Ujasusi na uongozi: Mafanikio ya rais Putin katika kuirejesha tena Urusi

herikipaji

JF-Expert Member
Aug 23, 2016
1,198
1,344
Mafanikio ya Urusi kwa sasa inayoongozwa na rais mwenye misimamo thabiti aliyekuwa KGB wa zamani Vladimir Vladimirovich Putin ni yakushangaza kwa wengi hasa western block USA na allies wake wa NATO.

Urusi hii nchi ina historia yake ndefu sana na ya kuvutia kwenye vitabu vya historia kwa wale wanaopenda kusoma vitabu ukitafuta utaipata hapa sitaweza kueleza hata humu jamvini wadau wengi wameandika.

Kiufupi miaka ya hivi karibuni ilipitia katika misukosuko ya kiuchumi na kuifanya USA iwe inatamba kwa mikogo na majigambo lukuki na hii misukosuko ilianzia mwanzoni mwa miaka ya 1990 mara baada ya vita baridi kumalizika na kupelekea kusambaratika kwa USSR.
USA na allies wake walichukulia hilo kama ushindi mkubwa sana kwao kwani waliamini huo ni mwisho wa zile nguvu kubwa za Urusi.

Sasa akatokea huyu mtu anaitwa Vladimir Vladimirovich Putin KGB wa zamani ambayo sasa inajulikana kama FSB hawa ni majasusi wa Urusi, aliapa kuiongoza Urusi kuwa na nguvu kubwa kijeshi, Urusi yenye nguvu kubwa na taifa lisiloyumba kiulinzi na kiusalama kuilinda Urusi dhidi ya maadui hasa USA na NATO.

Ameshafanya mengi na amepata mafanikio makubwa katika uongozi wake hadi sasa NATO wanashangaa imekuwaje hawa watu wanakuja tena?(Coming back of Russians.)
Lakini mafanikio na misimamo isioyumba ya uongozi wa Putin vimejengwa kwenye misingi ile ya ujasusi wake aliupata kule KGB, yani uongozi wake upo kiujasusi ujasusi.

Naamsha mjadala tu hapa kuwa kuna uhusiano upi kati ya ujasusi na uongozi hasa tukijenga hoja zetu kwa mfano wa rais wa Urusi Putin.
Majasusi wengi hutumia akili za kiwango cha juu kwenye kazi zao na wanakuwa wazalendo ingawa sio wote mimi huwa nafikiria pia ingesaidia sana hata marais wa hizi nchi maskini za kiafrika wapitie mafunzo ya ujasusi ili kuamsha akili na uzalendo na hatimaye kuongoza mataifa yao na kuushinda umaskini uliokithiri.


Wakuu mwaonaje haya mambo, karibuni kwa hoja.
 
Ni kweli kabisa ujasusi ni muhimu katika uongozi.lkn ndugu yangu nikwambie tu hawa wengi unaowaona kuwa ni viongozi wengi wanatokea tiss mfano h.polepole ni mtu wa tiss totally p.makonda kadhalika.shida ni vipaumbele vyao wanawaza watawale ili watajirike lkn si kwa manufaa ya nchi.yapo mengi kwa leo inatosha.
 
Putin alichokifanya 2016 kasaidia Russia kupata influence kiasi flani katika mashariki ya kati kwa kitendo cha kusimama na Bashir Al Asad hadi mwisho.

Marekani pia ameweza ku'influence election to his favor. Ulaya vyama pinzani vingi vyenye mrengo wa kulia inasemekana kavikopesha mabilion ya pesa. Hii itasaidia Russia kuondolewa vikwazo vya uchumi hapo baadaye endapo vyama hivi vya upinzani vikiingia madarakani.

Huko Marekani Trump ameshaahidi kuondoa vikwazo ambavyo tayari Russia amewekewa endapo akishaapishwa January 20.

Bottom Line ni kwamba Putin kasaidia Russia kuirudisha kwenye influence katika siasa za kimataifa.

Ila kiuchumi na nguvu za kijeshi bado Russia ipo katika hali mbaya sana. Ni Super Power in terms of military superiority waliyo nayo katika nuclear bombs lakin kwa technological sophstication na uwezo wa kiuchumi bado sanaaaaa.
 
Ni kweli kabisa ujasusi ni muhimu katika uongozi.lkn ndugu yangu nikwambie tu hawa wengi unaowaona kuwa ni viongozi wengi wanatokea tiss mfano h.polepole ni mtu wa tiss totally p.makonda kadhalika.shida ni vipaumbele vyao wanawaza watawale ili watajirike lkn si kwa manufaa ya nchi.yapo mengi kwa leo inatosha.
Ok nimekuelewa una maana hawa ulowataja pamoja na kuwa huko lakini bado wamekosa uzalendo yani ni wachumia tumbo tu mkuu
 
Putin alichokifanya 2016 kasaidia Russia kupata influence kiasi flani katika mashariki ya kati kwa kitendo cha kusimama na Bashir Al Asad hadi mwisho.

Marekani pia ameweza ku'influence election to his favor. Ulaya vyama pinzani vingi vyenye mrengo wa kulia inasemekana kavikopesha mabilion ya pesa. Hii itasaidia Russia kuondolewa vikwazo vya uchumi hapo baadaye endapo vyama hivi vya upinzani vikiingia madarakani.

Huko Marekani Trump ameshaahidi kuondoa vikwazo ambavyo tayari Russia amewekewa endapo akishaapishwa January 20.

Bottom Line ni kwamba Putin kasaidia Russia kuirudisha kwenye influence katika siasa za kimataifa.

Ila kiuchumi na nguvu za kijeshi bado Russia ipo katika hali mbaya sana. Ni Super Power in terms of military superiority waliyo nayo katika nuclear bombs lakin kwa technological sophstication na uwezo wa kiuchumi bado sanaaaaa.
Mkuu kwenye uchumi ni upo sawa hali ya Urusi sio nzuri sana kiuchumi lakini kwenye military tech hapa natofautiana nawewe.
Alichokifanya Putin na ndiyo kipaumbele chake ni millitary modernization hapa wamelifanya jeshi lao kuwa imara lenye uwezo mkubwa kuanzia majini, nchi kavu na angani.
wamefanya upgrade ya silaha zao submarines, heavy bomber&fighter jets, tanks, air defence systems.

Kama wangekuwa weak hata wasingeweza kurusha missiles kutoka umbali zaidi ya 2500 kms pale Caspian sea ile si kila nchi inaweza tena kwa kutumia light little warships.

Na lile tukio lina maana gani?
Walitaka kutuma ujumbe kuwa sasa Warusi wanaeza kushambulia na kufika kila kona ya dunia kwa urahisi zaidi kutoka Urusi hawana haja ya kujenga millitary base nyingi na hili linapunguza gharama na kujilinda zaidi na zaidi.
Pia asilimia kubwa ya tech ya wachina wanategemea Urusi yani China bila Urusi itatetereka pia.

Wamewekeza sana kwenye millitary tech sababu wanaamini maadui wao wameapa kuivamia na kuiangusha Urusi pale tu watapokuwa na uwezo huo.
Maadui hao wanashindwa kuivamia sababu tu wanaona hawatoeza ila kama Urusi wangekuwa hawana sophisticated millitary tech tungekuwa tunazungumza mengine hapa.
 
Urusi amepeleka jeshi lake siria tu anahangaika, mwenzake marekani yupo na amsha amsha karibu nchi sita lkn mambo hayayumbi
 
Ni kweli kabisa ujasusi ni muhimu katika uongozi.lkn ndugu yangu nikwambie tu hawa wengi unaowaona kuwa ni viongozi wengi wanatokea tiss mfano h.polepole ni mtu wa tiss totally p.makonda kadhalika.shida ni vipaumbele vyao wanawaza watawale ili watajirike lkn si kwa manufaa ya nchi.yapo mengi kwa leo inatosha.
Kama TISS ina hadi akina makonda basi ndo maana hadi sasa hatujielewielewi kama taifa
 
40 Reactions
Reply
Back
Top Bottom