Uhusiano wa Rais Magufuli na nchi za Magharibi una mengi yanayojulikana na yasiyojulikana

Keynez

JF-Expert Member
Feb 12, 2007
2,397
3,884
Huwa napenda kuushughulisha ubongo wangu kwa fikra mbalimbali, nikiwaza na kuwazua mambo kwa muda wa kutosha kabla sijaongea lolote. Ruksa kutofautiana na mimi kimtazamo.

Rais Kikwete alikuwa na maelewano mazuri sana na wale ambao leo wanaitwa 'Mabeberu'. Ukaja uchaguzi wa 2015 wakasema Kikwete ametoa jina la Magufuli kutoka mfukoni. Ikaonekana kama Magufuli amepata Urais kwa bahati-bahati tu lakini sidhani kama ilikuwa ni bahati-bahati kama wengi mnavyodhani.

Nitajikita katika kujibu swali moja. Je maslahi ya 'mabeberu' yameathirika kiasi gani katika utawala wa Magufuli kulinganisha na kipindi cha Kikwete?

Let us follow the money.....

Ukweli ni kuwa maslahi ya mabeberu siyo tu yamelindwa kwa kiasi kikubwa lakini pia yameboreshwa kipindi cha utawala wa Rais Magufuli.

Ndege, Ununuzi wa ndege mpya kwa ajili ya ATCL unaingiza si kiasi kidogo kwenye makampuni ya mabeberu huko Canada. Tena sisi tunalipa kwa CASH MONEY hakuna mambo ya kulipana kwa miaka 20 hapa!!

Madini, Wakati wengine wanashangilia songombingo lile la Acacia, dili mpya linaweza kuwa na manufaa zaidi kwa kampuni ya Barrick kuliko hata mkataba wa zamani.

Kwa kuongezea, hivi mmewahi kujiuliza nchi zingine ambazo nazo zilikuwa chini ya Acacia Mining yaani Kenya, Burkina Faso na Mali mbona hazikuwa zinapiga kelele kama sisi? Je wao wameathirika vipi na dili mpya au wamechukua direction ipi ya kibiashara na Barrick baada ya Acacia kufa?

Bagamoy,. Mahusiano yaliyopo kati ya Marekani na China yanaathiri maamuzi ya kiuchumi pia katika nchi zilizoko nje ya nchi zao husika. Mkataba mkubwa wa bandari ya Bagamoyo ungeipa China fursa na access kubwa ya kibiashara katika ukanda huu. Magufuli amekuja ameupiga stop.

Sitashangaa huu mkataba ukaja kubadilishwa ili Mabeberu wawe pia sehemu ya mkataba pamoja na China.

Usalama, Mabeberu huwa wana mtindo wa kusupport au kufumbia macho matendo ya viongozi wanaoonekana kupigiwa kelele kama viongozi wale watafanya mambo yanayowapendeza. Sera za Mabeberu zimejikita kwenye mambo makuu mawili - Access na Stability na Magufuli bado anawapa vyote hivyo kwa adabu na heshima.

Kwa kuwa zama hizi tumerudi nyuma sana kwenye uwazi serikalini, mengi yanayofanyika hayajulikani wazi. Imefikia hadi viwanja vya ndege vikubwa vinajengwa na haijulikani hela imetoka wapi, manunuzi yamefanyikaje, wapi vilijadiliwa, nk.

Mwana historia maarufu wa Marekani Noam Chomsky aliwahi kuandika kuwa Marekani wana zaidi ya military bases 800 duniani. Sijui toka ameandika hivyo kama idadi hiyo imeongezeka au kupungua.

Hizi bases zinatofautiana ukubwa na mifumo yake. Baadhi zinajulikana na baadhi zinahisiwa (suspected). Baadhi zina wanajeshi wa special operations na baadhi zinatumika tu kwa ajili ya drones na surveillance flights.

Wengi wamejenga mitizamo yao kuhusu uhusiano wa mabeberu na Rais Magufuli kwa kuangalia sababu zisizo na uzito sana. Mfano, Rais Magufuli kutozitembelea nchi hizo za Mabeberu, au kauli za kisiasa za majukwaani, au nyaraka za kibalozi ya 'kutoridhishwa na hili au lile' lakini mwisho wa siku ni muhimu turudi kwenye FACTS.

Ni muda tu kabla hatujajua ukaribu au umbali wa serikali ya Rais Magufuli na Mabeberu uko vipi lakini usidharau uwezekano kuwa Rais Magufuli ana sapoti yote ya Kikwete kwa yote ayafanyayo.
 
Huwa napenda kuushughulisha ubongo wangu kwa fikra mbalimbali, nikiwaza na kuwazua mambo kwa muda wa kutosha kabla sijaongea lolote. Ruksa kutofautiana na mimi kimtazamo.

Rais Kikwete alikuwa na maelewano mazuri sana na wale ambao leo wanaitwa 'Mabeberu'. Ukaja uchaguzi wa 2015 wakasema Kikwete ametoa jina la Magufuli kutoka mfukoni. Ikaonekana kama Magufuli amepata Urais kwa bahati-bahati tu lakini sidhani kama ilikuwa ni bahati-bahati kama wengi mnavyodhani.

Nitajikita katika kujibu swali moja. Je maslahi ya 'mabeberu' yameathirika kiasi gani katika utawala wa Magufuli kulinganisha na kipindi cha Kikwete?

Ukweli ni kuwa maslahi ya mabeberu siyo tu yamelindwa kwa kiasi kikubwa lakini pia yameboreshwa kipindi cha utawala wa Rais Magufuli.

Ndege. Ununuzi wa ndege mpya kwa ajili ya ATCL unaingiza si kiasi kidogo kwenye makampuni ya mabeberu huko Canada. Tena sisi tunalipa kwa CASH MONEY hakuna mambo ya kulipana kwa miaka 20 hapa!!

Madini. Wakati wengine wanashangilia songombingo lile la Acacia, dili mpya linaweza kuwa na manufaa zaidi kwa kampuni ya Barrick kuliko hata mkataba wa zamani.

Kwa kuongezea, hivi mmewahi kujiuliza nchi zingine ambazo nazo zilikuwa chini ya Acacia Mining yaani Kenya, Burkina Faso na Mali mbona hazikuwa zinapiga kelele kama sisi? Je wao wameathirika vipi na dili mpya au wamechukua direction ipi ya kibiashara na Barrick baada ya Acacia kufa?

Bagamoyo. Mahusiano yaliyopo kati ya Marekani na China yanaathiri maamuzi ya kiuchumi pia katika nchi zilizoko nje ya nchi zao husika. Mkataba mkubwa wa bandari ya Bagamoyo ungeipa China fursa na access kubwa ya kibiashara katika ukanda huu. Magufuli amekuja ameupiga stop.

Sitashangaa huu mkataba ukaja kubadilishwa ili Mabeberu wawe pia sehemu ya mkataba pamoja na China.

Usalama. Mabeberu huwa wana mtindo wa kusupport au kufumbia macho matendo ya viongozi wanaoonekana kupigiwa kelele kama viongozi wale watafanya mambo yanayowapendeza. Sera za mabeberu zimejikita kwenye mambo makuu mawili - Access na Stability na Magufuli bado anawapa vyote hivyo kwa adabu na heshima.

Kwa kuwa zama hizi tumerudi nyuma sana kwenye uwazi serikalini, mengi yanayofanyika hayajulikani wazi. Imefikia hadi viwanja vya ndege vikubwa vinajengwa na haijulikani hela imetoka wapi, manunuzi yamefanyikaje, wapi vilijadiliwa, nk.

Mwana historia maarufu wa Marekani Noam Chomsky aliwahi kuandika kuwa Marekani wana zaidi ya military bases 800 duniani. Sijui toka ameandika hivyo kama idadi hiyo imeongezeka au kupungua.

Hizi bases zinatofautiana ukubwa na mifumo yake. Baadhi zinajulikana na baadhi zinahisiwa (suspected). Baadhi zina wanajeshi wa special operations na baadhi zinatumika tu kwa ajili ya drones na surveillance flights.

Wengi wanatoa mitizamo yao kuangalia sababu zisizo na uzito. Mfano, Rais Magufuli kutozitembelea nchi hizo za mabeberu, au kauli za kisiasa za majukwaani, au nyaraka za kibalozi lakini mwisho wa siku ni muhimu turudi kwenye FACTS.

Ni muda tu kabla hatujajua ukaribu au umbali wa serikali ya Rais Magufuli na mabeberu uko vipi lakini usidharau uwezekano kuwa Rais Magufuli ana sapoti yote ya Kikwete kwa yote ayafanyayo.

Vague!
 
"The American strategic analyst Fareed Zakaria estimates that the US has 766 overseas bases, spread over 40 countries, home to 200,000 operatives and occupying 275,000 hectares of foreign land"
How They Rule the World by Pedro Banos

Natumaini nitarajea baadae, baada ya tafakuri
 
Nachojua Mabeberu wana remote ya uchumi wa African countries rejea ZIMBABWE nashangazwa na ndugu yetu kuwapiga majungu kwa kiswahili kwenye ziara zake huku akijua baadhi ya miradi anayozindua ni hela zao katika mtindo wa mikopo na misaada na mbaya zaidi jamaa yetu anasikika wazi akituomba wananchi tumuunge mkono kwenye hii vita ya mabeberu kuwa wana nia mbaya na nchi yetu na anaenda mbali na kusema kuwa ndo wahusika wa kuleta magonjwa mbali mbali kwenye nchi za Africa mfano EBOLA ili wavune mali.HII VITA SIO NZURI KUIPIGANA OPENLY KWA SABABU HATA WAO KAMA HIZO SHUTUMA NI ZA KWELI AU SIO ZA KWELI HAWAFANYI OPENLY HIVYO KUMTAJA FULANI NI ADUI YAKO NA KUANZA KUMSHAMBULIA HUKU WANAOWAZUNGUKA HAWAONI KITHIBITISHO CHOCHOTE CHA UADUI WA ADUI YAKO HUKU KUTAKUFANYA UONEKANE NI MCHOKOZI NA HATIMAE WANAWAZUNGUKA WATAKUPAKA UBAYA WEWE.Kujifanya yumekuwa wakubwa kiasi kwamba kuanzisha bifu na mabeberu always athari zake wananchi ku suffer ila alielianzisha anakula milo mitatu yote kwa siku.KAMA UMENIELEWA NA UANDISHI WANGU MBOVU NAOMBA GONGA LIKE.
 
Nachojua Mabeberu wana remote ya uchumi wa African countries rejea ZIMBABWE nashangazwa na ndugu yetu kuwapiga majungu kwa kiswahili kwenye ziara zake huku akijua baadhi ya miradi anayozindua ni hela zao katika mtindo wa mikopo na misaada na mbaya zaidi jamaa yetu anasikika wazi akituomba wananchi tumuunge mkono kwenye hii vita ya mabeberu kuwa wana nia mbaya na nchi yetu na anaenda mbali na kusema kuwa ndo wahusika wa kuleta magonjwa mbali mbali kwenye nchi za Africa mfano EBOLA ili wavune mali.HII VITA SIO NZURI KUIPIGANA OPENLY KWA SABABU HATA WAO KAMA HIZO SHUTUMA NI ZA KWELI AU SIO ZA KWELI HAWAFANYI OPENLY HIVYO KUMTAJA FULANI NI ADUI YAKO NA KUANZA KUMSHAMBULIA HUKU WANAOWAZUNGUKA HAWAONI KITHIBITISHO CHOCHOTE CHA UADUI WA ADUI YAKO HUKU KUTAKUFANYA UONEKANE NI MCHOKOZI NA HATIMAE WANAWAZUNGUKA WATAKUPAKA UBAYA WEWE.Kujifanya yumekuwa wakubwa kiasi kwamba kuanzisha bifu na mabeberu always athari zake wananchi ku suffer ila alielianzisha anakula milo mitatu yote kwa siku.KAMA UMENIELEWA NA UANDISHI WANGU MBOVU NAOMBA GONGA LIKE.

Wengi wa viongozi duniani ambao wanakuwaga na ajenda za nationalism na kutumia lugha za kebehi kwa nchi za magharibi, lakini baada ya muda huwa inagundulika wanawafanyia kazi hao hao mabeberu.

Mifano ni mingi.
 
Tuseme tu hakuna maslahi ya mabeberu iliyoguswa. Swala la kwenye madini kupitia Acacia lilikuwa wazi na pengine mabeberu waliona kuna pahali na wao walizingua pengine kwa kukiuka makubaliano au kuiba.
 
1 Reactions
Reply
Back
Top Bottom