Ugonjwa wa Ngiri (Hernia), Dalili na tiba yake

Polisi

JF-Expert Member
Nov 22, 2010
2,082
639
Wakuu,

Habari ya kazi. Nilikuwa Bugando kwa ajili ya kufanyiwa kipimo kinachoitwa endoscopy. Matokeo yalikuwa kama ifuatavyo

Esophagus – MILD DISTAL OESOPHAGISI 2”/HIATAL HERNIA
Stomach - HIATAL HERNIA
Duodenum – NORMAL
Final Diagnosis - GERD 2” HIATAL HERNIA

Sasa WIKI IJAYO nakwenda kuonana na daktari bingwa nimpe majibu haya. Kama mjuavyo watu ni wengi na hivyo kupata muda wa kujieleza na kudodosa vizuri kwa daktari inakuwa ni ngumu. Ndiyo maana nikaona ni bora nianzie hapa nipate mawili matatu mfano:

- Kwa matokeo haya ya vipimo nitegemee nini kutoka kwa daktari
- Baada ya kupitia humu jf nikagundua hiatal hernia ni ngiri, je inaweza pia kusababisha haya maumivu ya MIGUU na MIKONO?

HALI YANGU KWA SASA
Maumivu sehemu ya juu ya tumbo kama kuna kidonda ambayo yanapelekea maumivu hadi miguuni kwenye nyayo na mikononi. Maumivu yakipungua kifuani na miguu wala mikono haiumi. MAUMIVU PIA HUWA NAHISI MGONGONI

HISTORIA YA TATIZO
Ilianza mwaka 1998 baaada ya kupata stress sana. Ilitokea baada ya kuhisi kuwa msichana niliyetembea naye alikuwa ameathirika baada ya kumkuta amelazwa hospitalini na akadai anaumwa TB. Kwa kweli alikuwa amekonda sana. Kuanzia hapo mauza uza yakaanza kwa kukosa amani na mawazo tele. Mara tumbo, mara kifua mara miguu kuwaka moto nk. Hayo yote yalipelekea mimi kuconclude kwamba nimeathirika na sikutaka hata kujisumbua kupima

Niliishi na hali hiyo kwa miaka karibu 4 yaani hadi katikati ya 2002 ndipo nilipopata ujasiri wa kwenda kupima. Nilianzia CBBRT negative, the same day nikarush ANGAZA negative. Nikamshukuru mungu. Maumivu makali yaliendelea yaani tumbo, kifua, miguu na mikono kuwaka moto n.k. Nikaenda Muhimbili na kufanyiwa kipimo cha BARIUM na kukuta nina ULCERS. Nikaanza masharti ya ulcers na dawa mbalimbali za kitalaam na zile za asili but changes zilikuwa kidogo sana. Nakumbuka nilikuja humu jf na kueleza tatizo langu na mchangiaji mmoja nadhani ni Riwa (sijui kama yupo huyu ndugu, sijamwona siku nyingi) alionesha wasiwasi wake kama kweli ilikuwa bado ULCERS kwa jinsi nilivyotumia dawa mbalimbali

Mwaka 2011 nikarudi tena Muhimbili na kufanyiwa kipimo cha endoscopy na majibu yakawa nina oesophagistis fungus. X ray – normal na HIV negative. Nikapewa dawa awamu ya kwanza nikamaliza na dawa awamu ya pili kama aina nne hivi nikamaliza. Maumivu yakapungua kwa asilimia 50. Daktari mmoja aka-recommend tena nirudie endoscopy kwa kuwa ni HIV negative (Assumption kwamba hizo fungus huwapata walioathirika). Ndiyo maana nikaenda tena hosptali

Ndugu wana JF niko serious na wala ctanii, na naombeni mnipe ushauri utakaonisaidia mwenzenu.
Imetokea kuwa nasumbuliwa na ugonjwa wa ngiri na hapa nilipo nackia maumiv c kawaida. Imepelekea mpaka sehemu 1 ya yai la kushoto kwenye uume ina mishipa yenye uvimbe najihic ni utumbo umezama huko nikishika. Nilienda hsptl doctor akanipa 2 vidonge ambavyo havikunisaidia. NAOMBENI USHAURI KWA ANAEJUA DAWA YAKE NIWEZE KUPONA MANAKE NIMEKATA TAMAA YA KUPONA. Nakaribia mwaka nikiwa na haya maumiv.
Mara nyingi tumekuwa tukisikia watu (hasa wanaume) wakitakiwa kukaa mbali na baridi kuwaepusha wasipatwe na ugonjwa wa ngiri. Hivi kuna uhusiano gani kati ya ugonjwa wa ngiri (hernia) na baridi? Baridi huchangiaje uwepo wa ugonjwa huu?

Nauliza hivi kwa sababu kuna mtoto wangu wa kiume mwenye umri wa miaka 4 amepatwa na ugonjwa huu na ninahisi mara nyingi dada anamuacha anakuwa exposed sana kwenye baridi. Ana maumivu ambayo kuna wakati yanapungua na wakati yanaongezeka na sehemu zake za siri zimesinyaa sana (zinafanana kama za mtoto mchanga).

Kuna baadhi ya watu wananishauri nitafute tiba ya asili na wengine wanasema hakuna kitu kama hicho, wanadai kwamba tiba yake ni operesheni tu. Nipo njia panda. Ushauri wenu ni muhimu sana, wakuu. Natanguliza shukurani.
Kwa anaye fahamu ugonjwa huu wa ngiri atueleze kinaga ubaga maana kuna hali fulani hivi ndugu yangu wa karibu amenielezea eti anasikia maumivu kwa mbali upande wa kushot wa tumbo kwa chini na wakati mwingine tumbo lina jaaa gesi na pia akifanya mapenzi uw anajisikia tumbo lina jaa gesi ni itakua ngiri au nn


=========



Kuna magonjwa ya hernia ya aina nyingi kama zile ziitwazo kitaalamu inguinal, umbilical, femoral, epigastric, incisional, inguinal hernia na diaphragmatic hernia.

Lakini watu wengi hukumbwa na hernia iitwayo inguinal hernia ambayo hutokeza karibu kabisa na sehemu ya siri ambako hapa kimrija kinachochukua mbegu za kiume kutoka kwenye korodani na kuingia kwenye tumbo na kuingia kwenye kiungo cha kiume.

Hapa panaweza kuwa na uwazi na uwazi huo ukaingia utumbo mdogo na kusababisha hernia hii. Aina hii ya hernia kama nilivyosema hapo juu ndiyo inayosumbua sana watu wengi duniani. Kuna aina nyingine ya hernia inayoweza kutokea kwenye kitovu, sehemu ambayo kunakuwa na mshipa unaopitisha damu yenye chakula na hewasafi ya oksijeni kutoka kwa mama kwenda kwa mtoto akiwa tumboni.

Sehemu hiyo mtoto anapozaliwa panaweza pasijifunge vizuri, hivyo mtoto huyo kupata hernia hii baadaye kwani utumbo mdogo huingia katika kijinafasi hicho kisichojifunga vizuri, hivyo kusababisha uvimbe wa hernia hii. Lakini tatizo hili ikiwa mtoto amezaliwa na akaishi zaidi ya miaka miwili bila kujitokeza tena, basi atakuwa salama kwa sababu kwa muda huo sehemu hiyo huwa imejifunga kabisa.

TIBA
Ikitokea sehemu hiyo ikaacha kujifunga kwa kipindi hicho cha miaka miwili, basi daktari huamua kumfanyia upasuaji mtoto huyo. Kwa watu wazima hernia kwenye kitovu ambayo kitaalamu huitwa umbilical hernia inaweza ikatokea kwa akina mama wenye mimba au kwa wale ambao ni wanene kupita kiasi kwani presha kwenye tumbo inakuwa kubwa na kufunga sehemu hii ya kitovu ambayo inawezekana awali ilikuwa wazi.

Hernia nyingine huweza kutokea kwenye kiungo cha njia ya kumezea chakula kinapoungana na tumbo. Kama sehemu hii haikufunga vizuri utumbo unaingia kwenye kinafasi hicho na kujitokeza kwenye kimfuko kilichopo kifuani kinachoitwa kitaalamu diaphragm.

Ndiyo maana hernia hii huitwa diaphragm hernia.
Hernia nyingine iitwayo femoral hernia hutokea pale mishipa ya damu iendayo kwenye mguu inapopita kwenye tumbo na ikiwa kwenye maungio pana nafasi basi hernia hii hutokea kwenye paja karibu na kiunoni.

Kuna hernia ingine inayotokea kwenye chembe ya moyo ambapo misuli inaachia na kusababisha kingozi cha tumbo na utumbo kuingia katika sehemu hiyo hivyo kuvimba na kusababisha hernia.

Tiba za uhakika za hernia ni kufanyiwa upasuaji kama tulivyofafanua hapo juu.

======

UGONJWA WA MSHIPA WA NGIRI (HERNIA/HYDROCELE)
Ngiri au Hernia ni aina ya ugonjwa ambao unampata mtu baada ya misuli au kuta za tishu mwilini zinazoshikilia au kubeba viungo fulani mwilini kupoteza uimara wake au kuwa na uwazi na hivyo kusababisha viungo hivyo kutoshikiliwa ipasavyo katika sehemu vinapostahili kuwepo.

Katika mwili wa binadamu, maeneo ambayo tatizo hili hutokea mara kwa mara ni maeneo ya tumboni, katika eneo la kinena, eneo la paja kwa juu na pia ngiri inaweza kutokea katika eneo ambalo mtu alifanyiwa upasuaji. Ugonjwa huu wa ngiri unawapata wanaume na wanawake wa rika zote. Mshipa wa ngili ni jina linalokusanya magonjwa kama Ngiri kavu (Hernia), Ngiri maji (Hydrocele) na Ngiri nyinginezo kama vile kuvimba kokwa au mfereji unaopitisha manii unaojulikana kitaalamu kama Epididmorchitis.

Ngiri Kavu (Hernia), aina hii ya ngiri huwapata wanawake na wanaume wote kwa ujumla. Ngiri kavu inapompata Mwanamke huitwa Fermoral Hernia, na pindi inapompata mwanaume inaitwa Scrotal hernia. Kwa maana halisi ya ngiri au mshipa wa ngiri ni hali inayotokea katika mwili wa binadamu ambapo sehemu fulani ya nyama ya viungo mbalimbali vya mwili hujipenyeza kupitia sehemu dhaifu ya mwili na kutokeza upande wa pili. Sehemu hiyo inayoathiriwa mara nyingi huwa ni maeneo ya tumbo, kokwa, pumbu na kadhalika ambapo baadhi ya viungo vya mwili vilivyomo tumboni hujipenyeza kupitia vitundu vinavopitisha mishipa ya fahamu inayohudumia kokwa (Spesmatic Cord), hivyo baada ya kujipenyeza huteremka hadi ndani ya korodani hali ambayo hukamilisha kuwepo kwa ugonjwa wa mshipa wa ngiri.

Pamoja na hivyo mshipa wa ngili hujitokeza sehemu mbalimbali za mwili na hupewa majina tofauti kutokana na sehemu ulipojitokeza, kwa mfano ngiri ya tumbo inajulikana kitaalamu kama Abdominal Hernia, pia watoto wanaozaliwa na vitovu vikubwa inaitwa Umbilical Hernia, na pale ngiri inapojitokeza katika sehemu ya haja kubwa inaitwa Anal Herni. Dalili zake hazitofautiani sana hata hivyo ngiri hujitokeza bila maumivu yoyote isipokuwa kuna baadhi ya ngili hujitokeza na maumivu makali hutegemea ngiri ilivotokeza.

Miongoni mwa vitu vinavyoweza kumsababisha mtu apate ugonjwa wa ngiri ni pamoja na kuwa na uzito mkubwa wa mwili wa kupitiliza au kuongezeka uzito kwa ghafla, pia kua na kazi ya kubeba au kunyanyua vitu vizito, tatizo la kukohoa au kupiga chafya kwa muda mrefu, ujauzito au matatizo yanayojitokeza kwa mwanamke wakati wa kujifungua.

Mojawapo ya dalili za ugojwa wa ngiri ni pamoja na;
• Uvimbe unaoteremka kuingia ndani ya korodani unaojulikana kitaalamu kama Direct Scoratal inguinal Hernia.
• Uvimbe unaojitokeza tumboni na kuteremka hadi ndani ya korodani, uvimbe huu hauumi na unaweza kurudishwa kwa urahisi iwapo mgonjwa atalala chali na kusukuma kwa vidole, uvimbe huu.

• Na pindi ukikubali kurudi ndani ndipo unapoitwa Reduible direct scrotal inguinal hernia.
• Na pia endapo utashindikana kurudi tumboni ndipo unapoitwa Irreduible direct scrotal inguinal hernia.
Ugojwa huu wa ngiri unaweza kutibika

======

Ugonjwa wa ngiri ya kitovu (Umbilical Hernia)

Hili ni tatizo la kiafya ambalo huathiri ukuta wa tumbo na kitovu. Tatizo hili husababishwa na mambo makubwa matatu; kwanza ni kasoro ya kuzaliwa. Hapa ni kwamba kitovu kinakuwa na kasoro tangu pale mtoto anapokuwa tumboni kabla hajazaliwa.

Tatizo hili kwa watu wazima lipo mara tatu zaidi kwa wanawake ukilinganisha na wanaume ambapo lipo kwa kiasi kidogo sana. Kwa watoto kiwango cha tatizo hili vinalingana kwa wote wa kike na wa kiume na tafiti zinaonesha kwamba, tatizo ni kubwa kwa watoto wa Kiafrika ukilinganisha na mataifa mengine.

Aina ya pili ya tatizo hili ni ngiri ya kitovu. Hii inatokea tu pasipo na kasoro za kuzaliwa nazo. Hili linatokea kutokana na shinikizo la mgandamizo wa hewa na nguvu ndani ya tumbo kunakosababishwa na unene kupita kiasi, kunyanyua mizigo mizito au vitu vizito mara kwa mara, kikohozi cha muda mrefu na ujauzito wa mimba ya mapacha kwa mwanamke.

Aina ya tatu ya ngiri ya kitovu inaitwa ‘Paraumbilical hernia’. Aina hii ya ngiri hutokea zaidi kwa watu wazima na husababishwa na kasoro upande wa juu wa kitovu kuelekea kwa juu kufuata mstari wa kati wa tumbo.

DALILI ZA UGONJWA
Ngiri hutokea katika eneo la kitovu ambacho kwa lugha nyingine huitwa ‘Umbilicus’, ‘navel’ au ‘Belly button’. Kwa watoto wachanga wanapozaliwa kitovu huwa kirefu sana na huungana na kondo la nyuma la mama ili kupeleka lishe na hewa ya oksijeni kwa mtoto anapokuwa tumboni.

Baada tu ya kuzaliwa, mtoto hujitegemea hivyo kitovu hukatwa katika eneo maalum ili kipungue urefu. Baada tu ya kitovu cha mtoto kupona, mtoto anaweza kupatwa na tatizo hili la ngiri ya kitovu tangu anapokuwa mtoto mchanga ambapo akilia kitovu kinatokeza juu na anaponyamaza kinarudi ndani.

Hali hii wakati mwingine humsababisha mtoto apatwe na maumivu makali huku akilia kila wakati.

Aina hii ya ngiri huwa haipasuliwi kwani huisha yenyewe baada ya miaka miwili hadi mitatu, lakini baada ya umri huo kama haikuisha basi mtoto atafanyiwa upasuaji kurekebisha.

Endapo mtoto ngiri hiyo itakuwa inamsumbua kabla ya umri wa miaka mitatu, basi hatapasuliwa bali itafanyiwa utaratibu wa kuirudisha kitaalam ili isiendelee kutokeza na kuleta maumivu. Ngiri inapokuwa kubwa, tundu lake huwa haliongezeki hivyo husababisha matumbo na kila kitu kitachomoza na kubana nje kushindwa kurudi ndani na kusababisha hali iitwayo ‘Strangulation’.

Kama hali hii haitatibiwa mapema basi italazimika upasuaji wa dharura na ikichelewa huweza kuhatarisha maisha ya mgonjwa. Tatizo hili hutokea hata kwa ngiri nyingine ambazo tutakuja kuziona katika matoleo mengine.

UCHUNGUZI
Ngiri ya kitovu huonekana kwa macho pale inapochomoza ambapo dhahiri itaonesha imechomoza, wakati mwingine mgonjwa atalalamika maumivu na kama ni mtoto atakuwa analia mara kwa mara.

Vipimo vingine vitategemea na daktari kadiri atakavyoona inafaa.

MATIBABU
Matibabu ya ngiri ni kupasuliwa, haishauriwi kufungia sarafu kwani inaweza kukosewa na kusababisha sehemu ya utumbo kubanwa au kuleta maambukizi ya ngozi kwenye kitovu. Kwa mtoto huisha yenyewe taratibu na ikibidi hupasuliwa baada ya umri wa miaka mitatu.

Wakubwa ni lazima ipasuliwe kama inaleta shida. Wahi hospitali ya mkoa kwa uchunguzi na tiba

======

Ngiri au Hernia ni aina ya ugonjwa ambao unampata mtu baada ya misuli au kuta za tishu mwilini zinazoshikiria au kubeba viungo (organs) fulani mwilini kupoteza uimara wake au kuwa na uwazi (Opening) na hivyo kusababisha viungo hivyo kutoshikiriwa ipasavyo katika sehemu vinapostahili kuwepo.

Katika mwili wa binadamu, maeneo ambayo tatizo hili hutokea mara kwa mara ni maeneo ya tumboni, katika eneo la kinena, eneo la paja kwa juu na pia ngiri inaweza kutokea katika eneo ambalo mtu alifanyiwa upasuaji (operesheni).


Tatizo la ngiri huweza kumpata mtu yeyote. Miongoni mwa vitu vinavyoweza kumsababisha mtu apate ugonjwa wa ngiri ni: Kuwa na uzito mkubwa wa mwili au kuongezeka uzito kwa ghafla, kazi ya kubeba au kunyanyua vitu vizito, tatizo la kukohoa au kupiga chafya kwa muda mrefu, ujauzito au matatizo yanayojitokeza kwa mwanamke wakati wa kujifungua pia kuharisha au kuvimbiwa (Constipation). Vitu hivyo pamoja na mtu kuwa na misuli au tishu zilizopoteza uimara au uwazi (opening or hole) humfanya mtu apate ngiri (hernia).

Ngiri hutambuliwa kwa kutokea kitu kama uvimbe au kujaa katika eneo husika (baadhi ya maeneo yametajwa hapo juu) na pia kwa kufanyiwa uchunguzi wa mara kwa mara na daktari huwezesha kugundua tatizo hili.

Njia inayoweza kutatua tatizo hili ni kwa mtu mwenye ngiri kufanyiwa upasuaji ili kurekebisha misuli au tishu zilizolegea. Pia kutegemeana na kihatarishi cha tatizo hili, mtu unaweza kuwa unafanya mazoezi ili kupunguza uzito wako na kuweka utaratibu mzuri wa kula chakula kinachojumuisha mboga mboga au matunda yenye nyuzi nyuzi (fibers), hii itasaidia pia mmeng’enyo (digestion) wa chakula tumboni na kuepusha kuvimbiwa. Matunda (Vitamin C) husaidia kuunganisha tishu zilizolegea na pia husaidia kupona haraka kwa sehemu iliyofanyiwa upasuaji (operesheni).

Na kama tatizo lako ni la kukohoa kwa muda mrefu kunakosababishwa na uvutaji wa sigara, ni vyema ukasitisha uvutaji ili kupunguza madhara au makali ya ngiri lakini pia kusitisha sigara kwa ajili ya usalama wa afya yako.

Ngiri au Hernia ni aina ya ugonjwa ambao unampata mtu baada ya misuli au kuta za tishu mwilini zinazoshikiria au kubeba viungo (organs) fulani mwilini kupoteza uimara wake au kuwa na uwazi (Opening) na hivyo kusababisha viungo hivyo kutoshikiriwa ipasavyo katika sehemu vinapostahili kuwepo.

Katika mwili wa binadamu, maeneo ambayo tatizo hili hutokea mara kwa mara ni maeneo ya tumboni, katika eneo la kinena, eneo la paja kwa juu na pia ngiri inaweza kutokea katika eneo ambalo mtu alifanyiwa upasuaji (operesheni).


Tatizo la ngiri huweza kumpata mtu yeyote. Miongoni mwa vitu vinavyoweza kumsababisha mtu apate ugonjwa wa ngiri ni: Kuwa na uzito mkubwa wa mwili au kuongezeka uzito kwa ghafla, kazi ya kubeba au kunyanyua vitu vizito, tatizo la kukohoa au kupiga chafya kwa muda mrefu, ujauzito au matatizo yanayojitokeza kwa mwanamke wakati wa kujifungua pia kuharisha au kuvimbiwa (Constipation). Vitu hivyo pamoja na mtu kuwa na misuli au tishu zilizopoteza uimara au uwazi (opening or hole) humfanya mtu apate ngiri (hernia).

Ngiri hutambuliwa kwa kutokea kitu kama uvimbe au kujaa katika eneo husika (baadhi ya maeneo yametajwa hapo juu) na pia kwa kufanyiwa uchunguzi wa mara kwa mara na daktari huwezesha kugundua tatizo hili.

Njia inayoweza kutatua tatizo hili ni kwa mtu mwenye ngiri kufanyiwa upasuaji ili kurekebisha misuli au tishu zilizolegea. Pia kutegemeana na kihatarishi cha tatizo hili, mtu unaweza kuwa unafanya mazoezi ili kupunguza uzito wako na kuweka utaratibu mzuri wa kula chakula kinachojumuisha mboga mboga au matunda yenye nyuzi nyuzi (fibers), hii itasaidia pia mmeng’enyo (digestion) wa chakula tumboni na kuepusha kuvimbiwa. Matunda (Vitamin C) husaidia kuunganisha tishu zilizolegea na pia husaidia kupona haraka kwa sehemu iliyofanyiwa upasuaji (operesheni). Na kama tatizo lako ni la kukohoa kwa muda mrefu kunakosababishwa na uvutaji wa sigara, ni vyema ukasitisha uvutaji ili kupunguza madhara au makali ya ngiri lakini pia kusitisha sigara kwa ajili ya usalama wa afya yako.
07233ddc620ad54622005d7b46d9077f.jpg

 
habari wana jamii forum. Kwa muda mrefu nimekuwa nasumbuliwa na matatizo ya tumbo. nimeishakunywa dawa nyingi bila mafaniko. Tumbo linakuwa linaunguruma hasa saa kumi na moja alfajiri nikienda msalani sometimes kinatoka choo cha mbuzi, naenda haja mara kwa mara hasa nyakati za asubui.

Mbaya zaidi zakari nayo imeanza kusinyaaa inafanana kama ya mtoto, nawaza hata nifanyenye wakuu kwa hii hali.nimejaribu kuwauliza watu wameniambia kuwa ni ngiri. Naomba kwa mwenye kufaham tiba anisaidie maana nahisi kuelemewa.
 
habari wana jamii forum. Kwa muda mrefu nimekuwa nasumbuliwa na matatizo ya tumbo. nimeishakunywa dawa nyingi bila mafaniko. Tumbo linakuwa linaunguruma hasa saa kumi na moja alfajiri nikienda msalani sometimes kinatoka choo cha mbuzi, naenda haja mara kwa mara hasa nyakati za asubui. Mbaya zaidi zakari nayo imeanza kusinyaaa inafanana kama ya mtoto, nawaza hata nifanyenye wakuu kwa hii hali.nimejaribu kuwauliza watu wameniambia kuwa ni ngiri. Naomba kwa mwenye kufaham tiba anisaidie maana nahisi kuelemewa.
Pole kwa kuumwa na tumbo na hiyo Ndizi yako kusinyaaa itabidi kumuona Daktari Mtaalamu wa mambo ya Tumbo ili aweze kukufanyia Uchunguzi zaidi na pia aweze kukupatia dawa. na kuhusu kama ni tumbo kuuma tumia asali , kunywa kijiko kimoja Asubuhi kabla hujala kitu kutwa mara tatu fanya hivyo utaniambia matokeo yake ukisha kula hiyo Asali usile chakula mpaka saa moja ipite tangu ulipokula hiyo Asali.

Kuhusu tiba ya ngiri inatakiwa ufanyiwe upasuaji Operesheni inategemea Ngiri zipo za aina 2 ya kwanza ni ya ndani inaitwa kwa kiingereza ( Hernia)


Na Ngiri ingine ni ya Mshipa wa Kushuka ni hii hapa Mabusha kwa lugha ya kiswahili
IMabusha ni hali ya kujaa maji kwenye mfuko wa pumbu. Hali hii hutokea kunapokuwa na mkusanyiko wa maji kati ya tabaka mbili za utando unaozunguka korodani.
Inakadiriwa kuwa karibu asilimia moja ya wanaume wote kote duniani huathiriwa na tatizo hili. Kwa hapa nchini, tatizo hili ni maarufu sana maeneo ya mwambao wa Pwani ya Bahari ya Hindi, kiasi cha kuhusishwa na imani kadhaa.
Mojawapo ya dhana iliyozoeleka miongoni mwa watu wa mwambao ni kuwa mabusha yana uhusiano mkubwa na unywaji wa maji ya madafu. Aidha, tatizo hili limekuwa likichukuliwa na baadhi ya watu kuwa ni hali ya kudhalilisha ingawa kwa wengine huonekana ni hali ya kuwa mzee wa heshima au umwinyi.
Ifahamike pia kuwa, tatizo la mabusha halitokei kwa wanaume watu wazima tu. Watoto wa kiume hususani katika mwaka wa kwanza (infants) pia ni waathirika wakuu wa tatizo hili.
Kwa kawaida mabusha hayana maumivu na wala hayaleti madhara, isipokuwa kama yatapata uambukizi kwa sababu nyingine yeyote ile, hali inayowafanya wengi wa waathirika, hasa wa mwambao, kuwa wagumu kutafuta ufumbuzi wa tiba.
Hata hivyo, ni vyema kama mtu ana uvimbe wowote kwenye pumbu zake, kutafuta msaada wa kitabibu ili kuweza kuondoa uwezekano wa kuwepo kwa magonjwa mengine ya sehemu za siri kama vile saratani ya korodani (testicular cancer) n.k.
Mabusha husababishwa na nini?
Sababu za kutokea kwa mabusha hutofautiana kati ya watoto wa kiume na wanaume watu wazima.


Kwa watoto wa kiume
Kwa watoto wa kiume, mabusha huweza kuanza kutokea kipindi cha ujauzito.
Infant-hydrocele3.jpg
Wakati wa ujauzito, korodani za mtoto wa kiume huwa kwenye tumbo lake kabla ya kushuka taratibu kuelekea kwenye mapumbu. Wakati wa ushukaji huo, kifuko kinachozunguka korodani kinachoitwa processus vaginalishushuka sambamba na kurodani hizo na kufanya korodani kuzungukwa na maji.
Kwa kawaida, ndani ya muda wa mwaka mmoja, kifuko hiki hufunga na maji hayo yanayozunguka korodani yote hufyonzwa na kurudishwa kwenye tumbo la mtoto. Iwapo baada ya kifuko kufunga na maji yaliyomo kushindwa kufyonzwa kurudishwa kwenye tumbo la mtoto, mtoto hupata busha lijulikanalo kitaalamu kama busha lisilo na mawasiliano (non-communicating hydrocele).
Hali kadhalika, wakati mwingine inawezekana kifuko kikashindwa kufunga na hivyo maji yakaendelea kujaa ndani ya kifuko kuzunguka korodani. Aina hii ya mabusha kwa watoto ujulikana kama busha lenye mawasiliano (communicating hydrocele).
Kwa wanaume watu wazima
Hydrocele-2-150x150.jpg
Kwa wanaume watu wazima, mabusha husababishwa na mambo makuu mawili; Kwanza, kitendo chochote kinachochochea tando zinazozunguka korodani kuzalisha maji kwa wingi kuliko kawaida, na njia ya pili ni kupungua kwa ufyonzaji wa maji yanayozunguka korodani kwa sababu ya kuziba kwa mirija ya lymph (blockage of scrotal lymphatic system) au kuziba kwa mishipa ya damu inayosafirisha damu kutoka kwenye pumbu kwenda sehemu nyingine za mwili (blockage of scrotal venous system).
Ongezeko la uzalishaji wa maji linaweza kutokana na
  • Maambukizi au/na majeraha katika korodani (testicular inflammation auorchitis) au maambukizi katika mshipa ujulikanao kama epididymisyanayoweza kusababishwa na kifua kikuu (tuberculosis) cha makende, au maambukizi yanayosababishwa na vimelea wa filaria (filariasis) wanaosababishwa na kuumwa na mbu aina ya Culex.
  • Kujinyonga kwa korodani (testicular torsion) kunakoweza kuzifanya korodani kutenda kazi zaidi ya kiwango chake (hyperactive testis).
  • Uvimbe katika korodani (testicular tumors) ambao husababisha uzalishaji wa maji kupita kiasi.
Kupungua kwa ufyonzaji wa maji hutokana na
  • Kufanyiwa upasuaji kipindi cha siku za nyuma katika eneo la kinena, au operesheni ya upandikizaji figo ambazo zinaweza kuathiri mfumo wa lymph na vena na hivyo kupunguza ufyonzaji wa maji kutoka kwenye mapumbu.
  • Kuwahi kufanyiwa tiba ya mionzi kipindi cha nyuma nayo uhusishwa na kutokea kwa mabusha.
Kwa hapa kwetu Tanzania, kungatwa na mbu aina ya Culex anayeeneza vimelea vya filaria kunaelezwa kuwa sababu kuu mojawapo inayopelekea kuwepo kwa tatizo la mabusha na matende hususani maeneo ya Pwani na mwambao.
Dalili za Mabusha
Katika hatua za awali, mabusha huwa hayana dalili zozote (asymptomatic).
Hata hivyo, baada ya muda fulani, mapumbu hujaa na uvimbe huweza kuonekana hata kwa nje. Kwa kadiri uvimbe unavyozidi kuongezeka, dalili zifuatazo zaweza kujitokeza pia;
  • Muhusika kujihisi hali ya uzito na kuvuta sehemu za siri kutokana na kujaa na kuongezeka kwa uzito wa mapumbu.
  • Mgonjwa huweza kujihisi hali ya usumbufu na kutojisikia vizuri maeneo ya kinena mpaka mgongoni.
  • Kwa kawaida mabusha hayana maumivu yeyote. Hata hivyo, iwapo mgonjwa ataanza kujihisi maumivu, hiyo ni dalili ya kuwepo kwa uambukizi katika mshipa wa epididymis (acute epididymitis)
  • Uvimbe huwa na tabia ya kupungua iwapo mgonjwa atakaa kitako na huongezeka pindi anaposimama.
  • Iwapo mgonjwa atajisikia homa, kichefuchefu na kutapika, hizo ni dalili za kuwepo kwa uambukizi katika mabusha.
  • Kwa kawaida mabusha hayana muingiliano na uwezo na ufanisi wa utendaji wa ngono. Hata hivyo kuna taarifa tofauti za kitafiti kutoka bara Asia na Afrika Magharibi kuwa mabusha yanaweza kuathiri ufanisi wa ngono na kwa kiasi fulani kusababisha mhemko au msongo wa mawazo kwa muathirika.
Uchunguzi na Vipimo
Uchunguzi mzuri wa kitabibu (physical examination) huwezesha kugundua uwepo wa mabusha kwa kiasi kikubwa bila hata kuhitaji vipimo vya ziada. Vipimo uhitajika tu kwa ajili ya kuchunguza chanzo cha mabusha, madhara yaliyoletwa na mabusha au kujua hali ya korodani.
Vipimo ni pamoja na
  • Kupima damu (Full Blood Count) na mkojo (Urine Analysis) kuchunguza uwepo wa maambukizi kama vile vimelea wafilaria na mengineyo.
  • Ultrasound ya kinena pamoja na mapumbu: Aina hii ya kipimo hufanywa ili kuchunguza uwepo wa matatizo mengine tofauti na mabusha. Matatizo hayo ni kama vile ngiri, uvimbe, kujinyonga kwa korodani (testicular torsion), majeraha katika korodani, damu kuvuja kwenye kwenye korodani (traumatic hemorrhage) au maambukizi.
Matibabu ya Mabusha
Kwa watoto wadogo, kwa kawaida mabusha hupotea yenyewe ndani ya mwaka mmoja. Iwapo hayajapotea, mtoto uhitaji kufanyiwa upasuaji kama tiba.
Kwa wanaume watu wazima, mabusha pia huweza kupona yenyewe bila kuhitaji tiba. Iwapo mabusha hayajapotea na yanamletea mgonjwa usumbufu (discomfort) au hali mbaya ya kiumbo (disfigurement) hayana budi kufanyiwa upasuaji ili kuyaondoa.
Njia za tiba ni
  • Hydrocele-1.jpg
    Upasuaji: Upasuaji wa mabusha huweza kufanyika bila ya mgonjwa kuhitaji kulazwa (outpatient). Madhara yanayoweza kutokea wakati wa upasuaji wa mabusha ni pamoja na damu kuganda (blood clots), maambukizi au majeraha kwenye korodani. Hii ndiyo njia maarufu zaidi na ya kuaminika ya matibabu ya mabusha duniani kote.

  • Kunyonya maji kwa kutumia sindano maalum (Needle aspiration): Njia nyingine inayotumika kutibu mabusha ni kuyanyonya maji kwa kutumia sindano maalum (needle aspiration). Hata hivyo njia hii haitumiki sana sehemu nyingi duniani kwa sasa kwa sababu maji ya mabusha huwa yana tabia ya kujirudia baada ya muda mfupi hata kama yatanyonywa.
Baadhi ya matabibu hupendelea kudunga dawa maalum za kuzuia maji yasijae tena (sclerosing agents) mara baada ya kunyonya na kuyaondoa maji yote.
Njia hii ya kunyonya maji ya mabusha, hufaa zaidi kwa wagonjwa wasioweza kuhimili upasuaji. Madhara yanayoweza kusababishwa na tiba ya namna hii ni pamoja na maambukizi na maumivu kwenye korodani.
Hata hivyo wakati mwingine, bila kujali ni tiba gani imetumika, mabusha huweza kujirudia baada ya matibabu.
Madhara ya Mabusha
Kwa kawaida mabusha hayana madhara yeyote. Aidha mabusha hayawezi kuathiri uwezo wa mtu kuzaa. Hata hivyo mabusha yanaweza kuleta madhara iwapo tu kama yakiambatana na magonjwa mengine kwenye korodani.
Kwa mfano, kama mabusha yataambatana na maambukizi (testicular infection) au uvimbe kwenye korodani (testicular tumor), yanaweza kusababisha kupungua kwa uzalishaji na utendaji kazi wa mbegu za kiume (sperms) na kupelekea tatizo la ugumba kwa wanaume.
Hali kadhalika, iwapo sehemu ya utumbo mkubwa au mdogo imebanwa katika upenyo fulani kwenye sehemu ya ukuta wa tumbo, huweza kusababisha ngiri (strangulated hernia), hali ambayo ni hatari kama isipotibiwa haraka.

chanzo:Fahamu kuhusu Mabusha (Hydrocele)
 
Last edited by a moderator:
nashkuru mkuu kwa maelezo yako mazuri. Mimi sina busha, naona ni ngiri ya ndani yani ngiri ya kuvuta?? Naweza kupata tiba bila kufanyiwa uoasuaji??
 
Maelezo yk ni mazuri sn, je na tumbo kunguruma sn na kushindwa kufanya tendo la ndoa au ukifanya mara moja huwez tena nazo ni dalili pia?
 
Ndugu wana JF niko serious na wala ctanii, na naombeni mnipe ushauri utakaonisaidia mwenzenu. Imetokea kuwa nasumbuliwa na ugonjwa wa ngiri na hapa nilipo nackia maumiv c kawaida. Imepelekea mpaka sehemu 1 ya yai la kushoto kwenye uume ina mishipa yenye uvimbe najihic ni utumbo umezama huko nikishika. Nilienda hsptl doctor akanipa 2 vidonge ambavyo havikunisaidia. NAOMBENI USHAURI KWA ANAEJUA DAWA YAKE NIWEZE KUPONA MANAKE NIMEKATA TAMAA YA KUPONA. Nakaribia mwaka nikiwa na haya maumiv.
 
hiyo ndugu yangu dawa yake ni opreshen, hlo ni tatizo ambalo wanaume wengi huzaliwa nalo, gharama yake si chin ya elfu 50, baada ya opreshen huitajik kufanya tendo la ndoa miezi 6 wala kaz ngum. uckubal kudanganyika na dawa za kienyeji onana na madaktar hospital kubwa za serkal.
 
hiyo ndugu yangu dawa yake ni opreshen, hlo ni tatizo ambalo wanaume wengi huzaliwa nalo, gharama yake si chin ya elfu 50, baada ya opreshen huitajik kufanya tendo la ndoa miezi 6 wala kaz ngum. uckubal kudanganyika na dawa za kienyeji onana na madaktar hospital kubwa za serkal.
Asante sana mkuu kwa ushauri.
 
hiyo ndugu yangu dawa yake ni opreshen, hlo ni tatizo ambalo wanaume wengi huzaliwa nalo, gharama yake si chin ya elfu 50, baada ya opreshen huitajik kufanya tendo la ndoa miezi 6 wala kaz ngum. uckubal kudanganyika na dawa za kienyeji onana na madaktar hospital kubwa za serkal.
jitahidi kuzingatia hapo kwenye red
 
Ndugu God bell,
Pole kwa maumivu.

Kwanza niseme kuwa kwa kiswahili bado kuna mkanganyiko wa neno Ngiri. Wapo wanoiita ngiri kwa maana ya busha (hydrocele), na wengine huita ngiri (Hernia) ambayo ni sehemu ya viungo kuingia sehemu nyingine kwasababu ya kuwa l'oose'

Kwa maelezo yako nadhani unaongelea abdomen hernia ambayo sehemu ya utumbo hutumbukia katika hasua. Hii ni kwasababu sehemu inayozuia (kiwambo) inakuwa imeachia. Utumbo huingia huko na kukuletea maumivu. Siyo maradhi yanayosababishwa na wadudu, hutokea hata kwa watoto wadogo au watu wazima ambao hufanya kazi za nguvu n.k.

Hakuna dawa inayotibu bali zinazopunguza maumivu. Mara nyingi ukilala na taratibu kusukuma hicho unachokihisi kurudi juu, basi hali inaweza kutulia. Itajirudia tena tena kwasababu umesogeza tu lakini hujazuia.

Matibabu yake ni operesheni ya kufunga sehemu hiyo. Matibabu hayo ni muhimu sana kwasababu inaweza kutokea kuwa utumbo umeingia ukajikunja na kushindwa kupitisha damu (strangulated hernia) hivyo sehemu hiyo itaoza na kuweza kuleta madhara makubwa zaidi tusiyotarajia.
Hutokea nadra lakini inapotokea hujui utakuwa sehemu gani ya huduma muhimu na za haraka hapo unaweza kujikuta katika wakati mgumu sana kimaumivu na pengine kimaisha.

Tafadhali kawaone madaktari katika hospitali kubwa kwa ushauri zaidi.
 
Samahani wana jf nilikuwa napenda kujua hernia ni ugonjwa gani na husababishwa na nini,pia dalili na matibabu yake ni yapi. Nawasilisha
 
kwa kiswahili wanaita NGIRI


nadhani hukukwepa umande


[h=3]Hernia Causes[/h]Although abdominal hernias can be present at birth, others develop later in life. Some involve pathways formed during fetal development, existing openings in the abdominal cavity, or areas of abdominal-wall weakness.
  • Any condition that increases the pressure of the abdominal cavity may contribute to the formation or worsening of a hernia. Examples include
    • obesity,
    • heavy lifting,
    • coughing,
    • straining during a bowel movement or urination,
    • chronic lung disease, and
    • fluid in the abdominal cavity.
  • A family history of hernias can make you more likely to develop a hernia

[h=3]Hernia Symptoms and Signs[/h]The signs and symptoms of a hernia can range from noticing a painless lump to the severely painful, tender, swollen protrusion of tissue that you are unable to push back into the abdomen (an incarcerated strangulated hernia).
  • Reducible hernia
    • It may appear as a new lump in the groin or other abdominal area.
    • It may ache but is not tender when touched.
    • Sometimes pain precedes the discovery of the lump.
    • The lump increases in size when standing or when abdominal pressure is increased (such as coughing).
    • It may be reduced (pushed back into the abdomen) unless very large.
  • Irreducible hernia
    • It may be an occasionally painful enlargement of a previously reducible hernia that cannot be returned into the abdominal cavity on its own or when you push it.
    • Some may be chronic (occur over a long term) without pain.
    • An irreducible hernia is also known as an incarcerated hernia.
    • It can lead to strangulation (blood supply being cut off to tissue in the hernia).
    • Signs and symptoms of bowel obstruction may occur, such as nausea and vomiting.
  • Strangulated hernia
    • This is an irreducible hernia in which the entrapped intestine has its blood supply cut off.
    • Pain is always present, followed quickly by tenderness and sometimes symptoms of bowel obstruction (nausea and vomiting).
    • The affected person may appear ill with or without fever.
    • This condition is a surgical emergency.
 
kwa kiswahili wanaita NGIRI


nadhani hukukwepa umande


[h=3]Hernia Causes[/h]Although abdominal hernias can be present at birth, others develop later in life. Some involve pathways formed during fetal development, existing openings in the abdominal cavity, or areas of abdominal-wall weakness.
  • Any condition that increases the pressure of the abdominal cavity may contribute to the formation or worsening of a hernia. Examples include
    • obesity,
    • heavy lifting,
    • coughing,
    • straining during a bowel movement or urination,
    • chronic lung disease, and
    • fluid in the abdominal cavity.
  • A family history of hernias can make you more likely to develop a hernia

[h=3]Hernia Symptoms and Signs[/h]The signs and symptoms of a hernia can range from noticing a painless lump to the severely painful, tender, swollen protrusion of tissue that you are unable to push back into the abdomen (an incarcerated strangulated hernia).
  • Reducible hernia
    • It may appear as a new lump in the groin or other abdominal area.
    • It may ache but is not tender when touched.
    • Sometimes pain precedes the discovery of the lump.
    • The lump increases in size when standing or when abdominal pressure is increased (such as coughing).
    • It may be reduced (pushed back into the abdomen) unless very large.
  • Irreducible hernia
    • It may be an occasionally painful enlargement of a previously reducible hernia that cannot be returned into the abdominal cavity on its own or when you push it.
    • Some may be chronic (occur over a long term) without pain.
    • An irreducible hernia is also known as an incarcerated hernia.
    • It can lead to strangulation (blood supply being cut off to tissue in the hernia).
    • Signs and symptoms of bowel obstruction may occur, such as nausea and vomiting.
  • Strangulated hernia
    • This is an irreducible hernia in which the entrapped intestine has its blood supply cut off.
    • Pain is always present, followed quickly by tenderness and sometimes symptoms of bowel obstruction (nausea and vomiting).
    • The affected person may appear ill with or without fever.
    • This condition is a surgical emergency.

ahsante mkubwa ubarikiwe
 
Could u summarize is kiswahili so we can understand all of us. Thankx mkuu.
Kwanza niseme kuwa kwa kiswahili bado kuna mkanganyiko wa neno Ngiri. Wapo wanoiita ngiri kwa maana ya busha (hydrocele), na wengine huita ngiri (Hernia) ambayo ni sehemu ya viungo kuingia sehemu nyingine kwasababu ya kuwa l'oose'

Kwa maelezo yako nadhani unaongelea abdomen hernia ambayo sehemu ya utumbo hutumbukia katika hasua. Hii ni kwasababu sehemu inayozuia (kiwambo) inakuwa imeachia. Utumbo huingia huko na kukuletea maumivu. Siyo maradhi yanayosababishwa na wadudu, hutokea hata kwa watoto wadogo au watu wazima ambao hufanya kazi za nguvu n.k.

Hakuna dawa inayotibu bali zinazopunguza maumivu. Mara nyingi ukilala na taratibu kusukuma hicho unachokihisi kurudi juu, basi hali inaweza kutulia. Itajirudia tena tena kwasababu umesogeza tu lakini hujazuia.

Matibabu yake ni operesheni ya kufunga sehemu hiyo. Matibabu hayo ni muhimu sana kwasababu inaweza kutokea kuwa utumbo umeingia ukajikunja na kushindwa kupitisha damu (strangulated hernia) hivyo sehemu hiyo itaoza na kuweza kuleta madhara makubwa zaidi tusiyotarajia.
Hutokea nadra lakini inapotokea hujui utakuwa sehemu gani ya huduma muhimu na za haraka hapo unaweza kujikuta katika wakati mgumu sana kimaumivu na pengine kimaisha.


Tafadhali kawaone madaktari katika hospitali kubwa kwa ushauri zaidi.
Ukiwa na Shida yoyote ile
Usipo pona kwa Dawa za Hospitali nitafute mimi nipate kukutibia upate kupona ukihitaji matibabu yangu
Unaweza kunitafuta kwa Mawasiliano Herbalist Dr. MziziMkavu Email barua ya pepe.fewgoodman@hotmail.com What's App +905344508169 Au Ni add Kwa Facebook tumia jina hili Herbalist mzizimkavu. Au boonyeza hapa.Herbalist MziziMkavu
 

Similar Discussions

4 Reactions
Reply
Back
Top Bottom