Carina
Senior Member
- Jan 4, 2011
- 190
- 65
Wana JF,
Kuna issue moja hapa huwa siielewi elewi hivi .... ni pale mtu anapoibiwa vioo vya gari kama labda site mirros na ambapo ukienda eneo la Gerezani (huwa wanaita mnadani) unavikuta vioo vyako safi kabisa ila ukionekana mtata mtata wanavivunja mbele yako, otherwise ukionekana mwema, basi itabidi uvinunue tu kwa gharama.
Cha kushangaza ni kwanini polisi wanashindwa kufuatilia na kujua mzizi uko wapi? kwani inavyoonekana polisi wanajua issue nzima kama si wanashirikiana nao.
Nakumbuka niliwahi kuibiwa site mirrors wakati naenda kutafuta Kariakoo, polisi wakanikamata kwamba naendesha gari bila site mirros, nikawaambia ndio kwanza natafuta nyingine kwani niliibiwa jana usiku, cha kushangaza polisi hao hao wakanishauri niende Gerezani kwani vipo vingi.
Sasa sijui inakuwaje hapo wajameni ...
Kuna issue moja hapa huwa siielewi elewi hivi .... ni pale mtu anapoibiwa vioo vya gari kama labda site mirros na ambapo ukienda eneo la Gerezani (huwa wanaita mnadani) unavikuta vioo vyako safi kabisa ila ukionekana mtata mtata wanavivunja mbele yako, otherwise ukionekana mwema, basi itabidi uvinunue tu kwa gharama.
Cha kushangaza ni kwanini polisi wanashindwa kufuatilia na kujua mzizi uko wapi? kwani inavyoonekana polisi wanajua issue nzima kama si wanashirikiana nao.
Nakumbuka niliwahi kuibiwa site mirrors wakati naenda kutafuta Kariakoo, polisi wakanikamata kwamba naendesha gari bila site mirros, nikawaambia ndio kwanza natafuta nyingine kwani niliibiwa jana usiku, cha kushangaza polisi hao hao wakanishauri niende Gerezani kwani vipo vingi.
Sasa sijui inakuwaje hapo wajameni ...