Ugonjwa wa Selimundu (Sickle Cell anaemia): Dalili na matibabu yake

JamiiForums

JF Official Account
Nov 9, 2006
6,200
4,991
4F40DCD2-34AA-4CFA-8D46-A857439FFC92.jpeg


Watu walio na hali hii huwa wana upungufu wa chembechembe nyekundu kwenye damu mwilini. Hivi ni kumaanisha kuwa miili yao huwa haibebi hewa ya kutosha ya oksigeni. Hali hii inaweza kuwafanya wawe wagonjwa.

Kuna kitu chekundu katika damu kinachotwaa oksigeni katika hwa na kuipeleka kila mahali mwilini. Huwa kemikali ndani ya chembechembe zilizo asili ya kila kitu chenye uhai, kisipoumbika vizuri na kikose kupita ndani ya mishipa ya damu, mishipa inaweza kuziba na kusababisha maumivu makali.

Sickle Cell ni hali inayorithiwa. Mtu huipata kutoka kwa wazazi wake. Kila mtu hupata nusu ya jeni (genes) zake kutoka kwa mzazi wa kiume nusu na kutoka kwa mzazi wa kike. Iwapo wazazi wote (baba na mama) wana jeni ya Sickle Cell, wanaweza kupata mtoto aliye na ugonjwa huu hata kama wao wenyewe hawana.

Sickle Cell hali hii hupatikana sana sana kwa watu wanaotoka sehemu za Afrika ya Kati na Magharibi.

Watu walio hatarini zaidi ya kupata ugonjwa wa Anemia ya Sickle Cell

Wengi walio na hali hii katika damu yao hutoka sehemu za Afrika ya Kati, Amerika ya Kusini na Kati, India ya Kati na nchi za Mediterania kama vile Uhispania, Uturuki, Ugiriki na Italiano.

Kutambua iwapo una ugonjwa huu

Mtu yeyote anaweza kuenda kuangaliwa na daktari kuchunguza iwapo ana ugonjwa huu. Iwapo wewe na mpenzi wako mnapanga kuoana na kuwa wazazi, ni lazima ufanyiwe uchunguzi hasa iwapo mnatoka sehemu ya Afrika ya Kati au mna wazazi wanaotoka kwenye sehemu ambako ugonjwa huu upo. Daktari wako anaweza kukufanyia uchunguzi au akutume kwa daktari mwingine aliye na ujuzi wa kukagua tabia zinazorithiwa za kifamilia.

Iwapo mna mtoto ni muhimu afanyiwe uchunguzi iwapo ana ugonjwa huu au upo ndani ya uzao wake. Ni muhimu kutambua mtoto wako anapoendelea kukua iwapo ana huu ugonjwa.

Muone daktari mara moja kama utaona dalili zifuatazo:
  • Homa
  • Maumivu ya kifua
  • Kupumua haraka haraka
  • Uchovu
  • Kuvimba kwa tumbo au sehemu za chini yake
  • Kupoteza nguvu mara moja na kukosa hisi
  • Maumivu ambayo hayataisha hata baada ya kupewa dawa za kupunguza uchungu pale nyumbani
  • Kuhisi kujamiana ambako ni kuchungu mno na hakuwachi
  • Mabadiliko ya kighafla katika namna unavyoona vitu
=========
ZAIDI:

UGONJWA wa selimundu(sikoseli) ni ugonjwa wa kurithi ambao chimbuko lake ni familia kuwa na mtu anayekuwa na ugonjwa husika.

Ugonjwa huo unaambatana na dalili nyingi zinazotokana na kuvunjika kwa seli na kukwama kwenye mishipa ya damu kutokana na umbile lake.

Mgonjwa asipopata matibabu ya haraka na uangalizi wa karibu wa wahudumu wa afya na walezi wa wagonjwa hawa dalili hizi huchangia kwa kiasi kikubwa kwa waathirika wa ugonjwa huu kulazwa hospitali mara kwa mara na vifo vya utotoni.

Athari za ugonjwa wa sikoseli

Maumivu


Chembe nyekundu za selimundu hushindwa kupitika kwa urahisi katika mishipa midogo ya damu na hivyo kukwama na kuziba mzunguko wa damu. Hali hii husababisha maumivu yenye ukali tofauti.

Maambukizi ya vimelea vya magonjwa:

Wagonjwa wa sikoseli hasa watoto hupata maambukizi ya vimelea vya magonjwa mbalimbali kama vichomi (pneumonia), homa ya uti wa mgongo na homa ya ini.

Upungufu wa damu

Kutokana na chembe nyekundu za sikoseli kuwa na muda mfupi wa kuishi hii humuweka mgonjwa wa sikoseli katika hatari ya kupata upungufu mkubwa wa damu.

Kuvimba kwa mikono na miguu:

Mara nyingi huambatana na homa hali hii husababishwa na chembe nyekundu za sikoseli kukwama na kuziba mzunguko wa damu kwenda kwenye mikono na miguu.
 
Matibabu na njia za kukuwezesha kuishi na afya

Ugonjwa huu hautibiki. Lakini madaktari wanaweza kutibu dalili ndogondogo hata zile kubwa. Iwapo una huu ugonjwa na unahisi maumivu makali, madaktari watakupa dawa za kuzuia maumivu na vinywaji vingi.

Kuwekwa damu ingine kila mara kunasaidia kukabiliana na upungufu wa damu mwilini (Ni muhimu upewe damu nzuri)

Hapa kuna namna ambavyo unaweza kuishi ukiwa na afya nzuri.
  • Kila siku meza dawa ya asidi ya vitamini C (folate) ili ujenge upya chembechembe nyekundu zilizo asii ya kila kitu chenye uhai
  • Meza dawa za penisilini iliyoandikiwa kila siku mpaka utakapotimua miaka sita ili uzuie maambukizi
  • Kunywa maji mengi kila siku (kati ya glasi 8 – 10 kila siku kwa watu wazima)
  • Jiepushe kukaa mahali ambapo ni baridi sana au pana joto jingi sana
  • Jaribu usifadhaike au kuchosha sana mwili wako
  • Pumzika vya kutosha
  • Tazamwa inavyostahili kila mara na daktari anayejua sana kuhusu ugonjwa huu
 
Hellow guys,can you please tell me the diagnostic tests of sickle cells,
thank u!
 
Sickle cell haina dawa ila kuna dawa zinazotumika kupunguza makali ya ugonjwa - kwa ushauri zaidi nenda Muhimbili kuna Clinic maalum kwa ajili ya Sicklers. Nakutakia mafanikio mema.
 
docta na wana jf nadhan hamjambo!me sina ufaham na huu ugonjwa wa cycocell,naomba kufahamishwa nini chanzo chake!na unadalili zipi na matibabu kama yapo..
 
docta na wana jf nadhan hamjambo!me sina ufaham na huu ugonjwa wa cycocell,naomba kufahamishwa nini chanzo chake!na unadalili zipi na matibabu kama yapo..

sicle cell ni disorder ya redblood cells ambapo cell inakuwa na shape isiyo ya kawaida ina kuwa kama mwezi mchanga na rigid, inakua vigumu kupita kwenye blood vessel matokeo yake kufanya damu isipite kwa urahisi au kuzuia kabisa,matokeo yake ni kusababisha upungufu mkubwa wa damu sehemu zingine za mwili(anaemia) ambayo huitwa sicle cell anaemia.kawaida cells ni round na ni flexible.

Tabia nyingine ya sicle cell ni kufa mapema zaidi kuliko cell zingine kabla ya kuwa replaced,cell hizi hufa baada ya siku 10-20 na kusababisha anaemia,wakati cell za kawaida huchukua siku 120 ndipo hufa.

Sicle cell ni disorder ambayo mara nyingi ni ya kurithi toka kwa wazazi,hali hii husababishwa na mabadiliko yasiyo ya kawaida yanayotokea kwenye DNA,ambayo ndiyo huhusika na utengenezaji wa vinasaba(gene).DNA ni master plan ya cell so makosa yanapofanyika katika master plan hii husababisha magonjwa au disorder mbalimbali mwilini mfano sicle cell nk.s.cell huanza kujitokeza mtoto awapo kuanzia miezi 4 na kuendelea.

Dalili zinazojitokeza ni.
1.Kupugukiwa damu(anaemia).
2.Maumivu kwenye mifupa.
3.kuugua mara kwa mara.
4.kuvimba miguu kutokana na upungufu wa damu.
5.kushindwa kuona vizuri baadaye kadri ugonjwa unavyozidi.
6.kuchelewa kukua mtoto nk.

Matibabu:
Hakuna tba yake ila ni kutibu dalili zinazojitokeza.
 
Nitakuja badae ku-comment complications mbalimbali za sickle cell disease na tiba zake.
Kwa sasa mda umebana.
Kazi kwanza.
 
sicle cell ni disorder ya redblood cells ambapo cell inakuwa na shape isiyo ya kawaida ina kuwa kama mwezi mchanga na rigid, inakua vigumu kupita kwenye blood vessel matokeo yake kufanya damu isipite kwa urahisi au kuzuia kabisa,matokeo yake ni kusababisha upungufu mkubwa wa damu sehemu zingine za mwili(anaemia) ambayo huitwa sicle cell anaemia.kawaida cells ni round na ni flexible.

Tabia nyingine ya sicle cell ni kufa mapema zaidi kuliko cell zingine kabla ya kuwa replaced,cell hizi hufa baada ya siku 10-20 na kusababisha anaemia,wakati cell za kawaida huchukua siku 120 ndipo hufa.

Sicle cell ni disorder ambayo mara nyingi ni ya kurithi toka kwa wazazi,hali hii husababishwa na mabadiliko yasiyo ya kawaida yanayotokea kwenye DNA,ambayo ndiyo huhusika na utengenezaji wa vinasaba(gene).DNA ni master plan ya cell so makosa yanapofanyika katika master plan hii husababisha magonjwa au disorder mbalimbali mwilini mfano sicle cell nk.s.cell huanza kujitokeza mtoto awapo kuanzia miezi 4 na kuendelea.

Dalili zinazojitokeza ni.
1.Kupugukiwa damu(anaemia).
2.Maumivu kwenye mifupa.
3.kuugua mara kwa mara.
4.kuvimba miguu kutokana na upungufu wa damu.
5.kushindwa kuona vizuri baadaye kadri ugonjwa unavyozidi.
6.kuchelewa kukua mtoto nk.

Matibabu:
Hakuna tba yake ila ni kutibu dalili zinazojitokeza.

Asante sana kwa ufafanuzi mzuri maana kweli nilikuwa shalow hata spelling nimevuruga aha ha ha ha ha ha asante sana..
 
Sickle Cell Disease
Kama alivosema ngwana ongwa...
Ni tatizo la chembe hai (seli) nyekundu za damu ambazo ndo huhusika na kusafirisha hewa ya Oxygen mwilini.
Hizi seli zilizoathirika zina-assume shape ya MUNDU (=sickle) hence the name of disease.
Norma red cells ni mviringo bapa.
Hebu cheki picha hii itawasaidia kucatch-up.
sickle-cell-cell.jpg
 
Back
Top Bottom