Nikupateje
JF-Expert Member
- Dec 22, 2009
- 1,334
- 988
Mambo mengi humu duniani nayasoma katika English zaidi kuliko kiswahili. Lakini nimekutana na tatizo moja nimeshindwa kulivumilia, wale wenye uwezo nisaidieni.
Ninaposoma katika English, najua kwamba United Kingdom huitwa kwa kifupi UK au Great Britain (GB) na ndimo humo kuna England, Scotland, Wales na Northen-Ireland.
Lakini hiyo UK au Great Britain inapoandikwa kwa kiswahili panaandikwa Uingereza. Lakini wakati huohuo eneo mojawapo la UK liitwalo England utakuta nalo kwenye kiswahili panaandikwa Uingereza!
Ukitazama hata kwenye michezo, utakuta wanasema LIGI YA UINGEREZA, wakati ukweli si ligi ya UK kote, bali ni ile sehemu iitwayo England ambako Scotland kwao na Ferguson hakuguswi.
Hapa mnisaidie. Ukitaja neno Uingereza unakuwa una-refer ni hasa? Je, ni ile England au UK yote?
Je, au haya ndiyo yale ya kumezwa kwenye miungano ambapo unaweza kusema England imewameza akina Scotland na wenzake kiasi kwamba ikitamkwa England basi bila kujali utamaduni wa zingine inamaanisha UK yote.
Kama ni hivyo, basi nchi kama Zanzibar zilikuwa na haki ya kuwa na hofu kama hiyo, maana hata timu ya taifa ya ikiwa haina mzanzibar hata mmoja bado tunaiita TIMU YA TAIFA YA TANZANIA.
Saidia kutafakari?
Ninaposoma katika English, najua kwamba United Kingdom huitwa kwa kifupi UK au Great Britain (GB) na ndimo humo kuna England, Scotland, Wales na Northen-Ireland.
Lakini hiyo UK au Great Britain inapoandikwa kwa kiswahili panaandikwa Uingereza. Lakini wakati huohuo eneo mojawapo la UK liitwalo England utakuta nalo kwenye kiswahili panaandikwa Uingereza!
Ukitazama hata kwenye michezo, utakuta wanasema LIGI YA UINGEREZA, wakati ukweli si ligi ya UK kote, bali ni ile sehemu iitwayo England ambako Scotland kwao na Ferguson hakuguswi.
Hapa mnisaidie. Ukitaja neno Uingereza unakuwa una-refer ni hasa? Je, ni ile England au UK yote?
Je, au haya ndiyo yale ya kumezwa kwenye miungano ambapo unaweza kusema England imewameza akina Scotland na wenzake kiasi kwamba ikitamkwa England basi bila kujali utamaduni wa zingine inamaanisha UK yote.
Kama ni hivyo, basi nchi kama Zanzibar zilikuwa na haki ya kuwa na hofu kama hiyo, maana hata timu ya taifa ya ikiwa haina mzanzibar hata mmoja bado tunaiita TIMU YA TAIFA YA TANZANIA.
Saidia kutafakari?