Wiston Mogha
Senior Member
- Feb 13, 2014
- 149
- 96
Pamoja na kwamba viongozi wanaweza kuzaliwa na wengine kutengenezwa bado tuna upungufu mkubwa sana wa viongozi kwenye jamii zetu. Hii inasababishwa na kwamba jamii haitengenezi viongozi na hata viongozi waliofanikiwa katika uongozi wamekuwa wanafki na wenye roho mbaya katika kutenengeneza viongozi wa mfano wao. Hivyo viongozi pekee wanaopatikana ni wale waliozaliwa na sifa za uongozi au wachache waliotengenezwa na mifumo mibovu inayopelekea kupata viongozi mizigo.
Mfumo wa maisha wa jamii nyingi hautengenezi viongozi. Watoto wanakuzwa bila ya kujengewa misingi ambayo inawasaidia kuweza kufanya maamuzi kama viongozi. Jamii nyingi zinalea watoto kwa kuwaepusha wasikutane na changamoto ambazo zinawafanya wafikiri zaidi. Kwa njia hii jamii sio tu kwamba haitengenezi viongozi bali inaua sifa za uongozi kwa baadhi ya watoto waliozaliwa nazo. Kwenye jamii kuna watu wengi sana ambao hawana sifa za uongozi, kwa kuwa watoto wanaiga tabia za wanaowazunguka ni rahisi sana kwao kufanana na wanajamii ambao hawana sifa za uongozi.
Kitu kingine kikubwa kinachoua uongozi ni mfumo wa elimu. Mfumo wa elimu hasa kwa nchi yetu Tanzania haujakaa kutengeneza viongozi. Kwanzia darasa la kwanza mpaka elimu ya chuo mtoto anafundishwa kukazania vitu vichache ili kufaulu masomo. Hapewi nafasi ya kufikiri tofauti na kuibua na kupambana na changamoto. Pia mfumo wa elimu unajenga watu kuwa na UBINAFSI na kufikiria maisha yao tu badala ya kufikiri na ya wale wanaomzunguka. Kwa njia hii mfumo wa elimu unashindwa kutengeneza viongozi na inaua sifa za uongozi kwa baadhi ya wenye nazo.
Mfumo wa maisha wa jamii nyingi hautengenezi viongozi. Watoto wanakuzwa bila ya kujengewa misingi ambayo inawasaidia kuweza kufanya maamuzi kama viongozi. Jamii nyingi zinalea watoto kwa kuwaepusha wasikutane na changamoto ambazo zinawafanya wafikiri zaidi. Kwa njia hii jamii sio tu kwamba haitengenezi viongozi bali inaua sifa za uongozi kwa baadhi ya watoto waliozaliwa nazo. Kwenye jamii kuna watu wengi sana ambao hawana sifa za uongozi, kwa kuwa watoto wanaiga tabia za wanaowazunguka ni rahisi sana kwao kufanana na wanajamii ambao hawana sifa za uongozi.
Kitu kingine kikubwa kinachoua uongozi ni mfumo wa elimu. Mfumo wa elimu hasa kwa nchi yetu Tanzania haujakaa kutengeneza viongozi. Kwanzia darasa la kwanza mpaka elimu ya chuo mtoto anafundishwa kukazania vitu vichache ili kufaulu masomo. Hapewi nafasi ya kufikiri tofauti na kuibua na kupambana na changamoto. Pia mfumo wa elimu unajenga watu kuwa na UBINAFSI na kufikiria maisha yao tu badala ya kufikiri na ya wale wanaomzunguka. Kwa njia hii mfumo wa elimu unashindwa kutengeneza viongozi na inaua sifa za uongozi kwa baadhi ya wenye nazo.