Ugomvi katika kuzika wa nini?

Fundi Mchundo

Platinum Member
Nov 9, 2007
8,910
6,822
Mahakama yaamuru azikwe Kikristu

2008-04-04 08:43:26
Na Simon Mhina


Mahakama ya Wilaya ya Kinondoni jijini Dar es Salaam, imeamuru mwili wa marehemu Paul Goliama (40), uzikwe kwa imani ya Kikristo na kuwaonya Waislamu wasivuruge mazishi hayo.

Hukumu ya mgogoro wa mazishi ya Goliama ilitolewa jana na Hakimu Mkazi Mfawidhi Emilius Mchauru wa mahakama hiyo, huku ulinzi mkali wa polisi wenye bunduki mikononi ukiwa umeimarishwa.

Magari mawili Land Rover Defender yalikuwa yamejaa askari hao ambao pia walizunguka eneo la mahakama kuhakikisha kuwa utulivu unakuwepo.

Kesi hiyo ilivuta watu wengi waliokusanyika kuanzia saa 6:00 mchana jana hadi ilipomalizika saa 10:15 jioni.

Goliama alifariki Jumanne ya wiki iliyopita na mazishi yake yalipangwa kufanyika Ijumaa iliyopita katika makaburi ya Sinza, lakini ulizuka mtafaruku wa kugombea maiti yake baada ya Waislamu wa Msikiti wa Swafwa kudai alikuwa Muislam wakati jamaa zake walisisitiza kuwa aliacha Uislamu na kurudi kanisani.

Vurugu hizo zilitokea katika Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) Usharika wa Sinza baada ya ibada kumalizika, na waumini kujiandaa kwenda makaburini kwa maziko.

Hali hiyo ilipelekea uongozi wa kanisa hilo kuomba msaada wa polisi ili kutuliza vurugu na kutafuta muafaka, lakini ilishindikana na polisi wakashauri kuwa suala hilo lifikishwe mahakamani ili kupata muafaka wa kisheria.

Familia ya marehemu ilifungua kesi ya madai katika Mahakama ya Kinondoni na ilianza kusikilizwa Jumatatu wiki hii, na upande wa wajibu madai walifungua kesi katika Mahakama ya Kisutu, lakini ilifutwa kwa kuwa kulikuwa na kesi nyingine ya msingi iliyofunguliwa katika mahakama ya wilaya.

Ushahidi wa wadai uliowasilishwa na wakili wao, Mutakyahwa Charles ulithibitisha kuwa marehemu Goliama alikuwa Mkristo na kwamba hadi anakufa alikuwa muumini wa dini hiyo.

Ushahidi huo kama daftari la waumini wa Usharika huo lililotolewa kama kielelezo ulionyesha kuwa marehemu alirudia dini yake ya Kikristu Juni 2006.

Aidha maelezo ya mkewe Bi. Agnes Goliama, kuwa mumewe alikuwa muumini wa Kikristu ni ushahidi uliothibitisha kuwa alikuwa muumini wa dini hiyo.

Akizungumzia madai yaliyotolewa na upande wa wajibu madai, hakimu Mchauru alisema ushahidi uliotolewa na upande wa wajibu madai, umeonyesha kuwa marehemu alibadili dini ili aweze kumuoa binti wa Kiislamu ambaye ni Atala mwaka 1996 na kwamba hakuwa na dhamira halisi ya kuwa Muislam.

Alisema anaamini hivyo kwa kuwa marehemu baada ya kuachana na Atala, alirudia dini yake ya Kikristu na kuoa binti mwingine wa dini hiyo, Agnes, mwaka 2003 na mtoto waliyempata walimpa jina la Kikristu.

Aidha alihoji ushahidi uliotolewa na upande wa Waislam kuwa iwapo marehemu alikuwa muumini wao, iweje wasifahamu alikuwa mgonjwa hadi anafariki?

Alifafanua kuwa utata upo kwenye ushahidi juu ya ndoa kwa kuwa hawakujua kuwa ndoa ya Atala na Goliama ilivunjika na pia hawakueleza iwapo alikuwa na mtoto na waliieleza mahakama kuwa mtoto aliitwa Aina wakati vielelezo vinaonyesha kuwa anaitwa Anna.

Hakimu Mchauru akitoa ufafanuzi wa barua iliyotolewa mahakamani hapo kama ushahidi iliyodaiwa iliachwa na marehemu huyo ili atakapokufa azikwe Kiislamu, alisema ana mashaka na barua hiyo kwa kuwa haikuwa na sehemu ambayo Goliama aliandika azikwe Kiislamu.

Pia alisema haikuwa na nakala kwa kiongozi wala jamaa yeyote na badala yake mwenye barua hiyo ni Imamu Othman Njama wa msikiti wa Swafwa.

Alisema kisheria marehemu alichokifanya ni kuandika wosia akiagiza anachotaka atendewe atakapokufa kulingana na imani yake ambayo wakati huo ilikuwa Uislamu.

Baada ya hukumu hiyo iliyosomwa kuanzia saa 7:30 hadi saa 10:30 jioni, Waislam hao walionekana kutoridhika na kudai kwamba watakata rufaa.

Walisema hawakuridhika na hukumu hiyo kwa maelezo kuwa hakimu aliyeitoa amefanya hivyo kwa lengo la kuwatetea Wakristo wenzake.

Bw. Omar Hashim aliyejitambulisha kuwa ni kiongozi wa Vijana wa Jumuiya ya Kiislam Mkoa wa Dar es Salaam, alisema mbali na kukata rufaa, watafukua mwili huo na kuuzika kwa mujibu wa taratibu, sheria na dini yao kwa kuwa kushindwa kufanya hivyo ni dhambi.

Alifafanua kuwa kwa vile marehemu walisali naye msikitini na kuwaachia wosia, wasipopigania kumzika kwa imani aliyotaka hawawezi kuepuka adhabu ya Mwenyezi Mungu siku ya Kiama.

Baada ya hukumu hiyo kutolewa, msafara wa waombolezaji ulielekea nyumbani kwa marehemu Sinza huku wakiimba nyimbo mbalimbali za miziki ya Injili na mapambio.

Waombolezaji hao walionekana kuwa na nyuso za furaha na huku wakiimba kwa shangwe.

``Hakuna tena majonzi sasa ni furaha,`` alisema mmoja wa waombolezaji.

Hata mama mzazi wa marehemu huyo, Bi. Anna Goliama, alitoka mahakamani akiwa anarukaruka kwa furaha. Jamaa zake walipiga honi na miziki wa Injili na mapambio yalipamba msafara wa waombolezaji.

Marehemu Goliama anatarajiwa kuzikwa leo ambapo ndugu wanatarajia kupata nakala ya hukumu na kuiwasilisha polisi ili wakabidhiwe mwili wa ndugu yao.

SOURCE: Nipashe

Hii inawezekana imeishatoka kule kwenye mambo ya dini. Ninachojiuliza ni vitu viwili:
1) Mbona hatusikii watu wakigombania kuuguza?
2) Huyo Mungu atakuadhibu kutokana na utakavyozikwa(ambacho kiko nje ya uwezo wako maana ndio yameisha kukuta) na siyo ulivyoishi?

Mimi naona ni aibu kubwa watu kugombania mwili wa marehemu. Kama alikuwa muislamu au mkristu itajulikane mbele ya huyo ajuaye yote. Kwa vile ndugu zake ndio inaelekea walikuwa wanaishi naye na waliishafanya mipango ya mazishi wangeachiwa tu. Hao masheikh hawaitendei haki dini yao kwa kuendelezea huu ugomvi. Wauache MWILI wa marehemu ukapumzike wakati ROHO yake inakabiliana na tusiyoyajua.
 
Fundi,

Makasisi wa leo vimeo sana.

Hizi itikadi za dini siku za leo zimedhihirisha udhaifu, hata ule ufahamu wa kawaida hawana akilini.Aliyekufa kafa,hata kama asipozikwa au azikwe VYOYVYOTE yeye binafsi hana analolifahamu.Hata kama atazikwa na jiji.Au kulikuwa na michango ya fedha ambayo makasisi walitegemea kupewa baada ya mazishi?
Nia kuu ni kuhifadhi mwili uliotoka udongoni na udongoni umerudi.
Sasa haya ya kugombea maiti yatoka wapi?
Inanikumbusha mwaka 1996 wakati wa ajali ya MV BKB,Maiti zilikuwa dili baada ya serikali kutangaza kifuta jasho,Wakati wa kutambua maiti pale uwanja wa Nyamagana.Matapeli walikuwepo pia,tena waliingia kwa huzuni na vilio viwanjani kutafuta maiti zilizokuwa zinaonekana hazina wenyewe ili wapate fwedha za kusafirishia ambazo zingesaidia kuganga njaa yao ya muda mfupi
 
Binafsi sijawahi kuielewa hii dini ya Kiislamu,

really ni dini ya ajabu sana,wanang'ang'ania na kusisitiza vitu ambayo hata huyo Mungu sidhani kama huwa anavifikiria.

No wonder wanaweza kuchinja na kuua binadamu wenzao kama kuku kwa kisingizio cha Mungu as if Mungu hana uwezo wa kujilinda.
That aside:essence ya dini zote ni upendo,sasa iweje hawa wakristo na waislamu ambao kila upande unajidai kuuhubiri upendo na amani wasingelikaa chini na kuelewana tu kuhusu mazishi?
 
Nami nilikuwa nimeshindwa kuwashangaa hao wenzetu waislamu kwa kweli...hivi mko serious kweli mnagombea maiti ambayo hamkutokea hata kumuuguza marehemu?pia ni ugomvi usio na maana kuingia sehemu kuabudia na mapanga yaanai ni ufinyuu wa mawazo mlionaoo kabisaa......hamjui hata jinsi kufuatilia mambo..nimewashangaa na kuwaona watu wa ajabu kabisa...nendeni mkatafute watu walio hai na muwaingize msikitini sioo wafu...maana haitawasaidia lolote..amekufa na imani yake...ule mwili hauna lolote .......
 
Mi naona ingekuwa vizuri ungebadilisha title ya hii thread ili isomeke SHUTUMA DHIDI YA WAISLAM. Inaonekana kabisa kuwa nia na madhumuni ya hii thread ni kuwakusanya wana JF wooote wenye kuuchukia uislam sehemu moja.

Change title utapata wachangiaji wengi zaidi watakaofanya unalotaka.
 
Mkuu Mtumwa wa Allah! Sikuipeleka kwenye masuala ya dini kwa kuhofia hilo hilo. Hizi si shutuma dhidi ya waislamu bali watu wachache ambao wanadai ni wafuasi wa dini hiyo.Tatizo lako Mkuu, unaona muislamu yeyote ni malaika kwa hiyo hawezi kukosea! Ninachouliza mimi ni kwa nini katika jamii yetu (waislamu, wakristu, wasio na dini n.k)tunajitokeza sana mara mtu anapokufa lakini hatujitokezi wakati wa kuuguza? Kama jamii tunachangisha pesa nyingi kwa ajili ya tanga na wale wanaopenda kuzika kwao ndio usiseme. Lakini wakati mtu yu hai na anahitaji pesa za tiba, hatuonekani. usilazimishe mada ielekee unakotaka wewe. wenzako wako katika sehemu ya dini wanatoana ngeu. Hapa tuangalie kwa mapana zaidi bila kujali dini zetu. Unaweza hilo? Au unadhani kitendo cha hao wanaosema ni wenzio katika dini yako wana haki? Kugombea kuzika bila kuuguza?

Mimi nina rafiki na ndugu zangu waislamu na ninajua wengi wao wataona aibu kuhusishwa na vitendo kama hivi. nina rafiki zangu ambao walislimi na tuliwazika kama waislamu. Walipokuwa wana shida na walipokuwa wakiugua waislamu wenzao walishirikiana nasi kikamilifu kuuguza. Hawa hata jina la mtoto hawalijui na leo wanadai ati marehemu alikuwa mwenzao! Aibu tupu.
 
Binafsi sijawahi kuielewa hii dini ya Kiislamu,

really ni dini ya ajabu sana,wanang'ang'ania na kusisitiza vitu ambayo hata huyo Mungu sidhani kama huwa anavifikiria.

No wonder wanaweza kuchinja na kuua binadamu wenzao kama kuku kwa kisingizio cha Mungu as if Mungu hana uwezo wa kujilinda.

Namshukuru Allah hayo uliyoyataja ni maoni yako binafsi. Sasa naanza kusali tokea leo Allah asikupe urais wa Tanzania.
 
Fundi,

Makasisi wa leo vimeo sana.

Hizi itikadi za dini siku za leo zimedhihirisha udhaifu, hata ule ufahamu wa kawaida hawana akilini.Aliyekufa kafa,hata kama asipozikwa au azikwe VYOYVYOTE yeye binafsi hana analolifahamu.Hata kama atazikwa na jiji.Au kulikuwa na michango ya fedha ambayo makasisi walitegemea kupewa baada ya mazishi?
Nia kuu ni kuhifadhi mwili uliotoka udongoni na udongoni umerudi.
Sasa haya ya kugombea maiti yatoka wapi?
Inanikumbusha mwaka 1996 wakati wa ajali ya MV BKB,Maiti zilikuwa dili baada ya serikali kutangaza kifuta jasho,Wakati wa kutambua maiti pale uwanja wa Nyamagana.Matapeli walikuwepo pia,tena waliingia kwa huzuni na vilio viwanjani kutafuta maiti zilizokuwa zinaonekana hazina wenyewe ili wapate fwedha za kusafirishia ambazo zingesaidia kuganga njaa yao ya muda mfupi

Single D,unaposema Makasisi una maana watu gani? Hebu eleweka tafadhali kabla sijachangia kwenye hili..
 
Katika yote,wanadamu tunapaswa kubadilika na kuwa na mioyo yenye huruma zaidi katika kumtumikia Mungu,kwakuonyesha utayari wetu si tu katika kuzika, bali pia ktk kuelimisha (kujenga mshule bora), utabibu (kujenga mahospitali) na huduma nyingine za kijamii ambazo zitawafanya Wakristo na Waislam wazidi kukaa pamoja wakisubiri siku ya hukumu yao, badala ya kuelekeza nguvu zao kujenga uadui.

jamani Tupoteze muda mwingi kujenga madaraja ya kukuza uhusiano, na si kujenga kuta za kututenganisha.

Allah Akbar!
 
Mimi si muislam kwa Imani, lakini inapofika wakati mtu kuiponda Dini yoyote ile, kwa namna yoyote il;e naona gizani mbele kila mtu aheshimiwe kwa imani yake mauti,umwagaji damu hukaribia popote pale na machafuko ya DINI tuombe Mungu yasitupate hayo nawachukia wote wanaoponda Imani ya mtu iwe mkristo kwa Muislam au Muislamu kwa mkristo
 
Mimi si muislam kwa Imani, lakini inapofika wakati mtu kuiponda Dini yoyote ile, kwa namna yoyote il;e naona gizani mbele kila mtu aheshimiwe kwa imani yake mauti,umwagaji damu hukaribia popote pale na machafuko ya DINI tuombe Mungu yasitupate hayo nawachukia wote wanaoponda Imani ya mtu iwe mkristo kwa Muislam au Muislamu kwa mkristo

Mipasuko katika jamii inatokea si kwa sababu watu wachache wanakaa wakitukanana na kutupiana maneno ya chuki bali ni wale walio wengi wanapotazama vitendo hivyo bila kuvikemea. Kinachozungumziwa hapa si suala la dini bali ni hii ishu ya mtu ambaye hajahusika katika kuuguza kujitokeza dakika za mwisho na kugombea mwili kuuzika. Kwa bahati mbaya wako walio dini moja na wahusika na wanaangalia ishu nzima kwa misingi hiyo. Hadi hapo tutakapotoka kwenye kumtetea mtu kwa sababu tu ni mwenzetu, mipasuko haitaisha katika jamii yetu. Ni muhimu hali kama hizo zikijitokeza sisi wenzake tuweze kusimama na kusema wazi kuwa vitendo vya mwenzetu havituwakilishi sisi sote. kwa kufanya hivyo wale waovu wachache watashindwa kutugawa maana ukweli ni kuna mengi zaidi yanayotuunganisha kama jamii kuliko yanayotutofautisha.
 
Msimamo wangu ni kwamba naichukia sana migogoro ya kidini kwa sababu ugonvi wake mara nyingi huleta madhara makubwa ktk jamii.Enyi wakristu na waislamu kumbukeni kwamba hapa duniani sisi ni wakupita tu,sasa tunapogombana bila sababu za msingi kumbukeni ya kwamba tunamchukiza Mungu.

Mungu hakutuleta duniani kuja kulumbana juu ya imani zetu ila tuishi kwa kupenndana.Mimi naungana na hukumu iliyotolewa kwamba imezingatia masuala ya msingi katika kufikia maamuzi yake.Jamii ijifunze mambo haya na yasiwe yakujirudiarudia kwangu naona kama yanatia aibu.

Chanzo cha migogoro hii ni vijimambo vidogodogo tu na hii inaonyesha kwamba kuna watu wa imani fulani wanaona wao ni best kuliko wenzao,hii ni imani potofu.Hii ni siri ya Mungu.
 
Chanzo cha migogoro hii ni vijimambo vidogodogo tu

Ni hivi vijambo vidogo vidogo ndivyo vinavyoleta matatizo. Ndiyo maana vinapojitokeza tusivionee aibu kuvikemea. Hili suala zima ni la kipuuzi lakini kuna watu wanaotaka kulitumia kuwachonganisha waumini wa dini hizo. Marehemu ameugua, amekufa na hukumu imetolewa. Basi aachiwe akapumzike bila kusumbuliwa. Hao wenye mapenzi naye waende kuweka maua kwenye kaburi lake na kumuombea dua kwa mwenyezi Mungu ili amweke mahali pema peponi. Kazikwa vipi, aachiwe muumba wake kuhukumu.
 
Mbalamwezi
Ninaposema makasisi nimemaanisha Viongozi wote wa dini k.m padri,mchungaji,askofu,shehe,imam,mukhtari n.k.Nadhani waweza kuendelea sasa
 
Naona wengine wanafanya unafiki wa kuchukua neutral position hapa. Mimi sina neutral position, wala sitaki unafiki, hao wanaojiita waislamu hawakutenda haki hata kidogo kwa kitendo chao cha kuwavamia watu walioko kwenye huzuni ya msiba na kuwafanyia fujo. Ni tabia chafu inayoonesha kuwa wao ni genge la watu wasiokuwa na hata chembe ya huruma wala ubinadamu, na ni aibu kabisa kuwahusisha watu wa aina hii na Mungu. Yaani kuwahusisha watu waovu kama hawa na Mungu ni sawa na kumtukana huyo Mungu. Wanastahili kulaaniwa kwa nguvu zote. Na tena wale wafiwa walioathirika kwa kitendo hiki wanastahili fidia kwa maumivu ya kisaikolojia walioyapata. Nawashauri sasa wafungue kesi ya madai kufidia gharama za ziada walizoingia, kuzidishiwa muda wa msiba, na manyanyaso yote waliyoyapata.
 
Tatizo ni ufinyu wa mawazo tu,kugombaniana maiti wala hakuchangii kwa namna yoyote kukuza imani ya mtu au kumfikisha kwa mungu.mtu amekufa amekufa hata angezikwa na waislamu,hata angezikwa na wakristo kama ilivyofanywa sula linabaki imani yake marehemu binafsi wala sio ya wazikaji.Haka kamchezomchezo haka kanelekea kukua tanzania,nadhani kanapaswa kumalizwa.Kama watu wana hamu sana na wema wa kuzika ili kupata dhawabu kwa mungu,niwaulizeni,watu wangapi tena wenye dini au waislamu au wakristo wanafariki humo muhimbili,mwananyamala,temeke,mererani na kwingineko na hajitokezi mtu kuwazika hadi halmashauri zinaamua kuzika?au hata matangazo kutolewa redioni watu waje tambua marehemu?haya mambo ya kupenda umaarufu na kushindana bila sababu ndio yanayoleta matatizo.Hizi mie huwa naziita siasa za dini.
 
Naona wengine wanafanya unafiki wa kuchukua neutral position hapa. Mimi sina neutral position, wala sitaki unafiki, hao wanaojiita waislamu hawakutenda haki hata kidogo kwa kitendo chao cha kuwavamia watu walioko kwenye huzuni ya msiba na kuwafanyia fujo. Ni tabia chafu inayoonesha kuwa wao ni genge la watu wasiokuwa na hata chembe ya huruma wala ubinadamu, na ni aibu kabisa kuwahusisha watu wa aina hii na Mungu. Yaani kuwahusisha watu waovu kama hawa na Mungu ni sawa na kumtukana huyo Mungu. Wanastahili kulaaniwa kwa nguvu zote. Na tena wale wafiwa walioathirika kwa kitendo hiki wanastahili fidia kwa maumivu ya kisaikolojia walioyapata. Nawashauri sasa wafungue kesi ya madai kufidia gharama za ziada walizoingia, kuzidishiwa muda wa msiba, na manyanyaso yote waliyoyapata.

Hakuna aliye mnafiki humu ndani Mkuu.

Tatizo ni kuwa katika jamii yetu tunaogopa kuwakemea wale wanaojificha nyuma ya ngao ya dini. Mimi ningetegemea wale walio dini moja na huyu shehe wawe mstari wa mbele kumweleza kuwa anayofanya yanawa aibisha kama wanadini wenzake. Watu kama hawa wakiona kuwa hawana support hata katika wale ambao wanadhani wanawatetea kwa matendo yao yasio na maana wataacha kuyafanya. Kukaa kimya kwa kuogopa kumsema ndugu yao hakusaidii kitu bali kunajenga imani katika wale wasio itakia mema dini yao kuwa wote wako vile.

Wakristu nao inabidi tuelewe kuwa kwa jinsi uislamu ulivyo, hakuna central authority, kwa hiyo huyu shehe hawezi kuwakilisha dini au waislamu wote. Tusipende kuhukumu dini nzima kutokana na vitendo vya mmoja wao. Na sisi vile vile anapotokea mmoja kati yetu akatenda vitendo vya uovu naye akemewe pasipo kusita.

Kama jamii inatubidi tuukatae uovu wowote bila kuangalia dini ya mtu, kabila lake au jinsia yake. Kwa kufanya hivi, naamini tutaepusha shari itakayoweza kutokea hapo baadae.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom