makoye2009
JF-Expert Member
- Jun 12, 2009
- 2,638
- 1,218
Leo wakti nasikiliza vichwa vya habari vya magazeti nikasikia Gazeti la Uhuru linasema,"TUNDU LISSU ASHUSHULIWA''. Gazeti la Mwananchi likajinadi kwa kichwa cha habari ''TUNDU LISSU NA MNYIKA WAMPA SPIKA ANNE MAKINDA WAKATI MGUMU''.
Habari inayozungumziwa hapa ni kile kilichotokea jana Bungeni wakti wa mchakato wa kumpata PM mteule na Naibu wa Spika. Kwa mtu makini anayefuatilia kile kinachoendelea Bungeni hawezi kuandika kichwa cha habari cha kipuuzi kama hicho kilichoandikwa na Mhariri wa gazeti la Uhuru. Hapa ndipo mtu unajua ni kwanini gazeti la Mwananchi lilitaka kufungiwa kwa kuandika ukweli ili hawa wanaoandika uongo waendelee kudanganya watu.
Kichwa sahihi cha matukio ya jana ni cha Gazeti la Mwananchi. Kwa hiyo Mhariri wa gazeti la Uhuru anataka kuwadanganya Watanzania hasa wasiokuwa na TV na radio wasioweza kufuatilia kwa karibu. Huu ni uongo ambao hauwezi kukubalika kwa jamii ya Watanzania. Hii imekuwa ni tabia ya Magazeti yote yanayomilikiwa na CCM na Serikali yake kuandika habari zinazopotosha ukweli au uhalisia wa matukio kama yalivyo.
Ndiyo maana mimi sisomi Uhuru,Mzalendo,Habari Leo,Daily Noise(News) maana haya ni sawa na vijigazeti vya UDAKU kama Kasheshe,Ijumaa,Sani n.k.Angalia lugha iliyotumika,KUSHUSHUA, lugha ambazo tunazisikia kwenye vijiwe,kitchen party au send off za kina mama. Uhuru acheni hizo, hebu badilikeni.Kumbukeni mnatumia fedha za walipa kodi kuchapisha hayo magazeti kuna siku tutawauliza kwa kuchapisha magazeti yasiyonunulika kwa kuandika mambo ya Udaku badala ya kuwahabarisha Watanzania.
HIVI BARAZA LA HABARI mnautaratibu gani wa kuwashughulikia watu wanaoandika habari zenye kupotosha umma? Hebu liangalieni hili.
Habari inayozungumziwa hapa ni kile kilichotokea jana Bungeni wakti wa mchakato wa kumpata PM mteule na Naibu wa Spika. Kwa mtu makini anayefuatilia kile kinachoendelea Bungeni hawezi kuandika kichwa cha habari cha kipuuzi kama hicho kilichoandikwa na Mhariri wa gazeti la Uhuru. Hapa ndipo mtu unajua ni kwanini gazeti la Mwananchi lilitaka kufungiwa kwa kuandika ukweli ili hawa wanaoandika uongo waendelee kudanganya watu.
Kichwa sahihi cha matukio ya jana ni cha Gazeti la Mwananchi. Kwa hiyo Mhariri wa gazeti la Uhuru anataka kuwadanganya Watanzania hasa wasiokuwa na TV na radio wasioweza kufuatilia kwa karibu. Huu ni uongo ambao hauwezi kukubalika kwa jamii ya Watanzania. Hii imekuwa ni tabia ya Magazeti yote yanayomilikiwa na CCM na Serikali yake kuandika habari zinazopotosha ukweli au uhalisia wa matukio kama yalivyo.
Ndiyo maana mimi sisomi Uhuru,Mzalendo,Habari Leo,Daily Noise(News) maana haya ni sawa na vijigazeti vya UDAKU kama Kasheshe,Ijumaa,Sani n.k.Angalia lugha iliyotumika,KUSHUSHUA, lugha ambazo tunazisikia kwenye vijiwe,kitchen party au send off za kina mama. Uhuru acheni hizo, hebu badilikeni.Kumbukeni mnatumia fedha za walipa kodi kuchapisha hayo magazeti kuna siku tutawauliza kwa kuchapisha magazeti yasiyonunulika kwa kuandika mambo ya Udaku badala ya kuwahabarisha Watanzania.
HIVI BARAZA LA HABARI mnautaratibu gani wa kuwashughulikia watu wanaoandika habari zenye kupotosha umma? Hebu liangalieni hili.