Uhuru wa Vyombo vya Habari katika rasimu ya katiba iliyoandaliwa na Jaji Warioba

Kurzweil

JF-Expert Member
May 25, 2011
6,622
8,397
Ibara ya 31 -(1) Kila mtu ana haki na uhuru wa kutafuta, kupata, kutumia na kusambaza habari na taarifa na kuanzisha vyombo vya habari na njia nyingine za upashanaji wa habari bila kujali mipaka ya nchi

(2) Vyombo vya habari vitakuwa huru na vitakuwa na haki ya kupata, kutumia na kusambaza habari na taarifa wanazozipata

Aidha vyombo vya habari vitakuwa na wajibu wa;
(i) kusambaza habari na taarifa kwa wananchi;
(ii) kuheshimu na kulinda utu, heshima, uhuru na staha ya wananchi dhidi ya habari na taarifa wanazozitumia, wanazozitayarisha na kuzisambaza.

(3) Serikali na taasisi zake, asasi za kiraia na watu binafsi watakuwa na wajibu wa kutoa habari kwa umma juu ya shughuli na utekelezaji wa shughuli zao.

(4) Bunge litatunga sheria kwa ajili ya kulinda: (a) haki na uhuru wa vyombo vya habari; na (b) habari na taarifa kwa madhumuni ya usalama wa Taifa, amani, maadili ya umma, haki, staha na uhuru wa watu wengine.
 
Ibara ya 31 -(1) Kila mtu ana haki na uhuru wa kutafuta, kupata, kutumia na kusambaza habari na taarifa na kuanzisha vyombo vya habari na njia nyingine za upashanaji wa habari bila kujali mipaka ya nchi

(2) Vyombo vya habari vitakuwa huru na vitakuwa na haki ya kupata, kutumia na kusambaza habari na taarifa wanazozipata

Aidha vyombo vya habari vitakuwa na wajibu wa;
(i) kusambaza habari na taarifa kwa wananchi;
(ii) kuheshimu na kulinda utu, heshima, uhuru na staha ya wananchi dhidi ya habari na taarifa wanazozitumia, wanazozitayarisha na kuzisambaza.

(3) Serikali na taasisi zake, asasi za kiraia na watu binafsi watakuwa na wajibu wa kutoa habari kwa umma juu ya shughuli na utekelezaji wa shughuli zao.

(4) Bunge litatunga sheria kwa ajili ya kulinda: (a) haki na uhuru wa vyombo vya habari; na (b) habari na taarifa kwa madhumuni ya usalama wa Taifa, amani, maadili ya umma, haki, staha na uhuru wa watu wengine.
hili mpaka tulidai kwa nguvu zote...
 
Back
Top Bottom