Wandugu,
Napenda kufahamu kitaalamu juu ya imani au uvumi kuwa mtoto mchanga anapozaliwa lazima mzazi na hasa mama ahakikishe kuwa kitovu cha mtoto huyo kitakapokauka na kudondoka basi kisiguse sehemu nyeti za huyo mtoto. Inasemekana kuwa ikitokea kuwa kitovu hicho kimedondoka na kugusa sehemu hizo nyeti basi mtoto huyo kama ni wa kiume atakuwa bwabwa na kama ni wa kike nae atakuwa msagaji? (hatakuwa na feeling za kuhitaji mwanaume)..
Nahitaji maelezo ya kitaalamu na hasa kwenu nyie wataalamu wa tiba kuhusu hili kwani yanazungumzwa lakini hakuna justification ya kitaalamu inayotolewa zaidi ya kuonekana ni mapokeo ya imani tu.
Napenda kufahamu kitaalamu juu ya imani au uvumi kuwa mtoto mchanga anapozaliwa lazima mzazi na hasa mama ahakikishe kuwa kitovu cha mtoto huyo kitakapokauka na kudondoka basi kisiguse sehemu nyeti za huyo mtoto. Inasemekana kuwa ikitokea kuwa kitovu hicho kimedondoka na kugusa sehemu hizo nyeti basi mtoto huyo kama ni wa kiume atakuwa bwabwa na kama ni wa kike nae atakuwa msagaji? (hatakuwa na feeling za kuhitaji mwanaume)..
Nahitaji maelezo ya kitaalamu na hasa kwenu nyie wataalamu wa tiba kuhusu hili kwani yanazungumzwa lakini hakuna justification ya kitaalamu inayotolewa zaidi ya kuonekana ni mapokeo ya imani tu.
Kitaalamu hilo suala la kitovu kinapoangua na kugusa sehemu nyeti za mtoto na kumfanya awe hanidhi si ukweli. Mie nahisi ni mila za baadhi ya makabila.
Kitaalam mtoto kila anapokuwa katika kipindi fulani basi kuna mambo lazima atapitia,sasa mzazi ambaye atamkataza huyu mtoto kufanya haya mambo yanaweza kumuathiri kisaikologia.
Mfano watoto wengi katika umri fulani huwa wanacheza kama vile wazazi katika familia, mtoto wa kiume baba na mtoto wa kike ni mama, so hawatakiwi kukatazwa, kwani ni mambo ya kupitia na baadae wataacha.
Pia kuna umri fulani watoto huwa wanajisaidia haja kubwa au ndogo pasipo kujielewa. Mzazi hautakiwi kumpiga na kumtisha mtoto, kwasababu hiyo ni hali kutokana na kutokomaa kwa mfumo wake wa fahamu, pindi mzazi utapokuwa unampiga na kumtishia ili aache hiyo tabia ni kweli ataacha ila yaweza kuwa ikamuathiri ukubwani.
Si kweli...kitovu hicho kikiangukia kwenye sehemu za siri za mtoto wa kiume (uume) si kweli kwamba mtoto huyo hatasimamisha uume wake katu. Hii ni moja ya mila tu na stori za tangu zamani ambazo zimesaidia sana wamama wengi kuwa waangalifu kwenye kutunza kitovu cha mtoto, na hii imesaidia sana kupunguza maambukizi ya kitovu ambayo ni sababu kuubwa ya kusababisha cord sepsis na septicaemia, magonjwa ambayo yanaongoza kwa kuua vichanga.
Nashkuru sana kwa uvumi au imani hii kwani maisha ya watoto wengi sana yanalindwa simply kwa akina mama kuwa waangalifu kwa vitovu vya watoto. Nimeona hata kina mama wasomi kabisa na Masters na PhD zao japo hawaamini lakini they don't take any chances kitovu kuangukia uumeni mwa watoto wao, na hapo ndio matunzo mazuri ya kitovu yanapoanzia!
Bravo aliyeanzisha imani hii..
NB: Sikufanya research rasmi, lakini kwa observation tu wakati nipo Idara ya vitoto vichanga Muhimbili (Neonatal Unit), vitoto vingi vilivyokuwa na cord sepsis vilikuwa vya kike...inawezekana sababu ni kina mama wako makini na vitovu vya watoto wa kiume zaidi ya watoto wa kike (not published).
Kwa kuanzia....Imani hii si ya kweli, japo nachelea kuiita potofu (Kiswahili kigumu sometimes). Siiti potofu kwa sababu haina hasara kwa mtoto, bali ina faida!
Dhana hii ilianza zamani za mabibi zetu walipogundua kuwa kama hutunzi vyema kitovu cha mtoto mchanga basi mtoto huyo ataugua na kufariki. Na hilo ni kweli, kwani mtoto atapata 'umbilical infection/sepsis' na kama hatapata matibabu ya haraka na stahiki atafariki kwa 'septicaemia'.
Kwa hiyo imani hiyo ilitungwa ili wamama wawe makini kuchunga kitovu kisiangukie uume mtoto akawa h*nithi, wakati huo huo mama atachunga kitovu kisipate maambukizi. Hivyo japo si kweli kwamba mtoto akiangukiwa kitovu anakuwa h*nithi, lakini uongo huo una faida kwa mtoto kuangaliwa vyema kitovu chake.