Baba Heri
JF-Expert Member
- Jul 23, 2013
- 1,502
- 2,220
Unanunua nondo unaambia ina ukubwa wa inch 16 lakini ukipima hata kwa macho unaona kabisa umepigwa, flat bar ya 3 mm² ni nyembamba kama wembe, ukija kwenye aina zote za chuma ukipima hazifikii ukubwa unaoambiwa, bati ndo usiseme siku hz bati ya 32 gauge inakaribia kuwa laini kama foil wakati kuna nyumba za miaka ya 90 zimepauliwa na bati za 32 gauge hadi leo zipo vizuri, misumari hali kadhalika ni dhaifu vibaya sana. Halafu pia bati unanunua haimalizi mwaka imepauka haitamaniki.
Cha kusikitisha zaidi vifaa vya ujenzi jinsi vinavyopanda bei kila siku ndio vinazidi kuwa hafifu. Gypsum boards au ceiling boards siku hizi zipo kama maboksi. Mbao unanunua unaambiwa ni 3x2" lakini ukipima unakuta ni 2x2" iliyochangamka.
Cement kg 50 zamani ilikuwa kg 50 kweli lakini kwa sasa ule mfuko hata kg 40 sidhani.
Ukirudi kwenye ujazo na ubora wa haya marangi tunayoambiwa sijui silk au weather guard ndo usipime. Nyumba za miaka 40 iliyopita hadi leo zipo na rangi za mafuta hazijafubaa ni kuosha tu lakini hizi za sasa zikimaliza miezi 8 tu zinajikataa.
Najua kuna hoja kwamba watu wanapigwa wanauziwa vitu FEKI lakini je ni jukumu la nani kudhibiti ubora na usahihi wa vipimo? Maana si kila anayeenda kununua material ni muelewa au mzoefu, na ukimuamini fundi akununulie material anakupiga "kipeuo cha pili".
Nasikitika sana ofisi za wakala wa vipimo zipo mikoani, TBS wapo, wataalamu wapo wanalipwa, viongozi wapo lakini UBAYA unatamalaki tu.
Cha kusikitisha zaidi vifaa vya ujenzi jinsi vinavyopanda bei kila siku ndio vinazidi kuwa hafifu. Gypsum boards au ceiling boards siku hizi zipo kama maboksi. Mbao unanunua unaambiwa ni 3x2" lakini ukipima unakuta ni 2x2" iliyochangamka.
Cement kg 50 zamani ilikuwa kg 50 kweli lakini kwa sasa ule mfuko hata kg 40 sidhani.
Ukirudi kwenye ujazo na ubora wa haya marangi tunayoambiwa sijui silk au weather guard ndo usipime. Nyumba za miaka 40 iliyopita hadi leo zipo na rangi za mafuta hazijafubaa ni kuosha tu lakini hizi za sasa zikimaliza miezi 8 tu zinajikataa.
Najua kuna hoja kwamba watu wanapigwa wanauziwa vitu FEKI lakini je ni jukumu la nani kudhibiti ubora na usahihi wa vipimo? Maana si kila anayeenda kununua material ni muelewa au mzoefu, na ukimuamini fundi akununulie material anakupiga "kipeuo cha pili".
Nasikitika sana ofisi za wakala wa vipimo zipo mikoani, TBS wapo, wataalamu wapo wanalipwa, viongozi wapo lakini UBAYA unatamalaki tu.