Titus Dickson
Member
- Nov 14, 2016
- 49
- 20
Baada ya huu Uhakiki sijui unafuata upi
Wafanyakazi wa Chuo cha Ufundi Arusha nao wanaomba serikali kuhakiki mali za Mkuu wa chuo. Mkuu wa Chuo cha Ufundi Arusha anatuhumiwa kuwa na utajiri wa mali isiyohamishika ikiwa ni majengo, viwanja na mashamba mali ambayo ni ya gharama kubwa kuliko kipato chake. Inaaminika kwa wafanyakazi kuwa mali alizonazo Mkuu wa chuo alizipata mara tu alipopata nafasi ya kuwa Mkuu wa chuo mwishoni mwa mwezi Septemba, mwaka 2010.
Mkuu wa Chuo amejipatia mali hizo kwa kipindi kifupi kupitia miradi mbalimbali ya ujenzi, fedha za mishahara ya wafanyakazi, makato ya kodi ya nyumba kwa wafanyakazi, akaunti ya chuo inayofahamika kama ATC-PCB, vikao vya Bodi ya chuo, chakula cha wanafunzi, fedha za mafunzo viwandani kwa wanafunzi, fedha ya kununulia vifaa vya kujifunzia pamoja na fedha kwa ajili ya safari anazojitengenezea Mkuu wa Chuo.