NADHARIA Ugonjwa wa UVIKO-19 unadaiwa kurejea kwa kasi nchini

Taarifa hii ni nadharia tu, tumeitolea ufafanuzi kwa kadiri ilivyowezekana
Source #1
View Source #1
Salaam Ndugu zangu,

Zipo tetesi zimesambaa katika maeneno mbalimbali kwamba ugonjwa wa Covid-19 umerejea nchi. Kwa sisi tunaoishi Dar tunashuhudia kulipuka kwa mafua makali yakiambatana na kikohozi fulani na homa.

Je kuna ukweli kiasi gani kwenye hili?

Jamiiforums tunaomba mtusaidie kuuliza kwa mamlaka ili tahadhari ichukuliwe mapema.

1683960668068.png
 
Tunachokijua
Kutokana na kusambaa kwa tetesi ya kuibuka wa wimbi la Uviko-19 ambazo zimechochewa na kuwapo kwa sintofahamu ya Watu kuugua Homa za Mafua Makali, Kifua na Kichwa Serikali kupitia Wizara ya Afya imetoa ufafanuzi wa awali kuhusu madai hayo:

Wizara ya Afya imesema inachakata taarifa zilizokusanywa kutoka Hospitali na Vituo vya Afya ndani ya Wiki hii.

Waziri wa Afya, Ummy Mwalimu amesema kati ya Wagonjwa 288 waliopimwa UVIKO-19 kati ya Mei 6-12, 2023, 6 walithibitishwa kuwa na Corona. Idadi hiyo ni pungufu ikilinganishwa na waliopima kati ya 29 Aprili hadi 5 Mei 2023 na hakuna kifo chochote.

Zaidi ya hayo, Ummy amewataka Wananchi kuondoa hofu kwa kuwa Wizara inaendelea kufuatilia kwa karibu kwenye Hospitali mbalimbali na itatoa taarifa rasmi kuhusu tetesi za Uviko-19.

Kutokana na ufafanuzi huo wa Wizara Jamiiforums itasubiri uchunguzi wa wizara na taarifa kutoka mamlaka husika ili kujua kama hali hii ya mafua, homa na kikohozi ni wimbi la Uviko-19.

Aidha, kutokana na Wizara kuthibitisha kwamba bado kuna wagonjwa wa Uviko-19 nchini japo kwa idadi ndogo ya watu Jamiiforums inashauri wanajamii tuendelee kuchukua tahadhari wakati wote.
Ina maana kila mafua makali na homa ni COVID??

Kabla COVID19 haijaingia hakukuwaga na mlipuko wa Mafua makali na homa?
 
Kwani ilikwenda wapi ?

Ilikuwepo na itaendelea kuwepo ni kwamba either tume-adapt na kama kuna mlipuko usioeleweka basi ni kwamba na yenyewe strain imebadilika hivyo ni mwendo ule ule tu, maisha yako yote (lishe bora, na kuishi kwa afya) sio mpaka kuambiwa, sababu hata kama sio hili au lile kuna jingine litakuja tu.....; Kwahio ni muhimu likija likukute ngangali....

Healthy living ndio mpango mzima
 
Acheni uzushi, sisi tuliokulia maisha ya kawaida mtaani tunajua huwa kuna homa kali na mafua makali kipindi cha kati ya mwezi Machi na May na hii inasababishwa na kubadilika kwa hali ya hewa kutoka jua kali la February kuingia masika ya mwezi March, na homa hizi husababishwa na
1. Mazalia mengi ya mbu kunakosababisha malaria
2. Kifua kubana kinachosababishwa na baridi na unyevu mwingi kutokana na mvua lakini pia
3. Mafua makali huwa kutokana na baridi na unyevu mwingi hewani.
4. Pia homa hizi huchagizwa na mchafuko wa maji unaosababisha magonjwa ya tumbo (typhoid).

Kwa watu waliokulia maisha ya vijijini hali hii huwa hawaishangai kwa sababu hutokea kila mwaka, ila kuku wa kisasa hawawezi kuelewa haya.

Maisha ni kuishi kwa experience na ndicho jamii imetufunza, nyinyi kuku wa siku 28 endeleeni kulalamika kwa serikali maana mmezoea kukaririshwa kila kitu.
 
Sipendagi watu mnaopenda kuzudha taharuki?! Sasa COVID 19 ilikuwapo miaka ya nyuma mbona tulikuwa tunapata hali za hivi hivi?!
 
Hata tangu jana nilibanwa mno na mafua makali sana. leo kidogo nimeamka na nafuu kidogo.
 
Tuambieni mapema tuitume Bombardia yetu ikatuchukulie tena dawa kule Madagascar. cc. Mzee wa Jalalani
 
Atakayebisha kuhusu watu kuumwa abishe tu lakini binafsi nimeumwa two weeks ago, vichomi kwenye mbavu, fever kali na shortness of breath. Pia hapa napoandika Nipo hospital Nina ndugu yupo kwenye oxygen siku ya 6 sasa! X-ray inaonyesha ana pneumonia kali.
 
Salaam Ndugu zangu,

Zipo tetesi zimesambaa katika maeneno mbalimbali kwamba ugonjwa wa Covid-19 umerejea nchi. Kwa sisi tunaoishi Dar tunashuhudia kulipuka kwa mafua makali yakiambatana na kikohozi fulani na homa.

Je kuna ukweli kiasi gani kwenye hili?

Jamiiforums tunaomba mtusaidie kuuliza kwa mamlaka ili tahadhari ichukuliwe mapema.

Juzi nilienda Agakhan nikakuta madaktari na wafanyakazi wengi pale hospital wamevaa barakoa, nikamuuliza daktari wangu what is happening akachomoa barakoa akanigea hakujibu kitu na mimi nikavaa

Tangu jana naona hizi tetesi ndio napata jibu kwamba hizi tetesi yawezekana zina ukweli
 
Covid IPO wakuu Tena sirias kabisaa. Ukitaka kujua kweli wewe nenda hospitali yoyote ya wilaya kakae TB clinic mwambie clinician X-ray zenye CoVid akupe
 
2 Reactions
Reply
Back
Top Bottom