Uingereza ni nchi gani? Je, ni Britain au England?

Nafikiri kwa ujumla tayari unaelewa vizuri Nikupateje – kama Kiswahili changu kinafika kuelewa yote uliyoyaandika! Mimi ni mwingereza anayeishi hapa Uingereza na ninafundisha lugha ya Kiingereza kwa wageni katika shule ya kimataifa. Baadhi ya wanafunzi wangu (wanaotoka nchi mbalimbali) wanashangaa kabisa ninapowaambia kwamba England siyo nchi ya kujitegemea (it is not an independent country). England ni sehemu mmoja ya United Kingdom – kama unavyojua. Sasa tatizo silo tatizo la geografia bali ya matumizi! Watu wengi ulimwenguni wanatumia neno ‘England’ lakini wanafikiri lina maana ya nchi nzima (UK). Kosa hili ni kwa kawaida siku hizi – kosa hili lilikua kwa miaka mingi na sasa inakaribia siyo ‘kosa’ – ni jambo la matumizi ya watu tu – imekuwa ‘desturi’. Hata hapo Uingereza (England, siyo sehemu nyingine ya United Kingdom) watu wengi wanatumia neno ‘’England kumaanisha nchi nzima (United Kingdom)! Imekuwa lugha ya kila siku ya watu ulimwenguni! Lakini ni hatari kufanya ‘kosa’ hili katika Scotland – watu wa Scotland watakasirika kama ukifanya hivyo, yaani kusema ‘England lakini unamaanisha nchi nzima (the UK)! Basi watu wengi ulimwenguni (hata katika Tanzania) wanatumia neno England (Uingereza) lakini wanamaanisha the United Kingdom, yaani, nchi nzima! Lakini kwa rasmi au kama unataka kusema vizuri juu ya nchi ya kujitegemea, correct ni ‘the United Kingdom’ au ‘Great Britain’ (United Kingdom = Great Britain + Northern Ireland). Naamini tatizo hili ya machanganyiko ya maneno inahusu nchi yetu tu. (Nafikiri ulitoa mfano nzuri sana ulipotaja jambo la English League football!)
Sasa, natumaini niliweza kwa kiasi kukusaidia na swali hili, licha ya upungufu wa Kiswahili changu! Samahani kama sikuelewa vizuri!

are you ENGLISH or BRITISH???
 
Mambo mengi humu duniani nayasoma katika English zaidi kuliko kiswahili. Lakini nimekutana na tatizo moja nimeshindwa kulivumilia, wale wenye uwezo nisaidieni.

Ninaposoma katika English, najua kwamba United Kingdom huitwa kwa kifupi UK au Great Britain (GB) na ndimo humo kuna England, Scotland, Wales na Northen-Ireland.

Lakini hiyo UK au Great Britain inapoandikwa kwa kiswahili panaandikwa Uingereza. Lakini wakati huohuo eneo mojawapo la UK liitwalo England utakuta nalo kwenye kiswahili panaandikwa Uingereza!

Ukitazama hata kwenye michezo, utakuta wanasema LIGI YA UINGEREZA, wakati ukweli si ligi ya UK kote, bali ni ile sehemu iitwayo England ambako Scotland kwao na Ferguson hakuguswi.

Hapa mnisaidie. Ukitaja neno Uingereza unakuwa una-refer ni hasa? Je, ni ile England au UK yote?


Je, au haya ndiyo yale ya kumezwa kwenye miungano ambapo unaweza kusema England imewameza akina Scotland na wenzake kiasi kwamba ikitamkwa England basi bila kujali utamaduni wa zingine inamaanisha UK yote.

Kama ni hivyo, basi nchi kama Zanzibar zilikuwa na haki ya kuwa na hofu kama hiyo, maana hata timu ya taifa ya ikiwa haina mzanzibar hata mmoja bado tunaiita TIMU YA TAIFA YA TANZANIA.

Saidia kutafakari?

uingereza ni england.
 
Kumbe! Swali nzuri but also with a sense of humour (sijui 'sense of humour kwa Kiswahili)! Inategemea na muktadha. Kwa ujumla nasema mimi ni English kwa sababu watu wamezoea na jina hili. Kama muktadha (context) inahitaji niwe mahusi zaidi (more specific) au ni muktadha rasmi, nasema 'I am British'. Na wewe?
 
Mambo mengi humu duniani nayasoma katika English zaidi kuliko kiswahili. Lakini nimekutana na tatizo moja nimeshindwa kulivumilia, wale wenye uwezo nisaidieni.

Ninaposoma katika English, najua kwamba United Kingdom huitwa kwa kifupi UK au Great Britain (GB) na ndimo humo kuna England, Scotland, Wales na Northen-Ireland.

Lakini hiyo UK au Great Britain inapoandikwa kwa kiswahili panaandikwa Uingereza. Lakini wakati huohuo eneo mojawapo la UK liitwalo England utakuta nalo kwenye kiswahili panaandikwa Uingereza!

Ukitazama hata kwenye michezo, utakuta wanasema LIGI YA UINGEREZA, wakati ukweli si ligi ya UK kote, bali ni ile sehemu iitwayo England ambako Scotland kwao na Ferguson hakuguswi.

Hapa mnisaidie. Ukitaja neno Uingereza unakuwa una-refer ni hasa? Je, ni ile England au UK yote?


Je, au haya ndiyo yale ya kumezwa kwenye miungano ambapo unaweza kusema England imewameza akina Scotland na wenzake kiasi kwamba ikitamkwa England basi bila kujali utamaduni wa zingine inamaanisha UK yote.

Kama ni hivyo, basi nchi kama Zanzibar zilikuwa na haki ya kuwa na hofu kama hiyo, maana hata timu ya taifa ya ikiwa haina mzanzibar hata mmoja bado tunaiita TIMU YA TAIFA YA TANZANIA.

Saidia kutafakari?

Swali ni gumu majibu tofauti kabisa.....kutokana na mazoea ya lugha yetu....

1.England
2.Britain
3.Great Britain
4.United Kingdom
Viswahili vyake ni vipi?

Kama England ieleweke kabisa ni English Land yaani Nchi ya Waingereza ikimaanisha Nchi ya Waongea Kiingereza. ndiyo haswa Uingereza.

Britain ni maeneo mawili ambayo rasmi yalijulikana kama Brittania yaani England na wales pekee... Brit kifupisho cha British yaani Watu wenye asili ya Lugha ya Kiingereza... Wa British

Great Britain = Hii ni Kusema Eneo la England Scotland na Wales ndio haswa kwa pamoja huitwa Great Britain-Ukiita Uingereza ni Sawa pia

United Kingdom = Huu ni Muungano wa Falme kwenye ardhi ya England,Scotland,Northern Ireland na Wales - Hapo inakuwa si Uingereza tena kwa wale waliozoea kwani kuna mchanganyiko wa Lugha zao pia. uingereza ni Lugha. hapo huitwa Muungano wa Falme. kwa kuwa Lugha rasmi ya U.K ni English basi kuitwa Waingereza si kosa kwa kutumia wingi na si Neno Moja uingereza. kama sie Watanzania na Lugha yetu kiswahili watu wanaweza kutuita waswahili...

Tunaposema Ligi ya Uingereza inamaanisha Ligi ya England tu na hii inajulikna dunia nzima kama mtu anakosea ni makosa yake tu binafsi...

Ligi ya Scotland huwezi iita ligi ya uingereza vile vile na ya wales au N.ireland

Ukisema unaenda U.K lazima mtu akuulize eneo au Falme ipi
 
southern ireland inaitwa REPUBLIC OF IRELAND......ni nchi tofauti[inajitegemea] nje ya UK.....wanatumia EURO CURRENCY....UK wanatumia POUND STERLING

Na hii Northen Ireland nayo ilikuwa ni mojawapo kwenye UK kama hizi zingine, lakini ilijiondoa kwenye 1930s au 1940s ikawa Republic.

Haikuogopaogopa kama wazenji hapa Tanzania ambao wanaogopa kusema wanataka kujitenga lakini wanasingizia kwamba wanataka muungano wa Mkataba!
 
Kumbe! Swali nzuri but also with a sense of humour (sijui 'sense of humour kwa Kiswahili)! Inategemea na muktadha. Kwa ujumla nasema mimi ni English kwa sababu watu wamezoea na jina hili. Kama muktadha (context) inahitaji niwe mahusi zaidi (more specific) au ni muktadha rasmi, nasema 'I am British'. Na wewe?

yaani umenielewa kiundani kabisa....mi ni mtanzania.
 
Vipi na hawa wanaosema wanataka muungano wa mkataba???Si waseme wanajitenga tu tukajua moja lakini sio kila siku kelele nyingi mara tumemezwa cjui mara hiki sio cha muungano kwann wasijitenge tu kama Republic of Ireland kikaeleweka...nasema tu lakini siweki picha.
 
Ni vema sana umeileta hii changamoto mkuu Nikupateje.

Katika hili nadhani ni kasumba tu imetutawala katika matumizi ya kiswahili lakini tunaweza kabisa kupata mwafaka katika kutofautisha mamlaka hizo mbili. Binafsi naona yaweza kuwa hivi;-

England = Uingereza
UK = Muungano wa Kifalme wa Uingereza(MKU)
 
Last edited by a moderator:
Utahangaika sana mkuu. In short hakuna neno la kutofautisha kama wewe unavotaka.

Wakati mwingine nafikiria kwamba kiswahili kinauhaba wa maneno.

Mfano neno PIGA halina maana ya moja kwa moja mpaka ulitungie sentensi ndiyo lieleweke.
 
Utahangaika sana mkuu. In short hakuna neno la kutofautisha kama wewe unavotaka.

Wakati mwingine nafikiria kwamba kiswahili kinauhaba wa maneno.

Mfano neno PIGA halina maana ya moja kwa moja mpaka ulitungie sentensi ndiyo lieleweke.

Uingereza is a noun. Huhitaji kutunga sentensi ili ueleweke unasema nini.
 
Thanks Sir for enlighten me that the term is a worldwide confusion, but a confusion not pardoned in Scotland. Your post is a rich contribution to my long sought knowledge and I can say I've at least finally found what I have been looking for.

Say hallo to all colleagues in UK.

Cheers

hivi kwanini usingemjibu kwa kiswahili kama yeye alivyochangia kwa kiswahili?
 
umejitaidi kutoa mifano mingi ila hapo kwenye mfano wa ligi kuu ya uingereza umeenda chaka....kwenye mpira hakuna ligi inayoitwa England premier league bali kuna english premier league yaani ligi kuu ya uingereza..

ligi inaitwa hivyo kwa sababu timu zinazoshiriki kwenye ligi hiyo maridhawa sio zote zinatoka England bali kuna baadhi ya timu zinatoka Wales mfano wa timu hizo ni Cardiff City na Swansea ambazo zenyewe hazitoki England bali zinatoka Wales.

so hapo bila shaka tunapata jibu kuwa ni halali na wala hujavunja sheria ukisema ni ligi kuu ya uingereza..
 
Kumbe! Swali nzuri but also with a sense of humour (sijui 'sense of humour kwa Kiswahili)! Inategemea na muktadha. Kwa ujumla nasema mimi ni English kwa sababu watu wamezoea na jina hili. Kama muktadha (context) inahitaji niwe mahusi zaidi (more specific) au ni muktadha rasmi, nasema 'I am British'. Na wewe?

Wewe David [ mpendwa789 ] nakujua kama sikosei nilishakuona TBC 1 ukihojiwa na Shaaban Kisu kwenye kipindi cha lulu za kiswahili miezi mingi kidogo imepita na nafkiri ulikuwa pale ubalozi wa Uingereza-Tanzania kama sikosei.

Tokea naanza kusoma post yako ya kwanza nlikuwa naanza kukutambua hata kabla hujajitambulisha kama David, nnayo kumbukumbu kali mno kaka ila nakukubali kwenye Kiswahili uko njema kaka.
 
Kwa hiyo Southern Ireland iko sehemu gani. Au ndo haipo.

kusoma sawa hujui tumekubali hata picha huoni?northern inaonekana hiyo yenye rangi ya yanga unashindwa hata kujiongeza kuwa hiyo ya chini isio na jibu nio southern?
 
Na hii Northen Ireland nayo ilikuwa ni mojawapo kwenye UK kama hizi zingine, lakini ilijiondoa kwenye 1930s au 1940s ikawa Republic.

Haikuogopaogopa kama wazenji hapa Tanzania ambao wanaogopa kusema wanataka kujitenga lakini wanasingizia kwamba wanataka muungano wa Mkataba!

Nadhani ulikua unamaanisha Southern Ireland
 
Mkuu Nikupateje kwa kuzingatia swali lako, Uingereza ni tafsiri ya neno England na wala sio UK.

Ili kuweza kujiridhisha na jibu hili ni vyema ukazingatia historia kwa ufupi.

Mosi, lazima tutambue kwamba kuna kisiwa cha Britania(Britain au Great Britain) kinachojumuisha tawala tatu tofauti nazo ni Uingereza (England), Uskoti(Scotland) na Welisi (Wales).
Mwaka 1707 Uingereza pamoja na Welisi na Uskoti ziliungana kuwa Ufalme wa Muungano wa Britania (The Kingdom of Great Britain).

Pili, mnamo mwaka 1801, Ufalme wa Muungano wa Britania ukaungana na Eire (Ireland) na kutengeneza muungano mpya uliotambulika kwa jina la Ufalme wa Muungano wa Britania na Eire (United Kingdom of Great Britain and Ireland).

Tatu, mwaka 1916 utawala wa Eire ukaleta kashkash na sehemu ya ardhi ikajimegua kutoka United Kingdom of Great Britain and Ireland na baadaye mwaka 1922 kutengeneza taifa jipya lililojipa jina la Jamhuri ya Eire.

Nne, kutokana na kumeguka kwa Eire, mwaka 1927 ukazaliwa muungano mpya wa tatu ambao upo hata sasa ukiwa na jina la Ufalme wa Muungano wa Britania na Eire ya Kaskazini (United Kingdom of Great Britain and Northern Ireland).

Naamini utakuwa umenielewa na hatimaye umepata kilichokutatiza.
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom