Ujasusi na uongozi: Mafanikio ya rais Putin katika kuirejesha tena Urusi

Acha uoga na ulimbukeni, hicho kitabu kiko out of print huwezi kipata duka lolote, humu ndani hatuchunguzani, kama ni kazi unayoifanya basi ni wewe na siku ukitatizwa na ninachokisema au kukiandika, rejea kwenye ID yangu, ambayo ni jina langu halisi, nanimeweka picha yangu halisi, sina uoga na ninachokiandika wala kukisema humu, wewe kinachokuogopesha ni nini wakati kitabu chenyewe kilikuwa huru kununuliwa na mtu yeyote, huwezi kukifanananisha na Shadow World/Animal Farm au Satanic Verses, hiki hakijawahi kuwekewa pingamizi sehemu yoyote duniani kasoro Russia.
Haya ndugu
 
Niliwahi kumuuliza askari mmoja kutoka scandinavia kuhusu uwezo wa urusi hasa kijeshi na uwezekano wa USA na NATO kuivamia na kuishambulia alinambia ulaya na USA wakimvamia mrusi vita hiyo huenda itaisha baada ya miaka mitano na cjui mshindi ni nani ila akanambia ikitokea bahati mbaya mrusi akashindwa kujizuia akatumia nuclear basi ulaya magharibi itafutwa na USA ilishapangiwa siku nyingi ni miji gani ya kuteketezwa strategically kwa atomic bombs pia alinambia urusi hana story sana huwa hana propaganda ktk vita aliongeza kuwa ktk uzoefu urusi anauzoefu wa kupigana na mataifa makubwa tena kwa kumchangia lakini hajawahi shindwa kijeshi! Akanambia pia kuwa kwa uelewa wake USA, NATO hawana uwezo wa kumvamia mrusi na mataifa mengi ya NATO wanamfaham vizuri mrusi ndo maana kila wakati wanatafuta namna ya kuidhoofisha nchi hii kiuchumi ili asitulie ktk kuunda silaha za maangamiz ila alisema wamechelewa.
 
Wewe ndio wale mlio someshwa enzi zile kwa misaada ya kisovieti? Hapo Syria tu mrusi anatolewa kamasi kaaingia kichwa kichwa katika mtego wa wayahudi. Nato wamembeshesha yeye na uturuki zingo la kinyesi.

Na washawasha!


Niliwahi kumuuliza askari mmoja kutoka scandinavia kuhusu uwezo wa urusi hasa kijeshi na uwezekano wa USA na NATO kuivamia na kuishambulia alinambia ulaya na USA wakimvamia mrusi vita hiyo huenda itaisha baada ya miaka mitano na cjui mshindi ni nani ila akanambia ikitokea bahati mbaya mrusi akashindwa kujizuia akatumia nuclear basi ulaya magharibi itafutwa na USA ilishapangiwa siku nyingi ni miji gani ya kuteketezwa strategically kwa atomic bombs pia alinambia urusi hana story sana huwa hana propaganda ktk vita aliongeza kuwa ktk uzoefu urusi anauzoefu wa kupigana na mataifa makubwa tena kwa kumchangia lakini hajawahi shindwa kijeshi! Akanambia pia kuwa kwa uelewa wake USA, NATO hawana uwezo wa kumvamia mrusi na mataifa mengi ya NATO wanamfaham vizuri mrusi ndo maana kila wakati wanatafuta namna ya kuidhoofisha nchi hii kiuchumi ili asitulie ktk kuunda silaha za maangamiz ila alisema wamechelewa.
 
Hivi kwenye bible taifa kenye nguvu la magharibi ni lipi maana mnaota mchana kuwa siku USA apigwe
 
NIngependa usome kitabu cha The Death Of The Dissident, utakipenda sana na utakubali ambition aliyokuwa nayo Putin tangu kijana.
==============
Reviews
Nicholas Blincoe noted that the book is really a memoir by the former Russian dissident Alex Goldfarb who is an employee of Boris Berezovsky. Blincoe points out the problem, that "if everyone, including Goldfarb, is in Berezovsky's pay, there are no disinterested accounts, only potential apologists for his world-view." Blincoe further asserts that the fact that Berezovsky was the mastermind behind Putin's rise to power is evidence that no KGB-sponsored coup d'état took place - contrary to what was claimed in the book
Death of a Dissident | Wikiwand
------------------
Mkuu naweza kupata pdf yake ? nimetafuta mtandao nimekosa, ni PM !
 
Putin na Urusi wamefanikiwa sana kwenye kurudi kwenye siasa za dunia ila kwenye uchumi na technology bado sana. Putin kwa kuwadhibiti wapinzani wake na media amefanikiwa kuilisha dunia propaganda kuwa kila kitu kiko sawa kinyume na ukweli wenyewe.

Hata kijeshi nguvu za Urusi hazipo kwenye sophisticate military welfare bado anaamini katika jeshi lenye watu wengi wenye ujuzi duni. Mataifa mengi yaliyoendelea wanawekeza pesa nyingi kwenye R & D ya silaha na teknolojia za kivita za hali ya juu, hii ni pamoja na kuendesha vita kwa staili nyinginezo zikiwamo za kucontrol mind za wengine na silaha nyingine za kuathiri mienendo ya kibinadamu.

Kiuchumi hatuhitaji kuzungumza sana Urusi ana hali mbaya kupita maelezo. Unavyoona duniani watu wanarace kupigania rasilimali Afrika na kwingineko halafu yeye katulia si kwamba ameridhika na pesa, hana pesa ya kuwekeza huku.

Move mbovu aliyofanya ni kuweaken private sector nje ya Gazprom uwezo wa kufanya uwekezaji wa maana nje ya Urusi hana.
===========
Usifuatilie Western Media pekee kupata ukweli juu ya nguvu za Urusi. Tafuta Ukweli kote kote!
 
alipokuwa na miaka 16 alienda makao makuu ya KGB na kuomba kujiunga. wakamwambia wao ndiyo hufuata watu. akawauliza ni kozi gani itammsaidia kujiunga, wakamwambia sheria na chuo kweli alisomea sheria. mbongo leo ukienda makao makuu ya TISS unaweza chezea vitasa.


Mbongo bhanaaa hawajaribiwi kabisa.
 
Mm
Urusi amepeleka jeshi lake siria tu anahangaika, mwenzake marekani yupo na amsha amsha karibu nchi sita lkn mambo hayayumbi
Mmarekani anapo introduce jesh katk nchi,, mara nying ni kwaajilo ya uporaji wa resources kwa mwamvuli wa kutuliza ghasia na mengineyo..don't trust them that much
 
Ujasusi wa Tanzania ni wa kuhujumu Upinzani.
Kiwanda cha Matairi ya general tyre kilikufa kutokana na uzembe wa Tiss. ATC halikadhalika
Wakiriport tu kazini file la kwanza wanalokutana nalo ni chadema na tundu lissu na si kwann vyakula na bidhaa muhimu kwa mtanzania viko juu sana wakati tuko ktk kipindi cha mavuno....

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Putin alichokifanya 2016 kasaidia Russia kupata influence kiasi flani katika mashariki ya kati kwa kitendo cha kusimama na Bashir Al Asad hadi mwisho.

Marekani pia ameweza ku'influence election to his favor. Ulaya vyama pinzani vingi vyenye mrengo wa kulia inasemekana kavikopesha mabilion ya pesa. Hii itasaidia Russia kuondolewa vikwazo vya uchumi hapo baadaye endapo vyama hivi vya upinzani vikiingia madarakani.

Huko Marekani Trump ameshaahidi kuondoa vikwazo ambavyo tayari Russia amewekewa endapo akishaapishwa January 20.

Bottom Line ni kwamba Putin kasaidia Russia kuirudisha kwenye influence katika siasa za kimataifa.

Ila kiuchumi na nguvu za kijeshi bado Russia ipo katika hali mbaya sana. Ni Super Power in terms of military superiority waliyo nayo katika nuclear bombs lakin kwa technological sophstication na uwezo wa kiuchumi bado sanaaaaa.
watu wapo..hongera
 
Man will fly through the power of his mind , not the strength of his muscles" huu ni msemo maarufu sana nchini Russia Putin ni kati ya viongozi wachache sana wenye kipaji cha matumizi makubwa sana ya akili ktk uongozi wake na katika kuiendea dunia soon Trump will take orders from Putin
Russia bado ah tazidi kumtesa USA
 
Mkuu kwenye uchumi ni upo sawa hali ya Urusi sio nzuri sana kiuchumi lakini kwenye military tech hapa natofautiana nawewe.
Alichokifanya Putin na ndiyo kipaumbele chake ni millitary modernization hapa wamelifanya jeshi lao kuwa imara lenye uwezo mkubwa kuanzia majini, nchi kavu na angani.
wamefanya upgrade ya silaha zao submarines, heavy bomber&fighter jets, tanks, air defence systems.

Kama wangekuwa weak hata wasingeweza kurusha missiles kutoka umbali zaidi ya 2500 kms pale Caspian sea ile si kila nchi inaweza tena kwa kutumia light little warships.

Na lile tukio lina maana gani?
Walitaka kutuma ujumbe kuwa sasa Warusi wanaeza kushambulia na kufika kila kona ya dunia kwa urahisi zaidi kutoka Urusi hawana haja ya kujenga millitary base nyingi na hili linapunguza gharama na kujilinda zaidi na zaidi.
Pia asilimia kubwa ya tech ya wachina wanategemea Urusi yani China bila Urusi itatetereka pia.

Wamewekeza sana kwenye millitary tech sababu wanaamini maadui wao wameapa kuivamia na kuiangusha Urusi pale tu watapokuwa na uwezo huo.
Maadui hao wanashindwa kuivamia sababu tu wanaona hawatoeza ila kama Urusi wangekuwa hawana sophisticated millitary tech tungekuwa tunazungumza mengine hapa.
Naungana na wewe kwa 97% pia teknolojia ya nyukilia ya North korea ni ya urusi. Ukisoma vizur historia utakubaliana na mimi
 
Tungepata raisi kama huyo ,tungeendela inashangaza urusi ndio wenye technolojia nzuri ya umeme wa nuclear na kuchimba gesi lakini tunawakodolea macho tu hatuchangamki tunawaogapa USA. :eek::eek::eek::eek::eek:
 
Tungepata raisi kama huyo ,tungeendela inashangaza urusi ndio wenye technolojia nzuri ya umeme wa nuclear na kuchimba gesi lakini tunawakodolea macho tu hatuchangamki tunawaogapa USA. :eek::eek::eek::eek::eek:

Raisi Jakaya Kikwete alikuwa na mpango wa haya mambo ya nishati ya nyuklia.
Lakini Maveteran wengi wa Usalama walishauri kwamba itakuwa ni hatari kwa taifa kwasababu Tanzania kuna rushwa sana hivyo hiyo teknolojia ya Nyuklia au madini ya Uranium yanaweza yakaanguka kwenye mikono ya makundi hatari ya kigaidi.
Hata wataalamu (Scientists) wanaosomea haya mambo ya nyuklia duniani kote huwa wanaangaliwa sana kwa jicho la tatu,
sasa kwa jinsi mifumo ya nchi yetu inavyolega na watu wanauzana kwasababu za Kisiasa na kimaslahi kama ambavyo tumeshuhudia tokea awamu ya pili unategemea hawa wanasayansi hawatakuwa sumaku ya utekaji kweli ???

Ushauri mwingine walisema inawagharimu sana mataifa makubwa kwenye kutunza vile vinu,
Pamoja na utupaji taka za Nyuklia ambao inasemekana ni gharama mno kwa nchi kama yetu.
Isitoshe ukisoma hata mtaji unaohitajika kurutubisha ile Yellow Cake ni pesa kubwa sana sanaa.
Tupilia mbali bado hujapeleka mamia ya wanasayansi nchi za nje kusoma.
Wanasema Tanzania bado hatujajiandaa.

NB: Lakini kubwa zaidi wazungu wanasema sisi tunaweza kuuza madini kwa nchi korofi kama Korea Kaskazini na Iran,
Kwasababu Tanzania tumeshawahi kupata kashfa miaka mingi nyuma kwamba tunaongoza kwa kuficha magaidi hatari hapa nchini kwetu. Pia miaka ya karibuni tumeshutumiwa kuwasaidia Iran na Korea Kaskazini kukwepa vikwazo vya Umoja wa Mataifa. Hivyo kuwa na hii teknolojia kunaweza kuleta Unnecessary Attention ya mataifa makubwa nchini mwetu ambapo mambo yetu mengi ya kiulinzi na kiusalama yatakuwa hatarini. Inamaanisha Majasusi ya CIA, MI6, BND, MOSSAD na mengine yanaweza kupanua wigo wa kazi zao hapa nchini hadi wakapenya kila sekta kuhakikisha kweli tunakuwa na matumizi salama ya nyuklia (Watawala wetu hawatapendwa sana kumulikwa na hawa wazungu)

Japo, binafsi nasema kama nchi inabidi tubadilishe Mtazamo wa kifikra.
Hizi fikra za wale wazee wa miaka ya 60's, 70's na 80's inabidi zifanyiwe tathmini kwa upya ili nchi iendelee.
Dunia kila baada ya masaa 24 inapiga hatua kubwa sana ambazo hazimsubiri mtu, na taifa imara ambalo halitataka kuendana na kasi ya dunia basi ni lazima litakuwa katika huruma ya mataifa yenye nguvu. Kama tunahitaji viwanda basi ni lazima tujipange kuzalisha nishati ya kutosha kwa matumizi ya wananchi, wawekezaji na nyingine tuuze hata nje ya nchi.

Nawapenda sana wakina Dr. Kitine, Mzee Warioba, Mzee Mahiga na wengine wote ambao ni First Generation,
Lakini ili hili taifa liende mbele kuna mpaka ni lazima hawa wazee wawekewe, kwasababu naona wengi wao wana Nostalgia ya kutaka Tanzania ya mwaka 2018 ya karne ya 21 iwe kama ile ya miaka ya 1970's ya karne ya 20 ambayo wao waliishi na kuona ni Golden Age. Hatutawatenga kabisa lakini tunahitaji kutengeneza Mzani wa Chuma ambao utahakikisha mawazo ya wazee yanakuwa Realistic kuweza kulinganana hali ya sasa na pia mawazo ya kizazi cha vijana hayatishia misingi ya taifa. Hawa wazee wetu wameshachoka sana na ifike mahali hata kama tunawahitaji ni lazima wakae katika nafasi ya kushauri tu na siyo kimaamuzi. Japo Tanzania tuna changamoto kubwa sana ya kukosa Skilled Manpower hasa kwa vijana, japo naamini tukiweza kufanya Professional Synchronization tutaikabili hii changamoto.

ENOUGH WITH POLITICS OF FEAR......
THIS COUNTRY HAS TO MOVE FORWARD AT A GOD SPEED.
WE ARE 100 YEARS BEHIND THE WEST AND 60 BEHIND THE EAST,..WE NEED TO CATCH UP.
OR WE ARE GOING TO BE THE VICTIMS OF EASTERN ECONOMIC DEVELOPMENT JUST AS WE WERE TO THE WESTERN.
 
Back
Top Bottom