Uhuru, Haki, Amani na Demokrasia Vinatokomezwa Awamu hii ya tano

TL. Marandu

JF-Expert Member
Jul 12, 2015
3,625
5,807
Kwa Ufupi sana niseme, Afrika na Tanzania ikiwemo, miaka ya 1950 hadi 1990 kulikiwepo na Juhudi kubwa sana za Kudai uhuru, haki na Demokrasia. Jitihada hizi ziligharimu sana, kwa maana ya maisha kuharibiwa, mali na hata uhai wa wengine waliokuwa mstari wa Mbele wa Mapambano.

Mapambano ya Kudai Uhuru na Haki, Hayakuwa hasa mapambano ya Kudai Barabrara za Lami, maana Angola, Namibia hiyo vilikuwepo! Mapambano hayo hayakuwa Kudai kuwepo kwa Ndege mpya kwani SA sio tu walikuwa na Shirika la Ndege maarufu bali waliunda ndege, Magari na Vifaru. Mapambano haya hayakuwa ya Kutaka flyovers za mijini maana Pretoria na Johannesburg na Namibi hizozilijaa.

Mapambano haya hayakuwa ya Kudai Uwepo wa Panadol au Chloroquine hospitalini, Ingawa hayo yalikuwa ni ya Muhimu. Mapambano hayo yayakuwa ya Kudai mifumo ya maji maana mifumo ya maji ya Wajerumani na Waingereza ilikuwa The best!

Kumbe Tulimwaga damu kudai nini? UHURU, HAKI, DEMOKRASIA na Kuthaminiwa UTU wetu! Ati Leo Viongozi wanaolipwa Kututumikia Katika Taifa wanataka Tuwalipe sio kwa Mishahara tu Bali kwa Sarafu ya Uhuru wetu na Demokrasia yetu, Mbanu! Tena anataka Malipo hayo apewe kwa sera ambazo zimeshidwa, zinazopewa Budget ya asilimia 3% Nikitoa Mfano wa Sera ya Viwana ambapo Cherehani nne na Msishangae Mbuzi ya kukuna nazi vinazinduliwa na kuhesabika kama "viwanda" Masikini wa shetani"

SERIKALI:
Serikali ya Magufuli inafanya mambo mengi ya Moja kwa moja Ikiwa ni Pamoja na 1) kuzuia mikutano ya siasa, hivi je sheria inaruhuru leo hii kuanzishwa kwa chama kipya cha siasa? Na kama jibu ni ndio, je chama hicho kitawezaje kushiriki Uchaguzi 2020 iwapo mikutano ya siasa kinachoweza kufanya ni ike ya kampeni ya 2020?
2) Huna aibu Kumzuia Lowassa aliyeshinda Arusha, Dar es salaam, Moshi, Mbeya etc ambako pengine hata kura tatu maeneo hayo hukupata ati Lowassa au Mbowe akiwa kama Mwenyekiti wa Taifa hawezi kufanya mikutano kwa ajili ya Kukijenga CHAMA chake, lakini wewe Unatumia kisingizio cha Urais ambao Ulishakushinda tangu mapema, kujenga CHAMA chako kwenye maeneo hayo! Tena kwa siasa chafu sana na zilizojaa hila?

BUNGE:
Ndugai ni Speaker Mnafiki na Wa hovyo kupata kutokea Africa! Swala la Adhabu ya Mnyika, Halima Mdee na Ester Bulaya. 1) Ndugai, hivi iwapo Wewe unaweza kumfungia Mbunge kwa Muda wowote? Unataka Kutwambia Unaweza kwa adhabu, kufuta Ubunge wa Mbunge kwa Kumpa adhabu Mbunge ya Miaka mitano, Tena kwa Kutumia Kura za Wapinzani wa Chama cha Mbunge huyo!
2) Kwa Mtindo wako wa Kutumia Kura za CCM waliojipa wingi Bungeni kwa Kuiba kura! Ni lini unadhani Mpinzani atapata haki kwa adhabu hizo? Kwa wingi wa Wabunge wa CCM, Ni hekima gani inakupa uhakika kuwa ipo siku watapiga kura kumwadhibu Mbunge mwenzao kwa Kumtusi Mbunge wa Upinzani au Kukiuka taratibu za Bunge? Nachoona ni kuwa hawatasita kuwaadhibu Wabunge Principled wa CCM kama Hussein Bashe!

MAHAKAMA:
Ni nani anaamini sababu ya Magufuli ya Kumteua Kaimu Judge haina lengo la Unafiki wa kishetani wa Obstraction of Justuce, kwa Kumweka Judge kwenye Makucha ya Vitisho Kuwa asipofanya atakavyo Ataondolewa? Kuwepo na Kaimu Judge ni Lengo chafu na Ovu la Kupokonya Uhuru wa Mahakama na kuushikilia Mikononi mwa mtu Mmoja, Waziri wa Sheria na Katiba amabaye Nilimwona ni ovyo na mwenye Ngebe uchwara anaweza kutetea kwa umilele jshetani huu, Lakini ukweli Utabaki ni Rais Mwovu sana, anayeweza muwa na Utamani na Kutekeleza Azma ya kutaka kuikanyaga Mahakama chini ya Miguu!

Ni kwa sababu hii Nasema Kuwa Uhuru, Haki na Demkkrasia Tanzania, Vinashambuliwa, Na Vinashambuliwa na Aliyekabidhiwa Mkuki na Ngao Kuvilinda, sasa ameamua kutumia Mkuki na Ngao Kuvitangazia Vita! Ati iwe ni Malipo yake ya Kununua Vibonbardiar, Kutekeleza Programs za Kikwete za Reli Pana, na Kuzindua Flyover miradi aliyoianza Mh. Kikwete!

Magufuli, Kama Mshahara, Chakula, Mavazi, Unavyopewa na Watanzania habikutoshi Unataka Ulipwe kwa Sarafu ya Uhuru na Demokrasia, Hilo haliwezekani, bora Ujiuzulu waachie wengine watakaoridhika na Mshahara wa Kawaida.

Magufuli, Kama Zulia Jekundu unalowekewa from Time to time halikutoshi, na Unataka Zulia la Katiba na Utawala wa Katiba, ati tukutandikie hivyo Uvikanyage viwe ndio badala ya zulia Mkuu nakwambia Patachimbika! Sana na sio Kidogo!
 
Kwa Ufupi sana niseme, Afrika na Tanzania ikiwemo, miaka ya 1950 hadi 1990 kulikiwepo na Juhudi kubwa sana za Kudai uhuru, haki na Demokrasia. Jitihada hizi ziligharimu sana, kwa maana ya maisha kuharibiwa, mali na hata uhai wa wengine waliokuwa mstari wa Mbele wa Mapambano.

Mapambano ya Kudai Uhuru na Haki, Hayakuwa hasa mapambano ya Kudai Barabrara za Lami, maana Angola, Namibia hiyo vilikuwepo! Mapambano hayo hayakuwa Kudai kuwepo kwa Ndege mpya kwani SA sio tu walikuwa na Shirika la Ndege maarufu bali waliunda ndege, Magari na Vifaru. Mapambano haya hayakuwa ya Kutaka flyovers za mijini maana Pretoria na Johannesburg na Namibi hizozilijaa.

Mapambano haya hayakuwa ya Kudai Uwepo wa Panadol au Chloroquine hospitalini, Ingawa hayo yalikuwa ni ya Muhimu. Mapambano hayo yayakuwa ya Kudai mifumo ya maji maana mifumo ya maji ya Wajerumani na Waingereza ilikuwa The best!

Kumbe Tulimwaga damu kudai nini? UHURU, HAKI, DEMOKRASIA na Kuthaminiwa UTU wetu! Ati Leo Viongozi wanaolipwa Kututumikia Katika Taifa wanataka Tuwalipe sio kwa Mishahara tu Bali kwa Sarafu ya Uhuru wetu na Demokrasia yetu, Mbanu! Tena anataka Malipo hayo apewe kwa sera ambazo zimeshidwa, zinazopewa Budget ya asilimia 3% Nikitoa Mfano wa Sera ya Viwana ambapo Cherehani nne na Msishangae Mbuzi ya kukuna nazi vinazinduliwa na kuhesabika kama "viwanda" Masikini wa shetani"

SERIKALI:
Serikali ya Magufuli inafanya mambo mengi ya Moja kwa moja Ikiwa ni Pamoja na 1) kuzuia mikutano ya siasa, hivi je sheria inaruhuru leo hii kuanzishwa kwa chama kipya cha siasa? Na kama jibu ni ndio, je chama hicho kitawezaje kushiriki Uchaguzi 2020 iwapo mikutano ya siasa kinachoweza kufanya ni ike ya kampeni ya 2020?
2) Huna aibu Kumzuia Lowassa aliyeshinda Arusha, Dar es salaam, Moshi, Mbeya etc ambako pengine hata kura tatu maeneo hayo hukupata ati Lowassa au Mbowe akiwa kama Mwenyekiti wa Taifa hawezi kufanya mikutano kwa ajili ya Kukijenga CHAMA chake, lakini wewe Unatumia kisingizio cha Urais ambao Ulishakushinda tangu mapema, kujenga CHAMA chako kwenye maeneo hayo! Tena kwa siasa chafu sana na zilizojaa hila?
BUNGE:
Ndugai ni Speaker Mnafiki na Wa hovyo kupata kutokea Africa! Swala la Adhabu ya Mnyika, Halima Mdee na Ester Bulaya. 1) Ndugai, hivi iwapo Wewe unaweza kumfungia Mbunge kwa Muda wowote? Unataka Kutwambia Unaweza kwa adhabu, kufuta Ubunge wa Mbunge kwa Kumpa adhabu Mbunge ya Miaka mitano, Tena kwa Kutumia Kura za Wapinzani wa Chama cha Mbunge huyo!
2) Kwa Mtindo wako wa Kutumia Kura za CCM waliojipa wingi Bungeni kwa Kuiba kura! Ni lini unadhani Mpinzani atapata haki kwa adhabu hizo? Kwa wingi wa Wabunge wa CCM, Ni hekima gani inakupa uhakika kuwa ipo siku watapiga kura kumwadhibu Mbunge mwenzao kwa Kumtusi Mbunge wa Upinzani au Kukiuka taratibu za Bunge? Nachoona ni kuwa hawatasita kuwaadhibu Wabunge Principled wa CCM kama Hussein Bashe!

MAHAKAMA:
Ni nani anaamini sababu ya Magufuli ya Kumteua Kaimu Judge haina lengo la Unafiki wa kishetani wa Obstraction of Justuce, kwa Kumweka Judge kwenye Makucha ya Vitisho Kuwa asipofanya atakavyo Ataondolewa? Kuwepo na Kaimu Judge ni Lengo chafu na Ovu la Kupokonya Uhuru wa Mahakama na kuushikilia Mikononi mwa mtu Mmoja, Waziri wa Sheria na Katiba amabaye Nilimwona ni ovyo na mwenye Ngebe uchwara anaweza kutetea kwa umilele jshetani huu, Lakini ukweli Utabaki ni Rais Mwovu sana, anayeweza muwa na Utamani na Kutekeleza Azma ya kutaka kuikanyaga Mahakama chini ya Miguu!

Ni kwa sababu hii Nasema Kuwa Uhuru, Haki na Demkkrasia Tanzania, Vinashambuliwa, Na Vinashambuliwa na Aliyekabidhiwa Mkuki na Ngao Kuvilinda, sasa ameamua kutumia Mkuki na Ngao Kuvitangazia Vita! Ati iwe ni Malipo yake ya Kununua Vibonbardiar, Kutekeleza Programs za Kikwete za Reli Pana, na Kuzindua Flyover miradi aliyoianza Mh. Kikwete!

Magufuli, Kama Mshahara, Chakula, Mavazi, Unavyopewa na Watanzania habikutoshi Unataka Ulipwe kwa Sarafu ya Uhuru na Demokrasia, Hilo haliwezekani, bora Ujiuzulu waachie wengine watakaoridhika na Mshahara wa Kawaida.

Magufuli, Kama Zulia Jekundu unalowekewa from Time to time halikutoshi, na Unataka Zulia la Katiba na Utawala wa Katiba, ati tukutandikie hivyo Uvikanyage viwe ndio badala ya zulia Mkuu nakwambia Patachimbika! Sana na sio Kidogo!


Demokrasia ni pamoja na uhuru wa kuyoa mawazo kama ufanyavy sasa hivi..

Hizo za nani kashinda tulikuwepo na kushuhudia Lowasa akishinda baadhi ya maeneo na mengine mengi kushindwa kila overall winner ni Rais John P. Magufuli.
 
Demokrasia ni pamoja na uhuru wa kuyoa mawazo kama ufanyavy sasa hivi..

Hizo za nani kashinda tulikuwepo na kushuhudia Lowasa akishinda baadhi ya maeneo na mengine mengi kushindwa kila overall winner ni Rais John P. Magufuli.
Komputer wakapora za nini? Na kwa kuwa wewe Unajifanya Mkweli Zanzibar alishinda nani? Ule Uchaguzi wa halali uliofutwa na sio mazingaombwe ya Malaya Jecha!
 
Komputer wakapora za nini? Na kwa kuwa wewe Unajifanya Mkweli Zanzibar alishinda nani? Ule Uchaguzi wa halali uliofutwa na sio mazingaombwe ya Malaya Jecha!
upuuzi mmojawapo ni kuhisi lowassa angeshinda urais wakati asilimia 65+ ya wabunge wote ni CCM hiyo serikali ingekuwa ya UJUHA....upinzani acheni upuuzi ongezeni viti bungeni uraisi wekeni kapuni kwanza shika Bunge atleast 45%
 
Ahsanta ndugu TL. Marandu kwa andiko lako.
BUNGE: Spika ndugai hafanyi anayofanya kwa utashi wake mwenyewe. Ni kanunu za kudumu za bunge ndizo zinazofanya kazi. Kanuni za bunge zinampa spika mamlaka ya kumuwajibisha mbuge pale anapokiuka misingi na taratibu za bunge. Halima Mdee, Mnyika na Bulaya walipewa adhabu kwa kufuata misingi iliyowekwa na bunge, sio ndugai. Hawa walipewa adhabu kwa kuzingatia kanuni na si kwamba wabunge wa ccm ndio walishinikiza adhabu itolewe kwa misingi ya wingi wao bungeni. Bunge linayo mamlaka ya kumsimanisha mbunge kwa kipindi hadi miaka mitano.
MAHAKAMA: Raisi kamteua kaimu jaji mkuu kwa mujibu wa katiba ya jamhuri ya muungano. Inapotekea jaji mkuu hayupo katika ofisi lazima kuwe na kaimu au jaji mkuu mwingine, na katiba haimlazimishi raisi kuteua jaji mkuu kama kuna kaimu jaji mkuu.
sijaona kosa lolote lililofanywa na watu hawa wawili katika hili.
Demokrasia ni kutekeleza misingi ya katiba na sheria zingine. Spika na Raisi wakitekeleza matakwa ya sheria moja kwa moja wamejenga demokrasia, uhuru na haki. Muhimu ni kwa hao wanaoona haki, uhuru na demokrasia zinagandamizwa kufahamu misingi ya haki na uhuru wao, pamoja na kutambua wajibu wao.
Sioni mantiki ya kuwatetea wabunge waliokaidi kiti cha spika na kukanyaga tartibu za bunge. Kwa maoni yangu wao ndio wapinga uhuru, wakandamiza haki na wanadidimiza demokrasia.
 
upuuzi mmojawapo ni kuhisi lowassa angeshinda urais wakati asilimia 65+ ya wabunge wote ni CCM hiyo serikali ingekuwa ya UJUHA....upinzani acheni upuuzi ongezeni viti bungeni uraisi wekeni kapuni kwanza shika Bunge atleast 45%
Hawakushinda kihalali na hata kama walishinda kihalali? Kuwa na Wabunge wengi wa CCM huko mbugani hakuondoi ukweli kuwa Lowassa Alishinda Karibu majiji yote yenye Population kubwa na wanzojua tofauti ya Mchele na Mapumba!
 
Hawakushinda kihalali na hata kama walishinda kihalali? Kuwa na Wabunge wengi wa CCM huko mbugani hakuondoi ukweli kuwa Lowassa Alishinda Karibu majiji yote yenye Population kubwa na wanzojua tofauti ya Mchele na Mapumba!
ndugu yangu asilimia 65+ yote ya wabunge wameiba kweliiii?????niambie na majimbo ya ukawa mangapi mligawana Kura???niambie majimbo mangapi hamkuweka wawakilishi???niambie majimbo mangapi hamkuwapa ushirikiano wa kutosha kuratibu kampeni zao??acheni sababu za kipuuzi.
nakwambie tena Lowassa hakushinda kama mlikubali kuibiwa kura asilimia 65+ ya wabunge wote tuwaamini vipi kwenye uraisi??useless....
 
Ahsanta ndugu TL. Marandu kwa andiko lako.
BUNGE: Spika ndugai hafanyi anayofanya kwa utashi wake mwenyewe. Ni kanunu za kudumu za bunge ndizo zinazofanya kazi. Kanuni za bunge zinampa spika mamlaka ya kumuwajibisha mbuge pale anapokiuka misingi na taratibu za bunge. Halima Mdee, Mnyika na Bulaya walipewa adhabu kwa kufuata misingi iliyowekwa na bunge, sio ndugai. Hawa walipewa adhabu kwa kuzingatia kanuni na si kwamba wabunge wa ccm ndio walishinikiza adhabu itolewe kwa misingi ya wingi wao bungeni. Bunge linayo mamlaka ya kumsimanisha mbunge kwa kipindi hadi miaka mitano.
MAHAKAMA: Raisi kamteua kaimu jaji mkuu kwa mujibu wa katiba ya jamhuri ya muungano. Inapotekea jaji mkuu hayupo katika ofisi lazima kuwe na kaimu au jaji mkuu mwingine, na katiba haimlazimishi raisi kuteua jaji mkuu kama kuna kaimu jaji mkuu.
sijaona kosa lolote lililofanywa na watu hawa wawili katika hili.
Demokrasia ni kutekeleza misingi ya katiba na sheria zingine. Spika na Raisi wakitekeleza matakwa ya sheria moja kwa moja wamejenga demokrasia, uhuru na haki. Muhimu ni kwa hao wanaoona haki, uhuru na demokrasia zinagandamizwa kufahamu misingi ya haki na uhuru wao, pamoja na kutambua wajibu wao.
Sioni mantiki ya kuwatetea wabunge waliokaidi kiti cha spika na kukanyaga tartibu za bunge. Kwa maoni yangu wao ndio wapinga uhuru, wakandamiza haki na wanadidimiza demokrasia.
Hizo Kanuni katika Bunge hili la 11 zimemwadhibu Lusinde aliyekuwa akisema Atamfanya Mnyika Anyee Nguo, au badala ya kupokea au kukataa Taarifa ya Mnyika alisema Wabunge hao aina ya Mnyika wapimwe Bangi, Madawa na Pombe? Wewe Bro Unatete Ndugai ambaye ni swa Na Mwenye Rebies! Ovyo ovyo ovyo! Nina Taarifa Ndugai katishiwa indirect kuwa 2020 atanyimwa tiketi kama hatumia bunge kuangamiza Chadema! Ingawa pamoja na Vitisho Ndugai ni Mtu unstable, mwenye Bipolar na mithili ya &@%#€¢£ Mwenye Rebies!
 
ndugu yangu asilimia 65+ yote ya wabunge wameiba kweliiii?????niambie na majimbo ya ukawa mangapi mligawana Kura???niambie majimbo mangapi hamkuweka wawakilishi???niambie majimbo mangapi hamkuwapa ushirikiano wa kutosha kuratibu kampeni zao??acheni sababu za kipuuzi.
nakwambie tena Lowassa hakushinda kama mlikubali kuibiwa kura asilimia 65+ ya wabunge wote tuwaamini vipi kwenye uraisi??useless....
Sikusema hivyo? Ila ajabu iko wapi? Kama wanaweza kuiba 100% ya Urais wa Zanzibar? Hivi kama CCM walishinda kihalali, Computer za Ukawa za parallel Tabulation walipora za nini? Na kama Parallel Tabulation ni Uhaini? Kwanini Magufuli anamsadia Raila na ODM kusetup Parallel Tabulation center Dar es salaam?
 
Na hata kama nikisema, " Kishingo upande" kuwa Magufuli alishinda je huko kunampa uhalali gani kufanya Maduduli, kumradhi madudu anayofanya?
 
Sikusema hivyo? Ila ajabu iko wapi? Kama wanaweza kuiba 100% ya Urais wa Zanzibar? Hivi kama CCM walishinda kihalali, Computer za Ukawa za parallel Tabulation walipora za nini? Na kama Parallel Tabulation ni Uhaini? Kwanini Magufuli anamsadia Raila na ODM kusetup Parallel Tabulation center Dar es salaam?
eee bwana eeeh, daaah
 
ndugu yangu asilimia 65+ yote ya wabunge wameiba kweliiii?????niambie na majimbo ya ukawa mangapi mligawana Kura???niambie majimbo mangapi hamkuweka wawakilishi???niambie majimbo mangapi hamkuwapa ushirikiano wa kutosha kuratibu kampeni zao??acheni sababu za kipuuzi.
nakwambie tena Lowassa hakushinda kama mlikubali kuibiwa kura asilimia 65+ ya wabunge wote tuwaamini vipi kwenye uraisi??useless....
Hapo ndipo CCM wakaweza shinda huko porini ambapo mtu anashinda Ubunge kwa kura 8500 vs Majijini ambapo mbunge mmoja wa Chema, kumradhi, Chadema anapata kura 250,000, which means kura zake ni sawa na za Wabunge zaidi ya Walizoshindia Wabunge 25 kwa mpigo wa aina ya Ally Kessy wa Nkasi.
 
Ahsanta ndugu TL. Marandu kwa andiko lako.
BUNGE: Spika ndugai hafanyi anayofanya kwa utashi wake mwenyewe. Ni kanunu za kudumu za bunge ndizo zinazofanya kazi. Kanuni za bunge zinampa spika mamlaka ya kumuwajibisha mbuge pale anapokiuka misingi na taratibu za bunge. Halima Mdee, Mnyika na Bulaya walipewa adhabu kwa kufuata misingi iliyowekwa na bunge, sio ndugai. Hawa walipewa adhabu kwa kuzingatia kanuni na si kwamba wabunge wa ccm ndio walishinikiza adhabu itolewe kwa misingi ya wingi wao bungeni. Bunge linayo mamlaka ya kumsimanisha mbunge kwa kipindi hadi miaka mitano.
MAHAKAMA: Raisi kamteua kaimu jaji mkuu kwa mujibu wa katiba ya jamhuri ya muungano. Inapotekea jaji mkuu hayupo katika ofisi lazima kuwe na kaimu au jaji mkuu mwingine, na katiba haimlazimishi raisi kuteua jaji mkuu kama kuna kaimu jaji mkuu.
sijaona kosa lolote lililofanywa na watu hawa wawili katika hili.
Demokrasia ni kutekeleza misingi ya katiba na sheria zingine. Spika na Raisi wakitekeleza matakwa ya sheria moja kwa moja wamejenga demokrasia, uhuru na haki. Muhimu ni kwa hao wanaoona haki, uhuru na demokrasia zinagandamizwa kufahamu misingi ya haki na uhuru wao, pamoja na kutambua wajibu wao.
Sioni mantiki ya kuwatetea wabunge waliokaidi kiti cha spika na kukanyaga tartibu za bunge. Kwa maoni yangu wao ndio wapinga uhuru, wakandamiza haki na wanadidimiza demokrasia.
Kuzuia Misiba na Kukwapua Rambi rambi pia ni Kutekeleza Sheria kwa Mantiki yako! Ngoja nikatafute Kisadolini ikiwa Kichefu chefu kitanizidi, " Hey Olympia get me a little bucket"
 
Kuzuia Misiba na Kukwapua Rambi rambi pia ni Kutekeleza Sheria kwa Mantiki yako! Ngoja nikatafute Kisadolini ikiwa Kichefu chefu kitanizidi, " Hey Olympia get me a little bucket"
Mlaumu na kumkosoa aliyekwapua rambirambi, sio cheo chake au serikali. Mambo ya kukusanya rambirambi usiyahusihse na utendaji wa serikali katika misingi ya haki na demokrasia. Hata wewe ungeweza kwapua tu hizo rambirambi lakin haki na demokrasia vinabaki palepale
 
Hapo ndipo CCM wakaweza shinda huko porini ambapo mtu anashinda Ubunge kwa kura 8500 vs Majijini ambapo mbunge mmoja wa Chema, kumradhi, Chadema anapata kura 250,000, which means kura zake ni sawa na za Wabunge zaidi ya Walizoshindia Wabunge 25 kwa mpigo wa aina ya Ally Kessy wa Nkasi.
Ndio maana demokrasia yetu ya mdumo wa bunge ina utaratibi wa mbumbe mmoja kiti kimoja wala sio kura moja kiti kimoja. Kama nunyi mnang'ang'ania majimbo yenye watu wengi shauri yenu, mtaendelea kuwa kambi ya upinzani milele
 
Ndio maana demokrasia yetu ya mdumo wa bunge ina utaratibi wa mbumbe mmoja kiti kimoja wala sio kura moja kiti kimoja. Kama nunyi mnang'ang'ania majimbo yenye watu wengi shauri yenu, mtaendelea kuwa kambi ya upinzani milele
Sawa Mkuu!
 
Inaonekana Bwana yule anatamani sana nchi yetu irejee kwenye mfumo wa chama kimoja....

Hata hivyo jambo hilo haliwezekani hata kama anatamani hivyo kutokana na mfumo wa dunia yetu ya sasa.
 
Mlaumu na kumkosoa aliyekwapua rambirambi, sio cheo chake au serikali. Mambo ya kukusanya rambirambi usiyahusihse na utendaji wa serikali katika misingi ya haki na demokrasia. Hata wewe ungeweza kwapua tu hizo rambirambi lakin haki na demokrasia vinabaki palepale
Nonesense Bosi wake kama hakumtuma alimfanyaje? Uskinifuondishe siasa! Na hiyo sio Mara ya kwanza!
 
Back
Top Bottom