Ujasiri wa Rais Magufuli juu ya janga la korona katika ulimwengu wa roho

Hivi anachofanya ni ujasiri au uoga wa kuujua ukweli?
 
Watanzania walichagua kiongozi wa nchi atakaewaongoza,sio kiongozi wa dini.Kuleta assesment za ki dini wakati umepewa ridhaa ya kuongoza watu mchanganyiko wakiwamo wasoamini Mungu ni usaliti. Serikali haina dini,ivo masuala ya dini yabaki kwa mtu binafsi.
Ugonjwa wa Corona ni tatizo linalohitaji kupewa ufumbuzi wa kitaalamu na waliobobea kwenye taaluma za magonjwa. Corona ipo na inaua na itaendele kutumaliza kama mkiendelea na hizi hadithi zenu.
 
Awali ya yote napenda kutoa salamu za dhati kabisa kutoka katika kina cha nia yangu kwenu nyote nikiwa na uhakika salamu hii itapokelewa na kila mtu atakayesoma andiko hili na kuruhusu kuelewa zaidi ya uelewa ulivyo.

Natamani sana andiko langu niliweke katika lugha ambayo itamfanya kila mmoja kuelewa kwa urahisi kabisa kwa kuyaweka mambo ya ulimwengu wa roho katika hali ya wazi tofauti na yanavyochukuliwa na baadhi ya watu.

Ni vyema kabisa tukajua kuwa sisi sote ni viumbe wa kiroho tunaoishi katika mwili. Mwili ni kibebeo chetu na siyo sisi. Itakuwa vyema na wewe ukalitambua hili mapema kabisa ili unapoendelea kusoma andiko hili usitume shaka juu ya nitakayoyaandika.

Baada ya kutambua kuwa sisi ni viumbe wa kiroho tunaoishi katika mwili tunapaswa kufahamu pia sifa ya kuu ya ulimwengu wa roho na roho.

Zipo sifa nyingi mno za ulimwengu wa roho ila kwa kurahisisha uelewa wetu juu ya andiko hili ni kwamba ulimwengu wa roho ni ulimwengu wa milele, hauna mwanzo wala mwisho na pia hautawaliwi na mipaka ya mahali na wakati. Ulimwengu huu unaweza kuwa kila mahali na kila wakati.

Roho hayo ina sifa kama za ulimwengu wa kiroho ulivyo yaani haifungwi na gereza la mahali na muda kama ulimwengu wa mwili ulivyo ambao mwili wa kifuzikali huwa katika gereza la mahali na muda na hivyo kuwa katika mipaka mingi ya kuelewa na utendaji.

Kwanini natamani kuzungumzia ujasiri wa Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania katika ulimwengu wa roho juu ya janga la Korona?..Hapa ndipo lilipo kiini cha andiko hili na ninatamani kila mmoja kuelewa ulimwengu huu unavyotenda kazi ndani yetu.

Ikumbukwe kuwa ulimwengu wa vitu hauna nguvu na hatuwezi kumba ila ulimwengu wa roho ndiyo wenye nguvu na ndiyo unaoumba vitu vinavyoonekana na kuakisiwa na milango ya fahamu ya mwili.

Katika ulimwengu wa roho ndipo vilipo vyanzo vya kila kitu chenye umbile lolote lile linaloonekana katika ulimwengu wa vitu tunaouhusi kupitia milango ya fahamu.

Kwa mantiki hiyo kila kitu hufanyika katika ulimwengu wa roho kabla ya kuchukua umbile halisi na kuwa kitu kinachodhihirika katika ulimwengu wa vitu. Ieleweke kuwa hata magonjwa makubwa yanayoikumba Dunia ikiwemo Korona ina asili katika ulimwengu wa roho. Mambo mengi kabla ya kujidhihirisha huwa yanakuwa katika hali ya kukosa umbile "form less" na yanakuwa katika ulimwengu wa roho.

Jambo lolote ambalo hatulitambui au hatulioni kupitia macho ya kimwili haimaanishi halipo. Ulimwengu wa roho una utoselezo wa kila kitu na una sifa ya umilele. Ulimwengu huu wa milele una kila kitu hivyo ni jukumu letu kuangalia na kuumba maumbile ya vitu hivyo.

Ugonjwa huu wa Korona umepewa umbile na kudhihirika Duniani haimaanishi haukuwepo hapo awali, kama nimeliweka vizuri ni kwamba ulikuwepo ila ulikuwa hauna umbile la kuudhihirisha Duniani.

Ili kuweza kuharibu umbile la ugonjwa huu wa Korona Duniani kinachohitajika ni nguvu za kiroho kuweza kuona chanzo na kutambua namna ya kuharibu umbile bila woga wala wasiwasi.

Mheshimiwa Rais anapotuhamasisha kuendelea kumtanguliza Mungu huku tukijiwekea hadhari na kuendelea na majukumu ni dhahiri kauli hii haibahatishi ila inayoambatana na nguvu ya kutuunganisha na akili ya kiumbaji.

Amekuwa akisema ugonjwa huu ni vita ya kiuchumi mara kadhaa huenda tunaweza tukachelewa sana kuelewa kama tunaishia kuangalia kwa kutumia macho ya nyama na kusahau kuangalia kiroho.

Anaposema hii ni vita tuelewe hii ni vita habahatishi ni suala la sisi kurudi katika ulimwengu wa roho na kuangalia kwa sababu ulimwengu wa roho haukosei na haubahatishi.

Watanzania tunahitaji nguvu za roho ili kuelewa na kufanya sawasawa na tulivyoelewa na siyo tofauti na hapo.Chanjo ya Korona siyo muhimu kama chanjo ya roho zetu. Tukumbuke chanzo cha Korona siyo umbile la kimwili lililodhihirika Duniani na kusambaa kila mahali ila ni umbile la kiroho lilochukua umbile la ugonjwa katika ulimwengu wa kimwili.

Kujiweka vizuri kiroho ni vizuri kuliko kujiweka vizuri kimwili ndiyo maana ila mara anatusisitiza kuwa karibu na Mungu na kuwa karibu na Mungu ni kuwa karibu na ulimwengu wa kiroho. Kwa maana nyingine anatutaka tupambane na chanzo cha tatizo kwa kumtanguliza Mungu badala ya kupambana na matokeo ya tatizo kwa kuutanguliza mwili kupokea chanjo.
Hapa uko sahihi kabisa ndugu yangu
Unajua nini? Mimi nilichokiona kwenye ulimwengu wa roho ni kwamba Mungu aliamua kumrudia JPM akitaka kuhakikisha kama JPM bado yuko kama alivyokuwa mwanzo kipindi Corona inaingia, na ambayo alimponya nayo, au ameshabadilika baada ya kupata uponyaji. Ni kwamba kulikuwa na kipigo cha mbwa kingeshuka kama angekuwa amebadilika. Sasa hivi ni ushindi tu, hakuna baya lolote litakalotokea, haya mengine yanayoendelea muda huu ni upepo tu unaovuma kwa muda mfupi, utapita!
 
Akili yako ndivyo inavyoona.
Ushuzi n'tupu

Hapa uko sahihi kabisa ndugu yangu
Unajua nini? Mimi nilichokiona kwenye ulimwengu wa roho ni kwamba Mungu aliamua kumrudia JPM akitaka kuhakikisha kama JPM bado yuko kama alivyokuwa mwanzo kipindi Corona inaingia, na ambayo alimponya nayo, au ameshabadilika baada ya kupata uponyaji. Ni kwamba kulikuwa na kipigo cha mbwa kingeshuka kama angekuwa amebadilika. Sasa hivi ni ushindi tu, hakuna baya lolote litakalotokea, haya mengine yanayoendelea muda huu ni upepo tu unaovuma kwa muda mfupi, utapita!
Hapa uko sahihi kabisa ndugu yangu
Unajua nini? Mimi nilichokiona kwenye ulimwengu wa roho ni kwamba Mungu aliamua kumrudia JPM akitaka kuhakikisha kama JPM bado yuko kama alivyokuwa mwanzo kipindi Corona inaingia, na ambayo alimponya nayo, au ameshabadilika baada ya kupata uponyaji. Ni kwamba kulikuwa na kipigo cha mbwa kingeshuka kama angekuwa amebadilika. Sasa hivi ni ushindi tu, hakuna baya lolote litakalotokea, haya mengine yanayoendelea muda huu ni upepo tu unaovuma kwa muda mfupi, utapita!
Naam.
 
Mungu hana dini wewe.
Kumtanguliza Mungu ni tofauti sana na kutanguliza dini.
Watanzania walichagua kiongozi wa nchi atakaewaongoza,sio kiongozi wa dini.Kuleta assesment za ki dini wakati umepewa ridhaa ya kuongoza watu mchanganyiko wakiwamo wasoamini Mungu ni usaliti. Serikali haina dini,ivo masuala ya dini yabaki kwa mtu binafsi.
Ugonjwa wa Corona ni tatizo linalohitaji kupewa ufumbuzi wa kitaalamu na waliobobea kwenye taaluma za magonjwa. Corona ipo na inaua na itaendele kutumaliza kama mkiendelea na hizi hadithi ze
 
Ujinga Mtupu
Naomba nikujibu hivi hatuoni kilichopo nje yetu ila kilichopo ndani yetu .
Kama ulimwengu wako wa ndani unaonesha ujinga basi kusema unaona ujinga hukosei kabisa kwa sababu ndicho uonacho.
 
Watanzania walichagua kiongozi wa nchi atakaewaongoza,sio kiongozi wa dini.Kuleta assesment za ki dini wakati umepewa ridhaa ya kuongoza watu mchanganyiko wakiwamo wasoamini Mungu ni usaliti. Serikali haina dini,ivo masuala ya dini yabaki kwa mtu binafsi.
Ugonjwa wa Corona ni tatizo linalohitaji kupewa ufumbuzi wa kitaalamu na waliobobea kwenye taaluma za magonjwa. Corona ipo na inaua na itaendele kutumaliza kama mkiendelea na hizi hadithi zenu.
Kwa hiyo wataalamu hawapaswi kumtanguliza Mungu?..
 
Hivi anachofanya ni ujasiri au uoga wa kuujua ukweli?
Mkuu ukweli ni kuamini ipo nguvu kuliko nguvu za kimwili na nguvu hiyo ni nguvu ya kiroho.
Kumtanguliza Mungu ni kujua ukweli kama ulivyo.
 
Huezi eleweka! Roho na dunia wapi na wapi ww!?

Mathalani umeambukizwa korona, unapambanaje kiroho roho?
Na kipindupindu je?

Halafu ni lini kama nchi tulipambana kiroho?

Tupambane kuondoa ujinga, umasikini na maradhi, hayA ni mambo ya kiroho!?

Zipo taasisi za kidini zinazohusika na mambo ya kiroho na zinafahamika.

Serekali inayotoza watu kodi, inashtaki watu, kufilisi, kuwafunga na hata kunyonga watu. Wapi na wapi mkuu?

Acheni kutetea wanaokwepa majukumu kwa visingizio hewa.
Mkuu hakuna kinachofanyika katika ulimwengu wa vitu ambacho hakuna asili katika ulimwengu wa roho.
Jaribu kuvuka mipaka ya ulimwengu wa vitu ili uone vizuri. Ulimwengu wa roho upo,unafanya kazi, ni sahihi, haubahatishi na ndiyo asili ya wanadamu wote.
Kila kitu kilianzia kwenye ulimwengu wa roho kuja kwenye umbile linalodhihirika katika ulimwengu wa vitu.
Vuka mipaka ya milango mitano ya fahamu utanielewa vizuri mno.
Karibu sana.
 
Soma uelewe ndo hujibu,nilichosema ni 'assessment' yake ni ya ki dini.wataalamu wanatumia taaluma zao na hekima za dini sio vice versa.
Mkuu hivi kumtanguliza Mungu ni assessment ya Dini ipi?...Mungu ana Dini kweli?..
Kuna masuala kuyaelewa yanahitaji zaidi ya kufikiri.
 
Mkuu hivi kumtanguliza Mungu ni assessment ya Dini ipi?...Mungu ana Dini kweli?..
Kuna masuala kuyaelewa yanahitaji zaidi ya kufikiri.
Duh,we mbona mgumu kuelewa! Ok let's try again.kafanya assessment ya ugonjwa kwa kutumia dini,yeye kama kiongozi naona haijakaa sawa.ukienda kwa mwanasheria kama una tatizo unategemea kusikia sheria zinasemaje sababu ndo zinazotumika kuendeshea maisha,pia ukienda kwa daktari kama unaumwa malaria unatarajia akupime na akwambie dawa gani utumie,kwa sababu ndo mipangilio yetu ya kimaisha ilivyo na wakati unatumia dawa unaomba Mungu akusaidie upone.Lakin iwapo utaambiwa omba Mungu,wakati unataka msaada wa kitabibu,utakuwa umepewa assessment za ki dini sio kitaalamu.
 
Mkuu nakuelewa vizuri kabisa lakini ni katika mipaka...majibu ya hoja yako yanadhibitiwa na mipaka mingi mno kiasi kwamba yanakuwa kama gereza lisiloruhusu kuvuka nje ya mstari wa mahali na muda.
Huenda thread hii haijaeleweka vizuri kwako.
Duh,we mbona mgumu kueleunayo Ok let's try again.kafanya assessment ya ugonjwa kwa kutumia dini,yeye kama kiongozi naona haijakaa sawa.ukienda kwa mwanasheria kama una tatizo unategemea kusikia sheria zinasemaje sababu ndo zinazotumika kuendeshea maisha,pia ukienda kwa daktari kama unaumwa malaria unatarajia akupime na akwambie dawa gani utumie,kwa sababu ndo mipangilio yetu ya kimaisha ilivyo na wakati unatumia dawa unaomba Mungu akusaidie upone.Lakin iwapo utaambiwa omba Mungu,wakati unataka msaada wa kitabibu,utakuwa umepewa assessment za ki dini sio kitaalamu.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom