Baba Sangara
JF-Expert Member
- Dec 16, 2007
- 293
- 154
Dar es Salaam. Serikali ya Uingereza imeitaka Tanzania na Jumuiya ya Kimataifa kuiunga mkono katika kupinga kitendo cha Urusi kutumia sumu aina ya Novichok katika jaribio la kumuua Sergei Skripal na binti yake, Yulia.
Tukio hilo lilitokea mwishoni mwa wiki iliyopita huko Salisbury, Uingereza na kwa sasa Skripal na Yulia wana hali mbaya hospitali.
Akizungumza na vyombo vya habari jijini Dar es Salaam leo, Machi 16, Balozi wa Uingereza nchini, Sarah Cooke amesema nchi yake haitavumilia majaribio yoyote ya mauaji ya watu wasio na hatia ndani ya ardhi yake.
Cooke amesisitiza kwamba ni wazi Urusi ilihusika kwenye jaribu hilo na walipewa nafasi ya kujieleza kwanini waliamua kutumia sumu hiyo ndani ya Uingereza licha ya kwamba matumizi ya kemikali kama silaha ni kinyume cha sheria za kimataifa, hata hivyo, mpaka sasa hawajatoa maelezo kuhusu suala hilo.
“Baadaye leo nitaonana na waziri wa mambo ya nje ili kumweleza kuhusu jambo hili na kuomba ushirikiano wa Tanzania. Ninaamini Tanzania iko pamoja nasi katika hili,” amesema balozi huyo katika mkutano wake na vyombo vya habari.
Mpaka sasa Uingereza inaungwa mkono na Marekani, Ufaransa, Ujerumani, Austalia na Umoja wa Kujihami wa Nchi za Magharibi (Nato). Pia, imeripoti suala hilo kwenye Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa.
Tukio hilo linatishia uhusiano wa kidiplomasia kati ya Uingereza na Urusi.
Mpaka sasa Uingereza imechukua hatua mbalimbali ikiwamo kuwatimua maofisa 23 wa intelijensia wa Urusi nchini humo. Pia, Uingereza imefuta ziara ya Waziri wa Mambo ya Nje wa Urusi, Sergey Lavrov.
Vilevile, Waziri Mkuu wa Uingereza, Theresa May ametangaza kwamba hakuna waziri yeyote au mtu yeyote kutoka familia ya kifalme atakayehudhuria kombe la dunia linalotarajiwa kufanyika Juni mwaka huu huko Urusi.
Chanzo: Mwananchi
Tukio hilo lilitokea mwishoni mwa wiki iliyopita huko Salisbury, Uingereza na kwa sasa Skripal na Yulia wana hali mbaya hospitali.
Akizungumza na vyombo vya habari jijini Dar es Salaam leo, Machi 16, Balozi wa Uingereza nchini, Sarah Cooke amesema nchi yake haitavumilia majaribio yoyote ya mauaji ya watu wasio na hatia ndani ya ardhi yake.
Cooke amesisitiza kwamba ni wazi Urusi ilihusika kwenye jaribu hilo na walipewa nafasi ya kujieleza kwanini waliamua kutumia sumu hiyo ndani ya Uingereza licha ya kwamba matumizi ya kemikali kama silaha ni kinyume cha sheria za kimataifa, hata hivyo, mpaka sasa hawajatoa maelezo kuhusu suala hilo.
“Baadaye leo nitaonana na waziri wa mambo ya nje ili kumweleza kuhusu jambo hili na kuomba ushirikiano wa Tanzania. Ninaamini Tanzania iko pamoja nasi katika hili,” amesema balozi huyo katika mkutano wake na vyombo vya habari.
Mpaka sasa Uingereza inaungwa mkono na Marekani, Ufaransa, Ujerumani, Austalia na Umoja wa Kujihami wa Nchi za Magharibi (Nato). Pia, imeripoti suala hilo kwenye Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa.
Tukio hilo linatishia uhusiano wa kidiplomasia kati ya Uingereza na Urusi.
Mpaka sasa Uingereza imechukua hatua mbalimbali ikiwamo kuwatimua maofisa 23 wa intelijensia wa Urusi nchini humo. Pia, Uingereza imefuta ziara ya Waziri wa Mambo ya Nje wa Urusi, Sergey Lavrov.
Vilevile, Waziri Mkuu wa Uingereza, Theresa May ametangaza kwamba hakuna waziri yeyote au mtu yeyote kutoka familia ya kifalme atakayehudhuria kombe la dunia linalotarajiwa kufanyika Juni mwaka huu huko Urusi.
Chanzo: Mwananchi