Uharibifu wa miundombinu ya UDART

Gullam

JF-Expert Member
Dec 1, 2013
5,240
3,931
Salamu wana body.

Kwanza nianze kuwatakia waislamu wote funga njema ya mwezi mtukufu.
Leo kwa mara ya kwanza nimepita feri kupitia mwendo kasi, mara niliposhuka tu kivukoni terminal nikapatwa na haja ndogo, nikaona si uungwana kujibana wakati huduma ya choo ipo pale. Nikatoa dinari yangu, ili ninue ile huduma, lakini ghafla nilipo ingia ndani mambo niliyoyakuta nilishindwa kuvumilia.

Nilijiuliza maswali mengi mengi yasio na majibu, je kama kweli wameshindwa kuvilekebisha hivi vyoo ambavyo huduma yake inalipiwa, wateweza kweli kutengeneza stendi zao, au hata magari yao yatakapo haribika? Chonde chonde watanzania tuache kasumba ya kizamani, mradi usio hata na miaka mitatu hali iko hivi kweli!! Wajuzi wa mambo njooeni muwashauli hawa waungwana. Naambatanisha na picha hapa chini.
 
Mradi huu umezidiwa ila wanashindwa kukiri tu.Sasa hivi unaweza kukaa kituoni dakika 30 bila kupanda basi.Wakati mwanzoni ilikuwa kila dakika 5 basi inafika inachukua abiria na kuondoka.
 
Maintanance ni msamiati mgumu sana kwetu. Hakuna tunachoweza kutunza hasa kiwe mali ya uma
 
Nimeshindwa kuupload picha nilizopiga pale terminal kivukoni, ila nina hakika huu mradi hauna miaka 10 utakuwa umejifilia kabisa. Ukienda kwenye sub termina unakuta pool haina kiti hata kimoja unasima kusubili bus mpaka unaamua kuchuchumaa ni hatari sana. Halafu tuwe wa kweli, huu mradi pamoja ni biashara vilevile ni huduma, sass walishindwa kweli kuweka hata socket za umeme kwenye hizi terminal ili abilia basi wanaposubilia usafiri waweze kuwasiliana na wengine ili mambo yasikwame. Yaani mradi mkubwa supervision ilikuwa mbali sana, hata sijui consultant alikuwa anafanya kazi gani.
 

Similar Discussions

1 Reactions
Reply
Back
Top Bottom