Ujasiriamali wa kisiasa; sababu, matokeo na nini cha kufanya

Azizi Mussa

JF-Expert Member
May 9, 2012
9,172
7,428
1572161332338.png
Moja ya changamoto kubwa ambayo madhara yake hayawezi kupuuziwa ni ujasiliamali katika siasa. Tuna watu wengi ambao wanashiriki kwenye siasa kwa lengo la kuwekeza na kisha kuvuna kwa kutumia watu wengine na kimsingi lengo lao sio kusaidia mtu mwingine kwa namna yoyote ijapokuwa inaweza ikatokea kwa bahati, baadhi ya watu wakanufaika pia (lakini linakuwa si lengo la msingi).

Hata hivyo, kwa kuwa inafahamika kwamba kuwatumia watu wengine kuchuma, sio kitu kinacholeta picha nzuri “As universal law’ hoja ya kuwasaidia wanaochumwa hutumika, na kutokana na uelewa mdogo wa wachumwaji, hukubali kutumiwa na mchumaji.

Hebu jaribu kufikiri, mtu anachukua mkopo benki ‘wenye riba’, anaingiza kwenye kampeni za siasa, anakuahidi kwamba lengo lake ni ashinde ili akusaidie, na wewe unamwamini. Pamoja na kumwamini, hauko tayari kumuunga mkono mpaka akuhonge, na bado unaamini kwamba pamoja na kukuhonga ataenda kukusaidia tena wewe. Yaani daktari, akuhonge ili ukubali akutibu! halafu ukipigwa kekundu unashangaa hahahah!

Kinachosababisha ujasiriamali wa ki - siasa ni kuwa na idadi kubwa zaidi ya wastani ya watu wanaoamini kwamba wao wako duniani kupokea kutoka kwa wengine “Takers” licha ya kufahamu kwamba jambo hilo ki uadilifu si bora. Kwa hiyo mwanasiasa naye kama sehemu ya jamii hiyo hiyo; anakuwa anaamini anatakiwa a ‘Take’ lakini pia anafahamu kuwa mtu mmoja mmoja kwenye jamii anaamini anatakiwa ku ‘Take’ vilevile.

Kwa hiyo anaitumia saikolojia hiyo mbovu ya jamii kuiahidi kwamba ita ‘Take’ kutoka kwake, na kwa sababu uelewa ni mdogo, basi jamii inakubali.

Matokeo yake jamii inapigwa 3 bila asubuhiiiii, badala ya ku ‘take’ inapoteza. Hapo ndipo unakuta watu wanalalamika toka tuchague mbunge wetu hatujamwona tena huu ni mwaka wa 4, anaonekana sinza na Dodoma tu. Hachangii hata siku moja. Amenunuliwa. N.k. Wanasahau walishapewa chao wakati wa kampeni. Hivi hata kama ni wewe ulikopa benki ukagawa pesa ili upate cheo flani (ubunge kwa mfano), unarudi jimboni?Na ukirudi utakuwa serious?

Ni nini cha kufanya? Kwanza tuelewe kuwa, kila mtu kwenye jamii anapoamini kuwa anatakiwa kuchuma kutoka kwa wengine, na kuna mtu yuko mahali anatakiwa ndio awe anatoa (wakati naye pia anaamini anatakiwa kupokea); hilo ni tatizo kubwa na ndio msingi wa yote haya.

Ili kutoka kwenye huo mzunguko, tunatakiwa tuanze kujijengea utaratibu wa kila mmoja wetu kujiambia "mimi ndiye ninayetakiwa kufanyia wengine, mimi ndiye ninayetakiwa kutoa, mimi ndiye ninayetakiwa kusaidia na nimekuja duniani kutoa sio kupokea ".Na hilo linatakiwa kuanza na wewe unayesoma hapa sasa. Kwa kadiri tutakavyokuwa na watu wengi zaidi wenye mtizamo huo; ndivyo tatizo litakavyopungua na kinyume chake ndivyo tatizo litakavyozidi kukuwa.

Tukiliweza hilo, tutapata viongozi wengi na sio watafuta vyeo wengi. Tutakuwa na watu wengi ambao wako tayari kutoa muda wao, rasilimali zao na akili zao kusaidia wengine kuliko kukaa mahali kusubiria kupokea.

Hawa ndio viongozi wanaoweza kuwa na tija kubwa. Ikumbukwe kiongozi si lazima awe na cheo lakini mtu anaweza kuwa na cheo na asiwe kiongozi. Ukiona mtu anatafuta sana cheo, ujue huyo ni ‘Taker’ na ‘Taker’ hawezi kuwa kiongozi bora hata siku moja.Viongozi bora huwa ni ‘Givers by nature’ na unaweza kuwatambua kwa wao kutumia walivyo navyo kusaidia wengine bila kutafuta fidia.
 
Moja ya changamoto kubwa ambayo madhara yake hayawezi kupuuziwa ni ujasiliamali katika siasa. Tuna watu wengi ambao wanashiriki kwenye siasa kwa lengo la kuwekeza na kisha kuvuna kwa kutumia watu wengine na kimsingi lengo lao sio kusaidia mtu mwingine kwa namna yoyote ijapokuwa inaweza ikatokea kwa bahati, baadhi ya watu wakanufaika pia (lakini linakuwa si lengo la msingi).

Hata hivyo, kwa kuwa inafahamika kwamba kuwatumia watu wengine kuchuma, sio kitu kinacholeta picha nzuri “As universal law’ hoja ya kuwasaidia wanaochumwa hutumika, na kutokana na uelewa mdogo wa wachumwaji, hukubali kutumiwa na mchumaji.

Hebu jaribu kufikiri, mtu anachukua mkopo benki ‘wenye riba’, anaingiza kwenye kampeni za siasa, anakuahidi kwamba lengo lake ni ashinde ili akusaidie, na wewe unamwamini. Pamoja na kumwamini, hauko tayari kumuunga mkono mpaka akuhonge, na bado unaamini kwamba pamoja na kukuhonga ataenda kukusaidia tena wewe. Yaani daktari, akuhonge ili ukubali akutibu! halafu ukipigwa kekundu unashangaa hahahah!

Kinachosababisha ujasiriamali wa ki - siasa ni kuwa na idadi kubwa zaidi ya wastani ya watu wanaoamini kwamba wao wako duniani kupokea kutoka kwa wengine “Takers” licha ya kufahamu kwamba jambo hilo ki uadilifu si bora. Kwa hiyo mwanasiasa naye kama sehemu ya jamii hiyo hiyo; anakuwa anaamini anatakiwa a ‘Take’ lakini pia anafahamu kuwa mtu mmoja mmoja kwenye jamii anaamini anatakiwa ku ‘Take’ vilevile.

Kwa hiyo anaitumia saikolojia hiyo mbovu ya jamii kuiahidi kwamba ita ‘Take’ kutoka kwake, na kwa sababu uelewa ni mdogo, basi jamii inakubali.

Matokeo yake jamii inapigwa 3 bila asubuhiiiii, badala ya ku ‘take’ inapoteza. Hapo ndipo unakuta watu wanalalamika toka tuchague mbunge wetu hatujamwona tena huu ni mwaka wa 4, anaonekana sinza na Dodoma tu. Hachangii hata siku moja. Amenunuliwa. N.k. Wanasahau walishapewa chao wakati wa kampeni. Hivi hata kama ni wewe ulikopa benki ukagawa pesa ili upate cheo flani (ubunge kwa mfano), unarudi jimboni?Na ukirudi utakuwa serious?

Ni nini cha kufanya? Kwanza tuelewe kuwa, kila mtu kwenye jamii anapoamini kuwa anatakiwa kuchuma kutoka kwa wengine, na kuna mtu yuko mahali anatakiwa ndio awe anatoa (wakati naye pia anaamini anatakiwa kupokea); hilo ni tatizo kubwa na ndio msingi wa yote haya.

Ili kutoka kwenye huo mzunguko, tunatakiwa tuanze kujijengea utaratibu wa kila mmoja wetu kujiambia "mimi ndiye ninayetakiwa kufanyia wengine, mimi ndiye ninayetakiwa kutoa, mimi ndiye ninayetakiwa kusaidia na nimekuja duniani kutoa sio kupokea ".Na hilo linatakiwa kuanza na wewe unayesoma hapa sasa. Kwa kadiri tutakavyokuwa na watu wengi zaidi wenye mtizamo huo; ndivyo tatizo litakavyopungua na kinyume chake ndivyo tatizo litakavyozidi kukuwa.

Tukiliweza hilo, tutapata viongozi wengi na sio watafuta vyeo wengi. Tutakuwa na watu wengi ambao wako tayari kutoa muda wao, rasilimali zao na akili zao kusaidia wengine kuliko kukaa mahali kusubiria kupokea.

Hawa ndio viongozi wanaoweza kuwa na tija kubwa. Ikumbukwe kiongozi si lazima awe na cheo lakini mtu anaweza kuwa na cheo na asiwe kiongozi. Ukiona mtu anatafuta sana cheo, ujue huyo ni ‘Taker’ na ‘Taker’ hawezi kuwa kiongozi bora hata siku moja.Viongozi bora huwa ni ‘Givers by nature’ na unaweza kuwatambua kwa wao kutumia walivyo navyo kusaidia wengine bila kutafuta fidia.
Hongera kwa kuleta uzi mzuri uzi Kama hizi ni Mara chache Sana mashabiki wa vyama kuchangia wao wamezoea udaku alafu Cha ajabu utawasikia wanataka maendeleo wakati hawapendi kujifunza vitu vipya kama hivi wao wamezoea kuchangia uzi unaoponda serikali au wa kusifia wanasiasa yaani sisi watanzania tunasafari kubwa Sana.
 
Hongera kwa kuleta uzi mzuri uzi Kama hizi ni Mara chache Sana mashabiki wa vyama kuchangia wao wamezoea udaku alafu Cha ajabu utawasikia wanataka maendeleo wakati hawapendi kujifunza vitu vipya kama hivi wao wamezoea kuchangia uzi unaoponda serikali au wa kusifia wanasiasa yaani sisi watanzania tunasafari kubwa Sana.
Mkuu, kwa jamii yetu, ukitaka kupata wachangiaji wengi, unatakiwa uanzishe mjadala unaohusu kudhalilisha mtu mwingine, au kuonesha ni kwa jinsi gani mtu mwingine hana maana, alivyo mbaya au atakavyo kwama.

Na lakusikitisha Zaidi, kuna watu ambao walikuwa wanaleta mijadala ya maana sana, ila baada ya kugundua kuwa wachangiaji ni wachache, baadhi yao wameamua kuhamia kwenye mijadala pendwa na baadhi wamesusa.

Binafsi sifikiri kama huo ni uamuzi wa busara. Ni muhimu kwanza kukubali tatizo tulilonalo kwa sababu tayari tunalo na kisha tuanzie hapo tulipo kutoa elimu ambayo tunafikiri kuwa miaka kadhaa mbele itasaidia kujenga nchi yenye ustawi bora Zaidi. Ni vigumu lakini solution haiwezi kuwa kukata tamaa.
 
Mkuu, kwa jamii yetu, ukitaka kupata wachangiaji wengi, unatakiwa uanzishe mjadala unaohusu kudhalilisha mtu mwingine, au kuonesha ni kwa jinsi gani mtu mwingine hana maana, alivyo mbaya au atakavyo kwama.

Na lakusikitisha Zaidi, kuna watu ambao walikuwa wanaleta mijadala ya maana sana, ila baada ya kugundua kuwa wachangiaji ni wachache, baadhi yao wameamua kuhamia kwenye mijadala pendwa na baadhi wamesusa.

Binafsi sifikiri kama huo ni uamuzi wa busara. Ni muhimu kwanza kukubali tatizo tulilonalo kwa sababu tayari tunalo na kisha tuanzie hapo tulipo kutoa elimu ambayo tunafikiri kuwa miaka kadhaa mbele itasaidia kujenga nchi yenye ustawi bora Zaidi. Ni vigumu lakini solution haiwezi kuwa kukata tamaa.
Kwel kabisa mkuu.
 
Moja ya changamoto kubwa ambayo madhara yake hayawezi kupuuziwa ni ujasiliamali katika siasa. Tuna watu wengi ambao wanashiriki kwenye siasa kwa lengo la kuwekeza na kisha kuvuna kwa kutumia watu wengine na kimsingi lengo lao sio kusaidia mtu mwingine kwa namna yoyote ijapokuwa inaweza ikatokea kwa bahati, baadhi ya watu wakanufaika pia (lakini linakuwa si lengo la msingi).

Hata hivyo, kwa kuwa inafahamika kwamba kuwatumia watu wengine kuchuma, sio kitu kinacholeta picha nzuri “As universal law’ hoja ya kuwasaidia wanaochumwa hutumika, na kutokana na uelewa mdogo wa wachumwaji, hukubali kutumiwa na mchumaji.

Hebu jaribu kufikiri, mtu anachukua mkopo benki ‘wenye riba’, anaingiza kwenye kampeni za siasa, anakuahidi kwamba lengo lake ni ashinde ili akusaidie, na wewe unamwamini. Pamoja na kumwamini, hauko tayari kumuunga mkono mpaka akuhonge, na bado unaamini kwamba pamoja na kukuhonga ataenda kukusaidia tena wewe. Yaani daktari, akuhonge ili ukubali akutibu! halafu ukipigwa kekundu unashangaa hahahah!

Kinachosababisha ujasiriamali wa ki - siasa ni kuwa na idadi kubwa zaidi ya wastani ya watu wanaoamini kwamba wao wako duniani kupokea kutoka kwa wengine “Takers” licha ya kufahamu kwamba jambo hilo ki uadilifu si bora. Kwa hiyo mwanasiasa naye kama sehemu ya jamii hiyo hiyo; anakuwa anaamini anatakiwa a ‘Take’ lakini pia anafahamu kuwa mtu mmoja mmoja kwenye jamii anaamini anatakiwa ku ‘Take’ vilevile.

Kwa hiyo anaitumia saikolojia hiyo mbovu ya jamii kuiahidi kwamba ita ‘Take’ kutoka kwake, na kwa sababu uelewa ni mdogo, basi jamii inakubali.

Matokeo yake jamii inapigwa 3 bila asubuhiiiii, badala ya ku ‘take’ inapoteza. Hapo ndipo unakuta watu wanalalamika toka tuchague mbunge wetu hatujamwona tena huu ni mwaka wa 4, anaonekana sinza na Dodoma tu. Hachangii hata siku moja. Amenunuliwa. N.k. Wanasahau walishapewa chao wakati wa kampeni. Hivi hata kama ni wewe ulikopa benki ukagawa pesa ili upate cheo flani (ubunge kwa mfano), unarudi jimboni?Na ukirudi utakuwa serious?

Ni nini cha kufanya? Kwanza tuelewe kuwa, kila mtu kwenye jamii anapoamini kuwa anatakiwa kuchuma kutoka kwa wengine, na kuna mtu yuko mahali anatakiwa ndio awe anatoa (wakati naye pia anaamini anatakiwa kupokea); hilo ni tatizo kubwa na ndio msingi wa yote haya.

Ili kutoka kwenye huo mzunguko, tunatakiwa tuanze kujijengea utaratibu wa kila mmoja wetu kujiambia "mimi ndiye ninayetakiwa kufanyia wengine, mimi ndiye ninayetakiwa kutoa, mimi ndiye ninayetakiwa kusaidia na nimekuja duniani kutoa sio kupokea ".Na hilo linatakiwa kuanza na wewe unayesoma hapa sasa. Kwa kadiri tutakavyokuwa na watu wengi zaidi wenye mtizamo huo; ndivyo tatizo litakavyopungua na kinyume chake ndivyo tatizo litakavyozidi kukuwa.

Tukiliweza hilo, tutapata viongozi wengi na sio watafuta vyeo wengi. Tutakuwa na watu wengi ambao wako tayari kutoa muda wao, rasilimali zao na akili zao kusaidia wengine kuliko kukaa mahali kusubiria kupokea.

Hawa ndio viongozi wanaoweza kuwa na tija kubwa. Ikumbukwe kiongozi si lazima awe na cheo lakini mtu anaweza kuwa na cheo na asiwe kiongozi. Ukiona mtu anatafuta sana cheo, ujue huyo ni ‘Taker’ na ‘Taker’ hawezi kuwa kiongozi bora hata siku moja.Viongozi bora huwa ni ‘Givers by nature’ na unaweza kuwatambua kwa wao kutumia walivyo navyo kusaidia wengine bila kutafuta fidia.
Uzi wangu bora wa kufungia mwaka so far.
Umeongea kitu cha msingi sana Azizi. Na huko majimboni ndio jamii kubwa iliyoko. Manapata kiongozi mzuri ila mnamtoa kasoro za kuwa hana pesa au unamjengea mazingira ya hadi "akuhonge" akupatie chochote ndio uweze kumpatia kura yako, hapo ujue ni biashara hapo ujue amekununua na hakuna biashara inayolenga hasara tupu. Utasikia "jamaa ni anatufaa kabisa kuwa kiongozi wetu ila tatizo hana hela"

Matokeo yake ni kuliwa kekundu kila baada ya miaka mitano mitano, na uzuri wajasiriamali wa siasa wanalitambua hili wanawajua wananchi wao "takers" vema kwa sababu wengi wao wanaotafuta vyeo wanatoka miongoni mwao.

Na hao "takers" ndio wanaolalamika mara mwakilishi wetu hatumuoni hajawahi kukanyaga jimboni toka tumchague,...hatusaidii chochote wakati wa shida blah blah...my braza ukiona hivo ujue yuko anafanya marejesho ya mkopo aliochukua....kwa sababu mnakua mmechagua biashara na si uongozi...ni kwa sababu ulichagua kununuliwa ili umpatie cheo sasa unacholalamika nini? Aje huko kwani kasahau nini? Atakuja kufanya biashara nyingine baada ya miaka mitano mkae upya mezani.

Hii trend inatupotozea sana wawakilishi walio viongozi na matokeo yake inatupatia wasaka vyeo.
 
Uzi wangu bora wa kufungia mwaka so far.
Umeongea kitu cha msingi sana Azizi. Na huko majimboni ndio jamii kubwa iliyoko. Manapata kiongozi mzuri ila mnamtoa kasoro za kuwa hana pesa au unamjengea mazingira ya hadi "akuhonge" akupatie chochote ndio uweze kumpatia kura yako, hapo ujue ni biashara hapo ujue amekununua na hakuna biashara inayolenga hasara tupu. Utasikia "jamaa ni anatufaa kabisa kuwa kiongozi wetu ila tatizo hana hela"

Matokeo yake ni kuliwa kekundu kila baada ya miaka mitano mitano, na uzuri wajasiriamali wa siasa wanalitambua hili wanawajua wananchi wao "takers" vema kwa sababu wengi wao wanaotafuta vyeo wanatoka miongoni mwao.

Na hao "takers" ndio wanaolalamika mara mwakilishi wetu hatumuoni hajawahi kukanyaga jimboni toka tumchague,...hatusaidii chochote wakati wa shida blah blah...my braza ukiona hivo ujue yuko anafanya marejesho ya mkopo aliochukua....kwa sababu mnakua mmechagua biashara na si uongozi...ni kwa sababu ulichagua kununuliwa ili umpatie cheo sasa unacholalamika nini? Aje huko kwani kasahau nini? Atakuja kufanya biashara nyingine baada ya miaka mitano mkae upya mezani.

Hii trend inatupotozea sana wawakilishi walio viongozi na matokeo yake inatupatia wasaka vyeo.
Mkuu nimefarijika kuona angalau unaelewa vizuri changamoto hii. By the way wapo wachache wanaoelewa, swali la kujiuliza wanafanya nini? Je! wanafikiri hilo ni tatizo? je! wanaamini wana wajibu?
 
Kuna siku nilikuwa nimerudi likizo Dar. Nikaamua kwenda Zanzibar na wadogo zangu kuangalia sehemu tofauti.

Sasa katika kurudi wenzangu wakatangulia, mimi nikarudi mwisho.

Nilipofika Dar Forodhani, nikaamua kutembea kwa miguu nione mji ulivyobadilika. Nilitaka kutembea kutoka mjini mpaka Upanga kusalimia jamaa.

Nikakatiza mjini kati hapo, Sokoine mpaka Nkrumah, mpaka Mnazi Mmoja.

Nilipofika Mnazi Mmoja nikaanza kusikia kiu na njaa, nikasema hapa nitafute kihoteli nitulize njaa.

Nilipofika sambamba na ofisi ya CCM Lumumba, nikaona kuna sehemu ya maakuli nzuri tu upande wa mkabala na ofisi ya CCM.

Nikaingia hapo nikakagua mandhari, nikaridhika. Nikakaa chini, nikaagiza chakula na juisi.

Pembeni yangu walikuwa wamekaa watu wawili. Mimi kama kawaida yangu si mtu wa kufuatilia sana watu, mwanzo sikuwaangalia sana.

Lakini wao wenyewe hawakuwa na ustaarabu wa kuongea kwa sauti ya chini. Walikuwa wanapaza sauti kiasi mimi nikawa nasikia mazungumzo yao.

Nikaja kugundua kwamba, wale watu wawili ni wabunge wa CCM. Walikuwa wanajiandaa kuingia ofisi za CCM Lumumba.

Mmoja alikuwa analalamika kwamba Ubunge umempotezea hela tu, alifikiri akitumia hela nyingi kwenye kampeni, baada ya kupata ubunge, atazirudisha na kuzidisha mara nyingi, lakini anasikitika ubunge hauna fursa, na watu wengi wanamlilia njaa.

Nikajiwazia kwamba, huyu mtu hakutaka ubunge ili amalize matatizo ya watu, ametaka ubunge ili amalize matatizo yake.

Nikajiwazia kwamba huyu mtu haoni kwamba hayo maneno anayosema ni ya aibu, na anasema bila woga, bila kujua kwamba mimi niliyekaa pembeni naweza kuwa muandishi wa habari ninayeweza kuandika habari zake na kumtaja.

Huo ulikuwa mwaka 2012. Baadaye nilitembelewa ughaibuni na mzee mmoja kiongozi mstaafu Tanzania.

Nikamuhadithia habari ile.

Akasema wewe unashangaa habari kama hiyo kwa sababu huishi huku nyumbani, huyo mbunge hata hakuona kama hayo maneno ni ya aibu, na hivyo hakuhofia muandishi wa habari. Ni mambo ya kawaida sana kwenye siasa za Tanzania.

Ilivyoletwa mada ya ujasiliamali wa kisiasa, imenikumbusha kisa hiki.
 
Swali, unadhani ni kwa nini wanasiasa wengi wanaofanya siasa za majukwaani, hawatoi hoja zao hapa JF Licha ya kwamba hapa unaweza kufikia watu wengi zaidi ya unaoweza kuwakusanya mahali tena kwa gharama nafuu? Kinyume chake wanaweza kulalamika jinsi mazingira ya kufanya mikutano live yasivyokuwa rafiki (jambo ambalo ni kweli).

Unadhani ni kwa nini hata wale wachache wanaoweza kuthubutu kuleta hoja humu, huweka hoja na kukimbia bila kugeuka nyuma?
 
Swali, unadhani ni kwa nini wanasiasa wengi wanaofanya siasa za majukwaani, hawatoi hoja zao hapa JF Licha ya kwamba hapa unaweza kufikia watu wengi zaidi ya unaoweza kuwakusanya mahali tena kwa gharama nafuu? Kinyume chake wanaweza kulalamika jinsi mazingira ya kufanya mikutano live yasivyokuwa rafiki (jambo ambalo ni kweli).

Unadhani ni kwa nini hata wale wachache wanaoweza kuthubutu kuleta hoja humu, huweka hoja na kukimbia bila kugeuka nyuma?
Wengi sio viongozi wengi ni wasaka vyeo na washavipata. Hawana muda huo na wala creativity/vision ya leadership.
 
Hili linabakia kuwa moja ya changamoto kubwa tunazopaswa kuzi adress
 
Back
Top Bottom