Ugonjwa wa Homa ya Mgunda, ni kipimo kingine kwa Wizara ya Afya, NIMR pamoja na Wataalam wa Afya nchini

kifimbo5

Member
Jun 27, 2022
10
6
Wana Bodi tumesikia kuhusu ugonjwa wa Homa ya Mgunda hiki ni kipimo kingine kwa Wizara ya Afya, NIMR pamoja na Wataalam wa Afya nchini Kama ifuatavyo

1. Kuweza kutafuta ukweli wa ugonjwa huu pamoja na dalili zake

2. Kujua kutofautisha kati ya Siasa, Sayansi na Utaalamu wa kada ya Afya na kutoa majibu ambayo hayatazalisha maswali mengi kwa Watanzania

3. Je, inawezekana kufanya vipimo kwa muda wa siku mbili na kutoa majibu kwa umma kuwa ni ugonjwa gani ulioibuka ghafla, una dalili zipi, jinsi gani ya kujikinga na tiba yake sahihi ni ipi?

HAPA NDIPO TUNATAKIWA KUTOFAUTISHA SIASA NA AFYA, AFYA NI UHAI WA WATU, KWENYE SIASA HUKO TUDANGANYANE HAKUNA SHIDA TUTAFIKA TU.
LAKINI WIZARA YA AFYA
🇹🇿
ZINGATIENI HAYA:

Kusimamia masuala ya upatikanaji wa huduma za afya bora katika maeneo yote ya nchi, Ubora wa huduma za afya na unafuu wa gharama zake kwa wananchi wote.

Kutokana na mabadiliko kwenye pattern ya magonjwa msisitizo uwekwe kwenye mihimili yote minne (4) ya Afya ambayo ni:

1. Health Promotion

2. Health Prevention

3. Health Curative and

4. Health Rehabilitation

Siasa isiingie kila mahali, tutaumiza watu. Kazi kwenu. Uwe na siku njema.

no_photo.png
ReplyForward
 
Back
Top Bottom