Ujasusi - Umoja namba 97

SIMULZI YA KIJASUSI
UMOJA NAMBA TISINI NA SABA
KAULI YA MWISHO YA RAISI
MWANDISHI : ISSAI SINGANO
NAMBA : 0687151346

SEHEMU YA 12
Tulipoishia ni pale kijana damiani kutekwa na mtu asie fahamika
ENDELEA NAYO
Ilikuwa ni muda wa saa mbili asubuhi bwana kimbona akiagana na mke wake kwa ajili ya kuelekea ikulu , na hatimae alifanikiwa kupata nafasi ya kukutana na muheshimiwa , kutoka masaki mpaka ikulu hakukuwa na umbali mkubwa sana , dereva wake alitumia dakika ishirini kufika ikulu .
Alipita getini mara bada ya kukaguliwa na akaruhusiwa kisha akaongozwa na mwanadada mmoja mrembo alievalia suti nyeusi , ambae alikuwa ni sekretatary wa raisi .
“ karibu sana kimbona “ aliongea mheshimiwa henry huku wakikaa kwenye masofa .
“ mheshimiwa kwanza niseme nashukuru kwa kuitikia wito wangu wa kuonana na wewe “
“ ni kweli kabisa , hii ni mara ya pili tunaonana sasa , na nadhani tutazidi kuonana siku za usoni “
“ ni kweli muheshimiwa , nashukuru sana “
“enhe sasa twende kwenye swala lililokufanya uombe kuonana na mimi “
“mkuu kama siku ile kwenye kikao tulivyokubaliana juu ya mali za bwana Bruno , mpaka sasa imekuwa ngumu kupatikana kwa nyaraka zinazohusu mali zake , kwani bila nyaraka hizo hakuna uwezekano wa kuzitumia kwani zipo chini ya sheria mpaka sasa , mpaka pale mrithi halali atakapo tokea “
“ ndio nalielewa hilo kimbona “
“ sasa basi ni kwamba mpaka sasa juu ya upatikanaji wake umekwama hivyo nahitaji msaada wako “
“ msaada gani kwangu unaohitaji ??. “
“ kwa kifupi ni kwamba mpaka sasa nyaraka hizo tunaamini anazo danny “
“ unamaanisha danieli mtalemwa ?”.
“ ndio muheshimiwa , huyo ndio tunaamini anazo , kwani mtu wa kwanza tuliekuwa tukimshuku inaonekana kutojua juu ya nyaraka hizo “
“ kama anazo danieli mtalemwa itakuwa ngumu sana kuzipata , maana danieli kama amekabidhiwa na Bruno basi haitokuwa rahisi kumshawishi atupatie nyaraka hizo .“
“mheshimiwa sina mpango wa kukaa chini na danniel kumshawishi juu ya hili , nataka nizichukue kwa namna yoyote hata kama ni ya kimapigano “.
“ hahaha … kimbona , unafikiri hilo linawezekana , labda tupeleke jeshi , lakini hilo ni swala ambalo haliwezekani kabisa sheria haziruhusu “
“ naelewa muheshimiwa , kuna mtu anawezakuifanya kazi hio kwa umakini mkubwa na ikafanikiwa , hivyo nahitaji msaada wako “
“ mtu gani huyo unahitaji msaada kwangu ?”
“ carlos Cardoso “
“kimbona huyo mtu ndio nani , sina taarifa zake “
“ mheshimiwa huyo ni muuaji wa kimataifa , kwa taarifa nilizonazo ni kwamba carlos alikamatwa hapa nchini Tanzania katika moja ya kazi aliotumwa na U-97 ya kumuua Bruno , lakini kupitia TISS na jeshi walimkamata “
“ kimbona sina taarifa ya mtu huyo kushikiliwa hapa nchini “
“ inawezekana muheshimiwa huna hizo taarifa lakini mimi nina tarifa ya bwana huyo kushikiliwa hapa nchini na taarifa hizo lazima TISS wanazo ila ni top secret “
“ kama ni kweli unataka nikusaidije kuhusu hilo??. “
‘ nataka umtoe gerezani awe huru ili atufanyie kazi yetu kwani huyo ndio mtu pekee alieweza kumpiga danny mpaka akapoteza fahamu “.
“kimbona sina mamlaka ya kutoa wa fungwa wa aina hio gerezani “.
“mkuu humtoi gerezani kwa oda yako , ila kuna jambo nataka ulifanye nasisi tutamalizia kumuweka huru “
“ jambo gani ??“
“ kwanza kabisa inatakiwa tufahamu anashikilwa katika gereza lipi , baada ya hapo utoe agizo la mfungwa huyo kuhamishiwa gereza lingine na sisi tutamaliza kazi”. Mheshimiwa alifikiria kwa muda .
“ kimbona inabidi kwanza nijue taarifa kamili za huyu mtu , maana nimehudumu nchi hii kama makamu wa raisi lakini sina tarifa zake , nikishafanikisha hilo nitakupa jibu “ aliongea mheshimiwa kisha aliagana na kimbona .
Baada ya kimbona kuondoka , raisi hakutaka kabisa kulifumbia macho swala hilo , kwani kitendo cha kuwa mkuu wa nchi halafu jambo kama hilo halifahamu kwake ilimtia ukakasi kidogo .
Alitoa simu yake kisha aliongea na mkuu wa TISS bwana elly matinde .
“ nahitaji faili la carlos cardoso ofisini kwangu “ aliongea raisi . na kumfanya mkuu wa TISS anyamaze .
“ mkuu hilo swala ni classified na lipo chini ya umoja wa taifa mheshimiwa “. Henry alijikuta akianza kupandwa na hasira ila alijaribu kujizuia .
“ bwana matinde , mimi ndio mkuu wa nchi , hivyo nakupa masaa mawili nahitaji faili hilo hapa ofisini kwangu “ .alikata simu
“unanijibisha mimi , muda sio mwingi lazima nikutoe kwenye hio nafasi “ alijiongelesha mwenyewe , na alionekana alikereka sana. .
Masaa mawili baadae bwana matinde alifika ofisini hapo akiwa na faili husika , alisalimiana na mkuu wake .
Alichuku faili lile na kulisoma kwa umakini mkubwa kisha baada ya kumaliza alimwangalia matinde .
“nashukuru sana , unaweza kwenda nalo sasa “ aliongea henry na matinde aliaga na kaondoka .
Siku mbili mbele taarifa ya kubadilishwa kwa mkuu wa TISS na mkuu wa police IGP kizito kabwela zilitangazwa katika vyombo vya habari , kila mtu alishangazwa na uamuzi huo , huku kila mwananchi akiongea lake , lakini mamuzi yalikwisha fanyika na hakukuwa na wa kupinga, huku uapisho wa wakuu wapya ukifanyika siku ya pili yake .
Mkuu mpya wa TISS alikuwa ni bwana yusuph majid , huku mkuu wa polisi IGP akiwa ni aniseth kanyama wote waliapishwa ikulu .
Baada ya kuapishwa taarifa nyingine ya kuhamishwa kwa mkuu wa polisi kanda maalumu jiji la dar es salaam bwana hashimu juma alihamishiwa mkoni Arusha .
“nimekuita hapa ofisini , kuna mabadiliko kidogo yanatakiwa kufanyika katika magereza , wafungwa wafuaatao nataka wahamishiwe kutoka gereza la ukonga na kuwapeleka gereza la morogoro “ aliongea raisi akimpa maagizo bwana aniseth kanyama.”
“ ndio muheshimiwa nitafanya kama ulivyoagiza “
“hakikisha swala hilo linakuw siri “
“ sawa muheshimiwa “.
Baada ya agizo hilo raisi alitoa simu yake na kumpigia kimbona na kumwambia tayari wafungwa watapelekwa gereza la morogoro kesho kwa hio ahakikishe kazi inafanikiwa .
Baaada ya kimbona kupata simu hio kutoka kwa raisi alipanga timu yake na kuwapa ramani nzima ya magari yatakapo pitia na sehemu ya kufanya misheni yao .
“tukio litafanyikia mkese “ aliongea kimbona huku akiwaangalia vijana wake
“Kutoka dar mpaka mkese ni masaa mawili , mkifika hapa mkese mtapokea ujumbe wa gari alilopanda carlos , lakini mtasubiri mpaka mpate amri nyingine ya kuyasogelea magari , hakuna kufanya mauwaji ya aina yoyote , kazi ni moja tu kumchukua carlos Cardoso .” aliongea kimbona akiwa ofisini na vijana wake wa kazi .”
“ ndio muheshiiwa tumekuelewa “.
“ safi , kama mmenielewa mna swali lingine ?”
“ mkuu hatuna “
“ hahaha….. mnaona sasa msivyo makini , huyu carlos mnamjua ?”
“ hapana mkuu “
“ sasa hilo ndio swali , nataka muwe makini katika hili , picha yake hii hapa “ .
Vijana walitawanyika kwa ajili ya kusubiria siku ya kesho kwa ajili ya kuanza kazi , hatimae siku yenyewe iliwadia , kimbona alipokea muda wa wafungwa hao watakapotolewa gereza la ukonga .
“ watatolewa saa kumi na mbili kamili ukonga “” ilikuwa ni sauti kutokea kwenye simu na haikujulikanna alikuwa akiongea na nani .
Kiongozi aliekuwa akiongoza kundi la bwana kimbona alikuwa ni meja , ni bwana mmoja ambae alikuwa na mwili wa mazoezi , mwenye sura pana ambayo muda wote haikuwa na tabasamu , meja aliwapanga vikosi vyake ndani ya kijiji cha mkese kwa ajili ya kukamilisha misheni waliopewa na boss wao , hakutaka kabisa swala hilo lifeli na ndio maana alikuwa makini kabisa brabarani , saa moja na dakika kumi ndio muda waliokuwepo ndani ya eneo hilo wakiwa kwenye gari walilolipaki mita kadhaa kutoka kwenye makazi ya watu .
Ilipotimu muda wa saa moja na nusu alipokea ujumbe wa gari alilokuwa amepandishwa carlos Cardoso , aliwapa wenzie taarifa na kisha walijipanga kwa umakini mkubwa , kwanza kitu cha kwanza walichokifanya ni kusimamisha gari katikati ya barabara na kisha walijificha pembeni ya barabara .
Wakati wakiwa wamejificha meja , alipokea simu . namba ilikuwa mpya .
“ get ready “ ilisikika sauti ya mwanamke kwenye masikio yake .
Huku upande wa juu kabisa juu ya mti kulionekana kuna mtu aliekuwa amelalia tawi huku akiwa ameshikilia bunduki aina ya sniper riffle .
Saa mbili kamili magari matatu yalifika eneo la mikese mbele ilikuwa ni gari la polisi juma pia kulikuwa na gari la pollisi katikati lilikuwa na karandinga lililokuwa limebeba wafungwa , gari ilipita makazi ya watu na kusonga mbele na hapo ndipo polisi walipo ona gari iliokuwa imezuia barabara , kama ujuavyo polisi wa kitanzania kukereka , basi walishuka pasipo kuwa na umakini na kulisogelea gari lile aina ya noah .
Ndani ya kalandinga alionekana jamaa mmoja aliekuwa na midevu mingi , mwenye mwili uliokuwa umejazia , alikuwa ni bwana wa rangi nyeupe aina ya red Indians , jamaa mara baada ya kufika eneo lile , alijikuta akitabasamu , na ni kama mtu ambae alijua kinachoendelea , lakini kufumba na kufumbua bwana yule alionekana akidondoka chini palepale na kuwafanya wafungwa wengine wapige kelele na kushitua gari la polisi lililokuwepo nyuma.
Polisi wale walitoa bunduki zao aina ya SMG na kusogelea gari ile , lahaulah! Lilikuwa ni kosa kubwa , kwani polisi wale walidondoka mmoja baada ya mwingine , lakini cha kushangaza ni kwamba hakuna hata mmoja aliekuwa akivuja damu , polisi waliokuwa wametangulia mbele walikuwa wapo watatu na hawakujua nyuma wenziwe washaramba chuma , na kosa kubwa walilolifanya ni kutochukua tahadhari kwani ile wnalifikia gari walitokea watu watatu kwa nyuma yao na kuwazimisha pale pale .
“ mchukueni carlos , hakikisheni wafungwa wengine hawatoki “ ilikuwa ni sauti ya kimbona ikimpa maelekezo meja , aliwapa ishara wenzake na kuisogelea gari aliopandishwa carlos na kuchukua funguo kwa moja ya polisi .
“ wote geukieni nyuma , aliamrisha moja ya jamaa aliekuwa amejifunika uso na wafungwa wote waligeukia nyuma , wawili walibaki nje na mmoja aliingia ndani ya gari na kisha walimtoa carlos ambae muda huo alikuwa hajitambui , walimbeba mzobe mzobe na kutoka huku wale wawili wakifunga mlango .
“ ondokeni , watashituka baada ya dakika mbili “ ilisikika sauti ya mwanadada ikimpa maelekezo kwa njia ya simu .
Taarifa ilimfikia IGP mfungwa mmoja ametoroshwa na watu ambao hawajulikana ,huku polisi wakizimishwa na dawa ya usingizi wa muda mfupi kwa kutumia tranguilizer gun , IGP taarifa hio ilimchanganya kidogo , na hakutaka kubaki nayo mwenyewe , kwani alimjulisha raisi .
“ hakikish swala hilo linabaki siri , uchunguzi ufanyike siri kwa siri pasipo watu kujua , pili andika ripoti ya wafungwa hao kufikishwa salama katika gereza la morogoro “ yalikuwa maagizo kutoka kwa raisi na IGP alifanya kama alivyoambiwa .
Kimbona akiwa kwenye tabasamu zito mara baada ya kupokea simu kutoka kwa vijana wake , iliingia simu nyingine kutoka kwa raisi .
“habari mheshimiwa “
“ salama , sasa kimbona nimepata habari kwamba zoezi limefanikiwa , hongera sana , ila hakikisha baada ya nyaraka hizo kupatikana mtu wa kwanza kuzipata awe mimi “.
Kimbona alifikiria kwa muda na kisha alimkubalia mheshimiwa raisi .
Pembeni ya kiwanda cha katani cha kutengeneza magunia kilichopo morogoro , kulikuwa na jumba moja ambalo lilikuwa kama stoo , ndani ya jumba hilo ndio vijana wa kimbona ndio walimuingiza carlos huku wakiwa wamemfunga mikononi kwani walihofia bwana huyo akishituka anaweza akawapa kibano na akatoroka , baada ya kumuingiza walimuweka kwenye kiti na kumfunga tena na kisha meja alitoa simu na kumtaarifu boss wake kuwa wapo site huku wakimzindua na maji .
“muwekee simu sikioni “ aliongea kimbona na meja alifanya kama alivyo ambiwa .
“ carlos Cardoso “
“quem e` voce??( wewe ni nani ) aliongea kwa kireno .
“ My name is kimbona you probably don’t know me , I am the one rensponsible for getting you out of prison , I have a job I need you to do for me in exchange for your freedom ( naitwa kimbona kuna uwezekano hujawahi kunisikia popote , mimi ndio nimekutoa gerezani , kuna kazi nahitaji unifanyie , malipo ni kupata uhuru wako )
“falar estou ouvindo “ ( ongea na kusikiliza )
“Tomorrow we will meet to talk don’t try to escape because you will not be able to leave this country safely (kesho tutaonana , usijaribu kuwaletea vijana shida maana hutoweza kutoka nje ya hii nchi salama )“ aliongea kimbona kisha akakata simu .
Siku iliofuata asubuhi yake kimbona alifika ndani ya morogoro .
“There is documents I need and person who has them is Daniel(kuna nyaraka nazihitaji na mtu huyo anazo danieli )“ aliongea kimbona na kumfanya carlos ashituke .
“ danieli mtalemwa ?”
“yes , I think you know him well because you have met him , I released you from prison for that job (ndio , nafikiri unamfahamu vizuri maana ushawahi kukutana nae , sasa nimekutoa gerezani kwa ajili ya kazi hio “.)
“ I have condition “ akimaanisha kwamba ana sharti
“speak”
“ After your work I need you to assure my safety of leaving this country (baada ya kazi yako nataka unihakikishie usalama wa mimi kutoka nje ya nchi hii)”.
“ once the work is done you are free to go “ akiaamanisha kwamba pale kazi itakapokamilika ataweza kwenda .
“ not free to go , I want you to assure my safe exit “( akimaanisha kwamba sio kwenda tu , anataka amhakikishie kuwa atatoka kwenye nchi hii bila shida yoyote .
“ that is within my power , perhaps if there is onether “( akimaanisha kwamba hilo lipo ndani ya uwezo wake , labda kama kuna lingine “
“there is nothing more , important for everyone is to keep promise , if you go against it I will kill you “( hakuna la ziada muhimu ni kutimiza ahadi ukienda kinyume nitakutafuta popote pale na kukuua ).
“Well how many days will you complete the task , because at moment we don’t know where danny is”.(ni siku ngapi utakamilisha kazi kwasababu kwa sasa hatujui danny alipo ).
“I need week , I also need some informations about him to get me started , especially places where he recently appeared. ( akimaanisha kwamba anahitaji taarifa zinazomuhusu danny sehemu alizo onekna mara ya mwisho , pia kukamilisha hilo atachukua wiki moja ).
“The last time he appeared in Tanga Lushoto , when I sent my boys to kill Bruno, all you have to do is find damian rabani where he is, if you find him he will lead you to find him ( mara ya mwisho alionekana lushoto nilipotuma vijana wangu kumuua Bruno , unachotakiwa kufanya ni kumtafuta damiani na atakuongoza kumpata danny ).
“”and who is this damian and how close is he to this danny ?”(na huyu damiani ni nani na anah ukaribu gani na danieli ).
“thes are the questions I hoped for from you and my boys have given me this file , it contains all the information abaout him , car and other requirements about yur mission meja will give you , hope you will work out (hayo ni maswali ambayo nimetegemea kwamtu makini kama wewe hili ni faili nililotumiwa na kijana yangu kutoka kituo cha polisi lushoto lina taarifa zote zinazo muhusu damiani , mahitaji mengine kuhusu kazi yako utayapata kwa meja , natumaini kazi itafanikiwa kwa weredi )..
“ and last we will be communicating at every step you reach”( na jambo la mwisho tutakuwa tunawasiliana kwa kila hatua )
******
Ilikuwa ni siku kama tano tokea tukio la kutekwa kwa damiani litokee na siku mbili baada ya carlos kupewa kazi, upande mwingine ndani ya jiji la Tanga wilaya ya korogwe , kilomita chache kutoka mombo katikati kuna mji uliokuwa ukijulikana kwa jina la chekelei , ndani ya kijiji hiki mita kadhaa kutoka barabarani , kulikuwa na jumba kubwa lililokuwa limezungukwa na uzio mkubwa , ndani ya jumba hili liliingia gari moja aina ya brevis nyeupe , na kwenda kupark sehemu iliokuwa na gari lingine aina ya BMW , baada ya kupark alionekana mwanadada mmoja akitoka ndani ya gari hio ,alikuwa mweupe mrefu alievalia suruali ya jeans na sweta la mikomo mirefu huku nywele zake akiwa amezibana kwa nyuma .
Alizunguka upande wa pili nakufungua mlango na hapo alionekana kijana Damiani aliekuwa na mabendeji usoni akitoka nje ya gari hilo huku akichechemea , alisaidiwa na mwandada huyo kisha walifungua mlango na kuingia ndani .
"Danny tumefika " aliongea mwanadada yule akimuongelesha mwanaume aliekuwa amesimama akiwa anaangalia runinga .
Danny aligeuka na kuwaangalia na kumfanya damiani aanze kurudiaha kumbukumbu zake nyuma , kumbukumbu nazo zilimpeleka mpaka siku ya interview yake , mtu aliempa lift alimkumbuka vyema , lakini alishangaa mtu huyo kuwa pale mbele yake .
" Karibu damiani " aliongea daniel huku akiwaonyesha sehemu ya kukaa huku danny , alikuwana mwili ulioshiba mazoezi kwani siku hio alikuwa amevalia singlend tu na suruali ya jeans .
" asante " .
" Naona kwa mshangao huo utakuwa unanikumbuka vyema , maswali yako nitayajibu ,sasa hivi unatakiwa kupumzika kwanza " aliongea huku akimpa ishara yule mwanadada kwamba amfuate .
" suzzane nimepokea taarifa hapa carlos yuko huru , katolewa siku mbili zilizopita " .
" Unamaanisha carlos cardoso ?"
" Ndie huyo "
" imekuwaje akawa huru ?".
"Hilo silifahamu , lakini nina hisia raisi anahusika katika hili ".
" Kwanini unasema hivyo "
" kwasababu tukio la carlos kutoka limefanywa na watu ambao hawajulikani mpaka sasa , pili tukio limetokea mkese wakati alipo kuwa akihamishiwa gereza la morogoro , hapo unaweza kuona kuwa hakukuwa na sababu ya carlos kupelekwa morogoro , my feelings zinaniambia kuwa huu ulikuwa ni mpango wa kumtoa gerezani , kikubwa ni kwamba amri ya carlos kuhamishiwa morogoro inetoka kwa raisi , pili henry hakuwa akimjua carlos mpaka alipo pata taarifa hizo kutoka kwa mstaafu matinde "
" kwa muunganiko huo inaonekana kweli anahusika , lakini swali linakuja kwanini katolewa?? ".
"sababu lazima itakuwepo nafikiri unakumbuka moja ya kauli ya mwisho ya marehemu juu ya henry?? " .
" ndio nakumbuka ".
" Basi lazima tufahamu sababu kwanini katolewa , na njia ya kujua sababu ni kumkamata carlos tena na kuhakikisha anasema kike alicho agizwa , maana mpaka sasa kuna dalili zote za U-97 kurudi tena kwenye hii nchi na biashara ya madawa kuendelea , kazi ambayo tumeifanya kwa jasho kubwa kuitokomeza ."
" na vipi kuhusu damiani ?" ..
" Mpango uko kama ulivyopangwa , na utaratibu wa kumtoa nje ya hii nchi kwa ajili ya mafunzo uko pale pale kesho ataondoka rasmi kuelekea china.
Wakati ambao suzzane anaingia na damiani kwenye nyumba iliopo chekelei , gaidi wa kiamatafia carlos alikuwa hatua kwa hatua mpaka wakati gari ya suzzane ikiingia ndani hapo aligeuza gari na kuondoka
“vou voltar mais tarde “ ( nitarudi baadae usiku ) aliongea na kuondoka .
 
KAULI YA MWISHO YA RAISI
KABLA YA KIFO CHAKE
UMOJA NAMBA TISINI NA SABA
UNITY -97
MWANDISHI : SINGANO JR

SEHEMU YA 13
ILIPOISHIA
Iliishia pale tunapomuana bwana carlos Cardoso jambazi na muuaji wa kimataifa akiahidi kurudi baadae usiku kwa ajili ya kupambana na bwana danieli mtalewa jasusi wa kimataifa
INAENDELEA .
Ilikuwa muda wa saa mbili usiku carlos ndio muda ambao alifika nje ya ukuta wa jumba walilokuwemo Daniel , damiani na suzzane , aliangalia ukuta huo na kurudi hatua chache nyuma na kuuruka ukuta huo na kutua chini pasipo hata kelele , muda huo suzzane na danieli walikuwa ndani wakinyanduana , kwani miguno ilisikika hadi sebleni na kumfanya damiani asisimke sana , na hata kile alichokuwa akikiangalia kwenye tv hakikuwa na maana kwake tena kwani muda huoo alikuwa akisilizia sauti ya suzzane ikilalamika .
“oouh… daniiii… yeaah … siiiiiiiii ..arghhhhh…”. danny alionekana kumudu mchezo kweli kweli kwani wakati huo suzzane alikuwa amewekwa mbuzi kagoma , huku danieli akipump kama anacheza ngoma za kisukuma .
Hilo lilikuwa kosa kubwa walilolifanya la wote kuwa bize ,huku wakijua kwamba walikuwa wakiwindwa , carlos aliingia mpaka sebleni bila shida yoyote ama kushitukiwa huku akisikilizia miguno ya mwanamke ndani huko ,na wakati huo damian nay eye hakujua kuwa hapo sebleni kulikuwa kumeongezeka mtu maana wakati huo alikuwa amefumba macho akivuta hisia huku masikio yake yote akiwa ameyategesha kama antenna akisikiliza miguno ya suzzane ..
Carlos alitoa bastora yake aina ya blaser F3 akaikoki na hapo ndipo alipomshitua damiani na damiani alitaka kupiga ukulele lakini kabla hajaendelea aliambiwa atulie , huku miguno ya kimahaba ya suzzame ikizidi kutawala ndani ya nyumba hio na utadhania alikuwa akifanya makusudi .
“stand up slowly without shouting and walk towards the room where your fellows are ( simma taratibu bila kupiga kelele na tembea kuelekea kwenye chumba walipo wenzako).
Damiani kwa woga alinyanyuka na kuanza kutembea kuelekea upande wa chumba walichopo suzzane na daniel walipo .
“ am cumin .. aaah ooooh !” ilikuwa ni saui ya suzzane na muda huo huo walinyamaza na damiani alikuwa ashaufikia mlango huku carlos akiwa nyuma yake .
“gonga “ aliongea carlos kwa Kiswahili na damiani aligonga .
“ damiani ingia “.ilikuwa ni sauti ya suzzane .
Kitendo cha suzzane kusema ingia carlos alimpiga damiani pigo takatifu(silent holy blow) kwenye shingo ambalo halikusikia hata kidogo na kisha alishikiliwa na carlos na kulazwa chini taratibu kisha alifungua kitasa na kujirusha ndani huku bastola ikiwa mbele , lakini ile anaingia ni kama alikuwa wamemtegemea kwani danieli aliruka sarakasi na kumchota mtama na kupiga ngumi kiwiko cha mkono wa carlos na kupelekea bastola iende uvunguni .
Dakika chache nyuma wakati danieli akiwa amemuweka suzzane mbuzi kagoma , simu yake aliokuwa ameiweka kwenye kitanda upande wa kushoto ilitoa mwanga , akiwa anaendelea kumshughulikia mlimbwende huyo aliekuwa akipiga kelele alinyoosha mkono na kuichukua , alitoa lock na kuangalia meseji ilio ingia kisha akafungua app moja iliokuwa na kiji icon kama cha instagram cha zamani na kufungua , na hapo ndipo alipomshudia carlos sebleni akiwa amemnyooshea damiani bastola kwani alikuwa amefunga camera .
Wakati anaendelea kukata mauno alimuonesha suzzane na kisha akampa ishara ya kuendeleza miguno , kwa hio muda wote carlos na damiani wakati wakija upande wa chumba chao walikuwa wakishuhudia kila kitu na ni kama watu ambao hawakuwa na wasiwasi kwani danieli aliendelea kupush mpaka pale walipofikia mshindo wote kwa pamoja .
Sasa baada ya carlos bastola kumponyoka alichomoa kisu na pambano lilianza kupigwa humo ndani , carlos alikuwa mwepesi kweli , alikuwa akiruka sarakasi za haraka haraka sana kupiga na kukwepa mapigo ya daniel na wakati huo suzzane alikuwa akiangalia tu kinacho endelea ,
Carlos alifyetuka kama mpira na kuzungusha teke (roundhouse kick ) lililompata kisawasawa mbavuni daniel na kumfanya danieli ayumbe , danieli hakutaka kusikilizia maumivu kwani carlos alileta shambulio lingine la karate (foot sweep )ambalo lilimfanya Daniel alikwepe kwa kuruka sarakasi ( acrobatic flip )ilio mtoa nje ya chumba , na manusura amkanyage damiani usoni , carlos hakutaka kuchelewa alimfuata huko huko huku akisahau kuwa nyuma kulikuwa na mrembo suzzane , na alicho kosea yeye ni kumchukulia mrembo huyo kama mchumba tu wa kugegedwa na Daniel . .
“ simama hivyo hivyo kabla sijakutoa ubongo , nyoosha mikono juu “ aliongea suzzane , lakini bila kutegema carlos alijitupa kwenye chumba cha pembeni yake kama chui na kisha alifunga mlango , na suzzane hakutaka kuchelewa na yeye alifata huku huko kwa sambasoti , na hilo likawa kosa kubwa kwani ni kama carlos alilitegemea kwani ile anaingia tuh carlos alifyatuka kutoka kwenye dirisha na kwenda kutua nyuma yake na kumpiga teke la mgongo na kumfanya apepesuke na kwenda kutua kwenye kitanda huku bastora ikiwa imeingia uvunguni kupitia upande wa pili wa kitanda na wakati huo huo danieli na yeye alijifyatua na kuingia ndani , na kwenda kusimama kwenye kitanda , na carlos hakufanya ajizi kwani alivuta kwa nguvu duvet na kumfanya Daniel apepesuke lakini hakutaka kuta chini kizembe , aliruka juu na kumpiga carlos kwa kumbetua kifuani na carlos alienda kudondokea mbele ya mlango , na hakutaka kuchelewa , alitoka nje na huku suzzane nae alikwisha amka na alimsindikiza na na teke la mgongoni (cartwheel kick) lililompeleka carlos kwenda chini kifudi fudi , lakini kabla hajatua chini alipifa sarakasi kujizungusha kama taili na kwenda kutua mbele , huku suzzane hakutaka kuchelewa alifyatuka kama mshale , na hapo sasa ngumi zilianza , kwani carlos alikuwa akichangiwa na watu wawili , alimbahatisha suzzane teke moja lililompeleka kwenda kutua kwenye tv na kufanya soketi kupasuka na kutoa cheche lakini wakati huo huo na yeye alipokea teke la shingo iliompelekea kuhisi maumivu , na kabla hajatulia alipokea ngumi mfuliulizo za kifua zilizokwenda kumdondosha kwenye sofa dogo pembeni , lakini hakutaka kuzidiwa kizembe alifyatuka(beki au backflip) na kutua nyuma ya sofa lile na kulisukma kwa mbele na kufanikiwa kumgonga nalo danieli , lakini kwa umakini hakwenda chini Zaidi kuruka na kupanda juu ya sofa hilo , ilikuwa ni mtanange mzito kweli ,kiufupi carlos alikuwa vizuri kwani alikuwa akipangua mapigo yote yaliokuwa yakija kwake kwa kasi ya hali ya juu mno , lakini aliona anazidiwa hivyo alikuwa akilenga mlango ulipo akimbilie nje , baada ya danieli kukusudia kumpiga mtama , carlos aliruka juu na kujivingirisaha na kwenda kutua kwenye mlango , na kuchoropokea nje , lakini ile anapiga hatua mlio wa bastora ulisika na kumpiga kwenye paja na kudondoka chini huku akiugulia maumivu , alijaribu kunyanyuka lakini aliongezewa na aliekuwa ameshika bastora alikuwa ni suzzane
Hatimae carlos alitatiwa vyema na kukamatwa huku akivuja damu , walimfunga kwa mnyoro na kisha walimburuza mpaka kwenye chumba kilichokuwa ni stoo kwani kilikuwa na makorokocho mengi na na hakikuwa na ceiling board waliunga ule mnyoror kwenye moja ya nguzo , wakamfung na miguu kisha wakamkalisha .
“ nani kakutuma ?“:
“foda-se”( ilikuwa ni tusi)
“ who sent you ‘ aliongea suzzane huku akikanyga kwenye jeraha lile la mguu na kumfanya carlos agugumie maumivu .”
“tell me who sent you “ aliongea suzzane na carlos alitabasamu .
“ https://jamii.app/JFUserGuide yoursell “ aliongea na kumfana suzzane apandwe na hasira na kumpa ngumi za nguvu . suzzane alikuwa alimpa surubu ya uhakika carlos kwa kutumia staili zote ila carlos hakufumbua mdomo Zaidi ya kuwatukana
“suzzane , just kill him , he wont speak “ aliongea Daniel na suzzane hakuwa na huruma a alimnyooshea na kuvuta trigger .
“ kimbonaaa” aliongea carlos maana aliona watu waliokuwa mbele yake walikuwa hawana utani kabisa na maisha yake .
“kimbona is the one who sent me to kill you and take the document “.
“unamfahamu kimbona ?”. aliuliza suzzane
“ ndio namfahamu huyu mzee na sina ugomvi nae , inakuwaje anataka kuniua “.
“what he want from me ( anataka nini kutoka kwangu )“
“ there are documents he need from you (kuna nyaraka anazihitaji “)
“ nyaraka ? nyaraka gani kimbona anahitaji kutoka kwangu “ aliuliza .
“go ask him” nenda kamuulize.
“ labda zitakuwa ni hizo bruno alizompa damiani “ aliongea suzzane .
Walitoka mpaka sebleni ambako wlimkuta damiani kesharejewa na uhafamu wake , huku akionesha kuwa na wasiwasi mwingi
“ Damiani kwa sasa uko salama huna haja ya kugopa tena “ aliongea danieli akimtoa wasiwasi damiani .
“yule ni nani ?”
“damiani kwasasa tupo vitani na vita hii inahitaji ujasiri , mkubwa sana taifa kwa sasa lipo kwenye hatari “
“ wewe ni nani , hakuna mmoja wenu aliejitambulisha kwangu Zaidi ya kuniweka katika maswali mengi , nyie ni nani , najua mmenisaidia mpaka kunileta hapa kwa ajili ya usalama wangu lakini nahitaji kujua ninyi ni watu gani , na je ninaweza kuwaamini “.
“nishakujibu kwamba maswali hayo nitayajibu yote na utaelewa kwa undani kwanini pia uko mahali hapa kwa kifupi tu nikwambie sisi ni usalama wa taifa kutoka kitengo cha(TANZANI INTELLIGENCE SECURITY SERVICE ) TISS “.
“ kwa hio nyie ni ma agent?”.
Hapo damiani alijikuta akishangaa kwani kwenye maisha yake hio ndio mara ya kwanza kukutana na usalama wa taifa .
“ huna haja ya kushangaa upo tupo hapa kwa ajili ya kukupa ulinzi , una kazi kubwa mbeleni ya kufanya“.
“unasema nina kazi kubwa mbeleni ya kufanya , ni kazi gani hio “.
“ kwasasa ni mapema sana kukuambia “.
“kwanza niseme nashukurni kwa kunisaidia kutoka kwenye mikono ya wale maharamia , lakini kwasasa nataka mniruhusu kwani nina kazi ya kulipiza kisasi cha mama yangu , na kuhusu hio kazi kubwa sitaki kuifahamu shida yangu mimi ni kulipiza kisasi tu kwa wale wote waliohusika na kifo cha mama yangu “.
“ ninaelewa machungu yako bwana damiani , lakini kazi ambayo unatakiwa kufanya ndio itakayo kupeleka mpaka kujua ni nani aliehusika na kifo cha mama yako “.
“ unamaanisha nini kuhusu hilo ?”.
“mzungu uliemsaidia unajua jina lake ?”
“ ndio anaitwa bruno “
“ sasa sisi ndio tulokuwa walinzi wake , na ilitokea bahati mbaya akashambuliwa wakati tukiwa kwenye majukumu mengine na vijana tulio waacha kutoa ulinzi wakapoteza maisha kwa kushambuliwa na watu wengine wasiofahamika mpaka sasa , ambao tunaamini ndio walio fanikiwa kufanya mauaji ya mama yako na ya bruno “
Hapo damiani alielewa sasa , kwani alitingisha kichwa chake kuashiria kile anacho kizungumza anakiamini na amekielewa .
“miongoni ya watu ambao wamehusika na kifo cha mama yako ni hao waliokuteka na kukupa mateso mpaka pale suzzane alipokuja kukuokoa “
“ nashukuru sana suzzane kwa mara nyingine “.
“ huna haja ya kushukuru damiani ni kazi yangu kama mwana usalama kuhakikisha nchi hii na watu wake wanakuwa salama “.
“ nafikiri mpaka sasa ushajua ni kitu gani wana kihitaji kutoka kwako na ndio maana walikutesa si ndio ?”
“ ndio , walikuwa wakihitaji nyaraka alizo nipa bwana bruno , lakini sikuweza kutaja mahali zilipo japo najua “
“ safi sana umeonyesha ujasiri mkubwa sana kwa kutowaambia sehemu zilipo , lakini nataka nikwambie , japo unajua zilipo, lakini hazitokuwa salama mpaka pale tutakapo zipeleka sehemu salama Zaidi , labda nikuulize ni wapi ulizoziweka “.
“nimeziacha nyumbani sehemu salama “.
“ safi siku ya kesho , tutaenda mimi na wewe kuzichukua huku suzzane akiendelea kubaki hapa na kumlinda carlos “ aliongea danieli kisha walitakiana usiku mwema na kisha kila mtu alielekea chumbani kwa ajili ya kulala , huku suzzane na danieli kama kawaida yao waliingia kwenye chumba kimoja na kulala kwani walikuwa ni wapenzi.
Siku nyingine iliwadia , kila mtu aliamka mapema na kusalimiana , waliandaa kifungua kinywa na kisha baada ya kifugnua kinywa , danny na damiani walitoka wakiingia kwenye gari huku nyuma wakimuacha suzzane na kutoweka wakielekea lushoto kwa ajili ya kuchukua nyaraka .
Korogwe na lushoto hapakuwa mbali sana ni muda wa masaa mawili na nusu ndio muda waliofika , waliendesha gari kitahadhari sana , gari ilikuwa kwenye mwendo , walipita chuo cha mahakama na kusonga mbele dakika tano mbele danny alikunja barabara ya kuelekea chuo cha SEKOMU , walipita maghamba na hatimae waliingia mkuzi walisimamisha gari kwani mtaa waliokuwa wakiishia damiani hakukuwa kukifika gari , walitembea kwa kushuka mpaka ndani ya kijiji huku watu wengi wakimshangaa kwani walikuwa wakiamini kwamba bwana huyo alikuwa ametekwa .
“ inatakiuwa tufanye haraka kwani naamini polisi wanaweza kufika eneo hili kwa ajili ya kukuhoji “ aliongea danieli na kumfanya damiani akimbilie ndani kwao , nyumba ambayo kuna jirani yao alikuwa akikaa hapo , na wakati huo hakuwepo , hakutaka kuchelewa aliendea nyuma ya choo na kisha alifukua na kutoa bahasha ile na kisha danieli aliichukua na walitoka eneo hilo kurudi barabarani huku akiagana na baadhi ya wanamama .
“ katika hari ya ghafla , danieli alimrukia damiani na kumdondosha chini , na risasi ilimpiga kwenye paja la mguu na kuhisi maumivu makali huku akiwa ameangukia upande wa kichakani , risasi ambazo zilikuwa zikirindima kwa madakika kadhaa na kisha kutulia huku danieli akiwa amelala chini akijaribu kuangalia uelekeo wa risasi zinapotoka huku akiugulia maumivu yapaja lake . .
“damiani hii sehemu sio salama tena , na kama unavyo ona tayari inaonekana tumezungukwa , shika hizo hela ni nauli, hakikisha nyaraka hizo unaziweka salama , fanya lolote uweze kufika korogwe nitaangalia namna ya kutoka mahali hapa “ aliongea danny huku akijikaza maana alikuwa akihisi maumivu makali kwenye paja lake , aliangalia usalama na aliweza kuona mtu mmoja akiwa juu ya mti upande wa kulia akiwa ameshikilia sniper riffle ..
“ tambaa chini tokezea kwa juu kisha kimbia “ aliongea danieli kwa sauti ya chini iliosikika vyema kwenye masikio ya damiani , na damiani kama alivyoambiwa alinyanyuka na kuanza kutambaa , danieli alitoa bastora yake na kutoa kuifunga kiwambo cha kuzuia risasi na kisha alianza kuvurumusha risasi upande aliekuwepo yule sniper .
Lakini katika hali ya kutotegemea danieli alipigwa risasi nyingine ya mkono huku akishindwa kujua risasi hio ilikuwa imetokea wapi na bastola ilidondokea upande mwingine kichakani kabisa , hakutaka kufa kizemba , alinynyuka kwa kuchechemea na kuanza kukimbia , lakini hakufika mbali alipigwa nyingine ya paja na pale pale akadondoka chini na sniper aliekuwa amejifunga kitambaa usoni alitokezea na kusimama mbele ya damiani aliekuwa akitapatapa kwa maumivu .
“suzzane !!! , carlos “ alijikuta akipigwa na butwaa , kwani mwanamkealiekuwa mbele yake alikuwa ni mshirika wake , tena sio mshirika wake tu lakini pia alikuwa ni mpenzi wake .
“samahani sana danny , najua upo kwenye mshangao mkubwa , hukupaswa kuniamini na hilo ndio kosa lako na leo ndio mwisho wako “ aliongea suzzane huku akiwa na sura ambayo haikuwa hata na chembe ya huruma , usingezania kwamba ni watu waliokuwa wakifanya kazi zao pamoja.
“suzzane kwanini umeamua kunisa.. liti suzzane , unasahau ni mangapi tumefanya pamoja “
“ paa.. paaa” ulikuwa mlio mdogo wa risai uliofumua kichwa cha danieli na kupoteza maisha hapo huku alieruhusu risasi hiz alikuwa ni carlos .
Suzzane alijikuta akimwangalia danieli na kisha alitoa machozi .
“ nisamehe sana danieli , siwezi kuwa upande ambao utayafanya maisha yangu kuwa ya kutangatanga “ aliongea suzzane na kisha aliondoka .
“ where will this damian fled ,he got document I need “( huyu damiani amekimbilia wapi , anazo document ambazo nazihitaji ) aliongea carlos .
“ we will find him , he wont have gone far , and most of all he does not know if I am involved and he will go straight to chekelei “.( hawezi kwenda mbali , kwanza hajui kama nimehusika , na naamini atakwenda moja kwa moja chekeli kwani ndio atakuwa anaamini kuna usalama ).
“ so you are the sniper, you shot police at mikese ( kwa hio ndie uliekuwa sniper uliewapiga risasi polisi pale mikese )
“yes but I did not kill them , I made them sleep for a short time as it was for you ( ndio lakini siku waua , niliwafanya walale kama ilivyokuwa kwako ).
“you are dangerous woman ( wewe ni mwanamke hatari )”.
Gari waliokuwa wamepanda iliyoyoma huku suzzane akipanga awahi korogwe akamsubilie damini kwani aliamini kwa vyvyote vile lazima angeenda mahali hapo .
UKITAKA MWENDELEZO NICHEKI INBOX AU WATSAP KWA NAMBA 0687151346 NIKUPE UTARATIBU , TUMA MESSEGE USIPIGE SIMU
 
KAULI YA MWISHO YA RAISI KABLA KIFO
UMOJA NAMBA TISINI NA SABA
U-97

SEHEMU YA 15
Damiani pikipiki aliokuwa amepanda ilimfikisha , makuyuni na hakutaka kuendelea tena Zaidi kwani hakuwa na hela za kutosha na alikuwa na safari ndefu , alishuka sehemu ile , ilikuwa imechangamka kidogo , bahati nzuri kwake ni kwamba yule boda aliemleta baada tu ya kumshusha alipata abiria mwingine na kurudi nae .

Akili yake ilicheza kama mashine , baada ya kufika makuyuni kuna gari aina ya costa ilikuwa ikija na ilishusha abiria katika eneo hilo la makuyuni , na ilionesha ilikkuwa ikielekea lushoto , ni kama mtu aliekuwa na hisia kwani aliingia kwenye ile gari inayoelekea lushoto .

Na kweli hisia zake zilikuwa sawa kabisa kwani ile anafika katikati ya makuyuni na chekeli aliona gari ya suzzane , aliijua vyema gari hio na wakina suzzane hawakuhangaika na gari hio kwani walijia kwa vyvyote vile damiani alikuwa akielekea korogwe .

“ hapa nimewachenga chenga la macho , inabidi nishukie kwenye kijiji cha kati kati hapo , aliwaza na gari ilietembea umbali kama wa kilomita moja hivi na damiani alishuka , ilikuwa kwenye kijiji kimoja kilichokuwa kikiitwa mtindilu , ni moja ya vijiji ambavyo vilikuwa vimezungukwa na mashamaba ya katani .

Baada ya kushuka aliangalia sehemu ambayo kulikuwa na ujificho na kisha alienda kukaa japo watu wa hapo walikuwa wakimshgaaa ila hakutaka kujali sana na pia kilichomsadia ni kwamba kijiji hicii hakikuwa na watu wengi sana .

Upande wa suzzane walizidi kusonga , walivyo fika makuyuni walisimamisha gari na harakaharaka suzzane alishuka na aliwafuata moja ya watu waliokuwa wamekaa wakipiga soga na kuuliza , na jibu alilopata hapo lilimchosha . ,kwani aliambiwa kuwa mtu huyo alishushwa hapa muda si mrefu lakini katika hali ya kushangaza kapanda gari za lushoto .

Alirudi kwenye gari huku akiwa na hasira kali za kuchezewa akili na damiani alizidi kumchukia na alijipia akimtia mkononi lazima ampe mateso ya kulipizia kumsumbua kwa muda mrefu ...

“I think he saw us when we got there , because by the time he left , that`s the time we got there “ nafikiri alituona wakati tunafika pale chekelei kwani muda ambao sisi tulifika na yeye kuondoka vinalingana aliongea suzzane huku wakigeuza gari .
“ I think so too” nafikria hivyo pia
“ where do ou think he is headed now “(unafikiri ni wapi kaelekea kwa sasa )”
“ I don’t know but I believe he can`t go back lushoto. “.( sijui lakini naamini hawezi kwenda lushoto ).

Waliendesha gari huku wakiwa makini na barabarani kama watamuona , lakini mpaka wanapita kijiji cha mtindilu ambacho damiani kashuka hawakumuona na walipita eneo hilo na damiani aliona gari yao wakati inapita alitabasamu huku akiwa makini na kuangalia magari yanayoelekea korogwe apande ..

Bahati ilikuwa upande wake kwani muda mfupi gari iliokuwa ikielekea tanga ilifika na hakujiuliza mara mbili alipanda gari hio na kuondoka huku akishusha pumzi kwani kwa wakati huo aliaminni alikuwa salama ilikuwa imetimu saa tisa na madakika kwa kupitia saa ya gari hio .

Gari ilifika korogwe stendi ikapandisha abiria na ikaondoka , saa kumi na mbili kamili alikuwa ndani ya jiji la Tanga , ilikuwa moja ya mji ambao umejengeka kwa mpangilio mzuri ,hakujua aelekeee wapi kwani hakuwahi kufika ndani ya mji huo , alikuwa akihisi njaa kali kwa muda huo .

Alisogea mbele kidogo kutoka stendi ya tanga ya zamani na kisha aliona moja ya mgahawa watu waliokuwa wakiingia na ktuoka , aliangalia ana kiasi gani mfukoni kilicho baki , na aliona ilikuwa imebaki elfu arobaini tu .
“ alipata wali na samaki , huku akiwa anaangalia runinga kituo cha ITV na walikuwa wakionyesha habari za saa , lakini kuna habari ilimshitua
“ ZIKIWA NI SIKU KADHAA TOKEA MAUAJI YA TAJIRI BRUNO LAMBERK NA MAMA MMOJA ALIEFAHAMIKA KWA JINA LA SARAH RABANI LEO HII TENA KUMEOKOTWA MWILI ULIOTAMBULIWA KWA JINA LA DANIEL MTALEMWA UKIWA NA MAJERAHA YA RISASI , MKUU WA KITUO CHA POLISI LUSHOTO MJINI AMETHIBITISHA MAUAJI HAYO HUKU AKIWAASA WANACHI KUWA WATULIVU POLISI WANAFANYA UCHUNGUZI KUBAINI WALIOHUSIKA NA KUWAFIKISHA MBELE ZA SHERIA “

Damiani alijikuta hata hamu ya chakula ikimpotea kabisa , hakuamini kwamba danieli keshapoteza maisha , kuna hisia zilimwambia kabisa kuwa muhusika atakuwa suzzane lakini mawazo hayo aliyapinga kwani alijua kuwa wawili hao walikuwa wapenzi .
“ kama bro dannny ndio hivyo keshatangulia , inabidi niwe makini zaidi la sivyo nitapotea kabla ya kulipiza kisasi “ aliongea huku akijilazimisha kula maana hata hamu hakuwa nayo .

Baada ya kushiba aliulizia gesti zilipo na alionyeshwa na kulipa elfu kumi na tano na kisha alipewa chumba chake , alikuwa amechoka . mno .
“ hapa sina hata nguo , maisha yangu yamebadilika sana kwa muda mfupi “ aliongea huku akiwa ameangalia juu gypsum , alikaa hapo akiwa na mawazo ya hapa na pale , alijikuta akinyanyuka na kutoa ile bahasha na kutoa baadhi ya karatasi .

Aliangalia ile iliokuwa na account ya benk ya CRDB na kadi yake akapitia nyingine , akaingalia ile kadi nyingine ya SWISS BANK na kisha kurudisha kila kitu ndani
“ kesho ngoja nitajaribu kwenda kutoa pesa kama hii akaunti inazo , inabidi niwe jasiri , mimi ni mwanaume sitakiwi kuogopa “

Siku ya pili yake damini aliamka mapema na kuoga kisha alitoka hadi nje na kunnua supu na chapatti mbili kisha alirudi kwenye gesti ile na kunywa kisha alichukua ile kadi ya benki na kuangalia zile karatasi na kisha alikariri nywila (password ) na akatoka kuelekea benki , aliulizia na kuambiwa ipo mbele kidogo ya stendi .

Hakutaka hata kuingia ndani ya benki kwani aliona ingekuwa usumbufu na pili hakuwa hata na uhakika kama account hio ilikuwa na hela , moja kwa moja alienda mpaka kwenye ATM na kisha aliingiza kadi na ikamwambia iangize namba za siri , na uzuri ni kwamba alikuwa akizijua japo hakuwa na uhaika kama ndio zenyewe .

Namba zile zilikubali , na account ile ilionesha kuwa na pesa za kutosha na ilimfanya atabasamu , kwani ilikuwa ikimuonesha mafungu ya hela ya kutoa , lakini aliangalia kwanza salio .

Alijikuta akitoa macho , kwani hakuamini kiwango cha pesa kilichokuwa ndani ya kadi hio zilikuwa ni milioni 140 za kitanzania zilizokuwa zimehifadhiwa katika hio akaunti .

Hakutaka kujiuliza mara mbili mbili alitoa laki nane na kisha alitoka ndani hapo , alitemba mpaka kwenye duka moja kubwa ambalo lilikuwa likiuza vifaa vya electronics .. alinunua simu ndogo ya elfu therathini kisha alinuniua na laptop ya laki tano na nusu , alijaribishiwa vitu vyake na baada ya kuona viko sawa alimuomba muuza duka lile amhifadhie kwa muda anarudi , alitembea mpaka kwenye soko moja lililokuwa linajulikana kwa jina la tangamano , alinunua nguo tisheti na jeans na akanunua na begii kisha akarudi mpaka kwenye lile duka na kupewa vitu vyake na kuviweka kwenye lile begi , alitembea kurudi kwenye ile gest , alifika pale mapokezi na kuongea kiasi cha shilingi elfu therethini na kisha akaingia chumba chake , kitu cha kwanza aliwasha ile laptop na kisha alitoa ile flash aliopewa na bruno .

Nia yake ilikuwa ni kutaka kuchukua zile namba za simu ambazo bruno alimwambia kuwa azipige , alizinakili kwenye simu , lakini alikumbuka kuwa amenunua simu lakini hakuweka laini , na aliona akisajili ingekuwa ngumu kwani asingeweza kwani hana kitambulisho .
“ sista samahani “
“ bila samahani “.
“ unaweza kuniazima simu yako kuna mtu nimpigie “ alikuwa ni mdada wa mapokezi ndio mahali ambapo damini aliona ni sahihi kwa ajili ya kwenda kuomba kupiga simu.
“ aipewa na kisha alirudi ndani ya chumba huku dada yule akimwambia kuwa asicheleweshe simu yake “
“ hellow “ aliongea damiani kwani simu iliita na kupokelewa “. Kuna maneno ambayo aliambiwa aongee na bruno pindi apigapo hio namba kwenye ile video , alichukua zile karatasi na kutafuta maneno hayao na aliongea .
“please specify your identification number “.(tafadhari thibitisha namba yako ya utambuzi ) ilikuwa ni sauti ya mwanadada , sauti kama zile za kwenye mitandao ya simu akikwambia simu haipatikani
“0981S”.
“Please wait for identification “ ( tafadhari subiri kwa utambulisho ).

Damiani alijikuta akishangaa maana hakujua alikuwa anaongea na mtu gani , maana hakukuwa na maelezo mengine Zaidi ya taja subiri na mengineyo ila aliona ngoja asubirie aone mwisho wake
“your identification is complete , please wait to be connected to the person you are looking for ( utambuzi wako umekamilika tafadhari subiri uunganishwe na mtu unaemtafuta ..
“ habari , sasa kaa eneo hilo hilo ulipo utapokea maelekezo mengine ndani ya muda mfupi “. Ilikuwa ni sauti nzito na hakukuwa na maelezo mengine .
Na simu pale ilikatwa , huku damiani akijiuliza ni watu wa aina gani aliokuwa akiongea nao , maana sauti ilianza kama zile za mitandao , na ikabadilika ikawa ya mwanaume lakini safari hio alikuwa ni sauri ya mtu kamilii lakini pia hakukuwa na maelezo mengi , sasa alijisahau kuwa simu ile kaomba , alijikuta akitoka na kumuendea yule dada na kumwambia anaomba muda kidogo , huku akimpa elfu kumi na dada yule hakuleta ubishi alitabasamu na kumwambia hata atumie lisaa lizima (chezea pesa wewe ).
Ndani ya dakika kumi na tano danieli alipokea simu lakini awamu hii ilikuwa namba tofauti , alipokea .
“ sasa sikia toka sehemu hio njoo mpaka jengo la benki ya CRDB utaona gari aina ya benz nyeusi imesimama , hakikisha unakuja na kila kilichokuwa chako “.

Damiani alitoka na vitu vyake na kisha alimkabidhi yule dada wa mapokezi huku akimwabia hela aliotoa ya chumba atumie na kisha alitoka na kuelekea upande ambao alikuwa ameelekezwa , ni kweli ile anafika aliona gari ile nyeusi, aliisogelea na kisha akaingia .
alikuwa ni bwana mmoja mwenye umri kati ya miaka 30 kwenda 35, mweusi aliekuwa amevalia tisheti iliomkaa vizuri na kumchora kifua chake cha mazoezi huku alionekana alikuwa akitafuna bublish .
“ dogo unaitwa nani ?”
“ damiani rabani “.
“ tunaelekea dar mkubwa , funga mkanda “ aliongea bwana yule na gari ilitolewa hapo nduki , kwenye gari hakuna aliekuwa akimungelesha mwenzake .

Masaa manne tu walikuwa ndani ya jiji la dar wakapita tegeta , maana gari hio ilipitia bagamoyo , gari ilipita mbezi beach , ilivyofika lugalo ilikata barabara ya kuelekea kawe , baada ya dakika kadhaa walikuwa ndani ya kawe , gari ilisonga na kuingia upande ulioko na beach , nyuma kidogo ya kiwanda cha kuchakata mchanga na hapo ilisimama pembeni ya gari nyingine aina ya AUD A3 SEDAN nyeupe .
“ ingia kwenye gari hio dogo ushafika “ aliogea jamaa yule na kisha damiani alitoka kwenye gari hio na kisha aliisogelea na kushika mlangoo , lakini haukufunguka , gari ile ilishushwa kioo na mwanamama mmoja alievaa wigi mweupe makadirio ya miaka yake inaweza kuwa kati ya miaka 40 kwenda 45 , alimuonesha ishara ya damiani kuzunguka upande wa nyuma na alifungua mlango na akaingia .
“ ushawahi kutoka nje ya nchi ?”
Aliuliza yule mama huku akiwa makini na gari na muda huo walikuwa wakipita morocco .
“ hapana sijawahi , ‘ alijibu na mama yule hakuendelea kuuliza maswali mengine na alionekana kauzu kweli ,gari ile ilikuja kusimama mikocheni kwa warioba .
“ nifate “. Aliongea mama yule na damiani japo alikuwa na waswasi lakini alikuwa amejitoa muhanga tu kwani alijiambia mwenyewe lolote na liwe , waliingia kwenye nyengo la palm village , chini kabisa kulikuwa na duka la nguo , supermarkert , saloon na ATM za benki .

Waliingia kwenye duka la nguo na mama yula alimwambia achague nguo , na damiani japo alishangaa lakini alitii ,alichagua nguo baadhi lakini yule mama alimwambia hizo nguo ni chache achague nyingi apate na za kubadilisha, lakini damiani bado alichagua chache na kumfanya mama yule afanye kazi ile mwenyewe , alichaguliwa nguo nyingi mno kiasi cha damiani kushangaa , walinunua na begi kabisa na kuziweka .

Baada ya manunuzi ya nguo alipelekwa saluni na kunyoa vizuri na kufanyiwa scrub za kila aina na kisha yule mama alimwambia amfuate , waliingia kwenye lift na kwenda mpaka floor namba nane , na walikuja kusimama kwenye mlango uliokuwa una funguliwa kwa kuingiza namba , yule mama aliingiza namba na kisha waliingia ndani .
“ sasa bwana danieli unapaswa uogea utakate , kesho asubuhi utakuja kuchukuliwa , na maelekezo utapewa , pia ndani ya hii apartment huruhusiwi kutoka mpaka siku ya kesho , shika hii simu ndio watakupigia , mimi kazi yangu imeishia hapa nikutakie maisha mema huko uendako “ aliongea yule mama na hapo damiani alijikuta akizidi kushangaa maana yale maneno yule mama aliokuwa amemwambia hayakumuingia akilini .
Inakuwaje amtakie safari njema .
INAENDELEA
 
KAULI YA MWISHO YA RAISI
KABLA YA KIFO
UMOJA NAMBA TISINI NA SABA
MTUNZI : SINGANOJR

SEHEMU YA 16.
IKULU – DAR ES SALAAM .
Ilikuwa ni muda wa saa kumi na moja za jioni gari ya suzzane brevis, iliingia ndani hapo na kwenda kupark , na alionekana suzzane aliekuwa amevalia miwani na suruali ya jeans akitoka na moja kwa moja alielekea mpaka kwenye mlango wa kuingilia , alikaguliwa na siraha yake kuchukuliwa kisha alirushusiwa kuingia .
“Nifate miss suzzane mheshimiwa anakusubiria , aliongea mwanadada mmoja hivi mrefu maji ya kunde mwenye mwili mwembamba aliekuwa amevalia suti nyeusi , huku mkononi akiwa ameshika notebook .
Walienda mpaka ndani ya ofisi ya raisi na suzzane aliruhusiwa kuingia.
“ karibu suzzane “ aliongea henry , ambae alikuwa yuko bize na simu yake janja aina ya I phone macho matatu , huku akiwa amekalia masofa .
“nipe mpya suzzane “.
“ mheshimiwa tumeshindwa kumpata damiani , mpaka muda huu “ aliongea suzzane na kumfanya raisi kukunjua miguu aliokuwa amekunja nne “ alikuwa ni bwana mmoja aliekuwa na uso flani hivi ambao ilikuwa ni ngumu kujua kakasirika au katabasamu , kiufupi uso wake ulikuwa ukiwachanganya wengi waliokuwa wakimjua bwana huyu .
“unafikiri ni aina gani ya nyaraka ambazo bruno kampatia ?”.
“ mheshimiwa siwezi jua ni nyaraka za aina gani “ aliongea suzzane na kumfanya henry ainuke na kumkazia macho.
“ suzzane hivi unafikiri ni kitugani marehemu aliongea na bruno , unauhakika marehemu alikuwa anamuamini bruno mpaka kumkabidhi nyaraka za serikali ?”.
“mheshimiwa kuhusu uhakika sio asilimia , mheshimiwa akiwa anapigania uhai wake ni watu wanne walio ingia kumuoana, nakumbuka alikuwa ni mheshimiwa hassani jumbe ( raisi wa Zanzibar) , mohamedi abdukarim (shekhe mkuu wa dar es salaam ), George mayoghoya ( kadinali ) na bruno lamberk (mfanya biahara ), kati ya hao watu muheshimiwa ni wawili tu ambao wanaweza wakakabidhiwa hizo nyaraka ambao ni bruno na raisi wa Zanzibar .
‘ kama ni raisi wa Zanzibar , ningefahamu maana yule ni rafiki yangu , lakini kwa bruno ndio nina mashaka , na ndio maana suzzane nataka umkamate huyu kijana anaeitwa damiani kuna uwezekano nyaraka alizopewa na bruno ndio hizo”.
“ sawa muheshimiwa nitajitahidi “.
“ safi , kwa upande wangu nitasambaza picha hizi kwa kitengo cha TISS ili wamtafute popote pale “ aliongea henry na kisha waliangana na suzzane .
“ suzzane , hakikisha swala hili ni siri sana , pili hakikisha Nyaraka hizo hazimfikii kimbona kabla yangu “.
“ sawa muheshimiwa “..
*****
Ilikuwa ni siku nyingine tena , siku ambayo damiani hakupata hata lepe na usingizi , kwani usiku mzima alikuwa akifikiria hatima ya maisha yake kuwa katika hali aliokuwa nayo , aliona kabisa zile ndoto zake za kuwa mfanya biashara mkubwa zikididimia kwa madhira aliokuwa akipitia , alijizungusha kwenye kitanda muda huo ikiwa imetimu saa kumi na moja kamili .
Baada ya kuona hana hata usingizi , aliamua kutoka kitandani na kisha alielekea bafuni na kuoga na kisha alirudi na kujifuta maji , na hapo ndipo simu aliopewa na mwanamama ambae hakumjua jina mpaka wakati huo , simu hio iilitoa mlio kuashiria kuwa ilikuwa inaita .
“Damiani rabani “.
“ ndio ni mimi “
“jiandae saamoja kamili toka na mizigo yako shuka mpaka parking utaona gari aina ya BMW X7 nyeusi , fungua mlango kisha ingia , narudia saa moja kamili bila kuchelewa hata sekunde “ na simu ilikatwa hapo hapo , damiani aliangalia saa muda huo ilikuwa ni saa kumi na moja dakika arobaini na tano alijiandaa vizuri na kupark kila kitu kwenye begi , ilipotimu saa kumi na mbili dakika hamsini na tano , alitoka na vitu vyake kisha aliingia kwenye lift iliomteremsha mpaka chini , alizuga zuga chini hapo kwa dakika kama tatu ndio alipoingia ndani ya magari yaliokuwa yamepaki , na ile anatoka tu gari ya kwanza kuiona ilikuwa ni hio BMW na iliwasha indicator na damiani bila kuchelewa laifungua mlango na kuinhiza vitu na kuketi na kisha iliondolewa hapo kwa kasi ..
Gari ile iliingia barabara ya kuelekea masaki na ndani ya dakika kadhaa walisimama kwenye jengo moja jeupe , huku juu likiwa na maandishi KENYA HIGH COMMISSION( ubalozi wa kenya ) .geti lilifunguliwa na gari ile iliingizwa ndani .
“Mtu uliemtafuta jana kwa simu yupo thailland , shika hii ni passport na hii ni visa ya kutoka kenya mpaka mpaka thailland , ukifika jomo kenyata airport usitoke nje utaunganisha safari na ndege ya shirika la emirates kwenda Thailland Bangkok itashukia suvarnabhumi International aiport ukitoka nje utakutana na mtu atakuja kukuchukua “.damiani alikuwa alijikuta akishangaa .
“ naweza kuuliza swali “.
“ uliza”
“kwanini niende thailland ?”.
“sijui hilo bwana damiani , hayo ni maagizo niliopewa tuh na nisha yakamilisha” aliongea na alionekana hakutaka maswali mengi ,damiani alijipa ujasiri na kutka nje ya gari , na waliingia ndani na walikutana na balozi wa kenya bwana joseph njoroge .
“Sir I have brought him “ aliongea akimanisha kwamba amemleta .
“ I think it will never happen again , if this known I will be in bad position “( nafikiri hili halitajirudia tena , likifahamika nitakuwa kwenye nafasi mbaya ).
“sir you will forgive us in this , we had no other choice “( mheshimiwa utatusamehe katika hili tulikuwa hatuna njia nyingine “. Waliongea na kisha damiani rasmi alikabidhiwa kwa balozi , bwana moja mmoja hivi mtu mzima mwenye umri kati ya miaka 50 kwenda juu , alikuwa ni moja ya watu waliokuwa wameridhika na maisha maana afya yake haikuwa haba .
Nusu saa baadae damaini aliingia kwenye gari moja na balozi huyo na kisha gari hio iliondolewa ., hakukuwa na mongezi Zaidi kwani muda mchache baadae walikuwa gongo lamboto .JULIUS NYERERE INTERNATIONAL AIRPORT (JNIA ).
Walipita kwa utaratibu maalumu kwa kuonyesha passport na hata kwa damiani hivyohivyo , ilikuwa ni mara yake ya kwanza kupanda ndege , baada ya kupita hatimae waliingia kwenye ndege binafsi , ndege hii ilionekana ilikuwa ikimilikiwa na balozi huyu bwana joseph njoroge , maana ukiachana na kupewa ubalozi lakini pia alikuwa ni moja ya wafanya biashara wakubwa nchini kenya .
Lisaa limoja na madakika walikuwa ndani ya uwanja wa kimataifa wa jomo kenyata , damiani ilikuwa mara yake ya kwanza kufika ndani ya nchi ya kenya.
“ wish you the safe journey , better remember this day “ aliongea balozi na damiani aliagana nae , kwa utaratibu ule ule alifanikiwa kupita na kupanda ndege na kwenda thailland ., .
Kijana damiani alikuwa ndani ya ndege ya shirika la emirates kwa mara yake ya kwanza , kwake ni kama mtu ambae hakuwa akiamini kile kinacho endelea katika maisha yake , lakini kila kitu anachokiona kilikuwa ni uhalisia , maisha yake kwa ujumla yalikuwa yamebadilika , hakujua sehemu aliokuwa akienda lakini aliendelea kujipa ujasiri , kwani aliamini kwa kuwapata watu waliokuwa wamemuua bruno , basi angeweza kulipiza kisasi , hio ilikuwa moja ya sababu kubwa iliokuwa ikimpa ujasiri , aliamini ilikuwa ni kazi ngumu , lakini kwakuwa alikuwa ni mtu ambae hakuwahi kukata tamaa katika maisha yake licha ya vikwazo mbalimbali alivyopitia , basi aliamini hakuna kitu cha kumruddisha nyuma .
Masaa kumi na sita ya kuwa angani hatimae walikuwa kwenye anga la mji mkuu wa Bangkok , abiria walilifiwa kufunga mikanda kwani ndege ilikuwa ikikaribia kutua ..
Dakika ishirini mbele kijana damiani alikuwanje ya uwanja wa ndege huo , uliojengeka kwa usanifu wa hali ya juu , alitembea mpaka nje kabisa raia wa thailland hawakuwa na habari nae , kila mtu alikuwa kwenye shughuli zake .
Baada ya kutoka kabisa nje hapo ndipo alpokutana na jamaa mmoja alivalia suti akiwa ameshika bango lililokuwa na jina lake ., alimsogelea na bwana yule alitabamu .
“ welcome in thailland damian “karibu thailland damiani .

INAENDELEA
 
KAULI YA MWISHO YA RAISI
KABLA YA KIFO
U-97
SEHEMU YA 17
BAADA YA MWAKA MMOJA NA MIEZI MITANO .
JNIA – DAR ES SALAAM
Ni nje ya mlango wa kutokea uliokuwa na maandishi ya kingereza ‘ARRIVAL’ jengo terminal three alionekana mwanadada merina akiwa anatoka ndani ya mlango huo huku akiwa ameshikilia begi akiwa analivuta kwamshikio wake kwa kutumia mkono wa kushoto huku kulia akiwa ameshima pochi , alikuwa amependeza kweli kwani siku hio alikuwa amevalia suti nyeupe na viatu va mchuchumio , huku machoni akiwa amevalia miwani ya jua .
“ my love “.
Ilikuwani sauti ya mwanaume ilio na besi lakini sio sana , ni mwanaume mmoja mtanashati alievalia tisheti nyeusi ya GUCCI ilio ambatana na koti ambalo hakuwa amelifunga vifungo , chini kabisa alikuwa amevaa kiatu cha ngozi aina rangi nyeusi kisichokuwa na Kamba huku akipendezesha Zaidi na saa ya gharama aliokuwa amevalia , hakuwa mwingine bali alikuwa ni Patrick mtoto wa raisi wa jamhuri ya muungano wa Tanzania wa kwanza .
“ ouh Patrick , umekuja kunipokea jamani “.
“ wewe si haukutaka kuniambia kama unarudi “.
“ hahaha .. asante lakini , najua mage ndio kakuambia “.
“ nimeotea , unazidi kuwa mrembo merina , nilikumiss sana .”
“ nilikumiss pia Patrick “.
Walisogea mpaka kwenye gari alilokuja nalo Patrick , ilikuwa ni gari ya kifahari sana aina ya benzi new model nyeusi Patrick alimsaidia kupandisha begi na kisha alimfunglia merina mlango na akaingia , waliingia barabarani na kutoweka eneo hilo la uwanja wa ndege , dakika kadhaa mbele walikuja kusimama masaki nje ya geti moja lililokuwa limenakshiwa na madini ya dhahabu ..
Gari iliingizwa mpaka ndani na kwenda kusimamishwa kwenye moja ya magari mawili ya kifahari yaliokuwepo hapo ndani na Patrick alitoka na kwenda kumfungulia merina mlango .
“ thank you “
“ your welcome my lady “ aliongea Patrick na kumfanya merina atabasamu .
Alimsaidia begi kulitoa kwenye gari na muda huo huo alitoka moja ya msichana wa miaka kama kumi na nane kwenda juu alievalia gauni la maua rangi ya pink na kwenda kumrukia shingoni merina .
“ sister I missed you so much “.
“ I missed you too , cha umbea wangu “.
“ hahaha … na utanikoma “.
Patrick aliwaangalia kitu na dada yake na kisha akatabasamu huku wakiongozana kuingia ndani wakati huo Patrick akiwa amebeba begi la merina .
“merina nishahakikisha umefika nyumbani nataka kuondoka sasa “ aliongea Patrick .
“jamani bro pat , mbona unawahi hivyo hutaki kukaa na mwali wako hata kidogo “ aliongea mage .
“mage chukua begi nipelekee chumbani kwangu “. Aiongea ili kumkatiza asiongee Zaidi ili pia apate nafasi ya kuongea na Patrick
“ pat thank you so much kwa kuja kunipokea airport “.
“ usijali merina and if you are , unaweza kunisindikiza kesho kwenye party ya mama na baba , wanafanya sherehe ya kutimiza miaka 25 ya ndoa yao “.
“ wow! Okey pat , then I think I will see you tomorrow ( sawa basi tutaonana kesho ).
Walikumbatiana kishikaji na kisha Patrick akaondoka , hapo kwa kasi huku akimuacha merina akimwangalia .
“Am so sorry pat , my whole heart is still with damiani , its been a year I haven’t seen him but not even one day did I forget him .(nisamehe sana pat moyo wangu wte umamjaa damiani , imepita mwaka mmoja sasa , sijamuona lakini hakuna siku hata maoja ambayo niliweza kumsahau “).
“ sis brother pat loves you so much “.
“ kwa hio ndio ukamwambia kama nakuja ?”.
“ mh! Yaani dada , mkaka wa watu anakupenda vyote hivyo lakini huonyeshi hata kumpenda , isitoshe ni handsome anapesa , pia ni mtoto wa raisi .”
“ mage hebu achana na hizo habari bwana “.
Upande wa Patrick baada ya kumchukua merina moja kwa moja alielekea nyumbani kwake , lakini ile anafika alipokea simu kutoka kwa CEO wa kampuni zake .
“boss kuna muwekezaji mpya kutoka marekani anataka kuonana na wewe kesho “.
“ mwambie aje next jumatatu kesho ninazo ratiba nyingi “ aliongea huku akikata simu .
“ merina utakuwa wangu tuh siku moja , unayemuwaza kila siku ashakufa n ahata kama akitokea sitoweza kumruhusu kuwa na wewe nitapigana kufa “ aliongea Patrick huku akivua kot lake na kulitupia kwenye sofa .
******
Siku ambayo merina anaingia nchini muda wa saa nne upande mwingine kwenye moja a hoteli zilizokuwa katikati ya jiji , eneo la mikocheni ITV hoteli iliokuwa ikijulikana kwa jina la krebby`s nje kabisa ya parking alionekana bwana mmoja mwenye nwele ndefu lakini zilizochanwa vizuri akiwa amevalia koti la rangi nyeusi na suruali ya kitambaa , na miwani ya jua , bwana huyo baada ya kutoka hapo parking aliingia moja kwa moja mpaka ndani upande zilipokuwepo lift na kubofya kitufe namba nne .
Muda mchache kidogo alikuwa kutokea kwenye floor namba nne iliokuwa na baadhi ya vyumba vya kulala , alinyoosha na corrido hio ndefu na kuja kusimama mbele ya mlango mmoja uliokuwa na maandishi ya ‘ meeting hall “. Alifungua mlango na kisha aliingia ndani,.
“ mister matinde karibu sana , ndio tuliokuwa tunakusubiria tuanze “. Ndani ya hall hio kulikuwepo na wanaume wanne , alikuwa ni bwana kizito kabwela IGP mstaafu , alikuwa ni mkuu wa polisi kanda maalumu ya Arusha ndugu sospeter kabwe , alikuwepo mkuu wa majeshi ya ulinzi bwana Abdallah na katibu mkuu mstaafu wa chama cha NLP (national liberty party ) hiki kilikuwa ni chama tawala .
“jamani nadhani ni mwaka sasa tokea tukutane , lakini naamini pia ni muda muafaka wa sisi kukutana , kwani mkuu wa nchi kwa sasa anaonekana kutulia na kufanya majukumu yake , lakini hilo ni swala la sisi tena kuamka “ aliongea matinde .
“ ndio bwana matinde nilipopokea uumbe wako kidogo nilishtuka maana haukuwa na jina la mtu zaidi ya kusema tukutane mahali husika na muda “.
“ ni kweli nadhani mnaelea tokea henry atustaafishe amekuwa ni mtu wa kutufatilia kwa kila tunachofanya ndio maana nikaona nitumie njia ya siri ili asije akagundua mipango yetu ”.
“ nadhani twende moja kwa moja kwa kile ambacho umetuitia hapa bana matinde “ aliongea kizito .
“ kwanza kabisa niwapngeze ka uzalendo wenu mpaka sasa wa kuhudumia taifa hili kwa kadri ya uwezo wenu na hata kipindi kigumu cha nyuma tulichopitia cha msiba hakumteteleka lakini kuna jambo sikuwaeleza tokea msiba a mheshimiwa bendera “. Aliongea mstaaafu wa TISS bwana matinde
“ jambo gani hilo bwana matinde ?”>
“ kuna waraka ambao mheshimiwa bendera aliuandika kabla ya kufariki siku yake kabisa ya mwisho “.
“ unahusiana na nini huo waraka na uko wapi mpaka sasa “ aliuliza Abdallah .
“ kuhusu kilichopo kwenye huo waraka mpaka sasa sijajua ni kitu gani lakini kwa taarifa ambazo sio rasmi kutoka kwa vijana wangu serikalini ni kwamba waraka huo una siri kubwa mno ambayo mheshimiwa ameiandika na pili sijui nani mpaka sasa anao huo waraka “.
Wote waliangaliana huku kila mtu akionesha kustaajabishwa na maneno alio ongea bwana matinde kwani yalikuwa ni mageni kwenye masikio yao.
“ mheshimiwa naomba ni kuulize , wewe ulijuaje swala hili la waraka , na je kuna chochote kinachohusiana na kifo cha mheshimiwa? “.
“ kama nilivyotangulia kusema kwamba ndani ya waraka huo haifahamiki ni kipi kimeandikwa , lakini kutoka kwa taarifa zilizonifikia ni kwamba mheshimiwa raisi mpaka sasa kuna kijana anamtafuta ambae anaaminika kukabidhiwa huo waraka “
“ kijana gani bwana matinde na inakuwaje kijana ambae hafahamiki awe na waraka wa raisi ?”
“ kwa taarifa ambao nilizo nazo ni kwamba waraka huo alikabidhiwa bruno japo sina uhakika , na bruno katika haua za mwisho za uhai wake alimkabidhi kijana mmoja ambae mpaka sasa anatafutwa kwa siri na TISS , kwani picha zake zimesambazwa kote nchini na majasusi wanamfatilia “.
“ kama ni hivyo kuna ajenda gani raisi anaificha ikulu na kwanini kijana huyo afuatiliwe na raisi , wakati mheshimiwa henry na raisi walikuwa ni kitu kimoja , huo waraka unamaslahi gani kwa raisi mpaka autake kwa nguvu zote ?”.
“ jamani nadhani yote mnayo sema hapa ni maswali lakini hakuna alie na majibu na mimi kwa haraka haraka naona suluhisho ya hayo maswali ni kujua huyu kijana ni nani aliekabidhiwa huo waraka tukishamjua , inabidi kuutafuta huo waraka na kujua kile kilichopo “ aliongea sospeter kabwe .
“ umeongea kweli lakini ugumu upo kwenye hilo swala , nafikiri wote tunajua kuwa danieli alifariki mwaka jana , sasa kwa taarifa za siri ni kwamba danieli alikuwa kwenye kumlinda huyo kijana mpaka kupoteza uhai wake na baada ya hapo kijana huyo bado hajafahamika mpaka sasa yuko wapi, lakini kubwa Zaidi ni kwamba carlos Cardoso yupo huru na kwa udhamini wa mfanya biashara kimboona ameweka ngome yake ya kigaidi ya kusaidia mtandao wa U -97 kuweka mizizi yake hapa nchini “
“ kwa hio agent danieli aliuliwa na nani ?”
“ kwa habari ambazo hazijathibitika ni kwamba inawezekana ni carlos Cardoso , mwanzoni tuliamini aliefanya swala hilo ni miss k ( suzzane ) lakini kwa uzoefu wangu na ninavyomjua danieli ilikuwa ni ngumu kwa suzzane kumuua danny kwani hakuwa level sawa na yake lakini Zaidi ya yote walikuwa wapenzi wa siri “..
“ kwa hio unamaanisha carlos Cardoso yupo huru na ndie aliehusika na mauaji ya Danniel , na huyu carlos Cardoso ni nani haswaa maana mpaka hapa mmeniacha mbali , aliongea mstaafu katibu mkuu wa chama na ni kweli alikuwa ameachwa mbali kwani hakuwa katika upande wa usalama wa taifa wala maswala ya ulinzi .
“ carlos Cardoso ni gaidi alietumwaga nchini kwa ajili ya kutekeleza mauaji ya bwana bruno lamberk na U-97 , lakini kupitia ushirikiano wa TISS , police na jeshi tuliweza kumdhibiti mapema Zaidi kabla ya kutekeleza mauaji hayo huku kupitia maagizo ya umoja wa mataifa (UN) tuliambiwa kumshikiria katika magereza ya Tanzania mpaka pale kutakapo kuwa na maagizo mengine kwani hawa ndio walitupatia intel ya ujio wa carlos nchini “ alongea matinde na kumfanya .
“ kwa hio swala hili linafahamika katika umoja wa taifa kama yupo huru “.
“ hapana kwani mpaka sasa taarifa hii ni siri mno ndani ya ikulu na gerezani “
“ kwa hio unashauri nini bwana matinde , naamini mpaka ukatuita hapa ulikuwa na mpango wako kichwani .” aliongea kizito
“ labda niwaambie tu kwamba kabla ya mheshimiwa kunistaafisha kuna operation ambayo ilikuwa ikifanywa na undercover agent nchini sudani , na operation hii sikuiweka katika majarada ya usalama wa taifa, hivyo baada ya kustaafishwa nilifanya mawasiliano na agents waliopo huko na niliabort operation na wote wakarudi nyumbani huku wakiendelea na maisha yao ya kawaida mpaka sasa ninavyo zungumza wapo wanaendelea na maisha yao , hivyo kwa hambo ambalo nimeona linafaa kwa sasa ni kuwarudisha viijana hawa kazini .
“ wapo wangapi mpaka sasa ?”.
“ kwa wale ambao hawajulikani kama wanausalama yuko mmoja , mmoja ndio anajulikana kama mwanausalama lakini anaendelea na maisha yake na huyu ni agent Z , ambae hafahamiki mpaka sasa huyu ni nurya.
“ kwa hio unawaamini hawa vijana wataiweza kazi vizuri ?” aliuliza kizito .
“ hakika kwa mafunzo yao wataiweza kazi vizuri tu bila shida yoyote “.
“ basi waingize kazini walifanyie swala hilo kazi tutambue alipo huyu kijana damiani kwa sasa na waraka huo aliopewa unakitu gani ndani cha kumfanya raisi asitulie “.
“ hilo limepita , lakini swala la pili ni kwamba ili kuifanya kazi hio lazima tuwe na pesa , sasa nilichowatia hapa kikubwa ndio hilo swala la pesa , nataka tuambizane katika hili ..
“ kwa hio unataka tusaidie vipi katiika hilo ?” aliuliza Abdallah .
“ hapa zipo njia mbili za kupata pesa , ya kwanza tujichange sisi wenyewe kama wazalendo , pili tutafite mfadhili ambae aatatusaidia katika hilo , lakini swala hilo la mfadhili lazima liwe la siri sana kufanyika .
“ mimi nadhani swala mfadhili ndio swala zuri zaidi , lakini changamoto itakuja ni nani anaweza akaaminika ambae akakubaliana na sisi katika kutafuta waraka huo kwa kutupa ufadhili , maana ukizingatia ni kwamba swala hilo sio rahisi .
“ matinde nadhani hilo kwa sasa uniachie mimi nitakusaidia katika hilo , nina connectiona na watu wakubwa wa makampuni , naweza shawishi mmoja na akaungana na sisi .” alkiongea kizito na wote wakakubaliana kumuachia kazi hio.
“ basi nafikiri hili la kuwafatilia hawa ma agent lifanyike mara baada ya kupara ufadhili “ .
“ ndio Abdallah litafanyika baada ya kuwa na uhakika wa pesa “.
“ nadhani hakuna haja tena ya sisi kukutana kwa sasa , baada ya bwana kizito hapo akifanikiwa katika kumpata mfadhili , matinde tawafatilia hawa ma agent na kuwapa kazi , siku tutakayo kuja kuonana iwe ni siku ambayo waraka huo umepatikana.
ITAENDELEA A KESHOO

MWENDELEZO NICHEKI WATSAOP 0687151346
 
KAULI YA MWISHO YA RAISI
KABLA YA KIFO.
UMOJA NAMBA TISINI NA SABA (U-97)
MTUNZI SINGANOJR
NO:0687151346 WATSAPP

SEHEMU YA 18
Ni muda wa saa moja kamili ndani ya hoteli ya serena hoteli , aliingia bwana mmoja hivi aliekuwa amevalia tisheti na miwani huku chini ya miguuu akiwa amevalia raba nyeupe na jeans , bwana huyu alionekana kidogo alikuwa na mwili wa mazoezi , alikuwa ni bwana mmoja mwenye asili ya kiasia kwani alikuwa akionekana kama mhindi hivi , basi alipita mpaka mapokezi pale na akamkuta dada mmoja ambae alikiwa bize kwenye tarakishi ila alivyoinua macho na kumuona aliinuka haraka haraka na kutabasamu kisha akamkaribisha.
"karibu sana kaka ".
" Nahitaji kadi ya chumba changu " Aliongea huku akiweka tabasamu kwa mwanadada huyo na mdada huyu wa mapokezi akamrudishia tabasamu kisha akatoa kadi na akampa na bwana huyu alishukuru na kisha aliondoka eneo hilo kuelekea lift , huku mgongoni akiwa amebeba begi lake kama yale ya watalii .

Siku hio kulikuwa na pilika pilika nyingi ndani ya hoteli hii , lakini kama ujuavyo hoteli hizi kubwa hata kama kuna sherehe kubwa kiasi gani mara nyingi haiwazuii wahudumu kutohudumia wateja wengine , na pia hakuna bughuza ya aina yoyote ile kwa wateja wengine , na hicho ndicho kilikuwa kikiendelea ndani ya hoteli hii kwani siki hio pia kulikuwa na maazimisho ya miaka 27 ya ndoa ya raisi wa jamhuri ya muungano iliokuwa ikifanyika eneo hilo .
Makachero walikuwa tayari washafika kuweka hali ya usalama katika hoteli hii na kuhakikisha hakuna kitu kinacho haribika , moja ya kiongozi mkuu wa makachero hao alikuwa ni suzzane aka miss k.
alionesha kuwapanga vijana wake vyema kwani haikuwa eneo la hotelini tu lakini pia mpaka kwa maeneno ya karibu pia usalama ulikuwa umeimarishwa .
Muda huo wageni mbali mbali waliokuwa wakihudhuria' party 'hio walianza kumiminika huku wengi wao wakiwa ni matajiri wakubwa ndani ya nchi hii , kwani magari yaliokuwa yakifika eneo hilo yalikuwa yakiashiria kuwa watu hao walikuwa na ukwasi ambao si haba .
Moja ya watu waliopendeza siku hio alikuwa ni merina , alieingia ndani ya jengo hilo akiwa ameongozana na patrick , hakika walikuwa wamependeza sana siku hio , kwani gauni jekundu alililovalia merina lilimfanya kuonekana kama malikia wa usiku huo , lakini haikuwa kwake tu hata kwa patrick pia alikuwa amependeza kweli kweli na suti yake ya maua maua .

ukumbi ulikuwa umependeza kweli kweli , huduma ilikuwa ya hali ya juu wahudumu walikuwa wakifanya kazi yao kwa weledi mkubwa sana kuhakikisha wanaacha alama kwa kila atakayefika mahali hapo kama moja ya njia ya kujitangaza ili.mtu pale anapokuwa na sherehe yake asikose kuja mahali hapo na kukodi ukumbi , hakika ilikuwa vyema sana kwani bilauli zilikuwa zimetapakaa kila kona huku na uwepo wa watu waliopendeza ndani hapo ,ukumbi ulinoga .

Muda wa saa mbili kamili , ndio muda ambao mheshimiwa raisi alofika eneo la parking , wageni ndani walikuwa tayari washaarifiwa ujio wa wenye sherehe yao kwa jio walikuwa wakipaswa kusimama kwa ajili ya kuwapokea , muda mchache baadae waliingia bwana henry na wema sufiani wakiwa wamependeza kweli kweli , suti aliovalia mheshimiwa raisi ilikuwa ni moja ya suri za bei ghali sana kutoka kwa kampuni ya kimarekani ijulikanayo kwa jina la tomford , lakini haikuwa kwenge suti tu kwani kiatu pia tai na vinginevyo vikikuwa vya gharama ya juu sana , upande wa mwanamama wema na yeye alikuwa amependeza kweli kweli siku hio na ilidhihirisha kabisa kwamba yeye ndie aliekuwa na sherehe yake , kwani gauni , viatu na cheni alizovalia ukijumlisha na uzuri ambao japo alikuwa mwanamama lakini haukuonesha kuchuja, hakika ulimfanya azidi kung`aa mbele ya macho ya kila mmoja , aliachia tabasamu ambalo liliwafanya watu wazidi kuwapigia makofi , huku na mshereheshaji na yeye hakuwa nyuma katika kutia sukari na chumvi ili mradi kuleta ile radha inayotakikana na kuifanya sherehe hio kuwa 'superb '.

Walitembea mpaka katikati ya ukumbi na kisha walianza kusalimiana na wageni waalikwa huku wakionesha furaha kubwa machoni pao .
" mom and daddy huyu nj merina she is more than friend to me , merina hawa ni wazazi wangu , baba ba mama yangu kipenzi " patrick alifanya utambulisho mara baada ya kufikiwa na wazazi wake . lakini utambukisho ule ulimfanya mwanamama mwenye sherehe yake kutoa macho mbele ya merina na haikujulikana ni kipi kilichomshangaza lakini alionesha kabisa kutotulia na kutofurahia utambulisho huo kwa wakati mmoja .
" Nashukuru sana kukutana na nyinyi , siku hii ya leo kwangu imekuwa heshima kubwa sana , niwape pongezi kwa kutimiza miaka ishirini na saba ya ndoa yenu " aliongea merina na kumfanya Henry atabasamu na kupokea sifa hizo kwa mikono yote .
" Patrick rafiki yako ni mrembo haswa ,naona una jicho la utambuzi kama mimi baba yako " Aliongea huku akimwangalia mke wake alieishia kulazimisha tabasamu .
" Merina karibu sana , na karibu siku moja ikulu uje utusalimie , nafikiri patrick utamleta mkwe wangu " aliongea raisi na kumfanya patrick atabasamu kwani aliona kabisa baba yake alikuwa akimpigia chepuo , basi walipita na kuongea na watu wengine , lakini kwa mke wa raisi alionekana kabisa kukosa furaha .

Mpangilio wa sherehe ulikuwa ni wa kisomi zaidi sana , kwani kila kitu kiliandaliwa katika mpangilio wa kueleweka , mshereheshaji na yeye hakuwa nyuma katika kuhakikisha kuwa sherehe hio inaenda kwa ratiba ilio pangwa kwani alikuwa akijua watu aliokuwa akiwasherehesha siku hio walikuwa ni watu wakubwa mno na wenye majukumu yao ya kikazi .
"Patrick ! ilikuwa ni sauti iliomfanya patrick aliekuwa bize kuongea na merina ageuke nyuma huku akiwa ameshikilia mvinyo wake kwenye glass .
" Sabi ! sikutegemea kama utafika , aliongea patrick kwa furaha sana .
" nilikuwa bize lakini nimeona nifike , wewe ni rafiki yangu mkubwa sana siwezi kukutenga katika mambo kama haya , isitoshe na mimi ni mpenda sherehe " .
" I know you , by the way huyu mrembo hapa ni merina , the one i told you about , merina huyu ni rafiki yangu sana tumesoma wote chuo anaitwa sabi " .
" Nashukuru kukufahamu sabi "
" Me too merina , you are gorgeos , hakika sifa alizonieleza pat zinakustahili " aliongea sab .

Alikuwa ni bwana mmoja hivi mrefu mweusi mwili wake ulikuwa sio mnene sana wala mwembamba sana , alikuwa amevalia suti nyeusi yenye nakshi za maua maua , huku nywele zake akiwa ameziweka mtindo wa pin on short.
"Simuoni rafiki yako ahmed " Aliongea sabi huku wakiwa tayari washakaa kwenye viti maana wakati wote huo walikuwa wamesimama.
" Yuko safarini nje ya nchi , angefurahi sana kukuona , maana its been a while since muonane " .
" yeah that is true , pia niliwish kumuona hapa ".
" Wadogo zako pia siwaoni ??".
" wako masomoni " .

Basi sherehe iliendelea na hatimae ikifikia kipengele cha mwisho cha raisi henry kuongea maneno machache ..
" Ladies and gentlemen , ninayo fuaraha kubwa sana siku hii ya leo kwa wote mliofika mahari hapa na kiacha usingizi wenu na hata wengine majukumu yao mkaja kuniunga mkono katika sherehe yangu hii ya maadhimisho ya miaka 27 ya ndoa yetu , ni upendo mkubwa sana mmeuonesha kwangu , lakini niseme kwamba tutaendelea kushirikiana kwa karibu sana ,najua eneo hili wapo wanasiasa wafanya baishara na wasanii na wengineo , basi niseme kwamba wote nyie na mimi ni ndugu na tutasaidiana katika kuhakikisha tunaendeleza uchumi wa taifa hili na maslahi ya wananchi kwa ujumla .akanyamaza baada ya watu kupiga makofi na akaendelea .
"Ukiachana na kazi yangi ya kuwatumikia watnzania lakini mimi pia ni moja ya binadamu ambao tumetokea kupenda kweli kweli kwenye dunia hii , namimi nataka nitoe tamko la kwamba nampenda sana mke wangu kipenzi , ni miaka ishirini na saba sasa tumepitia changamoto mbalimbali za kimaisha lakini mke wangu hakuniacha wala kuhudhunika , ila alikuwa bega kwa bega na mimi .Watu walipiga makofi na shangwe juu .
" Kutokana na mapenzi yangu kwake leo nimemzawadia gari iana ya prosche new model kabisa " .
Aliongea mheshimiwa na wema alifurahi sana kwani aliinuka na kukumbatiaja na mumewe , na baadae na yeye akapewa maiki aongee .
" Mabibi na mabwana , nashukuru sana kwa uitikiaji wenu kufika mahali hapa , kama alivyosema mume wangu huenda wengine mngekuwa mmelala , na wengine mngekuwa mnajiandaa kwa majukumu yanayo wakabili lakini mmekuja mahali hapa , niseme kwamba asanteni sana kwa upendo wenu " Makofi na akaendelea .
" Mimi kama mwanamke niseme kwamba naipenda sana familia yangu , kuanzia mume wangu , patrick , jestin na jackline , japo watoto wamgu hawapo hapa ila nawapenda sana , mwisho niseme asante sana mume wangu kwa zawadi ulionipa nakupenda sana " watu walinyanyuka na kuanza kupiga makofi .
Sasa wakati hayo yanaendelea , nje kabisa ya ukumbi kulionekana kifaa aina ya drone ikipiwa mita kadhaa kutokea kwenye dirisha la ukumbi huo , na haikujulikana kimefikaje kwani suzzane na timu yake walikuwa wameimarisha ulinzi kila kona , drone ile baada ya kufika usawa maalumu ilisimama na kuanza kuscan na kuweka target na ilionekana ilikuwa ikitaka kumlenga raisi .
“ mister president get down " ilikuwa ni sauti kubwa ilioshitua watu lakini hapo hapo risasi kutoka kwenye ile drone ilipita , na kilichowaacha watu mshangao ni damu zilizotapakaa juu ya jukwaa huku raisi akiwa chini .
Suzzane alikimbilia mpaka kwenye dirisha huku akikoki bastora yake , na alitumia risasi moja tuh kuichangua drones ile na ikaenda chini , wageni walikuwa kwenye mshituko wa hali ya juu huku wengine wakikimbia , na wengine kulala chini .

Upande mwingine ndani ya hoteli hio hio alionekana bwana mmoja tuliemuona masaa machache akiingia ndani hapo na kuchukua ufunguo , bwana huyu akionekana kwenye chumba chake akiwa amelala kitandani huku akiwa ameshikilia tablet ya samsung , alionekana kutabasamu .
Dakika chache baadae alisikia ving`ora vya magali vikiingia ndani ya eneo hilo , aliinuka kutoka kitandani na wakati huo alikuwa kifua wazi tuh alisogelea dirisha na kuangalia magari yaliokuwa yakiingia hapo na mengine ya wanausalama kutoka ,alitabasamu kisha akachukua simu yake aina ya i phone na akatafuta namba na kupiga .
" boss my mission is done " .( boss misheni uangu tayari )
" welldone enjoy the view mpaka nitakapo kupa maelekezo mengine " ilisikika sauti nyingine upande wa pili
" okey boss ".
" Mister president are you okey ! , ilikuwa ni sauti ya suzzane baada ya kumfikia raisi ."
" nipo sawa suzzane " aliongea raisi kwa waswasi akimkagua mke wake aiekuwa amejikuyata kwa woga , huku upande mwingine alionekana kijana sabi akiwa anavuja damu begani , kwani alikuwa amejeruhiwa na risasi na hio ni mara baada ya kumwambia mheshimiwa alale chini na yeye alifyatuka na kwenda kuikinga risasi ile na ikampiga begani na damu zikatapakaa eneo hilo .
Suzzane alijikuta akivuta pumzi kwani roho yake ilikuwa juu mno

INAENDELEA ....
 
KAULI YA MWISHO YA RAISI
KABLA YA KIFO
U-97
BY SINGANOJR

SEHEMU YA 19
" Suzzane nimekasirishwa sana na uzembe mliofanya leo , yaani adui anataka mpaka kunidhuru nyie mpo , ni ulinzi gani mlioimarisha " Aliongea mheshimiwa henry na alikuwa amekasirikia mno na tukio la kushambuliwa kwa risasi katika sherehe yake .
" nisamehe sana mkuu , ni swala ambalo hatukulitegemea kabisa kutokea , kwani ulinzi ukikuwa wa hali ya juu " .
" unazungumza ulinzi gani , wakati kama sio yule kijana sasa hivi huenda ningekuwa marehemu , hii ni mara yako ya pili kuniletdown suzzane , ulishindwa kumkamata damiani akiwa mikononi mwako mpaka sasa hatujui alipo , lakini leo tena umeshindwa kudhibiti timu yako kutoa ukinzi mpaka adui anakuja kurusha drone na kutaka kuniua , unajua ni fadhaa gani leo nimeipata mbele ya wale wageni " .
" Siku nyingine nitakuwa makini mkuu , halitajirudia tena " aliongea suzzane .
" suzzane unanichanganya nenda tu kaendelee na majukumu yako , swala kama hili likijirudia kwa mara ya pili kazi huna " aliongea raisi na suzzane alitoka huku akiwa amevimba kwa hasira , alienda mpaka kwenye chumba kilichokuwepo timu yake na ile anaingia alimsogelea mwanaume mmoja na kumlamba ngumi ..
" unajua ni kiasi gani leo nimedhalikika , tulikuweka nje na timu yako kuhakikisha hakuna kitu kinachosogelea eneo la ukumbi lakini ukatuangusha mpaka raisi anataka kuuwawa , ulikuwa ukifanya ninj ???.
" Nisamehe boss nilikuwa makini kuangalia eneo la ukumbi muda wote lakini sikuweza kuiona drone kabisa ".
" suzzane alimwangalia mwanaume huyo kwa hasira na kuwageukia wengine waliokuwa kwenye fadhaa kubwa , alitoka na kuingia kwenye gari huku akionekana mwenye hasira kali , aliendesha gari lake mpaka hotelini pale alishuka na kuonyesha kitambukisho chake na kuzunguka nyuma ya tukio lilipo tokea .
" mtu aliefanikisha tukio hili ni mtaalamu mkubwa sana na kuna uwezekano drone hii haikutoka mbali na hapa bali ni humuhumu hotelini " alijiwazia suzzane na kisha akaelekea ndani ya hoteli hio , alifika mapokezi na kutoa kitambulisho na akaruhusiwa kwenda kwenye ukumbi ule .
Alifanya uchunguzi huku kuna baadhi ya mambo aliyagundua kwani hisia zake na kutumia mafunzo mbalimbali ya kiupelelezi aliweza kung`amua kuwa drone ile ilitokea katika moja ya vyumba vilivyokuwa humo ndani , lakini sasa swali lilikuwa ni chumba gani haswa?? .
Alitoka na moja kwa moja alielekea mapokezi na kuomba watu wanaohusika na camera , alipewa muongozo na kisha alipelekwa mpaka kwenye camera .
“ nataka unionyeshe kwenye corrido ilio na vyumba vinavyokaribiana na ukumbi “ aliongea suzane na mtaalumu yule alifanya kazi yake na dakika moja alikuwa ashapata video hizo , aliangalia kwa umakini mkubwa sana .
“ simamisha kwenye huyo kaka wa kihindi , hebu jaribu kuivuta hio picha karibu “ aliongea suzzane na jamaa huyu alikuwa ni yule tuliomuona akiongea na simu kwamba misheni amekwisha imaliza . suzzane aliangalia mpaka kwenye chumba alichoingia huyu jamaa na kisha ni kama mtu aliemtilia shaka , japo hakukua na ushahidi , lakini katika watu wote waliokuwa wamechukua vyumba karibu na kumbi huo aliemtilia shaka ni huyo mmoja .
“ nataka kumjua mtu aliechukua chumba namba 86 “ aliongea suzzane mara baada ya kufika mapokezi .
“ anaitwa seyd ally “ aliongea yule dada pale mapokezi .
“bado yupo kwenye chumba chake ??”.
“ ndio atakuwa yupo “ aliongea yule dada kiugawoga na suzzane hakutaka kuchelewa alitoka na kurudi juu kwenye kile chumba huku akitoa bastora yake na kuishika mkononi , baadhi ya watu alio waona walimshangaaa na wengine kuogopa , lakini hakuwajali .
Baada ya kufika mbele ya ule mlango , alijiandaa kwa kugonga mlango huku akijitayarisha kuingia ndani , aligonga kama mara tatu hivi lakini hakuna aliefungua , jambo ambalo lilimkasirisha , alirudi mpaka chini na kuchukua kadi yakufungulia , lakini ile anatoka kwenye lift alikosa umakini na kujikuta akigongana na mwanaume mmoja mrefu saizi ya kati alievalia kinadhifu kabisa huku mkononi akiwa ameshika tablet ya sumsung .
“ sorry “ aliongea suzzane kisha akapita hakusubiri hata kusikia kama mwanaume huyo kakubali msamaha wake, huku yule jamaa alimwangalia kwa nyuma na kisha alitabasamu na kuendelea kuingia kwenye lift kuelekea juu , alichukua kadi ya ziada na kisha alirudi mpaka kwenye mlango ule na kwa tahadhari kubwa aliweka kadi na mlango ule ukafunguka , alizama kama simba huku bastora ikiwa ipo tayari kwa shambulio lolote lile , lakini hali ya chumba ilimchekea kwani hakukua na mtu wa aina yoyote ile , chumba kilikuwa hakina mtu alizunguka chumba kizima kwa tahadhari , lakini hakuona mtu , aliangalia mezani na kukuta box lililotengenezwa kwa makaratasi kama dice flani hivi , lilikuwa lipo juu ya kimeza cha kiooo , alilichukua na kisha alilifungua .
“GOOD TRY SUZZANE by mzalendo “ suzzane alijikuta akisoma maneno hayo yaliokuwa yameandikwa kwenye karatasi ile , alichoka kwa mshangao , na hapo ndipo alipo amini kwamba mtu aliehusika kwa tukio zima la kutaka kumuua raisi alikuwa akilala kwenye chumba hicho , alighafirika sana kuona kuwa mtu huyo alikuwa akimjua yeye kwake hilo lilikuwa ni kama tusi , na moja ya vitu ambavyo suzane hakupenda kwenye maisha yake ni kutukanwa kwake swala hilo aliona ni kama udhalilishaji wa hali ya juu .
“ seyd ally “ aliongea huku aitoka kwenye chumba hicho , lakini ile anatoka , chumba cha pembeni alitoka yule mwanaume aliegongana nae akielekea upande sawa na wake kuelekea lift zilipo huku akiwa ameshikilia pombe , na wakati huu alikuwa amevaa pensi .
“ vipi mrembo , kumbe wewe ni jirani yangu , what coincidence “ aliongea bwana yule na kumfanya suzzane amwangalie bwana yule alieachia tabasamu lake huku meno yake yaliokuwa yaking`aa kuonekana nje Zaidi ukijumlisha na ngozi nyeusi ya bwana huyu , vilimfanya aonekane HB Zaidi , lakini kwa suzzane hakuwa hata na time nae maana akili yake muda hio ilikuwa ikiwaza kitu kimoja tu mwanume aliekuwa akiitwa seyyd ally .
“ endelea na mambo yako “ aliongea suzzane na kupita na kumfanya bwana yule aendelee kutabasamu huku akimwangalia kwa nyuma .
*******
Ilikuwa ni siku nyingine kabisa muda wa asubuhi siku ambayo ilikuwa imeamka na habari za raisi kutaka kuuwawa(assassination attempt) katika hoteli ya serena , habari hizo zilikuwa zimesambaa katika vyombo vya habari kila kona ya nchi huku kila mtu akiwa na maoni yake juu ya tukio hilo , kuna waliolaumu ulinzi unaomlinda raisi kuwa ni legelege , lakini pia kuna waliokuwa wakimsifia aliefanya tukio hilo kuwa jamaa alikuwamtaalamu wa hali ya juu kwani kuingia sehemu ambayo ilikuwa ikilindwa na makachero haikuwa jambo la wepesi , kwani lilikuwa jambo la kuhitaji ujasiri wa aina yake ;
Siku hio ndani ya ikulu raisi alikuwa na hasira kweli , kwani tukio lililotokea lilimpa fadhaa kubwa sana ndani ya moyo wake , kila akikumbuka tukio lile aliona kabisa mtu aliehusika na tukio hilo alikuwa ni mtu hatari sana na anaweza akamfanyia mashambulizi mahali popote pale na kumuua , hali ya kauoga ilichanganyikana na hasira kwa wakati mmoja .
Wakati akiendelea kuwaza hili na lile , aliingia suzzane aliekuwa ameongozana na mkuu wa TISS
“ pole sana mkuu kwa matukio yaliokukuta jana , nilipata taarifa kupitia vyombo vya habari na nikaona nifike ofisini hapa kabla hata sijaingia ofisini kuendelea na majukumu yangu “ aliongea bwana yusuph , lakini kabla hata hajaendelea aliingia mkuu wa majeshi bwana abdallah khalifa alietangulizana na na IGP bwana anisethi kanyama .
“ pole sana mkuu , tumeona sisi kama wadau wa ulinzi swala hili ni nyeti sana , na linagusa taifa kwa ujumla wake , majirani zetu mpaka sasa wanatuona ni wa hovyo sana kwa kilichotokea jana .
“ ni kweli kabisa muheshimiwa swala hili lazima lichunguzwe kwa umakini mkubwa sana na inawezekana hata hawa secret service agent kuna anaehusika na tukio hili , kwani nilijaribu kupitia formation ya ulinzi katika eneo lile nimegundua ulikuwa ni wa hali ya juu , na ilikuwa sio rahisi hata kwa panya kukatiza asionekane , lakini hili swala mpaka sasa linaniumiza kichwa “ aliongea yusuph .
“ kwangu mimi pia nitukio ambalo kama sio kijana alienikinga kwa risasi huenda nisingekuwa hai mpaka muda huu “.
“ huyu kijana ni nani muheshimiwa , na ilikuwaje mtu wa pembeni akakukingia risasi wakati una bodigadi afande chizzo alikuwa wapi “.
“ chizo nilimpa ruhusa ya kukaa mita kadhaa nyuma yangu kwani kama unavyojua nchi yetu, nilikuwa nikiamini haikuwa na matukio kama haya kwa hio niliamini usalama wangu ulikuwepo na ndio maana nika mdismiss chizzo “ aliomgea muheshimiwa.
“ suzzane umefikia wapi na uchunguzi ?“ aliuliza yusuph .
“ mkuu nimegundua muuaji alikuwa ametumia chumba namba 86 kukamilisha tukio lake la assassination atempt , nilimfatilia kwa njia ya camera na tumeweza kugenerate picha hizi hapa , kwa mujibu wa taarifa za data base ya taifa ni kwamba huyu bwana alijisajili hotelini pale kwa jina la seyyid ally , lakini hilo halikuwa jina lake halisi kwani kwa mujibu wa data base ya taifa , kwa kutumia face recognition system nikwamba kijana mwenye hio sura ni ridhiwani abubakar ni mwanafunzi wa chuo cha IFM .
“ unataka kumaaisha kwamba mwanafunzi wa IFM ndio aliehusika na tukio hilo? “.
“ tumefanikiwa kumkamata ridhiwani na kwasasa tupo nae , lakini kwauchunguzi wa mwili wa ridhiwani na huyu bwana aliejitambulisha kama seyyd haviendani kwani ridhiwani tofauti na sura yake kufanana lakini mwili wake ni mwembaba na hata tembea yake haiendani na ya ridhiwani kabisa .
“ swala hilo linawezekana vipi suzzane ,, kama sura yake imeonekana ni ya ridhiwani kwanini mwili na viungo vingine viwe vya mtu mwingine? .
“ mkuu hilo ni swala ambalo mpaka sasa tunalifatilia kwa ukaribu ili kujua , lakini Zaidi mtu aliefanya tukio hilo ndani ya chumba alichotumia nimekuta karatasi hii hapa “. Aliitoa na kumkabidhi raisi na kuisoma , na kisha alishangaa Zaidi .
“ inaonekana mtu aliefanya tukio hili ni mtu ambae anatufahamu sana nje ndani , na inawezekana tukio hili lilipangwa kwa muda mrefu sana “
“ uyazungumzayo ni ya kweli muheshimiwa , mimi naona swala hili ni la kufanyia upelelezi wa hali ya juu sana ili kujua muhusika ni nani ili tuweze kumkamata la sivyo tatazidi kudharaulika na mataifa ya nje kwamba hatuwezi kumlinda raisi wetu “ aliongea mkuu wa majeshi na kisha waliagana .
*****
Ndani ya kituo cha polisi cha magogoni ndani ya chumba cha mahojiano , alionekana kijana mmoja akiwa anatoa machozi mfululizo huku mbele yake wakiwa wamesimama police wakimuhoji , alikuwa ni bwana mmoja mweye muonekano sawa kabisa na yule tuliemuona pale hotelini serena kabla hata ya sherehe kuanza .
“ridhiwani abubakar si ndio jina lako? “.
“ ndio ni jina langu afande “.
“ unajua kwanini upo mahari hapa ?”. aliuliza sergeant manyusi huku akiwa hana hata chembe ya masihara .
“ sijui afande nimeshangaa nimekamatwa kutoka chuoni na kuletwa mahali hapa “.
“okey vipi jina lako la seyyd ally , umeacha kulitumia ?”
“ seyyd ally ndio nani afande simjui mtu huyoo .
“ unauhakika sio jina lako? “
“ ndio afande , mimi mmenileta hapa kwa kunifananisha na mtu mwingine “.
“ jana ulikuwa wapi muda wa saa moja mpaka saa saba usiku .
“ jana tulienda club mpaka saa nne nne hivi nilipata mwanamke nikaenda nae getto mpaka asubuhi nilipokuja kukamatwa na kuletwa mahali hapa
“ club gani ulienda ??”
“U-97 “ aliongea na kumfanya manyusi ashangae .
“ unamanisha hio casino inayopatikana upanga au kuna nyingine?? “.
“ ndio ni hio hio , unaweza hata ukapata taarifa zangu pale “ aliongea na kumfanya manyusi awaangalie wenzake aliokuwa nao hapo ndani .
“ wewe kwenu ni wapi ?”.
“ mwanza mheshimiwa “.
“ baba yako anafanya kazi gani “.
“ ni injinia anakampuni yake inaitwa wado constructor .
“ unamaanisha bwana wado ndio baba yako ?” aliitika kwa kichwa na manyusi hakuuliza swali lingine alitoka hap ndani akifuatwa na wenzake.
“ vipi taarifa alizozitoa ni za kweli kama ulivyomhoji yule mwanamke ?”.
“ ndio ni za kweli “.
Wakati wanafika kwenye ofisi ya sergeant walimkuta suzzane kaka kwenye kiti akiwa ana wasbiri .
“ vipi suzzane ?”
“ safi tu manyusi , nimefata ripoti”.
“ kwakweli ridhiwani anaonekana hahusiki kabisa katika hili , maelezo yake yalikuwa yakweli kwa asilimia mia , kwani jana muda wa tukio yeye alikuwa U-97 cassino “.
“ unamaanisha alikuwa U-97 ?”
“ ndio , vipi unaonekana kushituka , kuna jambo ambalo umegundua?s “.
“ hapana nashukuru manyusi kama kuna lingine nitakutafua , ila kwa sasa usimuachie mpaka nitakapo toa ruhusa hio , kuna uchunguzi unapaswa kufanyika “ aliongea suzzane na kisha alitoka ndani hapo huku akiwaacha wenzake katika mshangao .

ITAENDELEA
 
KAULI YA RAISI KABLA YA KIFO.
UMOJA NAMBA TISINI NA SABA.
MWANDISHI :SINGANOJR.

SEHEMU YA 20

Wakati wanafika kwenye ofisi ya sergeant walimkuta suzzane kaka kwenye kiti akiwa ana wasbiri .
“ vipi suzzane ?”
“ safi tu manyusi , nimefata ripoti”.
“ kwakweli ridhiwani anaonekana hahusiki kabisa katika hili , maelezo yake yalikuwa yakweli kwa asilimia mia , kwani jana muda wa tukio yeye alikuwa U-97 cassino “.
“ unamaanisha alikuwa U-97 ?”
“ ndio , vipi unaonekana kushituka , kuna jambo ambalo umegundua?s “.
“ hapana nashukuru manyusi kama kuna lingine nitakutafua , ila kwa sasa usimuachie mpaka nitakapo toa ruhusa hio , kuna uchunguzi unapaswa kufanyika “ aliongea suzzane na kisha alitoka ndani hapo huku akiwaacha wenzake katika mshangao .

INENDELRA

SEHEMU YA 20
Wakati hayo yakiendelea upande mwingine , alionekana mwanadada merina alievalia suti yake akitoka kwenye gari yake ya bei ghali aina ya AUD ndani ya parking iliokuwa na jengo kubwa refu kwenda juu , aliingia kwenye lift hio huku akiwa ameshikilia mkoba wake na akabonyeza kitufe namba saba na kisha lift ilimchukua mpaka kwenye floor iliokuwa na maandishi makubwa ukutani SWIFT TRANSIT LIMITED (STL).
Alitembea mpaka mapokezi na kusalimiwa kwa heshima zote na moja ya mdada ambae alikuwa akihusika na eneo hilo , na baada ya kusalimia wafanyakazi wengine kama ilivyokuwa tabia yake tabia ambayo ilimfanya apendwe na kila mfanyakazi , moja kwa moja alienda mpaka kwenye ofisi yake iliokuwa ikisomeka kwa juu CEO office .
Ilikuwa moja ya ofisi ‘pambe’ ndani ya jengo hilo , kwani ilikuwa na mpangilio unaovutia kweli na uliendana na uzuri aliokuwa nao merina , alijikuta akipumua baada ya kuketi kwenye kiti chake huku akigeukia upande wa kioo kilichokuwa kikimuonesha nje kabisa ya jiji , picha ya tukio la raisi kutaka kupigwa risasi lilikuwa halijampotea machoni kabisa , alikaa hivyo kwa muda huku akionekana kuwa kwenye mawazo , lakini alikuja kushitushwa na simu ya mezani .
“ boss kuna mgeni wako anahitaji kuonana na wewe ila hayupo kwenye orodha ya watu wanaotaka kuonana na wewe “
“ kasema ana shida gani ni ya kikazi au personal?? “
“ kasema ni personal lakini inakuhusu zaidi wewe “ aliongea secretary na merina alijiifikiria kwa sekunde na kisha alimwambia amruhusu .
Aliingia ofisini hapo bwana mmoja mwenye nywele ndefu kidogo nyeusi mwenye sura nyeusi kabisa kama watu wa njombe , mwenye sura yake isiokuwa ikivutia sana lakini pia haikuwa ikikera sana , alikuwa ni bwana mmoja mwenye mwili kidogo ulio jengeka na wenye afya nzuri alikuwa amevalia suti iliomkaa vyema mwilini .
“ karibu sana “ aliongea merina baada ya kuona mgeni huyo alionekana kuwa mtu mzima na aliemzidi umri .”
“ asante sana binti “ aliongea na kisha aliketi huku akimwangalia merina usoni na kusoma jina la slab iliokuwa inajina la ‘MERINA SOSTENES CHIEF EXECUTIVE OFFICER ‘ ni kama mtu ambae alikuwa akimpembua merina kwani kuwa mkuu kabisa kwenye kampuni kubwa kama hio halikuwa jambo dogo .
“ kwa majina yangu naitwa kizito kabwela ,mimi ni inspector general police (IGP ) mstaafu , nadhani haujawahi kuniona mahari .
“ ni kweli sijawahi kukuona ni mara yangu ya kwanza kukuona , karibu sana inspector”. Aliongea marina kwa adabu
“ asante sana , kama nilivyosema kwamba shida ilionileta hapa sio ya kikampuni , nataka niende moja kwa moja kwenye point yangu ya msingi ilionileta “ aliongea kisha akatoka bahasha aliokuwa ameshikilia mkononi na kuiweka mkononi huku merina akiwa amekaa kwa kujiamini kabisa akisubiria kuambiwa kile a ambacho bwana huyo alikuwa amekileta .
Alitoa picha tatu kwenye ile bahasha na akamkabidhi merina , ambae alijikuta akipatwa na mshituko wa hali ya juu , kwani picha ya kwanza ilikuwa ikimuonesha damiani , picha pili ilikuwa ikimuonesha akiwa hospitalini akiwa anamlilia damiani baada ya kutekwa kwake , na picha ya tatu alionekana akiwa kituo cha polisi lushoto mjini , bwana kizito alimwangalia mwanadada huyo alivyokuwa ameshituka na kumfanya atabasamu .
“ kwanini umeniletea picha hizi inspector? Aliuliza merina huku akiwa anajikaza kuto onesha mshituko wake waziwazi pasipo kujua kuwa tayari kizito keshamsoma .
“nadhani kabla ya kujibu swali lako nataka nifahamu kama umezitambua picha hizo ?”.
“ ndio nimezitambua inspector ndio nataka kujua dhumuni haswa la kuniletea picha hizi “.
“ hukondio ninakoelekea , na kwanza ni kwambie sina nia mbaya ya kukuletea picha hizi , kama ilivyokuwa kazi yangu kabla ya kustaafu kazi iliokuwa ikinihusha kulinda raia na mali zao , basi siku nilivyopata kusimuliwa mkasa huu wa kijana damiani na moja ya marafiki zangu kutoka kituo cha polisi lushto swala hili lilinigusa mno , kama lilivyokugusa wewe mpaka kumtolea machozi huyu kijana hivyo hata mimi pia lilinigusa , lakini nilikuwa kwenye nafasi ambayo tayari sikuwa na ule wezo wangu wa dhamani wa kulifatilia swala hili kwani nilikuwa nishakwisha kustaafu tayari , nadhani ulipewa taarifa kamili ya kijana damiani pale kituoni ?”.
“ ndio nilipokea afande , ilikuwa ni ya kuhudhunisha na nilijaribu kufatilia ile mwishowe nilikata tamaa , na mpaka sasa ni moja ya matukio ambayo tayari nishakwisha yakatia tamaa na kuyafuta katika kichwa changu , ndio maana nasema nataka kujua sababu haswa ya kuniletea picha hizi “
“ dhumuni langu kubwa ni kukusadia kumpata kijana damiani , mimi kama mmoja ya watu walioguswa na historia yake nataka kujua ni wapi damiani alipo kwani swala hili linanikosesha kabisa usingizi “.
“ kama unataka kumtafuta damiani kwanini unasema kwamba unataka kunisaidia ?”.
“I know this boy how he is important to you but just as he is important to you for me his story has touched me deeply and I need to know where he went , who kidnapped him , so after seeing these picture I came to know that you were one of his close associate , for me i thought it was the wisiest thing to do if we would get together to find out where he is”
“ najua ni kwa jinsi gani kijana huyu alivyo muhimu kwako , lakini kama alivyo kuwa muhimu kwako kwangu mimi historia yake ya maisha imenigusa sana na nahitaji sana kujua kwa sasa kijana huyu yuko wapi ni nani amehusika na kumteka , kwa hio baada ya kuona hizi picha niligundua kuwa wewe ulikuwa ni moja ya watu wake wa karibu japo sikujua ukaribu wenu ukoje , lakini niliwaza na kuona ni jambo la busara kama nitakushirikisha kama tunaweza saidiana kujua ni mahali gani kijana huyu yupo kwasasa “
Aliongea bwana kizito kwa kingereza maneno ambayo yalimgusa sana merina , merina hakujua ni wakati gani machozi yalikuwa yakimtoka , kwani kila akikumbuka mambo aliombiiwaga kuhusu damiani , yalikuwa yakimuumiza mno katika maisha yake , alikuwa akitamani sana kujua ni wapi damiani alipo lakini hakuwa na uwezo huo , kwani polisi wenyewe hawakuwa na majibu hivyo kwake pia alikosa mwanga.
“ so how do you want me to help you to find him?, beacause the police themselves are still stuck in their investigation “
“ kwa hio unataka mimi nikusaidiaje kwani polisi wenyewe wameshindwa na wamekwama katika uchunguzi wao “.
“ do you think they have failed ?, polisi wanamkono mrefu sana na hawawezi shindwa kwenye jambo kama hili “
“Unataka kumaanisha nini ??”
“ merina wewe ni bint mdogo na katika umri wako huo umefanikiwa kufika katika mafanikio ulio nayo sasa , mpaka kuona machozi yako nimejua ni kwa jinsi gani unampenda huyu kijana , lakini nataka nikwambie jambo moja, ni kwamba swala hili sio la kawaida kutokea ni swala ambalo huenda kwa namna moja ama nyingine wahusika wakawa ni hao hao polisi ama walio juu yao ,hivyo ili kufanikiwa kupata kujua ni wapi kijana huyu alipo lazima tutumie watu walio nje ya serikali “.
Hapo ndo merina alianza kuunganisha matukio na alijikuta akianza kuona kweli kulikuwa na ukweli katika maneno ya bwana kizito , kwani alikumbuka maneno ya kila siku aliokuwa akiambiwa na polisi wa lushoto yalikuwa akionesha kabisa hakukuwa na uchunguzi uliokuwa ukiendelea bali alikuwa akizungushwa tu .
“ kwa hio unataka nisadieje inspector nahitaji sana kumuona damiani tena na kujua ni wapi alipo .” aliongea merina na hpo kizito alitabasamu .
“ tunahitaji kutumia wana usalama wabobezi katika swala hili , lakini ili tuweze kufanikiwa lazima tuwe na pesa ya kutosha kuwalipa na mahitaji mengine yatakayo jitokeza wakati wa upelelezi , hivyo kwakuwa kampuni hii ni kubwa tunaomba kampuni itufadhili kwa siri sana hata serikali isijue “.
“ inspekta kwanza nashukuru kwa moyo wako wa kutaka kujua ni wapi kijana damiani alipo , kuhusu swala la pesa sio lazima kampuni iwafadhili kwani ninazo pesa za kutosha nitawafadhili mimi mwenyewe “ aliongea merina na hapo ilikuwa ushindi kwa kizito .
Walikubaliana na merina na kisha kizito aliondoka ofisini hapo huku akimtaarifu matinde hatua aliokuwa amefikia , na swala hilo lilipokelewa na matinde kwa furaha kubwa na kumuambia sasa kazi iliobaki ni ya kwake kuwaingiza vijana kazini.
*******
Patrik japo siku hio alikuwa ofisini lakini mawazo yake hayakuwa sawa hata kidogo , kila akifikiria tukio lililotokea weekend alijikuta akiogopa sana , kwani katika maisha yake hakuwahi kuwaza baba yake anaweza kuwa na maadui wanao weza kumfanyia tukio kama lile , alijaribu kuwaza biashara zote za mzee wake na hata pia kwa baadhi ya wanasiasa lakini hakuweza kumuhisi mtu ambae anaweza akawa adui na baba yake , kwani katika maisha yake aliamini baba yake alikuwa ni mtu mpenda haki sana , siku hio hakutaka kabisa kuonana na mtu , kwani alitoa maagizo kabisa kwa secretary wake asiruhusu mtu yoyote kuingia ofisini kwake .
Wakati akiendelea na kuwaza na kuwazua mara mlango wake ulifunguliwa na alieingia hapo alikuwa ni CEO wa moja ya kampuni zao( subsidiaries) aliekuwa akijulikana kwa jina la stivini mrema .
“ boss! ,sasha kanambia huhitaji kuoanana na mtu lakini imenilazimu kuingia kwani kuna jambo la muhimu sana lililonileta hapa “ aliongea kijana huyu machachri kabisa kwa kujiamini huku akimwangalia boss wake ambae aligeuza kitu na kumwangalia .
“ kaa bwana steve “.
“ boss kwanza pole kwa yaliomkuta mheshimiwa raisi “
“ asante sana , nadhani twende kwenye swala lililokuleta steve “.
“ kuna muwekezaji kaingia hapa nchini na tayari kesharuhusiwa na waziri wa viwanda na mpaka sasa ninapo zungumza ni kwamba tayari ashapata vibari vyote , kilichonifanya kinilete kwako nikwamba anawekeza kwenye maswala ya mawasiliano kama ilivyo kwenye kampuni yetu , lakini huyu bwana kwa aidia aliokuja nayo anasema ataweka mtandao wa 5G nchi nzima .” aliongea steve na kumfanya Patrick akae vizuri kwani habari hio ilimshitua .
“ kama ni hivyo itatupelekea kupoteza nusu ya mapato ya kampuni , na ni swala ambalo litaiyumbisha kampuni kama ataruhusiwa katika swala hilo “. Aliongea Patrick
“ ndio maana nikaja tuone ni jinsi gani tunafanya kulizuia jambo hili “.
“ huyo mwekezaji ni nani na anatkea nchi gani ?“.
“ni luang shu kutoka china na kwa taarifa za haraka haraka ni kwamba ni mtoto wa waziri wa mambo ya ndani wa china .
“ luang shu ???,kama ni mtoto wa waziri itakuwa ngumu kumzuia kufanya biashara hapa nchini “.
“ ni kweli kabisa , lakini swala kubwa Zaidi ni kwamba kiwanda anachotaka kutumia na ambacho amepewa ni cha marehemu bruno lamberk kutoka kurasini na kasema ana nyaraka zte zinazomuwezesha kukichukua kiwanda hicho na kukiendeleza kihalali katika kusuka mitambo yake ya 5G.
“unataka kusema nini kiwanda hiki si kilikuwa kipo chini ya mahakama mpaka pale mwenyewe atakapo tokea inakiuwaje akawa na nyaraka hizo ?”.
“ hilo ndio swala ambalo mpaka sasa sijajua , ila kwa taarifa nilionayo nikwamba kapitia vipengele vyte vya sheria na mahakama nidio ilioidhinisha kwa bwana luang shu kutumia kiwanda hicho “.
Patrick alijikuta akitetemeka kwani swala hilo hakulitegemea kabisa , kiwanda hicho alikuwa akikitegemea mno na aliamini katika kukitumia kiwanda hicho angeweza kupata siri zote za kitechnolojia zilizokuwa zikitumiwa na bwana bruno , hivyo alimuomba baba yake amuwezeshe kutumia kiwanda hicho lakini jibu alilopewa ilikuwa ni kusubiri mchakato wa mahakama uishe, sasa leo hii anasikia kuwa kiwanda kishamilikishwa kihalali kwa mtu mwingine .
“f***ckk , ngoja niongee na baba huenda hajui swala hili “ aliongea Patrick huku akionesha kuwa na hasira sana na swala hilo kwani alikuwa ameguswa penyewe
ITAENDELEA .
 
KAULI YA MWISHO YA RAISI KABLA YA KIFO
U-97
MTUNZI :SIMGANOJR

SEHEMU YA 21
MAWASILIANO 0687151346



ILIPOISHIA
“ luang shu ???,kama ni mtoto wa waziri itakuwa ngumu kumzuia kufanya biashara hapa nchini “.
“ ni kweli kabisa , lakini swala kubwa Zaidi ni kwamba kiwanda anachotaka kutumia na ambacho amepewa ni cha marehemu bruno lamberk kutoka kurasini na kasema ana nyaraka zte zinazomuwezesha kukichukua kiwanda hicho na kukiendeleza kihalali katika kusuka mitambo yake ya 5G.
“unataka kusema nini kiwanda hiki si kilikuwa kipo chini ya mahakama mpaka pale mwenyewe atakapo tokea inakiuwaje akawa na nyaraka hizo ?”.
“ hilo ndio swala ambalo mpaka sasa sijajua , ila kwa taarifa nilionayo nikwamba kapitia vipengele vyte vya sheria na mahakama nidio ilioidhinisha kwa bwana luang shu kutumia kiwanda hicho “.
Patrick alijikuta akitetemeka kwani swala hilo hakulitegemea kabisa , kiwanda hicho alikuwa akikitegemea mno na aliamini katika kukitumia kiwanda hicho angeweza kupata siri zote za kitechnolojia zilizokuwa zikitumiwa na bwana bruno , hivyo alimuomba baba yake amuwezeshe kutumia kiwanda hicho lakini jibu alilopewa ilikuwa ni kusubiri mchakato wa mahakama uishe, sasa leo hii anasikia kuwa kiwanda kishamilikishwa kihalali kwa mtu mwingine .
“f***ckk , ngoja niongee na baba huenda hajui swala hili “ aliongea Patrick huku akionesha kuwa na hasira sana na swala hilo kwani alikuwa ameguswa penyewe

INAENDELEA SEHEMU YA 21.
WIKI MOJA NYUMA
Ndani ya uwanja wa kimataifa wa mwalimu nyerere ilitua ndege ya shirika la ATCL na moja ya abiria alietoka katika ndege hio alikuwa ni bwana mmoja hivi aliekuwa kijana kabisa kwani mwili wake haukuwa mnene wala mwembaba ila bwana huyu alionekana kuwa ni mtu anaefanya mazoezi , bwana huyu baada ya kukaguliwa na kuonyesha passport yake alitoka mpaka sehemu ya kuchukulia mizigo na alichukua begi lake na kutoka kabisa nje ya uwanja , huyu bwana alikuwa ni mchina kabisa kwani rangi yake na hata sura yake na ongea yake ilikuwa ikifanana kabisa za wachina .
Baada ya kutoka kabisa nje ya uwanja aliona mwanamama mmoja mweupe alievalia wigi mweupe, umri wake ulikuwa ni makadirio ya miaka 40 kwenda 5 hivi .
“ miss Rebecca “ alitamka bwana huyu maneno hayo kwa lafudhi yake ya kichina .
“ luang shu you are welcome in Tanzania , I think its your first time in this country “
“ karibu sana Tanzania nafikiri ni mara yako ya kwanza kufika katika taifa hili “
“its true rebbecca and just by looking I can tell Tanzania is a very beutifull nation .”
“ ni kweli Rebecca lakini kwa kuangalia tu naweza sema Tanzania ni moja ya mataifa mazuri sana “. Rebecca alimuongoza bwana huyu mpaka kufikia kwenye gari moja aina ya AUD A3 SEDANI ilioneka imetumika lakini uzuri wake haukupotea .
“ baada ya kutoka pale bwana huyu alipelekwa moja kwa moja mpaka hoteli ya golden tulip iliokuwa ikipatikana msasani pembeni ya barabara ya seokoe toure drive , basi gari ile iliingizwa kwenye moja ya maegesho yaliokuwepo ndani ya hoteli hio na Rebecca alitoa begi la bwana luang shu na kisha waliongozana kuingia ndani ya hoteli hio .
Rebecca alienda mpaka mapokezi na kisha alichukua kadi kwani tayari alikuwa ashabook chumba , na waliongozana na bwana huyo mpaka kwenye chumba chake na wote waliingia ndani .
“ thank you rebbecca “ aliongea luang shu .
“ “ I think now you have to rest , tomorrow I will come with a lawyer for the purpose of reviewing the contract and steps to take to get the factory “.
“ Nafikiri unapaswa kupumzika sasa , kesho nitakuja na mwanasheria kwa ajili ya kupitia mkataba na hatua za kuchukua kupata kiwanda “
“Okey rebbecca”
Kesho yake ilivyofika rebbecca alifika hotelini hapo akiwa ametangilizana na bwana mmoja ambae alikuwa na ndevu nyingi huku mkononi akiwa amebeba briefcase , , walipita mapokezi na moja kwa moja walifika kwenye chumba cha luang shu na kugonga na bwana huyu alionekana alikuwa tayari ashaamka kwani alikuwa amebadilisha mavazi tayari na kuwa nadhifu .
“ hellow Rebecca morning “ aliongea luang shun a kuwakaribisha .
“ luang shu as I saidi yerstarday I wiil bring lawyer , this is mr juma bakari he is lawyer , juma this is luang shu son of the chinese interior minister and he is here for investing in telecommunication business but as I mentioned , years ago they signed a contract with bruno lamberk for the purchase of an existing factory in kurasini .
“ luang shu kama nilivyokuambia jana kwamba nitamleta mwanasheria , huyu ni bwana juma bakari ni mwanasheria , juma huyu ni luang shu mtoto wa waziri wa mambo ya ndani wa china yupo nchini kwa ajili ya kuwekeza katika maswala ya biashara ya mawasiliano , na kama nilivyosema kwamba kampuni ya luang shu nchini china walisaini mkataba na bruno lamberk ili kununua kiwanda kilichopo kurasini .
Basi walisalimiana na kisha bwana juma alipewa ule mkataba na aliupitia kwa umakini kubwa kwa kila kipengele .
“ hati inayo onyesha malipo yamekwisha fanyika iko wapi ?” aliuliza juma na luang shu alitoa hati ile na kumuoesha .
“ okey kwa ushahidi huu ni sawa kabisa kusema wewe ni mmiliki halali wa kiwanda kilichopo kurasini , lakini kwakuwa mali za bwana bruno mpaka sasa zipo chini ya serikali na mahakama basi kuna hatua ambazo nitapitia ili kuhakikisha unapata haki yako “ aliongea juma na kisha waliagana
Siku mbili mbele bwana luang shu alikabidhiwa rasmi kiwanda kilichopo kurasini , kiwanda ambacho kilikuwa kikihusika na utengenezaji wa vifaa vya electronics , na baada ya kupewa kiwanda hichi bwana luang sh alifata taratibu zote za kiwizara pamoja na kubadilisha jina la kiwanda hicho na kuweka wazi anataka kufanya biashara gani .
Mwana mama aziza kibwetere waziri wa viwanda alitia saini karatasi zilizowasilishwa ofisini hapo na luang shu , pamoja na Rebecca .
*****
Mara baada ya suzzane kutoka kituo cha magogoni moja kwa moja alienda mpaka ikulu na kuomba kuonana na muheshimiwa na aliruhusiwa na kuingia .
“vipi suzzane ??.
“ mheshimiwa ridhiwani kwa maelezo yake inaonekana hahusiki kabisa na kile kilichotokea pale serena ,lakini kwa maeneo aliokuwepo yananipa shaka “
“ unamaanisha nini suzzane kusema maeneo aliokuewepo , kwani ni maeneo gani aliokuwepo ?”
“ kwa maelezo ni kwamba muda wa saa moja alikuwa ndani ya U-97 cassino “ aliongea .
“ ndio kama alikuwa kwenye U 97 ulikuwa wataka kumaanisha nini hapo mpaka upatwe na shaka? “.
“ mkuu jambo ninaloliwaza, nataka kwanza kulifanyia uchunguzi nione kama ni kweli hisia zangu zipo sahihi na ndipo nitakuja kuekueleza kwa undani , lakini kama unavyo jua kuwa hatuna mamlaka ya kufanya upekuzi ndani ya U-97 swala hili linakuwa gumu kwangu , hivyo kwa ruhusa yako nataka nipate kibali cha kuingia ndani ya U- 97 CASSINO “ aliongea suzzane
“una uhakika jambo unalotaka kufanya, je litatupeleka mpaka kujua ni nani muhusika ?”
“ ndio muheshmiwa I m positive about it “
“ okey unaweza kwenda nitawasiliana na meneja wa casino na akuruhusu lakini hakikisha hakuna kibaya kinacho tokea kwenye ile casino kwani its beyond my reach “.
“ sawa mheshimiwa “ aliongea suzzane na kisha aliingia kwenye gari yake aina ya brevis na kisha alitoweka ikulu na kuelekea upanga ambako U-97 cassino ilikuwa ikipatikana , muda huo ilikuwa ni saa nane mchaana wakati akiingia eneo la casino hio , alienda mpaka mlangoni na kujitambulisha kisha aliruhusiwa kuingia .
Ebwana eeh kuna watu walikuwa wanafanya dhambi , kilichokuwa kinafanyika ndani ya casino hio ilikuwa sio mchezo , kulikuwa na kila aina ya ufuska , wadada mbali mbali walikuwa wakitembea uchi wengine walikuwa wakinyonya ‘rungu’ , kuna waliokuwa wakicheza Kamari , lakini ndani pia ya casino hilii kulikuwa na ofisi na zilionesha hizo ofisi zilikuwa zikitumika kwa ajili ya kazi za kutia mikataba , kwa wale waliokuwa wakicheza Kamari mezani kulikuwa na pakti za madawa ya kulevya , mwanga uliokuwa humo ndani haukuwa tofauti na usiku , kwani ulikuwa na giza na mwanga wa taa za kuvutia za rangi , suzzane hakuwa mgeni sana ndani ya casino hii
“ nahitaji kuonana na muongoza camera wa hapa ndani “ aliongea suzzane akimwambia meneja wa casino bwana mmoja alivalia kipensi huku akiwa ameshhikilai sigara yake kubwa aina vasobranie black russians, ilikuwa ni moja ya sigara ghali sana .
Meneja yule kwa ishara alimruhusu suzzane na kwenda upande wa camera .
“ nahitaji matukio ya jumapili kwanzia muda wa saa kumi na moja jioni “ aliongea suzzane na kuonyeswa na vijana hao wa IT , alianza kuangalia watu waliokuwa wakiingia ndani ya casino hilo , alijikuta akitabasamu baad aya kuona sura aliokuwa akiitafuta , sura hii ilikuwa ni ya ridhiwani na hata miondoko yake ilikuwa ni ya kijana ridhiwani na alionekana aliingia hapo casino saa kumi na mbili kama na nusu hivi , suzzane aliendelea kuangalia baadhi ya picha na hapo kuna sura ilimvutia Zaidi aliomba waikuze , hii ilikuwa ni ya mwanaume aligongana nae ndani ya hoteli ya serena usiku wa jana yake jumapili na hata kumjibu vibaya na mtu huyu alionekana aliingia ndani ya casino hilo kwenye muda wa saa kumi na moja za jioni .
“ rudisha , peleka mbele kidogo , kuza hio picha “ aliongea suzzane na alifanyiwa kama alivyo elekezwa na hapo ndipo alipo tabasamu kwani aliona kuna mwanga., alikuwa ni ridhiwani akitoka , lakini ridhiwani huyu alikuwa akitofautiana na ridhiwani alieingia , alimuona bwana huyu akiingia kwenye gari aina ya crown yenye namba XXX za gari na ikaondoka eneo hilo .
“ alingalia watu waliotoka saa nne kamili usiku , hapo ndipo alipomshuhudia ridhiwani akitoka na mwanadada na kuondoka eneo hilo na huyu alikuwa ni ridhiwani mwenyewe “.
Aliendelea kutafuta karibia camera zote lakini kuna sura aliona mara moja tu ikiingia lakini sura hio haikutoka kabisa , huyu alikuwa ni mwanaume aliekutana nae serena hoteli .
“ okey asanteni nilichokuwa nikikitafuta nimekipata “ aliongea na kisha kuondoka .
“ yule mwanume mweusi aliekuwa akinisemesha ndio kahusika lazima , lakini nawezekanaje akawa na sura ya ridhiwani , nitajua baada ya kumtia mikononi yule “ aliongea suzzane na kisha akawasha gari lake na kwenda mpaka serena , alisimamisha gari na kisha alienda hadi mapokezi na kutaja shida yake
“ kama aliingia ndani ya ile casino na hakuonekana kutoka basi anaweza akawa ni huyo alietoka na sura ya ridhiwani , japo sijui kama jambo hili linawezekana lakini hsia zangu zinaniambia hivyo “ aliwaza muda huo akifika mapokezi .
“ nataka taarifa za mgeni chumba namba 85 aliongea suzzane na kisha bwana mmnoja wa kiume aliekuwa hapo mapokezi alitaka agome , lakini baada ya kuoneshwa kitambulisho alifanya kazi hio .
“ jina lake ni DAMIANI RABANI “.
“ DAMIANI RABANI “ aliongea suzzane na kumfanya apatwe na mshangao ,
“ nataka kwenda kwenye chumba chake, ashaondoka au yupo??”
“ taarifa hapa zinaonesha hajarudisha chumba “ aliongea kijana yule na suzzane aliomba kadi ya ziada na akapewa na kisha alielekea mpaka kwenye kile chumba , baada ya kufika kwenye mlango wa kile chumba alitoa siraha yake na akagonga mlango , lakini hakukua na majibu , alichokifanya ni kuweka ile kadi na kisha akafungua mlango na kwa tahadhari ya hali ya juu alijirusha ndani , alkini alikutana na chumba kikimchekea , kwani hakukuwa na mtu , lakini kwenye kijimeza kulikuwa na box lililotengenezwa na karatasi , aliliangalia , lakini hisia zilimwambia kulikuwa na mtu bafuni , alienda kwa tahadhari ya hali ya juu na kufungua mlango , lakini holla .
Chumba hakikuwa na mtu kabisa . alienda mpaka kwenye meza na kuchukua lile box na kulifungua
GOOD TRY SUZZANE by mzalendo

KESHOOOOOOO........
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom