Uislam sio ugaidi na waislam sio magaidi: Sheikh Najih Shaker Al-Baldawi ni shujaa wa Iraq aliyemkumbatia "Suicide Bomber" kisha kuokoa maisha ya watu

Status
Not open for further replies.

Infantry Soldier

JF-Expert Member
Feb 18, 2012
15,893
16,317
UISLAM SIO UGAIDI NA WAISLAM SIO MAGAIDI: Sheikh Najih Shaker Al-Baldawi ni shujaa wa Iraq aliyemkumbatia "Suicide Bomber" kisha kuokoa maisha ya wenzake.

83074962_3252744551419505_6489122236186755072_n.jpg

UTANGULIZI: Kwa msio nifahamu mimi Infantry Soldier ni mkristo ila ninafahamu fika ya kuwa uislamu si ugaidi na wala waislamu si magaidi bali wahalifu wachache hujificha katika kivuli cha uislamu ili kutenda ugaidi na kuua watu.

Uislamu ni dini safi tena ya watu waungwana sana inayohubiri amani na upendo kama ilivyo dini ya kikristo.

BACK TO THE STORY: Mnamo tarehe 07 mwezi wa July mwaka 2016, takribani watu 56 waliuawa na wengine 75 kujeruhiwa baada ya kundi la magaidi kuvamia jengo la makumbusho ya Sayid Mohammed bin Ali al-Hadi, sehemu takatifu ya waislamu wa dhehebu la shiha huko mjini Balad katika nchi ya iraq.

Waliwashambulia mahujaji wa kishiha waliokuwa wakisherehekea sikukuu ya Eid al-Fitr, ambao inatamatisha mwisho wa mwezi mtukufu kwa waislam wa Ramadan. Kulikuwa na washambuliaji watatu (3) wa kujitoa mhanga (Suicide Bomber) na mmoja wao waliuawa na mlinzi wa makumbusho hayo.

Kulikuwa na washambuliaji wengine pia ingawa ISIL walivurumisha mashambulizi ya mortar. (Wanajeshi mtakuwa mnazifahamu vizuri sana hizi mortar)

Mtu aliyeuawa baada ya kumzuia muuaji wa kujitoa mhanga asiingie katika eneo hilo takatifu alijulikana kwa jina la Najih Shaker Al-Baldawi. Alimkumbatia moja ya wauwaji wa kujitoa mhanga na hivyo kupunguza nguvu ya mlipuko wa bomu katika suicide vest.

Al Baldawi, mkazi wa kawaida kabisa na mwenyeji wa mji wa Balad alifanikiwa kuokoa maisha ya makumi ya idadi ya watu wasiokuwa na hatia na hatimae kuitwa shujaa baada ya kupata umaarufu mkubwa huko mashariki ya kati.

Source: Nenda website ya Google kisha search neno "Najih Shaker Al-Baldawi"

Usipite bila kusema Allahu Akbar
 
Ingependeza sana kama the Muslim world wangesimama kidete kukemea vitendo vya magaidi wachache wanaochafua dini. The problem is their silence and since impliedly silence is assumed to be support of something which you were expected to stand otherwise then here comes the problem.
 
Vurugu zote hizi ni ujio wa waarabu, na wazungu barani afrika na kuharibu kabisa historia yetu kama siyo ujio wao tungekuwa wamoja na tusingebishana jambo lolote lenye mtazamo wa kidini, huwa inaniuma sana nilipokataliwa kuoa mdada niliyempenda kwa moyo wangu wote nikakataliwa kisa yeye ni mkristo nami muislamu.

Sikuwalaumu hawa wazazi ila niliwalaumu waarabu na wazungu waliokuja kutuvuruga
 
Kuna connection kubwa kati ya uslamu na ugaidi ndio maana waislamu wote wakisikia unataja magaidi wanaohofu kutajwa wao
Eeh bwana eeh... kumbe ndivyo inavyokua great thinker
 
Kama siyo ugaidi kwa nn wakisikia kuna magaidi yanatafutwa wanakuwa na hofu?
Sababu hali imetengenezwa hivyo, kama hali ilivyo tengenezwa ya kuwa nchi za magharibi ndiyo zimestaarabika sana.

Tuna msemo wetu sisi ya kuwa "Ukitaka kumuua mbwa,wewe mpe jina baya", na ubaya ulioje watu nao hawataki kuutafuta ukweli.

"400kV Tapped"
 
Babu Kijiwe, Kwanza muhammad swalahullah ailaih wasalam unamjua? Au labda ulishawai kuisoma historia yake ukajua alikuwa mtu wa aina gani? Au umesema kwa chuki tu zilizo moyoni mwako?! Jifunze kutumia akili ndugu sio unaambiwa kitu unakichukua km kilivyo ndio maana mpaka leo umeambiwa yesu ni mungu na umekubali upo tu kama zezeta unachokijua ni kutafuta hela ya kula tu
 
Nguvu kubwa itumike kuwakataza magaidi kutumia jina la kiisilamu kwenye Kazi zao badala ya kutumia nguvu kubwa kuwaaminisha watu kuwa wanachofanya magaidi hakihusiani na uislamu kitu ambacho kinaonekana ni uongo tu kwani sababu zao zote ni za kidini...pia Conspiracy theorists wanaomini kwamba Osama hajafa asilimia 90 ni waislamu kwani humuona kama shujaa...

Fanya tafiti hata hapa nchini...wakati Osama ameuawa Siku iliyofuata nikiwa kwenye Daladala kuelekea chuo nilikutana na maandamano ya kikundi kidogo cha waisilamu wavaa suruali fupi pale kituoni "faya" wakibeba mabango ya kumkashifu Obama kwa kitendo cha kumuua shujaa Huyo Osama...

Magaidi ni mashujaa kwa waisilamu walio wengi data zinaonyesha hivyo..la wawakataze kutumia jina la uislamu...Huwezi kusema Tembo ni mwanao wakati wewe ni Sungura.
 
Not all Muslims are terrorist but ALL Muslims support and like terrorism.

Cc bro Dalmine



Pata elimu kidogo 👇yani nyie hata mtoto wa miaka mitano wakiislamu anawaweka chini

Uislamu ni dini ambayo inahimiza amani, upendo na uvumilivu

SIFA zote njema anastahiki Mwenyezi Mungu mwingi wa rehema na mwenye kurehemu.

Sala na salamu zimthibitikie Mtume wetu Muhammad Swallallahu Alayhi Wasallam, maswahaba wake watukufu na watangu wema hadi siku ya Kiyaamah.

Neno Uislamu linamaanisha amani kwa Kiarabu. Uislamu ni dini iliyoteremshwa ili kumwakilisha mtu pamoja na maisha yaliyojaa utulivu na amani ambayo yana huruma isiyo na mwisho ya Allah iko waziwazi. Allah anawaita watu kuja katika maadili ya Uisilamu kuwa ndio kigezo ambacho huruma, uvumilivu na amani vinaweza kufanyiwa kazi. Yafuatayo yanaelezwa katika aya 208 ya sura al-Baqara:

“Enyi mlio amini! Ingieni katika Uislamu kwa ukamilifu, wala msifuate nyayo za She’tani; hakika yeye kwenu ni adui aliye wazi.”

Kama inavyoonekana katika aya, Allah anaeleza kuwa usalama wa watu unaweza kuhakikishwa tu kupitia kuukubali Uisilamu na kutekeleza kwa vitendo maadili ya Qur'an.

Uisilamu unaulinda uhuru wa kutafakari na uvumilivu

Uislamu, ambayo ni dini inayoeleza na kuhakikisha waziwazi uhuru wa kutafakari na maisha, imetoa maamrisho yanayozuia na kukataza kuwekana roho juu, migogoro kati ya watu, kusemana na hata kuwadhania watu vibaya.

Sio tu kutishia na matumizi ya nguvu, Uisilamu unakataza kuweka hata shinikizo dogo kwenye fikra za watu.

“Hapana kulazimisha katika Dini. Kwani Uwongofu umekwisha pambanuka na upotofu.” (al-Baqara, 2/256)

“Wewe si mwenye kuwatawalia.” (al-Ghashiya, 88/22)

Ni kinyume na maumbile na uhalisia wa Uislamu kuwateza nguvu watu ili waamini katika dini au kufanya ibada. Kwa kuwa, Uislamu umeweka utashi huru na ridhaa makini kuwa ndio sharti la imani. Bila ya shaka, Waislamu wanaweza kuonya na kuhamasishana hivyo wanaweza kutekeleza kwa vitendo sifa za kimaadili zilizofafanuliwa ndani ya Qur'an. Hata hivyo, hawawezi kutezana nguvu kuhusiana na hilo. Sio sawa kupendekeza vipaumbele fulani vya kidunia ili kumfanya mtu fulani afanye ibada.

Fikiria kuhusu kigezo cha jumuia kilicho kinyume cha mtindo wa hilo. Mathalani, jaalia kuwa watu wanatezwa nguvu kuabudu. Jumuia ya namna hiyo iko kinyume kabisa na Uisilamu. Kwa kuwa, imani na ibada vinakuwa na thamani vinapotekelezwa kwa ajili ya Allah. Ikiwa mfumo wa utawala utawalazimisha watu kuamini na kuabudu, watu watakuwa ni washika dini kwa sababu ya kuuogopa mfumo-tawala.

Kilichokuwa na thamani kwa upande wa dini ni kutekeleza dini kwa vitendo kwa ajili ya Allah katika mazingira huru kabisa.

Allah ameharamisha kuua watu wasio na hatia Kwa mujibu wa Qur'an, kumuua mtu asiye na hatia ni moja ya madhambi makubwa mno:

“…aliye muuwa mtu bila ya yeye kuua, au kufanya uchafuzi katika nchi, basi ni kama amewauwa watu wote. Na mwenye kumuokoa mtu na mauti ni kama amewaokoa watu wote. Na hakika waliwajia Mitume wetu na hoja zilizo wazi. Kisha wengi katika wao baada ya haya wakawa waharibifu katika nchi.” (al-Maida, 5/32)

“Na wale wasio mwomba mungu mwengine pamoja na Mwenyezi Mungu, wala hawaui nafsi aliyoiharamisha Mwenyezi Mungu isipo kuwa kwa haki, wala hawazini – na atakaye fanya hayo atapata madhara,” (al-Furqan, 25/68)

Kama inavyoonekanwa katika aya hapo juu, wale wanaoua watu wasiokuwa na hatia wanaonywa na adhabu kali. Allah anaeleza kuwa kumuua mtu mmoja ni uhalifu mkubwa mno kama kuua watu wote. Haiwezekani kwa mtu anayetii mipaka iliyowekwa na Allah kumdhuru hata mmoja achilia mbali kuua maelfu ya watu wasio na hatia.

Kukwepa haki

Wale wanaodhani kwamba wanaweza kuikwepa haki na kunusurika nayo hawatoweza kukwepa kisasi mbele ya Allah.

Kwa hivyo, waumini wanaojua kwamba watalipiziwa mbele ya Allah baada ya kifo wanatenda mambo kwa uangalifu mno ili kutii mipaka iliyowekwa na Allah. Allah anawaamuru waumini kuwa na huruma.

Maadili ya Mwislamu yanafafanuliwa kama ifuatavyo katika aya:

“Tena awe miongoni mwa walioamini na wakausiana kusubiri na wakausiana kuhurumiana. Hao ndio watu wa kheri wa kuliani.” (al-Balad, 90/17-18)

Moja ya sifa muhimu mno za maadili yaliyoteremshwa na Allah kwa waja Wake ili wapate wokovu Siku ya Kiama, rehema Zake na Pepo ni “kuamrishana subira”. Uisilamu, unaoelezwa katika Qur'an, una muundo wa kisasa, wenye kuelimisha na wa kimaendeleo. Mwisilamu wa kweli anayo haiba ya amani, uvumilivu, kidemokrasia, kitamaduni, utambuzi/usomi, uaminifu, jicho la sanaa na sayansi na ustaarabu.

Mwisilamu aliyelelewa na maadili ya juu yaliyotajwa na Qur'an anatangamana na kila mtu kwa upendo unaotumainiwa na Uisilamu.
 
Huwa sipendi watu wanaosemea vibaya Dini za wengine,asilimia kubwa wamelelewa malezi mabaya.Kwanini muwatukane Mitume wa Mwenyezi Mungu wamewakosea nini,hata kumsema vibaya mtu aliyekufa au ambaye hayupo uisilamu umekataza,sababu laiti angekuwepo angejitetea. Muwe na busara mliyeingiza matusi humu ndani
 
Huwa sipendi watu wanaosemea vibaya Dini za wengine,asilimia kubwa wamelelewa malezi mabaya.Kwanini muwatukane Mitume wa Mwenyezi Mungu wamewakosea nini,hata kumsema vibaya mtu aliyekufa au ambaye hayupo uisilamu umekataza,sababu laiti angekuwepo angejitetea.Muwe na busara mliyeingiza matusi humu ndani

Hawana cha kujitetea, hoja zao ni matusi na kumkashifu/kumtukana Mtume wetu Muhammad S.A.W na waislamu kwa ujumla.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom