Uhuni wanaofanyiwa walimu wa sekondari wa mkoa wa Tabora waliokuja marking ya mock mkoa tangu jana hauvumiliki!!

NAMBA MOJA AJAYE NCHINI

JF-Expert Member
Oct 29, 2019
8,509
17,411
Napewa taarifa za malalamiko ya walimu hawa waliotelekezwa tangu jana jioni kwa kutopewa walau hata chakula cha jioni hapo TABORA TTC! Wanalishwa milo miwili tu kwa siku yaani chai na chakula cha mchana bila chakula cha jioni!! Hadi hapa napoandika ujumbe huu ni kwamba walimu hao hawajala hadi sasa wanalalamika tu njaa zinawauma tangu walipokula saa saba!!!"

YAANI WANATUONA WAJINGA SANA HAWA MAAFISA ELIMU! HADI SASA SAA MBILI HII USIKU HATUJALA WALA HATA MALIPO YA AWALI HATUJAPOKEA" Akiongea kwa simu mwalimu mmoja kaniambia!! Nimeshangazwa sana hivi kwani Afisa elimu Mkoa na katibu Tawala Tabora wanajua haya??? Kuwa walimu wao wanashindishwa njaa usiku siku ya pili??

Tena wakiambiwa malipo ya kusahisha script moja sh.200 wakati kila mwanafunzi wa kidato cha nne kalipiwa shilingi 8000|= na serekali fedha elimu bure kwa mtihani huu wa mock mkoa!!

Natoa wito kwa waziri wa Elimu, Katibu wa wizara ya elimu, katibu tawala wa mkoa na afisa elimu wa mkoa wa Tabora pamoja na TAMISEMI Kuchukua hatua!! Serekali itambue walimu hawa wanaodhulumiwa haki zao nyingi kama hivi ni wasimamizi wa uchaguzi miaka yote! Kuwatenda haya ni kukoleza pili na chumvi kwenye kidonda cha miaka mitano ya utawala huu wa kutojali haki zao!! Ikumbukwe wana ndugu ambao ni wapiga kura!!

Mamlaka husika chukueni hatua kwa udhalilishaji huu wa walimu hawa!!

Tahadhari; Sitafuti cheo wala simtakii yeyote baya kwa bandiko hili!!

Tabora kuna matatizo sana ya watumishi wa umma kuliko kanda zote za nchi hii!

Asanteni kwa kusoma!!!
 
Haya sasa Ndugu Ndalichako na Magufulisi mpo Kigoma? Na kesho mko njiani kwenda Tabora kwenye kampeni? Anzeni na hilo!! Wasimamizi wa uchaguzi ujao wanapigwa hela za kusahihisha na chakula!!!! KAZI KWENU!!!
 
The breed. Kumbe wewe Ni mwalimu wa secondary.... Kila nikikuona nilidhani wa VETA
Mkuu mi sio ticha wa sec!! Sema na jamaa zangu wapo pale wamenitonya!! Halafu hizi harakati za walimu kujikomboa wanapaswa kuungana walitumie jukwaa hili kutoa changamoto zao! Na sio kuonewa onewa na watumishi wa halmashauri!!
 
Umetiririka poa, lakini ulipoingiza tu mambo ya siasa kwenye taaluma, nikaona ndiyo walewale, yaani wazee wa nongwa ama ngebe!

Sasa ukisimamia uchaguzi, kuna kitu utapindisha kwa chuki zako binafsi?

Kama haujaenda kuozea 'kwa zuberi' au Uyui kabisa ili kukutia adabu!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Umetiririka poa, lakini ulipoingiza tu mambo ya siasa kwenye taaluma, nikaona ndiyo walewale, yaani wazee wa nongwa ama ngebe!

Sasa ukisimamia uchaguzi, kuna kitu utapindisha kwa chuki zako binafsi?

Kama haujaenda kuozea 'kwa zuberi' au Uyui kabisa ili kukutia adabu!

Sent using Jamii Forums mobile app
Nilikuwa nawakumbusha wenye dhamana!!!wauache uhuni wao !hawaoni kuwa wana mchonganisha Raisi na wapiga kura wake???
 
Napewa taarifa za malalamiko ya walimu hawa waliotelekezwa tangu jana jioni kwa kutopewa walau hata chakula cha jioni hapo TABORA TTC! Wanalishwa milo miwili tu kwa siku yaani chai na chakula cha mchana bila chakula cha jioni!! Hadi hapa napoandika ujumbe huu ni kwamba walimu hao hawajala hadi sasa wanalalamika tu njaa zinawauma tangu walipokula saa saba!!!"

YAANI WANATUONA WAJINGA SANA HAWA MAAFISA ELIMU! HADI SASA SAA MBILI HII USIKU HATUJALA WALA HATA MALIPO YA AWALI HATUJAPOKEA" Akiongea kwa simu mwalimu mmoja kaniambia!! Nimeshangazwa sana hivi kwani Afisa elimu Mkoa na katibu Tawala Tabora wanajua haya??? Kuwa walimu wao wanashindishwa njaa usiku siku ya pili??

Tena wakiambiwa malipo ya kusahisha script moja sh.200 wakati kila mwanafunzi wa kidato cha nne kalipiwa shilingi 8000|= na serekali fedha elimu bure kwa mtihani huu wa mock mkoa!!

Natoa wito kwa waziri wa Elimu, Katibu wa wizara ya elimu, katibu tawala wa mkoa na afisa elimu wa mkoa wa Tabora pamoja na TAMISEMI Kuchukua hatua!! Serekali itambue walimu hawa wanaodhulumiwa haki zao nyingi kama hivi ni wasimamizi wa uchaguzi miaka yote! Kuwatenda haya ni kukoleza pili na chumvi kwenye kidonda cha miaka mitano ya utawala huu wa kutojali haki zao!! Ikumbukwe wana ndugu ambao ni wapiga kura!!

Mamlaka husika chukueni hatua kwa udhalilishaji huu wa walimu hawa!!

Tahadhari; Sitafuti cheo wala simtakii yeyote baya kwa bandiko hili!!

Tabora kuna matatizo sana ya watumishi wa umma kuliko kanda zote za nchi hii!

Asanteni kwa kusoma!!!
Wakipewa chakula cha jioni hawatapata half per diem! Wewe unataka wakiondoka wasiwe na pesa ya mfukoni.
 
Kwahiyo ukisahihisha script 100 ndio 2,000/=, mi nadhani dawa ni kuacha kusomea ualimu, the lower the supply the higher the price, tatizo lenu mnapenda kisomea vitu rahisi rahisi ndio maana mnajikutabwengi mmejazana humo
Hapana ni shs 20,000/= lakini sidhani kama kuna atajayefikisha hizo 100 kwa siku landa kama ni multiple choice questions. Pole yao ndiyo maana walimu wengi wa kike wanajiuza kirahisi kwa kila anayehitaji huduma yao.
 
Kwahiyo ukisahihisha script 100 ndio 2,000/=, mi nadhani dawa ni kuacha kusomea ualimu, the lower the supply the higher the price, tatizo lenu mnapenda kisomea vitu rahisi rahisi ndio maana mnajikutabwengi mmejazana humo
hebu rudi shule wakafundishe tena kufanya hesabu. Kama umeshindwa hesabu rahisi tu ya 200*100=? Sasa unaweza kitu gani.
 
Back
Top Bottom