Candid Scope
JF-Expert Member
- Nov 8, 2010
- 11,883
- 6,884
Askari wakiwatawanya Wananchi waliokusanyika
katika viwanja vya Soweto jijini Arusha
kuombeleza vifo vya wenzao waliouawa kwa bomu
Tangu Tanzania ianze kuwa na uhusiano wa karibu na Taifa la Marekani kipindi cha Rais wa zamani wa Tanzania William Mkapa hali ya amani ilianza kutoweka na papo ushindani wa Tanzania visiwani na Bara uliongezeka. Mara kadhaa tuliambiwa kwamba vyombo vya usalama kutoka nchini Marekani vinatoa mafunzo kwa vyombo vya usalama nchini Tanzania. Isije ikawa yatokeayo nchini ni mazoezi wanayopata toka vyombo vya usalama vya Marekani.
Pamoja na kwamba mfumo wa ushindani wa vyama vingi nchini unaweza kuwa ndio kichocheo, lakini jambo la msingi vyombo vya usalama badala ya kulinda usalama wa wananchi na vyama hivyo vimeguka kuwa kinga ya chama kimoja kilichoshinda uchaguzi mkuu nchini na kuvishinikiza vyama vingine vya siasa.
Kipindi cha awamu ya kwanza uongozi wa hayati Julius Nyerere hatukushuhudia hayo kutokana na ushupavu wake wa kutokukubali kuwalamba miguu wamarekani, hata pale Uingereza ilipotaka kutia mkono wake baada ya uhuru Tanzania iliamua kuvunja uhusiano na Uingereza. Kwetu hatujajifunza hayo ambayo yalisaidia nchi yetu kubaki na amani kutoingiliwa na mijusi ya kibeberu nchini.
Mataifa yaliyokuwa rafiki na Marekani kama Iraq na Libya baadaye walipokuja kugundua janja ya mabeberu na kuamua kuweka pazia wamarekani waligeuka na kuwafanyia propaganda kama za hayati Saadam Husein kumiliki silaha zenye sumu lakini baada ya kushambulia na kuiteka Iraq tuhuma hizo zilishindwa kuthibitishwa wakati wameshaitia nchi katika matatizo.
Baada ya Muamar Gaddafi kuilipua ndege ya Marekani ya PANAM ilishinikizwa kuilipa Marekani kwa kupeleka mafuta, na mkataba ulipoisha wakaamu kumfitini Gaddafi ili waendelee kuchota mafuta huko kwa kutumia propaganda za kuwashirikisha nchi za Ulaya kumwondoa Gaddafi.
Pamoja na nchi za Umoja wa Ulaya kuonyeshwa kutoafiki uvujikaji wa amani nchini hata kutishia hivi karibu kusipokuwa na umakini serikali kulinda amani kuna uwezekano wa kuwekewa vikwazo, Marekani katu haijashtuka na badala yake Serikali ya Tanzania pamoja na uvunjaji wa amani nchini kwa kutumia jeshi la posili simezawadiwa kutembelewa na Rais wa Marekani, kitu ambacho ni mwendelezo wa watangulizi wake Bill Clinton na George Bush.
Dhahiri machafuko nchini ni nafasi ya hawa mabeberu kutugonganishwa watanzania na hivyo kuja kujichotea Uranium kwa ulaini, na kabisa upinzani unavyoonekana kuonyesha sera za uwazi na ulinzi wa mali asili ya nchi yetu sera hizo katu haziwezi kupokeleka kwa Marekani.
Mapambando yakitokea Marekani itakuwa imejihakikishia kupato soko la bidhaa zake za kivita kwa vile kwa sasa wanaandaa soko hilo kwa kuanza kuleta mitafaruku ya hapa na pale, huu ni mwanzo tu kama hatuko makini na itafika siku yatatufika ya Rwanda na Burundi. Huko Kenya Kenyatta anaonekana kutokukubalika kwa Wamarekani, lakini angekuwa Odinga barabara ilishanyooka. Tanzania CCM kwa Marekani ni mwendo mdondo.