Meitinyiku L. Robinson
JF-Expert Member
- Aug 29, 2011
- 412
- 90
Nianze kwa kukiri kuwa ni mgeni humu jamvini ila wa kupost lakini ni mwenyeji sana wa kupita na kusoma yaliyojiri na yanayojiri kila kunapokuwa leo hasa ndani ya nchi yangu manake naipenda sana nchi yangu. Niwapongeze wanajamvi wote kwa kazi zenu za kijamii na kitaifa.
Lakini vile vile niwaombe kwa atakayeweza naamini yupo atusaidie ku-upload picha TATU hapa ili wanajamvi waweze kujadili swala hili critically; Moja Picha ya Mhe. Pro. Mark Mwandosya (si lengo letu kumjadili mgonjwa lakini naamini Mungu ni mwingi wa rehema atamponya) Picha ya pili ni ya Mhe. sana Mzee wetu Marehemu Mosses Nauye, Waraka wa Paulo kwa Wafilipi neno linasema kwa kuwa kuishi kwangu ni Kristo na kufa ni faida Mungu ampe uzima wa Milele) na Picha ya Tatu ni ya Katibu wa Itikadi na Uenezi (hereinafter to be referred to as Katibu).
Itambulike vile vile kuwa si nia yangu kujadili maisha binafsi ya mtu ila kwa kuzingatia Taifa langu na huko tunakoelekea na jinsi nafsi za kiuongozi ndani ya Taifa langu zinavyotolewa kwa watu wa namna flani imenibidi kufanya hivyo ili kujiridhisha na baadae Taifa linapochukua uamuzi lijue kabisa maamuzi hayo ni sawa na vile vile hakuna chembe yoyote ya uongo (earlier the best) Baada ya utangulizi huo naomba sasa nianze hivi;
Ndugu zangu katika mambo yanayokera katika Taifa letu sasa hivi ni hili wanaloliita "mtandao" ni ukweli usiopingika kuwa neno "gamba" limekuja tu lakini kiithbati mitandao ndiyo iliyozaa neno "gamba". Na binafsi hili linakera kwa kuwa kama wenzangu ambavyo mmekuwa mkilalamika wazi wazi Taifa limesimama hakuna kinachoendelea katika jamii ya watanzania ambao waliahidiwa "maisha bora kwa kila Mtanzania" kumbe ni maisha bora kwa kila mwana'system'.
Naanimi kabisa kabisa miaka mitano itaisha hakuna kilichofanyika kwa kuwa ni kweli hatuna kiongozi anayeweza kuamua chochote (maamuzi magumu juu Taifa kwa sasa). Kwa kuwa kwangu hayo makundi ndiyo nionayo kuwa chanzo cha yote na zaidi kuchochewa na Katibu chini ya mwamvuli wa ufisadi, na gamba natamani kujua nia yake halisi ni ipi katika Taifa hili alilotupa Mungu.
Wanajamvi wenzangu haitoshi tu kusema ndani ya Chama tawala kuna makundi na kutaja wahusika bila kujua chanzo (essence) hasa cha hayo makundi . Najua wengine ni kwa sababu flani alisababisha yeye apate nafasi flani hivyo inampasa amuunge mkono kwa gharama yeyote ile. Sasa napata taabu kidogo juu ya Katibu hasa kuhusu kundi lake na nafasi aliyo nayo (na kama kweli hivi ndivyo alivyo na ndivyo atakavyokuwa nawashauri watu wa Masasi wakatoe sadaka Kanisani na Misikitni kumshukuru Mungu huyo mtu kutoka huko).
Kuna wengi wanaodhani labda mtajwa ni kundi la yule Waziri wa Jumuiya eti kwa sababu walianzisha Chama ndani ya Chama pamoja lakini bado utata na migongano ipo. Japo ni habari za kusikika (hearsay) ila naamini kwa kauli ya jamvi hili "Home of Great Thinkers" (hereinafter be reffered to as HGT) naamini pasipo shaka mtachambua, mtafikiri na hatimaye tunaweza toka na kitu.
Lakini kuna wengine tunafikiri anaweza kuwa kundi moja na yule Waziri mwingine wa mambo ya nje na hii ni kutokana na hela (Takribani Dola Milioni 2) za uchaguzi alizozichangia kiongozi mmoja wa Africa alilyetolewa madarakani hivi karibuni. Fedha ambazo kiongozi huyo aliagiza zikachukuliwe Tripoli kwa kuwa asingeweza kuzituma kwa Bank, na akatmwa Mhe.
Waziri mmoja kwenda kuzichukua na zilipoingia nchini waligawana watu wawili tu (HGT watu hao wanafikirika kwa kuwa kuna aliyetuma na mtumwa mwenyewe) na fedha hizo hizo ndizo zinazotumika kutengeneza mitandao nchi nzima kwa ajili ya mwaka 2015 (mnaweza mkarejea kauli ya vijana wa Arusha kwamba "kuna Waziri amewapa fedha zaidi ya Milioni 60 ili atengenezewe mtandao na kuwatukana viongozi wajuu waandamizi waliopo na hata waliostaafu"). Sasa kwa mtazamo huu unaweza fikiri labda hela hizi nazo zinaweza kutulazimisha kufikiri kuwa Nape atakuwa kundi hilo lakini vile vile bado kuna utata.
Wengine tukadhani kuwa Katibu anatukana tukana baadhi ya viongozi kwa kuwa katumwa na "Mwenyekiti " wake kufanya hivyo lakini kadiri siku zinavyozidi kwenda haya nayo yanaonekana kama vile yalikuwa yake binafsi kwa kuwa alichotumwa na alichotakiwa kukifanya kapitiliza zaidi ya matarajio na zaidi ya kazi aliyopewa au aliyotumwa kufanya nadhani Serikali yake ingepata mtendaji wa namna hiyo Watanzania wenzangu haya matatizo tuliyonayo kila siku yangepungua kama si kuisha kabisa.
Bado vile vile tukadhani labda anafanya hivyo kwa kulipiza yale naye aliyofanyiwa wakati akigombea nafasi mbali mbali ila ukijaribu kuangalia katika nyanja za Kisiasa bado hili linaonekana kupwaya manake kwa kufanya hivyo basi angekutaka kafikia hatua flani mpaka leo lakini bado hajafika kokote. Zipo sababu nyingi ila zimetajwa hizo hapo juu kama baadhi.
Kuna kundi jingine ambalo hili linaoneana kuwa na sababu za msingi kwamba Katibu yumo kundi moja na Mhe. Waziri wa Maji na sababu zinazotolewa na watu hawa inahitaji sana umakini kusimami na kuamini katika yote. Kimtazamo tunaweza fikiri kuwa labda Katibu yumo kundi hilo kwa kuwa mtajwa Waziri hana Scandal nyingi nchi hii ila kwangu binafsi hilo halitoshi kuthibitisha kuwa ndiyo sababu ya Katibu kuwa kundi hilo manake hata Mhe. PM hakuwa na Scandal lakini Watanzania wameshapoteza imani kabisa na utendaji wake kama kiongozi wa Serikali Bungeni na vile vile kama Mtendaji Mkuu wa Serikali.
Watanzania wameonesha kuwa nci hii inahitaji Watendaji (emphasis added). Sasa sababu hiyo ambayo hata mimi nimeshindwa kabisa kuitambua mpaka leo ni kunipelekea kuomba wanajamvi humu (HGT) mnisaide kwa kufikiri na kiuchunguzi. Na hili limenipelekea kuwa na maswali mengi ila moja ntakalo anza nao ni hili
"is it possible that Katibu was borne out of the wedlock???" niliomba kwa atayeweza atusaidie ku-upload picha ili mazungumz haya yalete mantiki.
Naamini sana nafasi aliyonayo Katibu ni kubwa mno na ina heshima kubwa sana ndani na nje ya nchi kama akiitumia ipasavyo, kama ataithamini, ataiheshimu, na kuitambua nafasi hiyo. Katibu anadharaulika yeye mwenyewe kasababisha hayo kwa kutokujua umuhimu wa nafasi yake, nafasi aliyo nayo Katibu si ya kumtukana wala kutupiana maneno na Dr. Slaa, au kiongozi yeyote yule wa Upinzani ndani ya Taifa hili, nafasi aiyonayo si kuwatukana kina Edward, na wengine wastaafu au waliopo Serikalini, bali nafasi hiyo ni ya kuhakikisha kuwa Chama kinajengwa na kuaminiwa na wananchi.
Na kukijenga Chama si lazma atukane mtu na hapo ndipo neno kubwa na lenye thamani linapohitaji "BUSARA" kiongozi makini busara ndiyo pekee itakayo mvusha daraja moja kwenda jingine; Mimi leo sioni shida kumfuata Dr. Slaa na kuzungumza naye na kupata ushauri wake hiyo kwangu si dhambi hata kidogo kama kweli umekomaa kisiasa, hata kama si Dr. Slaa wakati mwingine huwa nafikiria watu kama kina Kinana, Mzee Mwinyi, Mzee Mkapa, Cleopa David, huwa wanakuwa wapi.
Kama kweli CCM wlifanya hivyo ili kuwafurahisha VIJANA naomba niseme tu hapa walikosea sana vijana hatukutaka kuwa impressed na mtu wa namna ile Taifa kwanza.........
Baada ya kusema hayo bila kujali itikadi ya vyama niwapongeze sana Mhe. January Makamba (Mb), Mhe. John John Mnyika (Mb), Mhe. Zitto Zuberi Kabwe (Mb), Mhe. David Kafulila (Mb) hiyo ndo sampuli ya vijana tunaowataka waliotulia kiakili, wenye mtazamo wa Taifa, wenye heshma kwa Bunge, Umma na Taifa kwa ujumla, wenye kujenga hoja kwa maslahi ya Taifa bila kujali vyama vyao, na wenye nidhamu ya hali ya juu hata pale ambapo chama chao kinaoneka kupwaya.
Naomba kutoa hoja
Lakini vile vile niwaombe kwa atakayeweza naamini yupo atusaidie ku-upload picha TATU hapa ili wanajamvi waweze kujadili swala hili critically; Moja Picha ya Mhe. Pro. Mark Mwandosya (si lengo letu kumjadili mgonjwa lakini naamini Mungu ni mwingi wa rehema atamponya) Picha ya pili ni ya Mhe. sana Mzee wetu Marehemu Mosses Nauye, Waraka wa Paulo kwa Wafilipi neno linasema kwa kuwa kuishi kwangu ni Kristo na kufa ni faida Mungu ampe uzima wa Milele) na Picha ya Tatu ni ya Katibu wa Itikadi na Uenezi (hereinafter to be referred to as Katibu).
Itambulike vile vile kuwa si nia yangu kujadili maisha binafsi ya mtu ila kwa kuzingatia Taifa langu na huko tunakoelekea na jinsi nafsi za kiuongozi ndani ya Taifa langu zinavyotolewa kwa watu wa namna flani imenibidi kufanya hivyo ili kujiridhisha na baadae Taifa linapochukua uamuzi lijue kabisa maamuzi hayo ni sawa na vile vile hakuna chembe yoyote ya uongo (earlier the best) Baada ya utangulizi huo naomba sasa nianze hivi;
Ndugu zangu katika mambo yanayokera katika Taifa letu sasa hivi ni hili wanaloliita "mtandao" ni ukweli usiopingika kuwa neno "gamba" limekuja tu lakini kiithbati mitandao ndiyo iliyozaa neno "gamba". Na binafsi hili linakera kwa kuwa kama wenzangu ambavyo mmekuwa mkilalamika wazi wazi Taifa limesimama hakuna kinachoendelea katika jamii ya watanzania ambao waliahidiwa "maisha bora kwa kila Mtanzania" kumbe ni maisha bora kwa kila mwana'system'.
Naanimi kabisa kabisa miaka mitano itaisha hakuna kilichofanyika kwa kuwa ni kweli hatuna kiongozi anayeweza kuamua chochote (maamuzi magumu juu Taifa kwa sasa). Kwa kuwa kwangu hayo makundi ndiyo nionayo kuwa chanzo cha yote na zaidi kuchochewa na Katibu chini ya mwamvuli wa ufisadi, na gamba natamani kujua nia yake halisi ni ipi katika Taifa hili alilotupa Mungu.
Wanajamvi wenzangu haitoshi tu kusema ndani ya Chama tawala kuna makundi na kutaja wahusika bila kujua chanzo (essence) hasa cha hayo makundi . Najua wengine ni kwa sababu flani alisababisha yeye apate nafasi flani hivyo inampasa amuunge mkono kwa gharama yeyote ile. Sasa napata taabu kidogo juu ya Katibu hasa kuhusu kundi lake na nafasi aliyo nayo (na kama kweli hivi ndivyo alivyo na ndivyo atakavyokuwa nawashauri watu wa Masasi wakatoe sadaka Kanisani na Misikitni kumshukuru Mungu huyo mtu kutoka huko).
Kuna wengi wanaodhani labda mtajwa ni kundi la yule Waziri wa Jumuiya eti kwa sababu walianzisha Chama ndani ya Chama pamoja lakini bado utata na migongano ipo. Japo ni habari za kusikika (hearsay) ila naamini kwa kauli ya jamvi hili "Home of Great Thinkers" (hereinafter be reffered to as HGT) naamini pasipo shaka mtachambua, mtafikiri na hatimaye tunaweza toka na kitu.
Lakini kuna wengine tunafikiri anaweza kuwa kundi moja na yule Waziri mwingine wa mambo ya nje na hii ni kutokana na hela (Takribani Dola Milioni 2) za uchaguzi alizozichangia kiongozi mmoja wa Africa alilyetolewa madarakani hivi karibuni. Fedha ambazo kiongozi huyo aliagiza zikachukuliwe Tripoli kwa kuwa asingeweza kuzituma kwa Bank, na akatmwa Mhe.
Waziri mmoja kwenda kuzichukua na zilipoingia nchini waligawana watu wawili tu (HGT watu hao wanafikirika kwa kuwa kuna aliyetuma na mtumwa mwenyewe) na fedha hizo hizo ndizo zinazotumika kutengeneza mitandao nchi nzima kwa ajili ya mwaka 2015 (mnaweza mkarejea kauli ya vijana wa Arusha kwamba "kuna Waziri amewapa fedha zaidi ya Milioni 60 ili atengenezewe mtandao na kuwatukana viongozi wajuu waandamizi waliopo na hata waliostaafu"). Sasa kwa mtazamo huu unaweza fikiri labda hela hizi nazo zinaweza kutulazimisha kufikiri kuwa Nape atakuwa kundi hilo lakini vile vile bado kuna utata.
Wengine tukadhani kuwa Katibu anatukana tukana baadhi ya viongozi kwa kuwa katumwa na "Mwenyekiti " wake kufanya hivyo lakini kadiri siku zinavyozidi kwenda haya nayo yanaonekana kama vile yalikuwa yake binafsi kwa kuwa alichotumwa na alichotakiwa kukifanya kapitiliza zaidi ya matarajio na zaidi ya kazi aliyopewa au aliyotumwa kufanya nadhani Serikali yake ingepata mtendaji wa namna hiyo Watanzania wenzangu haya matatizo tuliyonayo kila siku yangepungua kama si kuisha kabisa.
Bado vile vile tukadhani labda anafanya hivyo kwa kulipiza yale naye aliyofanyiwa wakati akigombea nafasi mbali mbali ila ukijaribu kuangalia katika nyanja za Kisiasa bado hili linaonekana kupwaya manake kwa kufanya hivyo basi angekutaka kafikia hatua flani mpaka leo lakini bado hajafika kokote. Zipo sababu nyingi ila zimetajwa hizo hapo juu kama baadhi.
Kuna kundi jingine ambalo hili linaoneana kuwa na sababu za msingi kwamba Katibu yumo kundi moja na Mhe. Waziri wa Maji na sababu zinazotolewa na watu hawa inahitaji sana umakini kusimami na kuamini katika yote. Kimtazamo tunaweza fikiri kuwa labda Katibu yumo kundi hilo kwa kuwa mtajwa Waziri hana Scandal nyingi nchi hii ila kwangu binafsi hilo halitoshi kuthibitisha kuwa ndiyo sababu ya Katibu kuwa kundi hilo manake hata Mhe. PM hakuwa na Scandal lakini Watanzania wameshapoteza imani kabisa na utendaji wake kama kiongozi wa Serikali Bungeni na vile vile kama Mtendaji Mkuu wa Serikali.
Watanzania wameonesha kuwa nci hii inahitaji Watendaji (emphasis added). Sasa sababu hiyo ambayo hata mimi nimeshindwa kabisa kuitambua mpaka leo ni kunipelekea kuomba wanajamvi humu (HGT) mnisaide kwa kufikiri na kiuchunguzi. Na hili limenipelekea kuwa na maswali mengi ila moja ntakalo anza nao ni hili
"is it possible that Katibu was borne out of the wedlock???" niliomba kwa atayeweza atusaidie ku-upload picha ili mazungumz haya yalete mantiki.
Naamini sana nafasi aliyonayo Katibu ni kubwa mno na ina heshima kubwa sana ndani na nje ya nchi kama akiitumia ipasavyo, kama ataithamini, ataiheshimu, na kuitambua nafasi hiyo. Katibu anadharaulika yeye mwenyewe kasababisha hayo kwa kutokujua umuhimu wa nafasi yake, nafasi aliyo nayo Katibu si ya kumtukana wala kutupiana maneno na Dr. Slaa, au kiongozi yeyote yule wa Upinzani ndani ya Taifa hili, nafasi aiyonayo si kuwatukana kina Edward, na wengine wastaafu au waliopo Serikalini, bali nafasi hiyo ni ya kuhakikisha kuwa Chama kinajengwa na kuaminiwa na wananchi.
Na kukijenga Chama si lazma atukane mtu na hapo ndipo neno kubwa na lenye thamani linapohitaji "BUSARA" kiongozi makini busara ndiyo pekee itakayo mvusha daraja moja kwenda jingine; Mimi leo sioni shida kumfuata Dr. Slaa na kuzungumza naye na kupata ushauri wake hiyo kwangu si dhambi hata kidogo kama kweli umekomaa kisiasa, hata kama si Dr. Slaa wakati mwingine huwa nafikiria watu kama kina Kinana, Mzee Mwinyi, Mzee Mkapa, Cleopa David, huwa wanakuwa wapi.
Kama kweli CCM wlifanya hivyo ili kuwafurahisha VIJANA naomba niseme tu hapa walikosea sana vijana hatukutaka kuwa impressed na mtu wa namna ile Taifa kwanza.........
Baada ya kusema hayo bila kujali itikadi ya vyama niwapongeze sana Mhe. January Makamba (Mb), Mhe. John John Mnyika (Mb), Mhe. Zitto Zuberi Kabwe (Mb), Mhe. David Kafulila (Mb) hiyo ndo sampuli ya vijana tunaowataka waliotulia kiakili, wenye mtazamo wa Taifa, wenye heshma kwa Bunge, Umma na Taifa kwa ujumla, wenye kujenga hoja kwa maslahi ya Taifa bila kujali vyama vyao, na wenye nidhamu ya hali ya juu hata pale ambapo chama chao kinaoneka kupwaya.
Naomba kutoa hoja