Uhuru wa Kuabudu Jumamosi: Kesi ya National Microfinance Bank Ltd (NMB) dhidi ya Neema Akeyo

Apr 26, 2022
64
98
NATIONAL MICROFINANCE BANK LTD (NMB) VS (DHIDI YA) NEEMA AKEYO, CIVIL APPEAL NO. 511 OF 2020, CAT.

Mwandishi: Zakaria Maseke
Advocate Candidate

Hii kesi inahusu mfanyakazi (Neema Akeyo) ambaye alifutwa kazi isivyo halali kwa sababu za ubaguzi wa kidini ambapo alikuwa anaenda kufanya ibada siku za jumamosi kama haki yake Kikatiba ya uhuru wa kuabudu.

Lakini pia, sheria haikufatwa ipasavyo wakati wa kumfuta kazi Neema Akeyo, mfano hakupewa nafasi ya kujitetea kabla ya kuamua kumuachisha kazi.

Watu wengi wameshaiongelea sana. Lakini kutokana na umuhimu wake nimeamua kuitafsiri tena na kuipost ili iwafikie watu wengi hasa waajiri. Kumekuwa na hulka ya kuwanyima wafanyakazi uhuru wa kuabudu, kwa kuwapangia kazi siku za Ibada.

Tuanze na FACTS (STORI YA KESI):

-Neema Akeyo aliajiriwa na Bank ya NMB kama Bank teller, Wilaya ya Karatu.

-Ajira hiyo ilianza tarehe 27/10/2010 mpaka tarehe 5/6/2015 alipofutwa kazi na NMB kwa sababu ya kutoenda kazini (utoro) siku za jumamosi na kutotii mwajiri.

-Neema akaenda kushtaki au kulalamika kwenye Commission for Mediation and Arbitration (CMA) yaani Tume ya Usuluhishi na Uamuzi/Upatanishi, akidai kwamba alifutwa kazi kimakosa na kwamba alipwe fidia kwa kitendo hicho cha NMB kuvunja mkataba wa ajira.

MBELE YA TUME:

-NMB ikakana kuvunja mkataba, ikasema mlalamikaji (Neema) alifutwa kazi kwa sababu halali na kwamba taratibu zote zilifuatwa.

-NMB ikasema kwamba, mlalamikaji alifutwa kazi KWA SABABU YA KUSHINDWA KWENDA KAZINI SIKU ZA JUMAMOSI (UTORO) ambapo ilikuwa ni kinyume na makubaliano ya kazi na kinyume cha sera na kanuni za NMB.

-Baada ya kusikiliza kesi mpaka mwisho, mwamuzi wa Tume aliridhika kwamba, mlalamikaji (Neema) hakufutwa kazi kihalali (was unfairly terminated), na kwamba utaratibu haukufatwa.

-Tume ikasema kwamba, hakuna ushahidi kutoka NMB unaothibitisha kwamba Neema hakuwa anaenda kazini siku za Jumamosi.

-Pia, hata baada ya mlalamikaji kukutwa na makosa, hakupewa nafasi ya kujitetea.

-Hivyo Tume ikasema Neema hakufutwa kazi kihalali.

-Tume ikaamuru, Neema alipwe mshahara wa miezi 36 kama fidia.

NB: (Usiporidhika na maamuzi ya Tume (CMA) unaomba revision (mapitio) kwenye Mahakama ya kazi (Labour Court) - ambayo ni Mahakama Kuu divisheni au kitengo cha Kazi. Zingatia sijasema unakata rufaa (appeal), kuna tofauti kati ya Appeal na Revision.)

-NMB hawakuridhika na maamuzi ya Tume, wakafungua maombi Mahakama kuu, wakiomba maamuzi ya Tume yapitiwe upya.

MAHAKAMA KUU:

-Neema akashinda kesi tena dhidi ya NMB.

- Mahakama Kuu ikatupilia mbali maombi ya NMB, na kupigilia msumari maamuzi ya Tume yaliyompa Neema tuzo ya kulipwa mshahara wa miezi 36.

-Mahakama Kuu nayo ikasema Neema hakufutwa kazi kihalali, na kwamba utaratibu haukufatwa.

-Mahakama Kuu pia ikasema, NMB wameshindwa kuthibitisha kwamba mlalamikaji alikuwa haendi kazini siku za jumamosi.

-Zaidi sana, Mahakama Kuu ikaongezea kwamba, kwanza KITENDO CHA NMB KUTAKA MFANYAKAZI WAO AENDE KAZINI SIKU ZA JUMAMOSI (wakati yeye jumamosi ni siku yake ya Ibada) ILIKUWA NI UBAGUZI AU UNYANYASAJI WA KIDINI (DISCRIMINATION) ambapo ni kinyume na Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya 1977, na sheria za kazi. (Emphasis added).

-Nanukuu kwa kiingereza, “High Court found the appellant's (NMB) conduct to have amounted to discrimination against the respondent on religious basis which was contrary to the Constitution of the United Republic of Tanzania, 1977 and the Labour Laws.”

-Mahakama ikasema kila mtu ana haki ya uhuru wa kuabudu kwa mujibu wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Ibara ya 19, ibara ndogo ya kwanza na kifungu cha 7(a) cha sheria ya Ajira na Mahusiano kazini. [Article 19(1) of the Constitution and section 7(4) (a) of ERLA].

-Hivyo basi, Mahakama ikasema kwamba sera na Kanuni za kazi za NMB zinakiuka Katiba pamoja na Sheria ya Ajira, kifungu cha 7(4).

-NMB haikuridhika na maamuzi ya Mahakama Kuu.

NB: (Usiporidhika na maamuzi ya Mahakama Kuu, unakata rufaa kwenda Mahakama ya Rufaa ambayo ni Mahakama ya juu na yenye Mamlaka ya mwisho nchini Tanzania.)

-NMB ikakata rufaa Mahakama ya Rufaa.

MAHAKAMA YA RUFAA

-Kesi ilisikilizwa na Majaji watatu wa Mahakama ya Rufaa.

-Mawakili wa pande zote mbili wakawasilisha hoja zao (ambazo sitaziandika hapa ili hii makala isiwe ndefu sana ikakushinda kusoma).

-Baada ya kuwasikiliza Mawakili wa pande zote, Mahakama ya Rufaa ikakaa sasa kuamua, ‘Je, Mlalamikaji alifutwa kazi kihalali na kwamba sheria ilifatwa au la!’

-Mahakama ikakuta Neema, akiwa katika eneo la kazi, alikuwa anatendewa tofauti na wafanyakazi wengine kuhusu haki ya Ibada.

-NMB waliruhusu baadhi ya wafanyakazi akiwemo Branch Manager kwenda kusali wanavyotaka lakini wakati huo huo wakamzuia Neema asiende kusali.

-Mfano Waislam waliruhusiwa kwenda kusali Ijumaa, lakini Neema alikataliwa siku ya Jumamosi.

-Mahakama ya Rufaa ikakubaliana na Mahakama Kuu na kusema kwamba, hicho kitendo cha mwajiri (kumzuia mfanyakazi kusali siku ya Jumamosi), ni kinyume na ni ukiukwaji wa sheria ya kazi kifungu cha 7(4)(g).

-Hicho kifungu kinakataza ubaguzi dhidi ya mfanyakazi kwa sababu mbali mbali ikiwemo dini au Imani.

-Nanukuu kwa kiingereza “as correctly found by the learned Judge of the High Court, the act of the appellant (NMB) as an employer contravened the provisions of section 7(4) of the ELRA which abhors discrimination at place of work”

-Mwisho Neema Akeyo akashinda kesi tena.

-Mahakama ya Rufaa ikasema imejiridhisha kwamba mlalamikaji hakufutwa kazi kihalali (the termination of Neema Akeyo was substantively unfair).

-Mahakama ya Rufaa ikasema, Tume ya usuluhishi (CMA) na Mahakama Kuu walikuwa halali kuamuru alipwe mshahara wa miezi 36 kama fidia.

-Rufaa ya NMB ikatupiliwa mbali, hivyo NMB wakawa wameshindwa kesi. (The appeal was dismissed)

-Na kwa kuwa Mahakama ya Rufaa ndiyo Mahakama ya juu na yenye Mamlaka ya mwisho nchini Tanzania, ukishindwa hapo basi hamna pa kwenda labda uombe review (marejeo) ambapo Mahakama ya Rufaa itakaa tena kupitia (ku review) uamuzi wake upya.

Wito wangu kwa waajiri, heshimuni uhuru wa kuabudu kwa watu wote. Yeyote ambaye Mungu amekupa dhamana ya kuongoza watu wake, usitumie nafasi yako kukandamiza uhuru wa dini. Watu wakiomba ruhusa kwenda kuabudu, wape ruhusa.

Tunapoomba tunaombea taifa, shule, chuo, ofisi, kampuni n.k.

Kesi hii ipo mtandaoni kwa lugha ya kiingereza. Ukitaka kujisomea kwa undani zaidi. Ingia Google (Tanzlii website) andika National Microfinance Bank Ltd (NMB) Vs Neema Akeyo, 2020.

IMETAFSIRIWA na kuletwa kwako nami Zakaria Maseke (0754575246 - WhatsApp).
 
NATIONAL MICROFINANCE BANK LTD (NMB) VERSUS NEEMA AKEYO, CIVIL APPEAL NO. 511 OF 2020, CAT.

Mwandishi: Zakaria.
Taaluma: Mwanasheria.

Hii kesi inahusu mfanyakazi (Neema Akeyo) ambaye alifutwa kazi isivyo halali kwa sababu za ubaguzi wa kidini ambapo alikuwa anaenda kufanya ibada siku za jumamosi kama haki yake Kikatiba ya uhuru wa kuabudu.

Lakini pia, sheria haikufatwa ipasavyo wakati wa kumfuta kazi Neema Akeyo, mfano hakupewa nafasi ya kujitetea kabla ya kuamua kumuachisha kazi.

Watu wengi wameshaiongelea sana. Lakini kutokana na umuhimu wake nimeamua kuitafsiri tena na kuipost ili iwafikie watu wengi hasa waajiri. Kumekuwa na hulka ya kuwanyima wafanyakazi uhuru wa kuabudu, kwa kuwapangia kazi siku za Ibada.

Wahanga wakubwa ni Waadventista Wasabato wanaosali Jumamosi. Kidogo kidogo, Jumamosi imeanza kuzoeleka kama siku ya kazi. Hata interviews nyingi za kazi sasa zinapangwa Jumamosi. Ina maana wasabato wengi watakosa kazi.

Dini zote ni sawa, na bahati nzuri nchi hii haina dini (ni secular State), hivyo isionekane dini au dhehebu moja linapendelewa sana au kuonewa. Naamini wahusika mtalishughulikia.

Turudi kwenye kesi yetu.

Tuanze na FACTS (STORI YA KESI):

-Neema Akeyo aliajiriwa na Bank ya NMB kama Bank teller, Wilaya ya Karatu.

-Ajira hiyo ilianza tarehe 27/10/2010 mpaka tarehe 5/6/2015 alipofutwa kazi na NMB kwa sababu ya kutoenda kazini (utoro) siku za jumamosi na kutotii mwajiri.

-Neema akaenda kushtaki au kulalamika kwenye Commission for Mediation and Arbitration (CMA) yaani Tume ya Usuluhishi na Uamuzi/Upatanishi, akidai kwamba alifutwa kazi kimakosa na kwamba alipwe fidia kwa kitendo hicho cha NMB kuvunja mkataba wa ajira.

MBELE YA TUME:

-NMB ikakana kuvunja mkataba, ikasema mlalamikaji (Neema) alifutwa kazi kwa sababu halali na kwamba taratibu zote zilifuatwa.

-NMB ikasema kwamba, mlalamikaji alifutwa kazi KWA SABABU YA KUSHINDWA KWENDA KAZINI SIKU ZA JUMAMOSI (UTORO) ambapo ilikuwa ni kinyume na makubaliano ya kazi na kinyume cha sera na kanuni za NMB.

-Baada ya kusikiliza kesi mpaka mwisho, mwamuzi wa Tume aliridhika kwamba, mlalamikaji (Neema) hakufutwa kazi kihalali (was unfairly terminated), na kwamba utaratibu haukufatwa.

-Tume ikasema kwamba, hakuna ushahidi kutoka NMB unaothibitisha kwamba Neema hakuwa anaenda kazini siku za Jumamosi.

-Pia, hata baada ya mlalamikaji kukutwa na makosa, hakupewa nafasi ya kujitetea.

-Hivyo Tume ikasema Neema hakufutwa kazi kihalali.

-Tume ikaamuru, Neema alipwe mshahara wa miezi 36 kama fidia.

NB: (Usiporidhika na maamuzi ya Tume (CMA) unaomba revision (mapitio) kwenye Mahakama ya kazi (Labour Court) - ambayo ni Mahakama Kuu divisheni au kitengo cha Kazi. Zingatia sijasema unakata rufaa (appeal), kuna tofauti kati ya Appeal na Revision.)

-NMB hawakuridhika na maamuzi ya Tume, wakafungua maombi Mahakama kuu, wakiomba maamuzi ya Tume yapitiwe upya.

MAHAKAMA KUU:

-Neema akashinda kesi tena dhidi ya NMB.

- Mahakama Kuu ikatupilia mbali maombi ya NMB, na kupigilia msumari maamuzi ya Tume yaliyompa Neema tuzo ya kulipwa mshahara wa miezi 36.

-Mahakama Kuu nayo ikasema Neema hakufutwa kazi kihalali, na kwamba utaratibu haukufatwa.

-Mahakama Kuu pia ikasema, NMB wameshindwa kuthibitisha kwamba mlalamikaji alikuwa haendi kazini siku za jumamosi.

-Zaidi sana, Mahakama Kuu ikaongezea kwamba, kwanza KITENDO CHA NMB KUTAKA MFANYAKAZI WAO AENDE KAZINI SIKU ZA JUMAMOSI (wakati yeye jumamosi ni siku yake ya Ibada) ILIKUWA NI UBAGUZI AU UNYANYASAJI WA KIDINI (DISCRIMINATION) ambapo ni kinyume na Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya 1977, na sheria za kazi. (Emphasis added).

-Nanukuu kwa kiingereza, “High Court found the appellant's (NMB) conduct to have amounted to discrimination against the respondent on religious basis which was contrary to the Constitution of the United Republic of Tanzania, 1977 and the Labour Laws.”

-Mahakama ikasema kila mtu ana haki ya uhuru wa kuabudu kwa mujibu wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Ibara ya 19, ibara ndogo ya kwanza na kifungu cha 7(a) cha sheria ya Ajira na Mahusiano kazini. [Article 19(1) of the Constitution and section 7(4) (a) of ERLA].

-Hivyo basi, Mahakama ikasema kwamba sera na Kanuni za kazi za NMB zinakiuka Katiba pamoja na Sheria ya Ajira, kifungu cha 7(4).

-NMB haikuridhika na maamuzi ya Mahakama Kuu.

NB: (Usiporidhika na maamuzi ya Mahakama Kuu, unakata rufaa kwenda Mahakama ya Rufaa ambayo ni Mahakama ya juu na yenye Mamlaka ya mwisho nchini Tanzania.)

-NMB ikakata rufaa Mahakama ya Rufaa.

MAHAKAMA YA RUFAA

-Kesi ilisikilizwa na Majaji watatu wa Mahakama ya Rufaa.

-Mawakili wa pande zote mbili wakawasilisha hoja zao (ambazo sitaziandika hapa ili hii makala isiwe ndefu sana ikakushinda kusoma).

-Baada ya kuwasikiliza Mawakili wa pande zote, Mahakama ya Rufaa ikakaa sasa kuamua, ‘Je, Mlalamikaji alifutwa kazi kihalali na kwamba sheria ilifatwa au la!’

-Mahakama ikakuta Neema, akiwa katika eneo la kazi, alikuwa anatendewa tofauti na wafanyakazi wengine kuhusu haki ya Ibada.

-NMB waliruhusu baadhi ya wafanyakazi akiwemo Branch Manager kwenda kusali wanavyotaka lakini wakati huo huo wakamzuia Neema asiende kusali.

-Mfano Waislam waliruhusiwa kwenda kusali Ijumaa, lakini Neema alikataliwa siku ya Jumamosi.

-Mahakama ya Rufaa ikakubaliana na Mahakama Kuu na kusema kwamba, hicho kitendo cha mwajiri (kumzuia mfanyakazi kusali siku ya Jumamosi), ni kinyume na ni ukiukwaji wa sheria ya kazi kifungu cha 7(4)(g).

-Hicho kifungu kinakataza ubaguzi dhidi ya mfanyakazi kwa sababu mbali mbali ikiwemo dini au Imani.

-Nanukuu kwa kiingereza “as correctly found by the learned Judge of the High Court, the act of the appellant (NMB) as an employer contravened the provisions of section 7(4) of the ELRA which abhors discrimination at place of work”

-Mwisho Neema Akeyo akashinda kesi tena.

-Mahakama ya Rufaa ikasema imejiridhisha kwamba mlalamikaji hakufutwa kazi kihalali (the termination of Neema Akeyo was substantively unfair).

-Mahakama ya Rufaa ikasema, Tume ya usuluhishi (CMA) na Mahakama Kuu walikuwa halali kuamuru alipwe mshahara wa miezi 36 kama fidia.

-Rufaa ya NMB ikatupiliwa mbali, hivyo NMB wakawa wameshindwa kesi. (The appeal was dismissed)

-Na kwa kuwa Mahakama ya Rufaa ndiyo Mahakama ya juu na yenye Mamlaka ya mwisho nchini Tanzania, ukishindwa hapo basi hamna pa kwenda labda uombe review (marejeo) ambapo Mahakama ya Rufaa itakaa tena kupitia (ku review) uamuzi wake upya.

Wito wangu kwa waajiri, heshimuni uhuru wa kuabudu kwa watu wote. Acheni kuwapangia wafanyakazi majukumu siku za Ibada. Ni heri umpe shift, badala ya Jumamosi afanye hiyo Kazi Jumapili, au umuongezee masaa ya kazi katikati ya week ili siku yake ya Ibada aende kuabudu.

Hata interview zisipangwe siku za ibada. Ukiweka interview siku au masaa ya ibada kuna watu watakosa kazi. Alafu, unakuwa umefaidika nini? Ukipewa nafasi na Mungu usiitumie kunyoosha au kukomesha wenzio.

Na wakuu wa shule, vyuo, waalimu, wahadhiri (lecturers), n.k msiwapangie wanafunzi vipindi na mitihani siku za Ibada.

Yeyote ambaye Mungu amekupa dhamana ya kuongoza watu wake, usitumie nafasi yako kukandamiza uhuru wa dini. Watu wakiomba ruhusa kwenda kuabudu, wape ruhusa. Tunapoomba tunaombea taifa, shule, chuo, ofisi, kampuni n.k. Mtu anakuomba ruhusa akasali unakataa je angekuwa anaenda kuvuta bangi? Kusali ni kitu cha kukataliwa, tena mara moja tu kwa wiki!

Hiyo nafasi yako hapo ofisini ni Neema. Umekalia hicho kiti kwa Neema, Mungu anaweza kuamua ukaondoka. Hivyo usimhuzunishe Mungu kwa kuonea watoto wake. Watendee wote sawa sawa. Awe ni Muislam au Mkristo wape wote uhuru wa kuabudu.

Kesi hii ipo mtandaoni kwa lugha ya kiingereza. Ukitaka kujisomea kwa undani zaidi. Ingia Google (Tanzlii website) andika National Microfinance Bank Ltd (NMB) Vs Neema Akeyo, 2020.

IMEANDALIWA AU KUTAFSIRIWA na kuletwa kwako nami Zakaria (0754575246 - WhatsApp). Lawyer by profession.

Mkuu Zakaria Emmanuel hongera kwa bandiko. Kwanza nikiri sijui sana Sheria za Kazi zinazoongoza Bank husika. Pili nikiri kwamba, Mimi ni Mkristo (Born again Christian) ambaye ninatamani muda wangu wa Ibada (Sio Siku ya Ibada) uheshimiwe na kila mtu. Kwenye hii kesi NINA HISI kuna mambo mengi hujayaeleza kuhusu hii kesi mfano hoja zilizovyoshindanishwa na kama kilichoamua kesi ni uwasilishwaji wa hoja toka kila upande na kama Bank ilikuwa imefanya uamuzi sahihi kwa kutumia njia isiyo sahihi au Bank ilikuwa imefanya uamuzi usio sahihi kabisa. Mwisho niseme tu umetumia mahaba yako makubwa kiimani (Kisabato) kuwasilisha maamuzi ya kisheria.

Ahsante
 
Namimi nianzishe dini ambayo ntakuwa nasalikila siku kasoro jumanne...Hapa kazini ntawakazia wasinifukuze
 
Kesi ameshinda Ney. Ila amewaharibia Wasabato wengine. Itakuwa ngumu kwao kupata ajira hapo.
Nakumbuka muhindi fulani aliwahi kuniomba nimtafutie machine operators. But alikuwa specific kuwa anataka watu wa dini fulani!
 
Mkuu Zakaria Emmanuel hongera kwa bandiko. Kwanza nikiri sijui sana Sheria za Kazi zinazoongoza Bank husika. Pili nikiri kwamba, Mimi ni Mkristo (Born again Christian) ambaye ninatamani muda wangu wa Ibada (Sio Siku ya Ibada) uheshimiwe na kila mtu. Kwenye hii kesi NINA HISI kuna mambo mengi hujayaeleza kuhusu hii kesi mfano hoja zilizovyoshindanishwa na kama kilichoamua kesi ni uwasilishwaji wa hoja toka kila upande na kama Bank ilikuwa imefanya uamuzi sahihi kwa kutumia njia isiyo sahihi au Bank ilikuwa imefanya uamuzi usio sahihi kabisa. Mwisho niseme tu umetumia mahaba yako makubwa kiimani (Kisabato) kuwasilisha maamuzi ya kisheria.

Ahsante

Huenda kwako siku sio hoja sana kwa sababu Imani yako inaruhusu kusali kwa masaa na kuendelea na kazi masaa yaliyobaki, tofauti na wengine ambao wanasali (kupumzika) siku nzima.

Pili, niseme tu hiyo ni summary ya kesi, sijaweka kila kitu mpaka hoja (submissions) za mawakili kwa sababu wabongo unawajua , makala ikiwa ndefu sana, wengi huwa hawawezi kusoma yote, na kama watu hawasomi, ina maana ujumbe hautafika.

Sasa ukiandika fupi mtu anasema hujaweka baadhi ya vitu, ukiandika kila kitu, watu wanasema ndefu sana tupe summary.

Lakini kama nilivyosema, kesi full ipo. Ukitaka kuona submission za mawakili wa pande zote mbili, kasome kesi yote

Kuhusu hoja yako ya pili kwamba nimependelea wasabato, kwanza nani amekwambia mimi ni Msabato? Inawezekaa kweli mimi ni Msabato, lakini je hao Majaji wote, kuanzia kwenye Tume, Mahakama Kuu hadi Mahakama ya Rufani, wote walikuwa wasabato?

Mimi nimewasilisha kilichotokea Mahakamani, Mlalamikaji alishinda kila stage, hivi hata ungekuwa ni wewe ungeandikaje tofauti na hapo? Au unataka nipotoshe kesi?

Kiufupi, kutokuweka kila kitu hapa au kuandika summary tu, haina maana napendelea Wasabato, mimi nilikuwa naeleza kilichotokea na kilichoamuliwa na Mahakama.

Ikumbukwe sikuwa naandika kitu kipya bali kufasir kilichopo. Tena nimetafsir almost neno kwa neno, sijui kama kuna maneno yangu hapo labda utangulizi na hitimisho tu. Sasa kama huo ni upendeleo sawa!

Bahati nzuri hata huyo mlalamikaji (Neema Akeyo) mimi sijui ni dhehebu gani, watu ndo naona wanasema hapa MSABATO. Lakini kesi nzima sijaona neno Msabato.

Na sina hakika kama wanosali jumamosi ni wasabato tu.

Asante mkuu nawasilisha
 
NATIONAL MICROFINANCE BANK LTD (NMB) VERSUS NEEMA AKEYO, CIVIL APPEAL NO. 511 OF 2020, CAT.

Mwandishi: Zakaria.
Taaluma: Mwanasheria.

Hii kesi inahusu mfanyakazi (Neema Akeyo) ambaye alifutwa kazi isivyo halali kwa sababu za ubaguzi wa kidini ambapo alikuwa anaenda kufanya ibada siku za jumamosi kama haki yake Kikatiba ya uhuru wa kuabudu.

Lakini pia, sheria haikufatwa ipasavyo wakati wa kumfuta kazi Neema Akeyo, mfano hakupewa nafasi ya kujitetea kabla ya kuamua kumuachisha kazi.

Watu wengi wameshaiongelea sana. Lakini kutokana na umuhimu wake nimeamua kuitafsiri tena na kuipost ili iwafikie watu wengi hasa waajiri. Kumekuwa na hulka ya kuwanyima wafanyakazi uhuru wa kuabudu, kwa kuwapangia kazi siku za Ibada.

Wahanga wakubwa ni Waadventista Wasabato wanaosali Jumamosi. Kidogo kidogo, Jumamosi imeanza kuzoeleka kama siku ya kazi. Hata interviews nyingi za kazi sasa zinapangwa Jumamosi. Ina maana wasabato wengi watakosa kazi.

Dini zote ni sawa, na bahati nzuri nchi hii haina dini (ni secular State), hivyo isionekane dini au dhehebu moja linapendelewa sana au kuonewa. Naamini wahusika mtalishughulikia.

Turudi kwenye kesi yetu.

Tuanze na FACTS (STORI YA KESI):

-Neema Akeyo aliajiriwa na Bank ya NMB kama Bank teller, Wilaya ya Karatu.

-Ajira hiyo ilianza tarehe 27/10/2010 mpaka tarehe 5/6/2015 alipofutwa kazi na NMB kwa sababu ya kutoenda kazini (utoro) siku za jumamosi na kutotii mwajiri.

-Neema akaenda kushtaki au kulalamika kwenye Commission for Mediation and Arbitration (CMA) yaani Tume ya Usuluhishi na Uamuzi/Upatanishi, akidai kwamba alifutwa kazi kimakosa na kwamba alipwe fidia kwa kitendo hicho cha NMB kuvunja mkataba wa ajira.

MBELE YA TUME:

-NMB ikakana kuvunja mkataba, ikasema mlalamikaji (Neema) alifutwa kazi kwa sababu halali na kwamba taratibu zote zilifuatwa.

-NMB ikasema kwamba, mlalamikaji alifutwa kazi KWA SABABU YA KUSHINDWA KWENDA KAZINI SIKU ZA JUMAMOSI (UTORO) ambapo ilikuwa ni kinyume na makubaliano ya kazi na kinyume cha sera na kanuni za NMB.

-Baada ya kusikiliza kesi mpaka mwisho, mwamuzi wa Tume aliridhika kwamba, mlalamikaji (Neema) hakufutwa kazi kihalali (was unfairly terminated), na kwamba utaratibu haukufatwa.

-Tume ikasema kwamba, hakuna ushahidi kutoka NMB unaothibitisha kwamba Neema hakuwa anaenda kazini siku za Jumamosi.

-Pia, hata baada ya mlalamikaji kukutwa na makosa, hakupewa nafasi ya kujitetea.

-Hivyo Tume ikasema Neema hakufutwa kazi kihalali.

-Tume ikaamuru, Neema alipwe mshahara wa miezi 36 kama fidia.

NB: (Usiporidhika na maamuzi ya Tume (CMA) unaomba revision (mapitio) kwenye Mahakama ya kazi (Labour Court) - ambayo ni Mahakama Kuu divisheni au kitengo cha Kazi. Zingatia sijasema unakata rufaa (appeal), kuna tofauti kati ya Appeal na Revision.)

-NMB hawakuridhika na maamuzi ya Tume, wakafungua maombi Mahakama kuu, wakiomba maamuzi ya Tume yapitiwe upya.

MAHAKAMA KUU:

-Neema akashinda kesi tena dhidi ya NMB.

- Mahakama Kuu ikatupilia mbali maombi ya NMB, na kupigilia msumari maamuzi ya Tume yaliyompa Neema tuzo ya kulipwa mshahara wa miezi 36.

-Mahakama Kuu nayo ikasema Neema hakufutwa kazi kihalali, na kwamba utaratibu haukufatwa.

-Mahakama Kuu pia ikasema, NMB wameshindwa kuthibitisha kwamba mlalamikaji alikuwa haendi kazini siku za jumamosi.

-Zaidi sana, Mahakama Kuu ikaongezea kwamba, kwanza KITENDO CHA NMB KUTAKA MFANYAKAZI WAO AENDE KAZINI SIKU ZA JUMAMOSI (wakati yeye jumamosi ni siku yake ya Ibada) ILIKUWA NI UBAGUZI AU UNYANYASAJI WA KIDINI (DISCRIMINATION) ambapo ni kinyume na Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya 1977, na sheria za kazi. (Emphasis added).

-Nanukuu kwa kiingereza, “High Court found the appellant's (NMB) conduct to have amounted to discrimination against the respondent on religious basis which was contrary to the Constitution of the United Republic of Tanzania, 1977 and the Labour Laws.”

-Mahakama ikasema kila mtu ana haki ya uhuru wa kuabudu kwa mujibu wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Ibara ya 19, ibara ndogo ya kwanza na kifungu cha 7(a) cha sheria ya Ajira na Mahusiano kazini. [Article 19(1) of the Constitution and section 7(4) (a) of ERLA].

-Hivyo basi, Mahakama ikasema kwamba sera na Kanuni za kazi za NMB zinakiuka Katiba pamoja na Sheria ya Ajira, kifungu cha 7(4).

-NMB haikuridhika na maamuzi ya Mahakama Kuu.

NB: (Usiporidhika na maamuzi ya Mahakama Kuu, unakata rufaa kwenda Mahakama ya Rufaa ambayo ni Mahakama ya juu na yenye Mamlaka ya mwisho nchini Tanzania.)

-NMB ikakata rufaa Mahakama ya Rufaa.

MAHAKAMA YA RUFAA

-Kesi ilisikilizwa na Majaji watatu wa Mahakama ya Rufaa.

-Mawakili wa pande zote mbili wakawasilisha hoja zao (ambazo sitaziandika hapa ili hii makala isiwe ndefu sana ikakushinda kusoma).

-Baada ya kuwasikiliza Mawakili wa pande zote, Mahakama ya Rufaa ikakaa sasa kuamua, ‘Je, Mlalamikaji alifutwa kazi kihalali na kwamba sheria ilifatwa au la!’

-Mahakama ikakuta Neema, akiwa katika eneo la kazi, alikuwa anatendewa tofauti na wafanyakazi wengine kuhusu haki ya Ibada.

-NMB waliruhusu baadhi ya wafanyakazi akiwemo Branch Manager kwenda kusali wanavyotaka lakini wakati huo huo wakamzuia Neema asiende kusali.

-Mfano Waislam waliruhusiwa kwenda kusali Ijumaa, lakini Neema alikataliwa siku ya Jumamosi.

-Mahakama ya Rufaa ikakubaliana na Mahakama Kuu na kusema kwamba, hicho kitendo cha mwajiri (kumzuia mfanyakazi kusali siku ya Jumamosi), ni kinyume na ni ukiukwaji wa sheria ya kazi kifungu cha 7(4)(g).

-Hicho kifungu kinakataza ubaguzi dhidi ya mfanyakazi kwa sababu mbali mbali ikiwemo dini au Imani.

-Nanukuu kwa kiingereza “as correctly found by the learned Judge of the High Court, the act of the appellant (NMB) as an employer contravened the provisions of section 7(4) of the ELRA which abhors discrimination at place of work”

-Mwisho Neema Akeyo akashinda kesi tena.

-Mahakama ya Rufaa ikasema imejiridhisha kwamba mlalamikaji hakufutwa kazi kihalali (the termination of Neema Akeyo was substantively unfair).

-Mahakama ya Rufaa ikasema, Tume ya usuluhishi (CMA) na Mahakama Kuu walikuwa halali kuamuru alipwe mshahara wa miezi 36 kama fidia.

-Rufaa ya NMB ikatupiliwa mbali, hivyo NMB wakawa wameshindwa kesi. (The appeal was dismissed)

-Na kwa kuwa Mahakama ya Rufaa ndiyo Mahakama ya juu na yenye Mamlaka ya mwisho nchini Tanzania, ukishindwa hapo basi hamna pa kwenda labda uombe review (marejeo) ambapo Mahakama ya Rufaa itakaa tena kupitia (ku review) uamuzi wake upya.

Wito wangu kwa waajiri, heshimuni uhuru wa kuabudu kwa watu wote. Acheni kuwapangia wafanyakazi majukumu siku za Ibada. Ni heri umpe shift, badala ya Jumamosi afanye hiyo Kazi Jumapili, au umuongezee masaa ya kazi katikati ya week ili siku yake ya Ibada aende kuabudu.

Hata interview zisipangwe siku za ibada. Ukiweka interview siku au masaa ya ibada kuna watu watakosa kazi. Alafu, unakuwa umefaidika nini? Ukipewa nafasi na Mungu usiitumie kunyoosha au kukomesha wenzio.

Na wakuu wa shule, vyuo, waalimu, wahadhiri (lecturers), n.k msiwapangie wanafunzi vipindi na mitihani siku za Ibada.

Yeyote ambaye Mungu amekupa dhamana ya kuongoza watu wake, usitumie nafasi yako kukandamiza uhuru wa dini. Watu wakiomba ruhusa kwenda kuabudu, wape ruhusa. Tunapoomba tunaombea taifa, shule, chuo, ofisi, kampuni n.k. Mtu anakuomba ruhusa akasali unakataa je angekuwa anaenda kuvuta bangi? Kusali ni kitu cha kukataliwa, tena mara moja tu kwa wiki!

Hiyo nafasi yako hapo ofisini ni Neema. Umekalia hicho kiti kwa Neema, Mungu anaweza kuamua ukaondoka. Hivyo usimhuzunishe Mungu kwa kuonea watoto wake. Watendee wote sawa sawa. Awe ni Muislam au Mkristo wape wote uhuru wa kuabudu.

Kesi hii ipo mtandaoni kwa lugha ya kiingereza. Ukitaka kujisomea kwa undani zaidi. Ingia Google (Tanzlii website) andika National Microfinance Bank Ltd (NMB) Vs Neema Akeyo, 2020.

IMEANDALIWA AU KUTAFSIRIWA na kuletwa kwako nami Zakaria (0754575246 - WhatsApp). Lawyer by profession.
NAOMBA KUJUA KESI IKIFIKA MAHAKAMA YA RUFAANI AFU MLALAMIKWA AKASHINDA ILA MLALAMIKAJI AKACHELEWA KUKATA RUFAAA JE KiSHERIA Hii imekaaje?

Swal la pili lipo hewani
 
NAOMBA KUJUA KESI IKIFIKA MAHAKAMA YA RUFAANI AFU MLALAMIKWA AKASHINDA ILA MLALAMIKAJI AKACHELEWA KUKATA RUFAAA JE KiSHERIA Hii imekaaje?

Swal la pili lipo hewani

kwa Tanzania, Mahakama ya Rufani (Court of Appeal) ndio Mahakama ya juu kabisa na yenye mamlaka ya mwisho, hivyo ukishindwa hapo ndio mwisho hakuna pa kukata rufaa tena (labda uombe marejeo).

Sasa labda nijibu swali lako hivi, kama kesi iko kwenye Mahakama za chini, na umechelewa kukata rufaa hadi muda umeisha, unaweza kuomba kuongezewa muda (application for extension of time).
 
kwa Tanzania, Mahakama ya Rufani (Court of Appeal) ndio Mahakama ya juu kabisa na yenye mamlaka ya mwisho, hivyo ukishindwa hapo ndio mwisho hakuna pa kukata rufaa tena (labda uombe marejeo).

Sasa labda nijibu swali lako hivi, kama kesi iko kwenye Mahakama za chini, na umechelewa kukata rufaa hadi muda umeisha, unaweza kuomba kuongezewa muda (application for extension of time).

Ahsante kwa jibu zuri,naomba kuuliza kisheria ukishika mali kwa jina la baba alafu ndugu zako baadaye wakajakufungua kesi wakidai mali ni ya baba ile hali nmetumia jina tu malipo zote ni yangu hii imekaaaje kisheria,wakili msomi ZAKARIA
 
kwa Tanzania, Mahakama ya Rufani (Court of Appeal) ndio Mahakama ya juu kabisa na yenye mamlaka ya mwisho, hivyo ukishindwa hapo ndio mwisho hakuna pa kukata rufaa tena (labda uombe marejeo).

Sasa labda nijibu swali lako hivi, kama kesi iko kwenye Mahakama za chini, na umechelewa kukata rufaa hadi muda umeisha, unaweza kuomba kuongezewa muda (application for extension of time).
Mkuuu hii KESI ilkua mahakama ya rufaaani mlalakaji akashindwa kukata rufaaa baada ya muda kupita
 
Kwa kuongezea

1) Mzee Ally Hassan Mwinyi akiwa Rais wa Tanzania ndie aliridhia ombi la Wasabato kwa kuifanya Jumamosi kuwa siku ya Mapumziko kwa watumishi wa Umma ili kuruhusu ndugu zetu hawa wapate kuabudu

2) Japokuwa Ruhusa ya Waislam kwenda kuabudu kwa dakika 60 tu siku ya Ijumaa imekuwa tatizo sana na wakuu wa kazi kwny ofisi za Umma hasa wasio Waislam wamekuwa wakiumia sana kwa kuruhusu Mwislam kwenda kuabudu na hata baadhi wakawa wanapanga vikao kuanzia saa 6 na nusu mchana ili tu kukomoa Waislam wasipate ruhusa hii ya kuabudu

pia Walimu wakawa wanapanga mitihani na programs zingine za shule wakati wa Ibada wakati tayari kuna Circular kutoka Wizarani juu ya Ruhusa hii

ilipofika mwaka 2000 Waislam chini ya Sheikh Juma Mbukuzi wakaingia barabarani kufanya Maandamano yasiyo na ukomo kupata kauli nyingine rasmi ya Serikali dhidi ya wanaokandamiza haki hii nchi nzima

hapo ndipo Hayati Mzee Benjamin Mkapa akakemea na kutoa karipio kali sana kwa wenye tabia hizo


Kuheshimu na kutambua imani ya mwingine haikugharimu chochote
 
Hili timbwili litalipuka tena hivi karibuni dhidi ya sekretarieti ya ajira katika utumishi wa umma. Wamefanya usaili jana na juzi (jumamosi na jumapili) tarehe 18/06/2022 na 19/06/2022 pamoja na kuwa walitahadharishwa mapema ili wabadili tarehe. Kuna wanaodai kuwa wameathirika na wanajipanga kudai fidia ya mamilioni na kubatilisha matokeo ya usaili huo.
 
NATIONAL MICROFINANCE BANK LTD (NMB) VERSUS NEEMA AKEYO, CIVIL APPEAL NO. 511 OF 2020, CAT.

Mwandishi: Zakaria.
Taaluma: Mwanasheria.

Hii kesi inahusu mfanyakazi (Neema Akeyo) ambaye alifutwa kazi isivyo halali kwa sababu za ubaguzi wa kidini ambapo alikuwa anaenda kufanya ibada siku za jumamosi kama haki yake Kikatiba ya uhuru wa kuabudu.

Lakini pia, sheria haikufatwa ipasavyo wakati wa kumfuta kazi Neema Akeyo, mfano hakupewa nafasi ya kujitetea kabla ya kuamua kumuachisha kazi.

Watu wengi wameshaiongelea sana. Lakini kutokana na umuhimu wake nimeamua kuitafsiri tena na kuipost ili iwafikie watu wengi hasa waajiri. Kumekuwa na hulka ya kuwanyima wafanyakazi uhuru wa kuabudu, kwa kuwapangia kazi siku za Ibada.

Wahanga wakubwa ni Waadventista Wasabato wanaosali Jumamosi. Kidogo kidogo, Jumamosi imeanza kuzoeleka kama siku ya kazi. Hata interviews nyingi za kazi sasa zinapangwa Jumamosi. Ina maana wasabato wengi watakosa kazi.

Dini zote ni sawa, na bahati nzuri nchi hii haina dini (ni secular State), hivyo isionekane dini au dhehebu moja linapendelewa sana au kuonewa. Naamini wahusika mtalishughulikia.

Turudi kwenye kesi yetu.

Tuanze na FACTS (STORI YA KESI):

-Neema Akeyo aliajiriwa na Bank ya NMB kama Bank teller, Wilaya ya Karatu.

-Ajira hiyo ilianza tarehe 27/10/2010 mpaka tarehe 5/6/2015 alipofutwa kazi na NMB kwa sababu ya kutoenda kazini (utoro) siku za jumamosi na kutotii mwajiri.

-Neema akaenda kushtaki au kulalamika kwenye Commission for Mediation and Arbitration (CMA) yaani Tume ya Usuluhishi na Uamuzi/Upatanishi, akidai kwamba alifutwa kazi kimakosa na kwamba alipwe fidia kwa kitendo hicho cha NMB kuvunja mkataba wa ajira.

MBELE YA TUME:

-NMB ikakana kuvunja mkataba, ikasema mlalamikaji (Neema) alifutwa kazi kwa sababu halali na kwamba taratibu zote zilifuatwa.

-NMB ikasema kwamba, mlalamikaji alifutwa kazi KWA SABABU YA KUSHINDWA KWENDA KAZINI SIKU ZA JUMAMOSI (UTORO) ambapo ilikuwa ni kinyume na makubaliano ya kazi na kinyume cha sera na kanuni za NMB.

-Baada ya kusikiliza kesi mpaka mwisho, mwamuzi wa Tume aliridhika kwamba, mlalamikaji (Neema) hakufutwa kazi kihalali (was unfairly terminated), na kwamba utaratibu haukufatwa.

-Tume ikasema kwamba, hakuna ushahidi kutoka NMB unaothibitisha kwamba Neema hakuwa anaenda kazini siku za Jumamosi.

-Pia, hata baada ya mlalamikaji kukutwa na makosa, hakupewa nafasi ya kujitetea.

-Hivyo Tume ikasema Neema hakufutwa kazi kihalali.

-Tume ikaamuru, Neema alipwe mshahara wa miezi 36 kama fidia.

NB: (Usiporidhika na maamuzi ya Tume (CMA) unaomba revision (mapitio) kwenye Mahakama ya kazi (Labour Court) - ambayo ni Mahakama Kuu divisheni au kitengo cha Kazi. Zingatia sijasema unakata rufaa (appeal), kuna tofauti kati ya Appeal na Revision.)

-NMB hawakuridhika na maamuzi ya Tume, wakafungua maombi Mahakama kuu, wakiomba maamuzi ya Tume yapitiwe upya.

MAHAKAMA KUU:

-Neema akashinda kesi tena dhidi ya NMB.

- Mahakama Kuu ikatupilia mbali maombi ya NMB, na kupigilia msumari maamuzi ya Tume yaliyompa Neema tuzo ya kulipwa mshahara wa miezi 36.

-Mahakama Kuu nayo ikasema Neema hakufutwa kazi kihalali, na kwamba utaratibu haukufatwa.

-Mahakama Kuu pia ikasema, NMB wameshindwa kuthibitisha kwamba mlalamikaji alikuwa haendi kazini siku za jumamosi.

-Zaidi sana, Mahakama Kuu ikaongezea kwamba, kwanza KITENDO CHA NMB KUTAKA MFANYAKAZI WAO AENDE KAZINI SIKU ZA JUMAMOSI (wakati yeye jumamosi ni siku yake ya Ibada) ILIKUWA NI UBAGUZI AU UNYANYASAJI WA KIDINI (DISCRIMINATION) ambapo ni kinyume na Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya 1977, na sheria za kazi. (Emphasis added).

-Nanukuu kwa kiingereza, “High Court found the appellant's (NMB) conduct to have amounted to discrimination against the respondent on religious basis which was contrary to the Constitution of the United Republic of Tanzania, 1977 and the Labour Laws.”

-Mahakama ikasema kila mtu ana haki ya uhuru wa kuabudu kwa mujibu wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Ibara ya 19, ibara ndogo ya kwanza na kifungu cha 7(a) cha sheria ya Ajira na Mahusiano kazini. [Article 19(1) of the Constitution and section 7(4) (a) of ERLA].

-Hivyo basi, Mahakama ikasema kwamba sera na Kanuni za kazi za NMB zinakiuka Katiba pamoja na Sheria ya Ajira, kifungu cha 7(4).

-NMB haikuridhika na maamuzi ya Mahakama Kuu.

NB: (Usiporidhika na maamuzi ya Mahakama Kuu, unakata rufaa kwenda Mahakama ya Rufaa ambayo ni Mahakama ya juu na yenye Mamlaka ya mwisho nchini Tanzania.)

-NMB ikakata rufaa Mahakama ya Rufaa.

MAHAKAMA YA RUFAA

-Kesi ilisikilizwa na Majaji watatu wa Mahakama ya Rufaa.

-Mawakili wa pande zote mbili wakawasilisha hoja zao (ambazo sitaziandika hapa ili hii makala isiwe ndefu sana ikakushinda kusoma).

-Baada ya kuwasikiliza Mawakili wa pande zote, Mahakama ya Rufaa ikakaa sasa kuamua, ‘Je, Mlalamikaji alifutwa kazi kihalali na kwamba sheria ilifatwa au la!’

-Mahakama ikakuta Neema, akiwa katika eneo la kazi, alikuwa anatendewa tofauti na wafanyakazi wengine kuhusu haki ya Ibada.

-NMB waliruhusu baadhi ya wafanyakazi akiwemo Branch Manager kwenda kusali wanavyotaka lakini wakati huo huo wakamzuia Neema asiende kusali.

-Mfano Waislam waliruhusiwa kwenda kusali Ijumaa, lakini Neema alikataliwa siku ya Jumamosi.

-Mahakama ya Rufaa ikakubaliana na Mahakama Kuu na kusema kwamba, hicho kitendo cha mwajiri (kumzuia mfanyakazi kusali siku ya Jumamosi), ni kinyume na ni ukiukwaji wa sheria ya kazi kifungu cha 7(4)(g).

-Hicho kifungu kinakataza ubaguzi dhidi ya mfanyakazi kwa sababu mbali mbali ikiwemo dini au Imani.

-Nanukuu kwa kiingereza “as correctly found by the learned Judge of the High Court, the act of the appellant (NMB) as an employer contravened the provisions of section 7(4) of the ELRA which abhors discrimination at place of work”

-Mwisho Neema Akeyo akashinda kesi tena.

-Mahakama ya Rufaa ikasema imejiridhisha kwamba mlalamikaji hakufutwa kazi kihalali (the termination of Neema Akeyo was substantively unfair).

-Mahakama ya Rufaa ikasema, Tume ya usuluhishi (CMA) na Mahakama Kuu walikuwa halali kuamuru alipwe mshahara wa miezi 36 kama fidia.

-Rufaa ya NMB ikatupiliwa mbali, hivyo NMB wakawa wameshindwa kesi. (The appeal was dismissed)

-Na kwa kuwa Mahakama ya Rufaa ndiyo Mahakama ya juu na yenye Mamlaka ya mwisho nchini Tanzania, ukishindwa hapo basi hamna pa kwenda labda uombe review (marejeo) ambapo Mahakama ya Rufaa itakaa tena kupitia (ku review) uamuzi wake upya.

Wito wangu kwa waajiri, heshimuni uhuru wa kuabudu kwa watu wote. Acheni kuwapangia wafanyakazi majukumu siku za Ibada. Ni heri umpe shift, badala ya Jumamosi afanye hiyo Kazi Jumapili, au umuongezee masaa ya kazi katikati ya week ili siku yake ya Ibada aende kuabudu.

Hata interview zisipangwe siku za ibada. Ukiweka interview siku au masaa ya ibada kuna watu watakosa kazi. Alafu, unakuwa umefaidika nini? Ukipewa nafasi na Mungu usiitumie kunyoosha au kukomesha wenzio.

Na wakuu wa shule, vyuo, waalimu, wahadhiri (lecturers), n.k msiwapangie wanafunzi vipindi na mitihani siku za Ibada.

Yeyote ambaye Mungu amekupa dhamana ya kuongoza watu wake, usitumie nafasi yako kukandamiza uhuru wa dini. Watu wakiomba ruhusa kwenda kuabudu, wape ruhusa. Tunapoomba tunaombea taifa, shule, chuo, ofisi, kampuni n.k. Mtu anakuomba ruhusa akasali unakataa je angekuwa anaenda kuvuta bangi? Kusali ni kitu cha kukataliwa, tena mara moja tu kwa wiki!

Hiyo nafasi yako hapo ofisini ni Neema. Umekalia hicho kiti kwa Neema, Mungu anaweza kuamua ukaondoka. Hivyo usimhuzunishe Mungu kwa kuonea watoto wake. Watendee wote sawa sawa. Awe ni Muislam au Mkristo wape wote uhuru wa kuabudu.

Kesi hii ipo mtandaoni kwa lugha ya kiingereza. Ukitaka kujisomea kwa undani zaidi. Ingia Google (Tanzlii website) andika National Microfinance Bank Ltd (NMB) Vs Neema Akeyo, 2020.

IMEANDALIWA AU KUTAFSIRIWA na kuletwa kwako nami Zakaria (0754575246 - WhatsApp). Lawyer by profession.
niache tkupiga kazi nikimbilie ibada
 
Back
Top Bottom