Uhamiaji YAZINDUKA: Jandu Singh na wenzake 18 kupanda kizimbani!

Hao ni wa Dar vipi pale Makao Makuu kwao Arusha maana wamefungiwa mule karakana hawatoki;Nahao vigogo mbona hawatajwi jameni au umekua msemo sasa vigogovigoo,Naanza nahuyu SHAYO,Wengine nii!
 
Wakuu Mkienda pale Blue Pearl Hotel ubungo
Ndio mtashangaa wapo wahindi zaidi ya 11 ambao wanafanya kazi wanalala hapohapo hotelini hawana vibali vya kuishi nchini
achilia mbali kufanya kazi. tumepeleka taarifa mara kibao uhamiaji hakuna hatua. Ukienda pale diamond motors hivyo hivyo.

Hawa wa blue pearl wako active usiku zaid kuliko mchana. Ukitaka info zaidi wasiliana na wafanya kazi wa pale. napendekeza kama
kweli uhamiaji wanataka kumaliza huu uozo wa wageni wasio na sifa za kufanya kazi nchini tupo tayari kushirikiana nao kuwapatia majina, simu number zao, wanaishi wapi wanafanya kazi saa ngapi ili wawakamate.

Mtanzania asilia.
Halafu sijui kama bado ipo,ila polisi pia kuna wakati walikuwa wanakamata watu hovo hovyo tu,eti mzururaji,na ukweli hizo kazi hazipo,basi tu unyanyasaji,halafu pia inajulikana kabisa kuingia polisi ni bure,lakini kutoka ni pesa,sasa sijui wanategemea mzururraji atoe wapi hiyo pesa?

Yani wana assume kuwa kazi zipo ila watu hawataki kufanya.Na ukweli viongozi hawafanyi kazi kwa maslahi ya wananchi na ndiyo maana haya yanatokea!

Kipindi cha nyuma nakumbuka kabisa ukitembea tu hata mjini lazimi uwatch your back la sivyo karandinga la poisi litakupitia na zoa zoa yao.

Na mara nyingi weekend kama kuanzia ijumaa ndiyo wanakusanya pesa zaidi kwasababu wanatumwa tu kwenda kukusanya raia,na hakuna raia hata mmoja kati ya watakaokusanywa atatoka bure bila kuonga,akishindwa atapewa kesi atapandishwa mahakamani kwa kesi za wengine,na mdhamana huwezi kutoka hadi jumatatu,labda uonge.Na usipoonga ni hadi jumatatu.Na hapo hata kosa huna!

Bongo hakuna uhuru kabisa ni wakoloni weusi wako madarakani.
 
Safi sana

Topical,,hii ndo inayotia kichefuchefu hadi unaona watu wanaisema sana serikali ya ccm. Yaani Idara husika kufanya kazi yake na kudeliver ni mpaka wasukumwe/watishwe na ma boss. sasa unajiuliza kama sio Nahodha kukaripia isingetokea hii! Thats pity!
 
Hii ni human trafficking ambayo ni kinyume cha haki za binadamu. Zile NGO zinazofuatilia ukikukwaji wa haki za binadamu szisielekeze nguvu na macho yao serikalini tu inabidi zimulike waajiri wote wa umma na binafsi kwani ndiko uozo ulipokuwa sugu. Tumegumdua wahnidi lakini raia wa nchi nyingi tu kama Somalia, Ethiopia,Eritrea hat majirani zetu wa EAC pia!
Nina uhakika wakiweka informers kila kampuni zinazotiliwa shaka watawabana kirahisi..... Njia ya kumtambua mbwamwitu aliyevaa ngozi wa kondoo ni kumchekesha.... Hakika utaona meno yake si ya kondoo!!! Bravo!!! lakini haitoshi..Uhamiaji safisheni hiii takataka na dhuluma kwa binadamu!!!
 
Mwanzo mzuri tuwape nafasi wafanye maamuzi, tusiwabeze, lazima pawe pa kuanzia
 
Bado Wakenya na Wasomali, Hawa uhamiaji wanatakiwa kuzinga Madukani, maofisini, Viwandani hata majumbani kuwakama wahamiaji haramu hapa nchi sio kulalala huko Ofisini.
 
jandu_phixr-245x250.png

Jandu Singh

Katika kile kinachoaminika kuwa ni utekelezaji wa agizo la Waziri wa Mambo ya Ndani Bw. Shamsi Vuai Nahonda la kuwataka maafisa uhamiaji kuonesha ndani ya wiki tatu wamefanya nini kudhibiti uhamiaji haramu mmiliki wa kampuni ya Jandu Construction & Plumbing, Indertit Sigh Jandu, amekamatwa na Uhamiaji kwa tuhuma za kuwahifadhi na kuwatumikisha wahamiaji haramu 18.

Jandu ambaye ameshiriki kujenga jengo la Uhamiaji Kurasini, alionyesha jeuri akidai kuwa na mahusiano na vigogo Uhamiaji, serikalini na wanasiasa lakini sasa yuko mahabusu. Walikamatiwa eneo la kampuni hiyo Buguruni Dar es Salaam Jumatatu usiku. Kumi na saba (17) ni raia wa India na mmoja wa Pakistan.

Jandu aliamua kutafuta njia ya kuzima sakata hilo kwa ‘wakubwa' kwa kwenda makao makuu ya Uhamiaji lakini akakwaa kisiki.

Wafanyabiashara wenye asili ya Kiasia wamekua wakifanya biashara ya watu kwa kuingiza wahamiaji wengi na kuwatumikisha katika kampuni zao, baadhi wakiwa katika maandalizi ya kwenda kufanya kazi Afrika Kusini

HABARI ZAIDI HAPA

Tatizo ni kuwa hawa ni wachangiaji wakubwa wa CCM kwa njia moja ama nyingine. Wengi wa hawa hupewa kazi za serikali kwa masharti ya kurudisha percentage fulani mifukoni mwa viongozi, wanajua fika kuwa viongozi wetu ni chaka la rushwa na uhalifu na ndiyo maana wana kiburi cha ku-bypass front liners na kwenda kwa vigogo.

Tatizo si Jandu bali ni corrupt system tuliyopo. Usije shangaa aliyemtia mbaroni aka hamishiwa Tandahimba kikazi, sooner or later.
 
Asante Mzee Mwanakijiji kwa hili.
Pamoja na hili naomba ifike wakati sisi Watanzania wenyewe tujitathmini utendaji wetu wa kazi.

Tangu enzi za ujenzi wa reli ya kati, leba force ilitoka India na ndio wakapata fedha wakajenga hayo maghorofa uhindini.

Ukienda hoteli nyingi za kitalii, leba force kubwa ni Wakenya kwa hoja kuwa Watanzania ni wavivu, na wanaongoza kwa absentisim kwa visingizio kibao.

Naunga mkono hoja zozote za empowerment kwa Watanzania ila pia naunga mkono let foreign labor force itake place for doing dirty jobs Watanzania hawawezi kuzifanya.

Maeneo ninakoishi mimi, asilimia 80% ya mashamba boy ni Wamalawi. Wakowapi hao mashamba boy wa Kitanzania?.

Angalieni makampuni ya ujenzi na gereji za Wachina. Kazi ni usiku na mchana, hakuna Jumapili wala sikukuu. Nyumba ya kuishi unakabidhiwa within one month. Ukipeleka gari almost write off, inakuwa restored within a week!. Jee Watanzania tunaweza au kazi kulalamika.

Juzi nimepita pale Doha, kuanzia wahudumu wa vyooni mpaka wahudumu hotelini wote ni Wahindi. Zamani dada zetu angalau walitamba japo kwa kale kabiashara, sasa wachina, wafilipino na warusi wamewapiku!. Watanzania tunaweza nini zaidi ya majungu na kulalamika kwa sana!.

Kwa wapitaji wa Bagamoyo Rd, yale Maghorofa marefu karibu yote ni ya wawekezaji wa Kisomali hebu tembeleeni vitegauchumi vyao, wafanyakazi wote mpaka wafagiaji ni Wasomali, Kiswahili hawajui, Kiingereza hawajui ila utahudumiwa kila utakacho kwa sign language!. Watanzania tuko wapi?.

Shoprite walipokuja walifingua masuper market lukuki, JM Mall, My Fair Plaza, Lumumba, etc, waliajiri wabongo, wamewaibia mpaka maduka yamefilisika sasa yamefungwa!. Mtu akileta Wahindi kwa sababu ni waaminifu ni makosa?,
 
Anatoka kesho huyo..hakuna legal system ya kueleweka., pesa ndo kila kitu...yule jamaa aliyeuwawa kigamboni kesi yake waliimaliza juu kwa ju.
 
Huyo Jhandu ni cha mtoto,Manji,Mohamed Dewji,yule jamaa wa Estim construction pamoja na kiwanda cha chuma pale mwenge wamejaza Indian immigrants kwenye makampuni yao na wengine wamejengewa apartments ndani ya viwanda vyao na wanaishi kwenye magodown.Hawa wote wanauhusiano wa kibiashara na viongozi wetu ikiwemo familia ya Rais Jakaya Kikwete na kiwanda cha Sayona.
 
hao uhamiaji wanafanya kazi kwa kusukumwa...hakuna lolote kabisa...baada ya mda watakaa kimya
 
Asante Mzee Mwanakijiji kwa hili.
Pamoja na hili naomba ifike wakati sisi Watanzania wenyewe tujitathmini utendaji wetu wa kazi.

Tangu enzi za ujenzi wa reli ya kati, leba force ilitoka India na ndio wakapata fedha wakajenga hayo maghorofa uhindini.

Ukienda hoteli nyingi za kitalii, leba force kubwa ni Wakenya kwa hoja kuwa Watanzania ni wavivu, na wanaongoza kwa absentisim kwa visingizio kibao.

Naunga mkono hoja zozote za empowerment kwa Watanzania ila pia naunga mkono let foreign labor force itake place for doing dirty jobs Watanzania hawawezi kuzifanya.

Maeneo ninakoishi mimi, asilimia 80% ya mashamba boy ni Wamalawi. Wakowapi hao mashamba boy wa Kitanzania?.

Angalieni makampuni ya ujenzi na gereji za Wachina. Kazi ni usiku na mchana, hakuna Jumapili wala sikukuu. Nyumba ya kuishi unakabidhiwa within one month. Ukipeleka gari almost write off, inakuwa restored within a week!. Jee Watanzania tunaweza au kazi kulalamika.

Juzi nimepita pale Doha, kuanzia wahudumu wa vyooni mpaka wahudumu hotelini wote ni Wahindi. Zamani dada zetu angalau walitamba japo kwa kale kabiashara, sasa wachina, wafilipino na warusi wamewapiku!. Watanzania tunaweza nini zaidi ya majungu na kulalamika kwa sana!.

Kwa wapitaji wa Bagamoyo Rd, yale Maghorofa marefu karibu yote ni ya wawekezaji wa Kisomali hebu tembeleeni vitegauchumi vyao, wafanyakazi wote mpaka wafagiaji ni Wasomali, Kiswahili hawajui, Kiingereza hawajui ila utahudumiwa kila utakacho kwa sign language!. Watanzania tuko wapi?.

Shoprite walipokuja walifingua masuper market lukuki, JM Mall, My Fair Plaza, Lumumba, etc, waliajiri wabongo, wamewaibia mpaka maduka yamefilisika sasa yamefungwa!. Mtu akileta Wahindi kwa sababu ni waaminifu ni makosa?,
Mkuu hakuna uvivu ni namna organisation behaviour inavyojengwa!! Tuadhibiwe kwa kutoku perform na si kwa kukosa nafasi sababu ya wageni! Hatuwezi kujiadhibu na kugeuza nchi shamba la bibi kisa eti sisi wavivu! Tuna matatizo yaliyochangiwa na historia na utamaduni wetu lakini haya hayatufanyi vilema!! Hii ni nchi yetu mgeni yeyote lazima afate sheria zetu.hatuwezi kuwafundisha watu wetu kwa njia hii pasco! Lakini pia kujituma kwa hawa wageni si bure,ukifuatilia walikotoka,namna walivyopenya nchini na masharti wanayopewa na hao wanaowaleta ingekuwa hata watz wangekuwa hivyo! Hawatuzidi ubinadamu wowote!! Tuna madhaifu yetu lakini pia tuna nchi yetu na sheria zetu Pasco!!
 
Wakuu hiyo ni cha mtoto, Subash Patel mbona anawafuga wengi tu! Nendeni kiwanda cha mm steel pale karibu na itv kile cha kutengeneza nondo, mbona wako wa kumwaga na ni marufuku kutoka nje. Kuna wahindi na wapikistani wengi wanafugwa kama wafanyakazi ndani ya kiwanda cha nondo.
 
Kumkamata Jandu pekee haitosaidia. Lazma uhamiaji nao wahusike ktk hilo.
 
jandu_phixr-245x250.png

Jandu Singh

Katika kile kinachoaminika kuwa ni utekelezaji wa agizo la Waziri wa Mambo ya Ndani Bw. Shamsi Vuai Nahonda la kuwataka maafisa uhamiaji kuonesha ndani ya wiki tatu wamefanya nini kudhibiti uhamiaji haramu mmiliki wa kampuni ya Jandu Construction & Plumbing, Indertit Sigh Jandu, amekamatwa na Uhamiaji kwa tuhuma za kuwahifadhi na kuwatumikisha wahamiaji haramu 18.

Jandu ambaye ameshiriki kujenga jengo la Uhamiaji Kurasini, alionyesha jeuri akidai kuwa na mahusiano na vigogo Uhamiaji, serikalini na wanasiasa lakini sasa yuko mahabusu. Walikamatiwa eneo la kampuni hiyo Buguruni Dar es Salaam Jumatatu usiku. Kumi na saba (17) ni raia wa India na mmoja wa Pakistan.

Jandu aliamua kutafuta njia ya kuzima sakata hilo kwa ‘wakubwa’ kwa kwenda makao makuu ya Uhamiaji lakini akakwaa kisiki.

Wafanyabiashara wenye asili ya Kiasia wamekua wakifanya biashara ya watu kwa kuingiza wahamiaji wengi na kuwatumikisha katika kampuni zao, baadhi wakiwa katika maandalizi ya kwenda kufanya kazi Afrika Kusini

HABARI ZAIDI HAPA

Wanamshughulikia alikataa kuchangia kampeni za CCM
 
Sijaelewa amewaingiza vipi, kawabeba kwenye contena la vifaa vya ujenzi?
 
Oktoba 22 nikiwa kwenye basi ya kampuni ya Ng'tu inayofanya safari Dar-Mtwara wahindi zaidi ya 10 walipanda ndani ya basi umbali kama 15km hivi kutoka jijini Dar tena ktk eneo ambalo halina makaazi ya watu (porini) wakitokea ndani ya basi dogo lililokuwa limeegeshwa kando ya barabara likiwa na vioo visivyoonyesha. Wahindi wale walishuka umbali wa kama 10km kabla ya kufika Mikindani na hapo gari dogo aina ya Nissan Safari nayo ikiwa na vioo vya giza ilikuwa ikiwasubiri. Kulikuwa na kila dalili ya wafanyakazi wa basi ile kufahamu kila kitu kuhusu mpango huo. Kwa bahati mbaya sikufanikiwa kukariri nambari za gari zile zilizohusika. Maswali ni mengi bila majibu... Mtandao ni mrefu na dhamira ya kuutokomeza ni fupi.
 
Kuna siku nilikuwa airport ya Dar es salaam ndani kabisa kule nikisubiria wageni wangu ambao nao ratiba zao za kufika zilikuwa hazieleweki nikajikuta nakaa asubuhi mpaka jioni. Hapo ndo nikaona ni jinsi gani watu wa uhamiaji wanavyofanya shughuli zao pale bila utaratibu maalum. Ilikuja Qatar Airways watu kibao wameshuka including wahindi kama 15 hivi au 20. wahindi wasioukuwa na mbele wala nyuma hawaeleweki na wenyewe pia hawajielewi. wakaunga mstari kama wageni wengine lakini ikaonekana kuwa hawakuwa na viza ya kuingia nchini. lakini wao wakawa wanadai kuwa kuna mtu anawasubiri nje na mkononi wameshika some sort of a letter kuwa wanakuja kufanya kazi kwenye kampuni ya ujenzi ilikuwa morogoro nadhani....that was the only proof they had they didnt even have contacts of whoever would meet them at the arrivals gate. Lugha haipandi wala nini basi ikawa tabu tupu. na hawana hela ya aina yoyote just a few rupees.

Wakakaaa pale kwenye mabenchi kwa muda mrefu sana....walikaaa kweli kweli mpaka jioni saa 12 ndo wakawaachia. sasa hii inaonyesha kabisa kwamba kuna tatizo kuanzia mwanzoni kabisa. kwa sababu watu kama hawa ambao hawana kibali chochote cha kuingia ndani ya nchi wangepaswa warudishwe walikotokea. kwa sababu hata uhamiaji wenyewe hawakuwa na any prior info kuwa there will be a group of this people coming from this country(s) etc etc etc....

Lakini kwa sababu sisi watanzania suala la kufanya kazi kwa ufanisi na umakini halipo wakaachia na hiyo ni inatokea kila siku. wanaachiwa dola 100 au 20 au 50 siku inapita. wenzetu walioendelea huvuki geti huoni hata nje kunafananaje. ni utarudi on the next available flight whether una hela au hauna.

Its about time uhamiaji should be serious with their work we have enough problems on our plate to start chasing illegal immigrants. Mpaka waziri anawajia juu ndo wanakurupuka ni aibu kubwa.
 
Shoprite walipokuja walifingua masuper market lukuki, JM Mall, My Fair Plaza, Lumumba, etc, waliajiri wabongo, wamewaibia mpaka maduka yamefilisika sasa yamefungwa!. Mtu akileta Wahindi kwa sababu ni waaminifu ni makosa?,
...Pasco, unataka kusema kwamba kufungwa kwa Shoprite pale JM Mall, Lumumba, Mayfair Plaza na Slipway ilitokana na wizi wa waswahili? Mbona maduka ya wahindi mjini ndio yanayoibiwa sana kuliko hata hao. Kumbuka kuwa si kila eneo unalofungua biashara linakuwa na mzunguko wa wateja kutosha kukurudishia mtaji, gharama na kukupatia faida.

...Nadhani issue sio wageni kuja na kufanya kazi nchini, bali, ni wao kutokuwa na vibali halali au kutohitajika kwakuwa kuna watanzania wenye ujuzi huo.

...Pamoja na kwamba kula suala la maadili ya kazi dhaifu, miongoni mwa wafanyakazi wa kitanzania, lazima tufahamu kwamba wageni wanatumika sana kuficha uovu wa waajiri wao. Ukwepaji kodi ni moja ya vitu vikubwa vinavyochangia wageni kuajiriwa maeneo mengi ambayo watanzania wanayamudu. Natumai unayafahamu.
 
Back
Top Bottom