Wildlifer
JF-Expert Member
- May 12, 2021
- 1,883
- 5,186
Leo ni siku ya kumbukizi ya kifo cha Mfalme wa Muziki wa Reggae barani Afrika, Lucky Dube. Nimejikuta nakumbuka kisa kimoja ambacho huwa nacheka na kujiona mpumbavu sana kila nikikumbuka.
Enzi za uvulana, niliwahi kuwa na uhusiano na binti mmoja. Kwa kweli nilikuwa nampenda sana (at least kwa fikra za ujana wakati huo). Baba yake alihamishwa kikazi, na binti naye ikabidi ahame shule.
Siku moja kabla hajaondoka, nikajikunja kuandika Barua ya kuagana na kukumbukana. Jambo moja nililiweka kwenye ile barua hadi leo nikikumbuka huwa najicheka sana.
Niliweka dedication ya wimbo wa Remember Me ya Lucky Dube. Ile title ya Remember Me, ndio ilinifanya nione chaguo sahihi, maana kwa kiingereza changu cha Percentage moja wakati huo, iliniambia Maana yake 'Nikumbuke mimi'.
Nilikuja kufahamu maana ya huu wimbo niko kidato cha nne. Ni wimbo ambao msimuliaji anamuimbia baba yake aliyeikimbia familia. Huwa kila nikiusikiliza huu wimbo, basi nakumbuka, 'blanda' hii niliyofanya.
Ulishawahi fanya 'blanda' enzi za ujana/uvulana kwenye mapenzi ambao ukikumbuka, unajiona ulikuwa mpumbavu sana?
Enzi za uvulana, niliwahi kuwa na uhusiano na binti mmoja. Kwa kweli nilikuwa nampenda sana (at least kwa fikra za ujana wakati huo). Baba yake alihamishwa kikazi, na binti naye ikabidi ahame shule.
Siku moja kabla hajaondoka, nikajikunja kuandika Barua ya kuagana na kukumbukana. Jambo moja nililiweka kwenye ile barua hadi leo nikikumbuka huwa najicheka sana.
Niliweka dedication ya wimbo wa Remember Me ya Lucky Dube. Ile title ya Remember Me, ndio ilinifanya nione chaguo sahihi, maana kwa kiingereza changu cha Percentage moja wakati huo, iliniambia Maana yake 'Nikumbuke mimi'.
Nilikuja kufahamu maana ya huu wimbo niko kidato cha nne. Ni wimbo ambao msimuliaji anamuimbia baba yake aliyeikimbia familia. Huwa kila nikiusikiliza huu wimbo, basi nakumbuka, 'blanda' hii niliyofanya.
Ulishawahi fanya 'blanda' enzi za ujana/uvulana kwenye mapenzi ambao ukikumbuka, unajiona ulikuwa mpumbavu sana?