Malyenge
JF-Expert Member
- Jan 16, 2012
- 6,658
- 3,646
Wakuu leo hii nimeamua nilete mada hiyo hapo juu tuijadili.
Imekuwa ni kawaida ya wanasiasa wakati wa sherehe za uhuru zinazofanyika kila mwaka kutuhubiria kuwa wananchi walimwondoa mkoloni wa Kiingereza kwa kuwa alikuwa mnyonyaji. Na wamekuwa wakitujaza mawazo hayo ya kiukombozi ili kuhalalisha utawala uliopo madarakani kwamba upo hapo "kihalali'.
Lakini katika kutujaza mawazo hayo ya kiukombozi bado huwa wanashindwa kufafanua ni wapi mkoloni huyo alitunyonya au kutudhulumu kiasi kwamba ikaonekana ni vema mkoloni huyo aondolewe. Kwa mfano, unyonyaji wa mkoloni unaozungumzwa saaaana ni ule wa kutumikisha watu mashambani au viwandani bila malipo au kwa malipo (ujira) kidogo sana . Na udhalimu mbaya kabisa ni ule wa kuwalazimisha watu kufanya kazi na kwa waliokadidi walichapwa viboko. Madai ya uovu wa mkoloni ni mengi sana na yanahadithiwa kwa namna mbalimbali na watu waliokuwapo kipindi kabla ya uhuru.......
Lakini mimi nimefanya utafiti kwa kipindi cha miaka ishirini kwa kutafuta ushahidi wa madai hayo. Napenda kumshukuru Mungu kwa kuniwezesha kuja na ushaidi wa yale niliyoyapata kama ushahidi wa "ubaya" wa mkoloni.Na ushahidi huu nilioupata (conclusion) ni ule unaoitwa ushahidi linganifu kwa minajiri kutafakari kama uhuru tulionao sasa ni uhuru wa kweli na ama hakukuwa na haja ya kudai uhuru huo kwa maana ya kwamba ilikuwa bado mapema ama hakukuwa na haja kabisa. Historia tunayoijua kuhusu Afrika kwa sasa ni ile ya upande mmoja yaani haielezi uzuri wa sisi Waafrika ulikuwaje kipindi tunatawaliwa. Na historia hiyo haielezi kutawaliwa tulikotawaliwa na wakoloni kosa lilikuwa ni la nani au nani alifanya uzembe mpaka tukatawaliwa.
Yafuatayo ndiyo matokeo ya utafiti wangu. (Nawaomba wana JF wakosoe namna nilivyowasilisha utafiti wangu na si hoja zilizomo, maana muda wa kuipanga hii conclusion yangu sina kwa sababuu naandika huku nikiendelea kufanya kazi za watu ofisini). Na isitoshe nimewaomba mchangie na ninyi mnasemaje.
Nawasilisha wakuu.
Imekuwa ni kawaida ya wanasiasa wakati wa sherehe za uhuru zinazofanyika kila mwaka kutuhubiria kuwa wananchi walimwondoa mkoloni wa Kiingereza kwa kuwa alikuwa mnyonyaji. Na wamekuwa wakitujaza mawazo hayo ya kiukombozi ili kuhalalisha utawala uliopo madarakani kwamba upo hapo "kihalali'.
Lakini katika kutujaza mawazo hayo ya kiukombozi bado huwa wanashindwa kufafanua ni wapi mkoloni huyo alitunyonya au kutudhulumu kiasi kwamba ikaonekana ni vema mkoloni huyo aondolewe. Kwa mfano, unyonyaji wa mkoloni unaozungumzwa saaaana ni ule wa kutumikisha watu mashambani au viwandani bila malipo au kwa malipo (ujira) kidogo sana . Na udhalimu mbaya kabisa ni ule wa kuwalazimisha watu kufanya kazi na kwa waliokadidi walichapwa viboko. Madai ya uovu wa mkoloni ni mengi sana na yanahadithiwa kwa namna mbalimbali na watu waliokuwapo kipindi kabla ya uhuru.......
Lakini mimi nimefanya utafiti kwa kipindi cha miaka ishirini kwa kutafuta ushahidi wa madai hayo. Napenda kumshukuru Mungu kwa kuniwezesha kuja na ushaidi wa yale niliyoyapata kama ushahidi wa "ubaya" wa mkoloni.Na ushahidi huu nilioupata (conclusion) ni ule unaoitwa ushahidi linganifu kwa minajiri kutafakari kama uhuru tulionao sasa ni uhuru wa kweli na ama hakukuwa na haja ya kudai uhuru huo kwa maana ya kwamba ilikuwa bado mapema ama hakukuwa na haja kabisa. Historia tunayoijua kuhusu Afrika kwa sasa ni ile ya upande mmoja yaani haielezi uzuri wa sisi Waafrika ulikuwaje kipindi tunatawaliwa. Na historia hiyo haielezi kutawaliwa tulikotawaliwa na wakoloni kosa lilikuwa ni la nani au nani alifanya uzembe mpaka tukatawaliwa.
Yafuatayo ndiyo matokeo ya utafiti wangu. (Nawaomba wana JF wakosoe namna nilivyowasilisha utafiti wangu na si hoja zilizomo, maana muda wa kuipanga hii conclusion yangu sina kwa sababuu naandika huku nikiendelea kufanya kazi za watu ofisini). Na isitoshe nimewaomba mchangie na ninyi mnasemaje.
| WAKATI WA MKOLONI | BAADA YA UHURU (HASA MIAKA YA KARIBUNI) |
1. | Watu walilazimishwa kulima mashamba ya serikali na yao binafsi. | Watu wanahiari ya kukaa bila kufanya kazi |
2. | Reli ilijengwa kwa minajiri ya kusafirisha mazao na abiria | Reli imekufa na hakuna mizigo inayosafirishwa na abiria wachache sana wanaosafiri wanakwama njiani usafiri hauaminiki |
3. | Magereza yalijengwa na kila mhalifu aliingia humo | Magereza yapo lakini ukiwa na pesa huingii kabisa ama ukiingia unaishi kama uko uraiani |
4. | Watu walichapa kazi kwa moyo japokuwa waliogopa viboko | Moyo wa kufanya kazi haupo na kila mtu anataka kufanya kazi lainilaini |
5 | Pesa ilikuwa na thamani japo upatikanaji wake ulikuwa mgumu | Pesa haina thamani upatikanaji ni mgumu kwa watu wa hali ya chini tu. |
6. | Madaraka yalipatikana kwa sifa na uwezo wa mtu | Madaraka yanapatikana kwa pesa na kwa kujuana |
7. | Mahakama na jeshi la polisi ilikuwa ni vyombo vinavyojitegemea | Mahakama na jeshi la polisi ni vyombo vinavyotegemea wanasiasa wanasemaje |
8. | Watu tulikuwa tunapendana sana ! | Watu tumejaa chuki. |
9. | Umoja wa kitaifa ulikuwa katika kiwango cha juu sana. | Utaifa limebaki ni neno la kuombea kura tu. |
10. | Mwananchi alikuwa anategemea kazi na taaluma ndio msingi wa yeye kupata pesa | Kazi na taaluma si kigezo cha mtu kupata pesa. Kupata pesa ni ujanja wa mtu husika. |
Nawasilisha wakuu.