Helicobacter pylori
JF-Expert Member
- Feb 15, 2013
- 419
- 277
Ugonjwa huu hushambulia kuku wa Umri wote, lakini Vifaranga na walioko chini ya miezi mitano wapo kwenye hatari zaidi. Husababisha vifo mpaka 50% ya kuku wote waliougua.
Coccidia ndio wadudu wanaosababisha ugonjwa wa kuhara damu, wapo kwenye kundi la Protozoa, jamii ya Eimeria spp, wadudu hawa huathiri wanyama karibia wote.
Wadudu hawa wamegawanyika kulingana na Sehemu wanayoshambulia kwenye utumbo.
1. Ceacal coccidia(appendix/ceca/kidole tumbo) kuku ana vidole tumbo viwili, basi wadudu hawa wa coccidia (Eimeria tenelle) hushambulia na ndio chanzo cha kuhara damu.
2. Intestinal coccidia (Utumbo mwembamba) Eimeria necatrix ndio pamoja na wengine ndio hushambulia utumbo mwembana, damu huchanganyikana na chakula ndio maana choo huonekana cha Kahawia/ugoro.
MAMBO HATARISHI
1. Msongamano wa kuku wengi ndani ya banda.
2. Uchafu(unyevu nyevu wa matandiko, vyombo vya chakula na maji)
3. Kuingia na kutoka bandani pasipo Utaratibu (Biosecurity).
4. Lishe duni
MAAMBUKIZI/KUENEA
Kuku hupata maambukizi kwa kula vimelea vya wadudu hawa iwe kwenye maji, chakula, kinyesi, chini kwenye matandiko.
Ugonjwa unaweza kutokea pasipo dalili kuonekana na hii Husababisha hatari ya magonjwa nyemelezi.
DALILI ZA UGONJWA.
1. Kuzubaa/kusinzia
2. Kujikunyata na kushusha mabawa
3. Kukosa hamu ya kula
4. Kupungua uzito/utagaji/kudumaa
5. Manyoya kusimama/rafu
6. Kuharisha choo cha kahawia/ugoro
7. Kuharisha choo chenye rangi nyekundu(damu)/nyeusi
8. Kuku kufa(Vifo).
UTAMBUZI
1. Kwa kutazama dalili na Mazingira pia (Choo chenye damu au rangi ya ugoro)
2. Utambuzi wa Maabara (sampuli ya choo)
KINGA/KUZUIA
1. Usafi wa vyombo vya maji na chakula
2. Kuhakikisha Matandiko/banda ni kavu muda wote na safi.
3. Kuweka dawa mlangoni, kukanyaga dawa kabla ya kuingia bandani.
4. Kuepusha Msongamano.
5. Kutunza kuku kulingana na rika.
6. Chanjo
Chanjo Hutolewa kiwandani (Hatchary) au Shambani kwa vifaranga wa siku moja(DOC-1~3), Chanjo hii hutolewa kwa kunywa au kupulizia (spray).
Chanjo hii hutolewa mara moja tu kwa maisha yote ya kuku/bata mzinga.
Hutakiwi kutumia dawa yeyote (Antiboitics eg, Amprolium, Tetracycline or Sulpha’s) kwa muda wa siku 30 baada ya chanjo.
MATIBABU
Ugonjwa huu unatibika kwa kutumia dawa mfano. Toltrazuril 25mg, Amprolium (200mg, 250mg), Potentieted sulphonamide (Sulfaclozine SMH 30%, Sulphadimidine-sulphaquinoxaline, Trimethoprim & Sulphadiazine; etc.) kwa muda wa siku 3-5/7 au kilingana na Maelekezo ya Daktari.
MUHIMU: Dawa hizi lazima zitolewe kwa kufuata ushauri wa Daktari maana kuna baadhi ya dawa zimekuwa na athari hasa kwa kuku wanaotaga (hupunguza utagaji).
Imeandaliwa na
Dr. Godwin Mkami, DVM
SipyVet.centre
Kinyerezi-Mbuyuni DSM
+255 764 667 503