story inawashiriki wengi Sana kunawakati sikulaum kabisa ila nakupongeza maana umejitahidi kutengeneza taswira halisi..

Japo jingine Ni wahusika kutokuvaa uhusika wao haswaaa au kumtegemea mtu 1 ndo wavae uhusika, ngoja nikupe mfn, damiani anafuatiliwa na karib watu wote kwenye hadithi hii ila akilala tu na wao wanaacha kumfuatilia as if kazi inakuwa imeisha, heb angalia gap la kutoka kisemvule mpka kesho yake mpka Damian anaenda sijui mbez kwenye ile nyumba yaan wapelezi woooote hakuna anaeshughulika nae , halafu kimbembe kikianza wooote wanaamka, na wakati nlitaraji kwa namna anavyowindwa asee Sina uhakika ila hyo nmeona weakness kwa wahusika nakupa 5/10

Jambo jingine Ni teknolojia na wanausalama wenyewe asee broo tupo karne 21 hii hadidhi iweke kuwa ya hii karne, madhari yake iko very low, yaana kwa jinsi teknolojia ilivyo humatafuti mtu kwa kumfuatilia unamtafuta mtu kwa gps, yaan hyo nguvu ilikuwepo kipindi Cha Willy gamba huko, somo hum ndani kunahadithi za karn 21 uone wanavyotia teknolojia, kwa kwel hapa pamoja na yote nakupa 4/10..

Ila kilichokizuri hadithi inacode nyingi Sana ambazo ukiwa makini utajua kuwa umeficha mambo mengi Sana kwenye maelezo yako ambayo kiuhalisia yanaonekana ila kiutendaji kunajumbe mhim mno kwangu nakupa kongole9/10..

Mkuu mengine ntasema nikimaliza hadithi, kwa ujumla mpka hapa hadithi yako nmeipa 6/10, bigup broo..
 
Mkuu Kwanza nikupongeze kwa uandishi, maana kuandika tu Ni kipaji tosha kabisa

Pili, nikupongeze Sana kwa mchoro wa hadithi, umejitahidi kuweka madhari halisi hapa nakupa 8/10

Tatu hadithi yenyewe umetumia njia ya masimlizi, nafsi ya Kwanza umoja inadhani ulihitaji Sana kueleza ww binafsi kuliko wahusika, (Sina uhakika Kama umeelewa) na kwa nyakati fuln ukajikuta unamasimlizi marefuuu kiasi ambacho unaporudi kwenye hadithi yenyewe unachanganya, mfano kunawakati ulichanganya Kati ya suzani na zakayo Kama sikosei, na kunakipindi pia unachanganya na kumuita merina Ni mtoto wa mke wa raisi, na hii Ni kwa kuwa unasimlia zaidi.. kwenye simliz mpka Sasa nakupa 7/10

Kwenye washiriki asee umejitahidi story inawashiriki wengi Sana kunawakati sikulaum kabisa ila nakupongeza maana umejitahidi kutengeneza taswira halisi..

Japo jingine Ni wahusika kutokuvaa uhusika wao haswaaa au kumtegemea mtu 1 ndo wavae uhusika, ngoja nikupe mfn, damiani anafuatiliwa na karib watu wote kwenye hadithi hii ila akilala tu na wao wanaacha kumfuatilia as if kazi inakuwa imeisha, heb angalia gap la kutoka kisemvule mpka kesho yake mpka Damian anaenda sijui mbez kwenye ile nyumba yaan wapelezi woooote hakuna anaeshughulika nae , halafu kimbembe kikianza wooote wanaamka, na wakati nlitaraji kwa namna anavyowindwa asee Sina uhakika ila hyo nmeona weakness kwa wahusika nakupa 5/10

Jambo jingine Ni teknolojia na wanausalama wenyewe asee broo tupo karne 21 hii hadidhi iweke kuwa ya hii karne, madhari yake iko very low, yaana kwa jinsi teknolojia ilivyo humatafuti mtu kwa kumfuatilia unamtafuta mtu kwa gps, yaan hyo nguvu ilikuwepo kipindi Cha Willy gamba huko, somo hum ndani kunahadithi za karn 21 uone wanavyotia teknolojia, kwa kwel hapa pamoja na yote nakupa 4/10..

Ila kilichokizuri hadithi inacode nyingi Sana ambazo ukiwa makini utajua kuwa umeficha mambo mengi Sana kwenye maelezo yako ambayo kiuhalisia yanaonekana ila kiutendaji kunajumbe mhim mno kwangu nakupa kongole9/10..

Mkuu mengine ntasema nikimaliza hadithi, kwa ujumla mpka hapa hadithi yako nmeipa 6/10, bigup broo..
Shukrani sana kaka .. kwa ushauri wako .. Very nice nitalifanyia kazi
 
SEHEMU YA 76

SINGANOJR
DEAL MARRIAGE(NDOA YA DILI )
Ilikuwa ni muda wa saa mbili za usiku hivi Damiani akiwa yupo ndani ya nyumba yake maeneo nya Makongo juu , siku hio alikuwa yupo na Janeth wamekaa wakiangalia runinga , na kwa jinsi walivyokuwa wakionekana utadhania walikuwa wapenzi ,, basi wakati muvi imekolea ndipo simu ya Damiani ilipata uhai na aliichukua na kuiweka sikioni huku akiwaza anaempigia wakati huo wa usiku ni nani , kwani haikuwa kawaida kupigiwa nyakati za usiku tena na namba ngeni .
“Sabi mboneche , Stephano lamberk , Janeth bendera , Wema sufiani mmekuwa target ya U-97 na mpaka sasa watu wanaotakiwa kukamilisha vifo vyenu wapo Nchini kuweni makini .“ .
“Wewe ni nani ?”
“ Tiii.. tii “ Simu ilikatwa pale pale na kumfanya Damiani azidi kushangaa ,lakini sauti alioiskia ni sauti aliokuwa akiikumbuka vyema , sauti hii ni sauti aliosikia alipopiga simu kwa namba alizokuwa amepewa na Bruno , na mtu huyo ndio huyo aliekuwa akimpa maelekezo .
“ Kuna nini ?” Aliuliza janeth .
“U-97”
“Wamefanya nini ?”
“ Unawajua ?”
“Ndio nishawahi kusikia taarifa zao kutoka kwa baba , ila bado sijawajua vizuri , lakini ninacho jua mpango wa MZALENDO ni kuitoa huu umoja hapa nchini”
“Baba yako alikuambia nini kuhusu huu umoja ?”
“ Hakuniamba maneno mengi , ila alisema niwe makini , ndio hapo nilipo anza kufatilia umoja huu na niligundua baadhi ya mambo kabla hata ya kuja hapa Tanzania .
“Mama yako ,, mimi , wewe na Sabi ndio targeti yao kwa sasa na wau walioandaliwa kwa ajili ya kutupoteza duniani washafika Tanzania , ndio ujumbe niliopewa sasa “
“Hata mama yangu ?”
“ Ndio , inabidi tumtahadharishe juu ya hili “
“ Nitampigia simu “
“ Hapana mpigie Sabi simu atapeleka ujumbe “ Aliongea Damiani na hapo hapo mawasiliano yalifanyika kwa Sabi .
******
“ Vipi Sam “
“ Safi , yaan leo nina furaha tunywe tulewe “.
“Furaha gani tena ?”
“ Vijana washaingia nchini “
“ Vijana gani ?”
“ Boko haramu “
“ Unamaanisha kwa ajili ya kukamilisha lile jambo ?”
“Ndio “
“ Hapo safi , inabidi swala hili lifanikiwe mapema “
“ litafanikiwa “
“ Unazungumziaje mtoto wa raisi kuolewa na mtoto wa tajiri Mahmood ?”.
“Ni fursa kwetu”
“Kivipi ?”
“Ndio nilivyoambiwa na wakuu kwamba ni fursa kwa Umoja wetu “
“ Unamaanisha ni fursa dhidi ya Umoja wetu “
“ Ndio nilivyoambiwa “ aliongea Sam na kumfanya Kimbona ashangae kwani yeye aliona jambo hilo lingempa raisi nguvu , lakini ilikuwa nje ya mategemeo yake .
Na hio ni baada ya kutoka ikulu na kwenda kupata bia , na mazungumzo hayo yalikuwa yakifanyika ndani ya Casino la las vegas Posta karibu na hospitali ya Aghakhani.
“ vipi marie , hajaonekana bado ?”
“Vijana wanakisia huenda yupo mateka ndani ya lile jumba kule kibaha “
“ Unamaanisha lile jumba Ambalo damiani alionekana akiingia “
“ Ndio na nina uhakika huo , kwani Marie alipotea kwenye harakati hizo , japo jambo hii linanifikirisha yule ni jasusi wa CIA kukamatwa kizembe ni kosa kubwa “
“ una mpango gani sasa ?”
“ Wa kumtoa pale , kuna kitu kinaendelea pale , na hili swala nataka nimshirikishe mheshmiwa “
“unamaanisha mheshimiwa raisi ?”
“ Ndio , Hisia zangu zinaniambia hivyo “
“ lakini si vijana waliona magari ya Ikulu ndani ya hilo eneo , je kama muhusika mkuu ni Raisi mwenyewe”
“Lakini pia kumbuka moja ya watu ambao wapo kwenye Death notice ni Madam wema na Damiani , mheshimiwa yeye anamtafuta Damiani kwa hali na mali Inawezekanaje akawa anahusika na magari yale yalionekana mahali pale “
“ hapo umeongea , huenda yote yale ni mipango ya Wema , na kwa maelezo hayo nina uhakika kuna jambo kubwa linaendelea hapo , lakini mimi naona jambo hili tusilipeleke moja kwa moja kwa Raisi , kwanini tusimshirikishe Suzzane kwani ndio mshirika wake mkuu , na kumbuka pia yeye ndio anahusika kumfatilia Damiani “
“ hapo kweli Inabidi nionane nae “.Aliongea kimbona
Kulivyokucha tu kimbona hakutaka kuchelewesha mambo alimtafuta suzzane , na suzzane alimwambia kimbona kwamba anakuja kwenye ofisi yake , haikuchukua muda mrefu suzzane alifika .
“Ndio Kimbona nadhani una jambo la muhimu la kuniambia “
“ Ndio Suzzane “.
“Kuna mtu nilimpa kazi kwa ajili ya kumfatilia Damiani , lakini mtu huyo amepotea mpaka sasa haonekani “
“ Ni nani huyo “.
Kimbona hakuongea mengi alimpa faili linalomuhusu marie na kisha Suzzane alianza kulisoma na aliishia kutoa macho , kwani hakujua kuwa Kimbona anaweza kukod jasusi wa CIA .
“kwa hio unataka nikusaidiaje ?”
“Nataka ukamtoe sehemu ambayo naamini anashikiliwa “.
“Ni sehemu gani ?”
“Kibaha kwa mathiasi , kuna jengo ambalo Damiani alionekana akiingia pamoja na Madam wema “ aliongea kimbona na kwa suzzane alionekana hakushituka kabisa .
“Najua unazungumzia kambi N “
“ unaifahamu ?”
“ Ndio naifahamu vyema , ni sehemu yenye ulinzi mkubwa sana , na ipo chini ya jeshi “
“kama ipo chini ya jeshi unadhani kwanini mke wa raisi akaingia ile sehemu , na vipi kuhusu damiani ?”
“hayo yote nayafanyia uchunguzi ,”
“ mheshimiwa anajua juu ya hili ?”
“ bado sijamueleza chochote , mpaka nitakapo kamilisha uchunguzi wangu” .
“hakikisha uchunguzi wako ukikamilika unanipa taarifa na pia nataka umtoe Marie ndani ya eneo hilo “
“hayo ni mambo ya kisualama wa Nchi , nadhani nitakalo kusaidia ni kumtoa huyu Marie , lakini jambo hili lazima mheshimiwa alijue “.
“hakuna shida suzzane , lakini kumbuka unayoyafanya yote sio kwa ajili ya mheshimiwa tu bali kwa ajili ya U-97 “.
Suzzane alijikuta akipandwa na hasira ila hakutaka kulionyesha hilo mbele ya Kimbona Zaidi ya kunyanyuka na kuondoka.
*****
Upande wa NLT siku hio damiani alifika kwenye kampuni yake kwa ajili ya kuendelea na majukumu kama kawaida , kwani walikuwa mbioni kutangaza bidhaa yao mpya ambayo ingeambatana na ufunguzi wa kampuni .
Wakati akiendelea na majukumu yaka ndipo alipo ingia secretary wake na kumuambia kuna mgeni anahitaji kuonana na yeye , na Damiani hakujifikiria sana aliruhusu mgeni huyo aingie , na hapo ndipo Damiani alipokutana na sura ambayo hakuwa akiijua vyema , sura hii haikuwa nyingine bali alikuwa ni mwana Matinde ,Mkurugenzi mstaafu wa TISS , Damiani alimkaribisha vyema na kisha walisalimiana na kujitambulisha .
“karibu sana mheshimiwa “
“ Asante , jambo lillilonileta hapa sio la kiofisi Zaidi bali ni swala binafsi “
“ hakuna shaka karibu sana na kusikiliza “
“Najua ndani ya kampuni unafahamika kwa jina la Stephano lamberk , lakini kihalisia wewe ni Damiani rabani “ aliongea mkuu huyu na kumfanya damiani ashangae kidogo kwani siku zote Damiani akiingia ndani ya kampuni yake kikazi , huwa anakuja kama Stephano , yaani akiwa amevalia FULL BODDY MASK .
“Huna haja ya kushangaa Damiani ,nimekuwa moja ya watu ambao nilikuwa nikikufatilia kwa muda mrefu sana tokea kifo cha mama yako “.
“kwanini ulikuwa ukinifatilia mheshimiwa “ Damiani alijibu baada ya kuvuta pumzi na kuzishusha .
“Nadhani unaweza ukajiuliza nimefahamu vipi siri yako ya kuvaa ngozi ya kizungu , lakini mtu ambae ananifanyia kazi ya kukufatiia ni Zakayo “ aliongea na hapo Damiani alijikuta akitaka kutoa tusi , ashajua jasusi mpenda pesa ashauza taarifa zake .
“Endelea mheshimiwa”.
“Nataka unidokeze juu ya nyaraka ulizoachiwa na Bruno , kwanini mheshimiwa raisi anazitafuta sana”
“kwanini nikwambie juu ya hilo mheshimiwa ?”
“Kwasababu mimi ni moja ya wanausaama walioaminiwa na mheshimiwa Bendera , na nafanya yote haya kwa ajili ya usalama wa Nchi hii , na nayajua mengi ambayo pengine huyajui “.
“ mheshimiwa najua wewe ni mwanausalama na ni jambo la kawaida sana kwako wewe kuwazia usalama wa taifa , lakini pia hata mimi kama raia mwema ni kawaida kuwazia jambo la usalama wa nchi yangu , lakini bado sina sababu ya kukwambia nini bruno kaniachia”Matinde alijikuta akikaa kimya kwa muda kwani aliona kabisa mtu anaeongea nae hamwamini mtu na hilo alilitegema .
“Kwa nafasi yako ni sahihi kutoamua kuniambia na nililifahamu hilo kabla ya kuja, lakini naamini kupitia hili utaniamini “Aliongea matinde na kisha alitoa bahasha flani ndogo kabisa za kuhifadhia barua na kisha alimkabidhii.
Ilikuwa ni barua ilitoka kwa raisi Bendera kwenda kwa Matinde , barua hio iilikuwa ikimpa maelekezo ya Matinde kumtafuta Damiani .
Damiani alijikuta akianza kukumbuka baadhi ya mambo , alikumbuka mambo mengi hususani yela alioambiwa kuwa mheshimiwa Bendera alikuwa akimjua vyema na kumfatilia kwa ukaribu , barua hio ilikuwa na sahihi kabisa ya mheshimiwa Bendera marehemu .
“Nadhani mpaka hapo unaweza kuniamini na unaweza ukajua ni sababu gani nilikuwa nikikufatilia kwa muda mrefu , ni maagizo niliopewa kama ulivyosoma katika hio barua “.
“Nimekuelewa muheshimiwa, lakini kwanini unataka kujua ni kipi bruno ameniachia , maana ni vitu ambavyo havihusani kabisa na mheshimiwa Bendera wala Henry”
“Mimi na wewe tuna adui mmoja Damiani “
“ Adui yupi “
“ U-97”
“Sina uadui na huo umoja mimi dhumuni langu kuu ni kulipiza kisasi kwa wale waliohusika na kifo cha mama yangu “
“ na watu hao ni nani kama sio U-97, na kama ni hao jua swala hilo hauwezi ukalifanya peke yako na ndio maana niko hapa , wote sisi ndio tuliongoza mapambano ya kuutoa umoja huu ndani ya nchi hii , lakini kwa sasa unarudi kwa kasi Zaidi hapa nchini jambo mbalo linaonyesha juhudi zetu tulizozifanya wakati wa uongozi wa bendera zilikuwa bure “
“kwa hio mheshimiwa unaamini kwa kukuonesha nyaraka hizo unaweza ukautokomeza umoja huu?”
“ Dhumuni langu ni kutaka kujua ni kwanini mheshimiwa raisi anataka nyaraka hizo , fikiria mambo yote yaliotokea nyuma hadi kifo cha Danny , unafikiri ni kwanini ?”
“hilo hata mimi sijui kwasababu nyaraka hizo hazijamzungumzia kabisa “
“Lakini unajua kuwa mheshimiwa ni mwanachama wa U-97”.Damiani alishangaa .
“kuna Umuhimu bwana Damiani kuniambia nyaraka hizo zinahusu nini “
“Nyaraka hizo zinahusu juu ya malii za Bruno basi hakuna lingine linalomuhusu mheshimiwa Henry” aliongea Damiani , japo kamsilikilza sana bwana huyu ila hakuwa akimuamini moja kwa moja , tabia yake ya kutoamini watu ndio ili,mfanya kumshuku kila mtu aliekuwa akimsogelea .
“una uhakika ?”
“ Ndio “.
“Kama ni kweli naomba nikupe nasaha , najua unataka kulipiza kisasi llakini kumbuka sana watu ambao unapambana nao sio watu bali ni shirika hivyo swala hili huwezi kulifanya mwenyewe , ukihitaji msaada wowote kutoka kwangu nipigie na hii “ alimpa kadi na kisha aliaga na akaondoka .
******
“Patrick kwanini uliongea maneno yale mbele ya mheshimiwa ilihali unajua kabisa mimi na wewe sasa hivi hatuna mahusiano na hilo lipo wazi”
Aliongea merina kwa msisitzo kabisa huku akionekana amechukizwa na kitendo cha Patrick , huo ni wakati ambao Merina na Patrick kama walivyo ahidiana walikutana ndani ya peacock hotel .
“Sina nia mbaya juu ya hilo Merina , wewe ndio hutaki kunielewa ,kwanini unakuwa mgumu kunipa nafasi merina nakupenda lakini hutaki kuliona hilo “
“Patrick hilo tushaliongea sana tu na nishakueleza juu ya hisia zangu juu yako na siwezi kujilazimisha nipo hapa kwa jambo moja tu nataka umwambie mheshimiwa kuwa mahusiano yetu yashakwisha isha .
“Unaamini Stephano lamberk au Damiani anakupenda kama ninavyo kupenda mimi” .
Merina alijikuta akipatwa na mshangao hakujua kama na Patrick alikuwa akijua kuwa Stephano lamberk ndio Damiani .
“Unamaanisha nini ?”
“Huna haja ya kuwa hivyo Merina najua kila kitu kwamba Stephano ndio Damiani na kwa ninavyo ona kabisa Stephano hakupendi kama ninavyokupenda mimi “
“ una uhakika gani juu ya hilo Pat , na hata kama hanipendi hilo ni juu yangu , swala lililonileta hapa nataka umwambie mheshimiwa kwamba mahusiano yetu yameisha , ukishindwa nitafanya hivyo “.
“ siwezi kufanya hivyo merina , nishamhakikishia baba nitakuoa “
“na mimi siwezi kujilazimisha kuolewa na wewe”
“Huna jinsi kama unampenda Damiani inabidi uolewa na mimi “
“Unamaanisha nini?”
“Nadhani unajua ninacho maanisha Merina “
“Damiani anaishi kama Stephano lamberk unafikiri ni kwasabu gani , jibu ni kwamba yupo hatarini kuna watu wanamtafuta na ni wewe wa kumlinda kwasasa vinginevyo nitaweka ukweli wazi “
“ Unataka nini Patrick “ Aliongea Merina maana aliogopa sana Damiani kuingia kwenye matatizo zaid na zaidi
“Najua hunipendi Merina , ila nataka tufunge ndoa “
“Nini ?”
“Ndio , njia pekee ya damiani kuwa salama , kwani mpaka sasa najua maadui zake wote”
Merina alijikuta akivuta pumzi na kuzitoa kwa kasi na kumwangalia Patrick ,na alimuona Patrick kama mtu ambae anamaanisha kwa kile anachokiongea , hakujua ajibu nini maana alijiona kama yupo kwenye mtego , aliwaza mambo mengi kwa wakati mmoja , kwanzia Janeth kuwa na mahusiano na Damiani na mengine mengi kwanzia siku ambayo wamekutana mpaka kufikia wakati huo.
“Nimekubali , ila sharti langu ni moja ukikubaliana na swala hilo basi nitakubali kufunga ndoa na wewe “ Patrick meno yote nje
“ jambo gani ?”
“Nataka unihakikishe usalama wa damiani , siku damiani atakapo patwa na shida yoyote inayohatarisha maisha yake basi mimi na wewe basi”
“kwa hio unataka niwe mlinzi wa Damiani ?”
“ Ndio namaanisha hivyo , kama huwezi basi hakuna ndoa na swala hili linawezekana sana kwani wewe ni mtoto wa raisi , unaweza kumwambia baba yako aweke wanausalama watakao mlinda “
“ahahahah… Merina naona hunipendi kabisa , ila kwasababu sitaki kukukosa na mimi nina sharti , hatuishii kufunga ndoa tu , ila nataka unizalie na mtoto ama watoto “.
“Ndio jukumu la kuwa mke hilo”
“ Then deal , ndoa tutafunga siku moja na mdogo wangu “.
ITAENDELEA
SEHEMU YA 77.
I AM BACK ( NIMERUDI )
Zikiwa zimepita siku kadhaa , viongozi wawakilishi wa U-97 walikaa kikao cha kusaini karatasi ya mkataba ambao ulikuwa ukihusu makubaliano ya Tanzania kutoa binadamu kwa ajili ya majaribio zidi yampango Zero , kikao hichi kilikuwa kikifanyika ndani ya hoteli ya Hyatt regency maeneo ya posta na kama kawaida Sam ndie aliekuwa akiongoza kikao hichi .
Watu waliokuwepo ndani ya hiki kikao walikuwa ni wale wale wakiongozwa na raisi mstaafu Ndalu lakini mheshmiwa Henry hakuwepo , mpango huo wa majaribio ulisomwa kwa kila mwanachama lakini pia walitoa mafanikio ya mheshimiwa Raisi kutia sahihi yake katikampango huo .
Baada ya kila mtu kuelewa hakuna hata mmoja aliepinga kutoweka sahihi katka mpango huo , kwani licha ya kusaini lakini pia mpango huo uliambatana na dau kubwa la pesa kwa kila mwanachama .
Baada ya mpango huu kusaniwa ndani ya usiku huo wa kikao siku iliofata waziri wa pesa alitangaza Tanzania kupata msaada wa matirioni ya pesa kutoka IMF huku pesa hizo zikielekezwa katika maswala ya afya.
Moja ya watu walifurahi pesa hizo kuingia nchini alikuwa ni Sam , kwani alijua pesa hizo hazikukusudiwa kuingizwa kwenye maswala ya afya bali kukamilisha mpango Zero ., bwana huyu ambae tamaa ya pesa ilikuwa imemgubika hakutaka kabisa kuwaza juu ya mpango huo ulikuwa ukihusu nini haswa , alichokuwa akiwaza ni pesa tu na sio kwake tu na kwa washilika wake pia, hakuna alifikiria kwa jicho la tatu juu ya athari za mpango huo kwa watanzania kwa ujumla.
****
Upande mwingine siku ambayo kikao cha UMOJA NAMBA TISINI NA SABA kinafanyika upande mwingine ndani ya hoteli ya Tulip kulikuwa na kikao kilichokiuwa kikifanyika , na kikao hiki kilikuwa kikiongozwa na Bwana matinde na wafuasi wake ukimtoaMerna hakuwa ameitwa kwenye kikao hichi lakini pia hakuwa mwanachama rasmi kwani alikuwa akishiriki kama mfadhili wa kuchangia upelelezi wa kupatikana kwa Damiani na jambo hilo lilikuwa lishafanikiwa kwa asilimia mia moja.
.” vipi alikutafuta ?”
“ bado hajanitafuta , ila naamini atanitafuta “
“ ni vyema akikutafuta kwani damiani ndio njia ya sisi kumtoa Henry madarakani “
“ haina haja ya kuwa na shaka juu ya hilo , nadhani kwa namna moja ama nyingine Damiani anaweza asiwe na Waraka wa mheshimiwa Bendera”
“ kwanini unasema hivyo “
“ Kama mwanausalama naamini kuna mtu mwingine anaweza akawa amekabidhiwa waraka huu , na mtu ambaye waraka huu umemlenga lazima ni damiani “
“Ni kweli kabisa , lakini kijana anaonekana japo ya kufoji barua ile ,bado hajakuamini , unaonaje tukiweza kufanya jambo la maana Zaidi kwake ili aweze kutuamini ?”
“ Nimelifikiria hilo pia , ila kwasasa nimemuweka Nurya aendelea kufatilia nyendo zake “
“Kwanini Nurya sio Zakayo ?”
“ Zakayo sio Mzalendo , zakayo anachowaza ni pesa tu na ni rahisi sana kutusaliti kama mtu atamuwekea dau kubwa”
“kama ni hivyo hakuna shida , kama Nurya kazi anaiweza basi swala hilo hatuna pingamizi nalo , lakini inabdi tuzungumzie ajenda ya pili kwa siku ya leo”
“Ni kweli , lazima tujue ni nani atashika madaraka baada ya Henry kung`olewa “.
“ mimi naamini mheshimiwa Matinde anatufaa “.aliongea kizito kabwela
“hapa hakuna anaefaa kushika madaraka kwa nchi hii “ aliongea Matinde na kuwafanya wote wamshangae
“ unamaanisha nini ?”
“mtu atakae shika madaraka inabidi sisi tumtengeneze na hawezi kutoka hapa ,kwani akitoka katika kundi letu ni ngumu kumkotrol”
“ umeongea vyema bwana Matnde “ aliongea mkuu wa majeshi Abdala .
“kwa hio mtu huyo atakuwa nani “.
“Askofu “Aliongea matinde
“ Unamaanisha askofu Jembe mbunge “. Aliuliza kizito .
“Inabidi tumuweke Jembe , na mipango yetu ya kuliongoza taifa hili kupitia yeye itafanikiwa , kwani Jembe anatamaa ya hela , na hata uchungaji wake sio wa halali kutoka kwa Mungu ni wa sadaka na nguvu za miujiza ni za kufoji.na ushahidi ninao”
“Naungana na Matinde juu ya hilo, tukifanikiwa kumuweka pale ikulu itakuwa rahisi kumuongoza kwa kila tunachotaka maana tutakuwa na udhaifu wake”
Kila mtu alikubaliana na Matinde juu ya kumuweka Askofu Jembe madarakani baada ya Henry kumuondosha .
Wakati hayo yanaendelea upande mwingine ndani ya hoteli hiyo bwana Pancho alikuwa na mashine yake ya kusikiliizia taarifa zake , na kila kitu kilichokuwa kikiendelea katika kikao hicho alisikia vyema , na swala hilo kwa namna Fulani lilimuongopesha sana , ila alitabasamu kwani alikuwa amekamilisha kazi aliokuwa amepewa na mheshimiwa .
******
Patrick alikuwa amedhamiria kweli kumuoa msichana Merina , haku wa na utani hata kidogo , alikubali dili la mwanamke huyo kwa asilimia mia moja na baada ya mazungumzo yake na Merina hakutaka kukawia Zaidi , kwani aliamini akizembea kuna uwezekano wa damiani kupatwa na shida na ndoa kufa hivyo baada ya kufikiria sana hatimae swala hilo ilibidia amshirikishe baba yake , na siku tatu mbele alikuwa ashaongea na baba yake , na mheshimiwa Alikubalia na kile mwanae alichokuwa akihitaji na hivyo aliamua kumtimizia kwa kuhakikisha kuwa Damiani anakuwa salama lakini jambo hilo lilazaa linguine kwa muheshimiwa , kwani ndio siku aliokuja kugundua kuwa Stephano lamberk ndie damiani jambo ambalo lilimshangaza sana/.
Baada ya siku kadhaa ya Patrick kuongea na baba yake juu ya swala hilo agent z aliitwa ikulu tena , na mheshimiwa raisi .
“kwanzia sasa kazi zako zote ulizo nazo zimesitishwa “
“unamaanisha nini mheshimiwa ?”
“ unayo kazi moja tu kwa sasa ni kuhakikisha Damiani anakuwa saama , lakini wakati huo ukinifanikishia jambo moja “
“ jambo gani ?”
“nataka kujua nayaraka Damiani alizoachiwa na Bruno zinahusiana na nini na ili kulifanikisha hilo nataka umfanye akuamini katika mipango yake yote”
“Nimekuelewa muheshimiwa “.
“ Swala hili ni juu yangu mimi na wewe lakin pia kwa usalama wa taifa , nahitaji lifanyike kwa siri sana , mafunzo yako ya kipelelezi yalifadhiliwa na taifa , hivyo ni jukumu lako kuhakikisha taifa lipo salama kama mwanausalama”
“ nimekuelewa muheshimiwa “
Baada tu ya zakayo kumaliza mazungumzo na mheshimiwa , Suzzane na yeye aliingia ndani ya ofisi hio ya mheshimiwa kwani na yeye alikuwa ameitwa.
“Suzzane nataka kwanzia sasa uachane na kumfatilia Damiani , ila kazi yako iwe ni kuhakikisha unawajua hawa wanaojiita WAZALENDO ni kina nani na wana dhumuni gani kwangu na kwa taifa hili “
“Mheshimiwa lakini Damiani ni Stephano na tayari tuna kila sababu ya kumkamata kwanini niachane na hilo “.
“Suzzane hio kazi kwa sasa achana nayo , na swala lolote linalohusiana na Damiani naomba linifikie kabla ya kufanya maamuzi “.
“Sawa mheshimiwa “
*****
DAR ES SALAAM –JNIA
Ndege ya shirika la Emirates ilitua ndani ya uwanja huu wa kimataifa , na baada ya madakika kadhaa ya kutua , mbele ya mlango katika jengo la terminal 3 alitoka kijana mmoja wa makamo mnene kidogo na mrefu saizi ya kati huku akiwa amevalia suti yake nyeusi kabisa ya bei ghali , huku mkononi akiwa na begi .
Kijana huyu alitembea mpaka upande wa Taksi na kisha alipokelewa na kuingia na kuondoka maeneo hayo ya uwanja wa ndege , dakika kadhaa mbele alikuwa ndani ya hoteli ya nyota tano ya Seerena , alifanya utaratibu wa kawaida na kisha alipatiwa chumba , na mara baada ya kuingia kwenye chumba hiko kikubwa cha hadhi hatimae alitoa simu yake ambayo ilionekana ilikuwa imezimwa kwa muda mrefu na kisha mara baada ya kuiwasha , alitafuta namba Fulani na kisha alipiga.
“I am back “
“ welcome back Karim in Tanzania “
“Asante sana madam “
“ kazi yako ni moja , ni kuhakikisha unafanya yale ulioagizwa na marehemu kabla ya kifo chake”
“ Nimejiandaa kwa ajili ya jilo madam wala usiwe na wasiwasi “
“ safi , nikutakie kazi njema “
“ asante madam “
“ hatimae nimerudi tena Tanzania kwa mara nyingine , Mheshimiwa bendera nipo tayari kukamilisha lile ulilolianzisha chini ya mpango wa MZALENDO “aliongea kijana huyu kwa sauti yake nzito .
ITAENDELEA IJUMAA JIONI
Bado Tunaendelea Wadau Bado Sana Hatujaufahamu Vyema Umoja Namba Tisini Na Saba
Nani Anao Waraka Wa Raisi Kabla Ya Kifo Chake Unahusiana Na Niini ?.
Mpango X Ni Mpango Gani , Mpango Zero Ni Mpango Gani ??
Endelea Kujiuliza Hayo Maswali Tukisubilia Mwendelezo
Tuma 1500 kwa namba 0687151346 jina ISSAI SINGANO nikutumie mwendelezo watsapp huo ni mchango tu kwa ajili ya vocha .
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom