Uimara wa gari aina ya Nissan X trail.

MWAKYONIKE

New Member
May 26, 2014
4
0
Habari za leo ndugu wadau wa Jamii forum. Naomba kufahamu uimara wa gari aina ya Nissan X trail kwa matumizi ya kila siku mfano nchini Tanzania . Mfano kwa matumizi ya kila siku hapa Dar es salaam ukizingatia mie nakaa kilomita 45 kutoka katikati ya jiji na ninalazimika kutembea km 20 za barabara yavumbi. Kwa hiyo kila sikuninatembea km 90 na wakati mwingine ninalazimika kwenda mkoani Mbeya kijijini kwetu wilaya ya Rungwe. Naomba msaada kwa wale wenye uzoefu wa gari hii au wenye utaalam wa kiufundi kuhusu gari hii. Endapo hainifai vp kuhusu Toyota voltz?
 
Habari za leo ndugu wadau wa Jamii forum. Naomba kufahamu uimara wa gari aina ya Nissan X trail kwa matumizi ya kila siku mfano nchini Tanzania . Mfano kwa matumizi ya kila siku hapa Dar es salaam ukizingatia mie nakaa kilomita 45 kutoka katikati ya jiji na ninalazimika kutembea km 20 za barabara yavumbi. Kwa hiyo kila sikuninatembea km 90 na wakati mwingine ninalazimika kwenda mkoani Mbeya kijijini kwetu wilaya ya Rungwe. Naomba msaada kwa wale wenye uzoefu wa gari hii au wenye utaalam wa kiufundi kuhusu gari hii. Endapo hainifai vp kuhusu Toyota voltz?


Uimara wa gari haupimwi kwa kilometa ngapi unatembea kwa siku au barabara ya vumbi, mahitaji hayo unayosema hata ukinuniua toyota diut au vits zinaweza kuhumili bila shida yoyote

Angalia barabara unazotembea ni mbovu kiasi gani ndio itasmini gari gani itafaa kitumia, lakini kama ni vumbi tu bila madimbwi au mashimo then nunia hata diut nini hiyo hiyo xtrail
 
Nashukuru sana kwa mchango wako alphonce.net kifupi kwanza barabara ninayotembea ndio ina mashimo tukizingatia barabata nyingi za vumbi hasa dar es salaam huwa zina mashimo sana kutokana na wingi wa magari na mvuazisizotarajiwa.
Nahitaji gari ambayo ni 4x4 . Nimeona huenda nikiwa na xtrail ya kati ya 2001 na 2004 huenda ikanifaa. Thats whynaomba ushauri wa kitaalam na pia uzoefu kwa waliowahi kuzitumia hizi gari.
 
Bwana mwakyonike nakushauri ununue kati ya hizi hapa toyota rav4,toyota kluger au subaru forester naona kama ni gari zinazohimili shida kuliko x-trail
 
kama pesa ipo extrail ni sex na stong...ila spare parts zake naziuza bei ya juu kuliko nyingine.....alafu sio kila duka unaweza pata spare ...
 
Ok iko hivi it was just jokes ,ni kwamba nis ni gari nzuri out of tz ulaji wa mafuta uko juu,availability ya spare ni bei sana,vox sina uzoefu nayo but go to rav 4....
 
kaka Xtrail ni NISSAN , hivyo kwa swala la spare hapo kuna kazi sana,spare zipo juu hala kuna baadhi ya spare za maana ni mpaka nairobi, hapa bongo ni msiba. mimi nikushauri uangalie unataka gari luxury,sexy, economical au gari ya kazi ya kawaida.


  • Nadia
  • corolla fielder
  • rav 4
  • harrier
  • klugger
hayo ndio mawazo yangu kwako.....

Habari za leo ndugu wadau wa Jamii forum. Naomba kufahamu uimara wa gari aina ya Nissan X trail kwa matumizi ya kila siku mfano nchini Tanzania . Mfano kwa matumizi ya kila siku hapa Dar es salaam ukizingatia mie nakaa kilomita 45 kutoka katikati ya jiji na ninalazimika kutembea km 20 za barabara yavumbi. Kwa hiyo kila sikuninatembea km 90 na wakati mwingine ninalazimika kwenda mkoani Mbeya kijijini kwetu wilaya ya Rungwe. Naomba msaada kwa wale wenye uzoefu wa gari hii au wenye utaalam wa kiufundi kuhusu gari hii. Endapo hainifai vp kuhusu Toyota voltz?
 
X.trail ndo yenyewe itakufaa mi nimetumia miaka miatano sijasikia cha mwai wala bwayy usiwasikilize hawa jamaa wamezoea kwenda garage mwenge kwenye miembe mafundi. Vilaza full spana hawana akili hata moja ukipeleka Gari wanakuqmbia tushushe engine ndo maana wameua bmw nyingi dar
 
Ndugu nunua rav4. Mimi ninauzoefu na rav4 kwa takribani miaka 5. Ni gari ambayo huwezi kutofautisha na land cruiser mkonge iwe kwenye rough road,mud au lami. Ulaji wake unategemea na mwendo pamoja na uimara wa engine. Ingawaje kuna aina nyingi za rav4 ila za kwangu ni za mwaka miaka ya nyuma kwa muundo wa bodi ila kwa engine zinatofautiana kwani moja speed ni hadi 180 na nyingine ni 200. Xtrail tatizo lake ni spare kwani siyo mikoa yote unaweza kupata spare zake
 
Back
Top Bottom