Uganda yawashikilia wanyarwanda kwa tuhuma za upelelezi (spy)

Hii habari nimeona kwa kifupi kwenye tv kwamba Museveni amegoma kuudhuria mkutano wa mambo ya uchumi utaofanyika nchini Kigali
Hahah Museveni aangalie,asije akatolewa hapo ikulu na PK kichwa chini miguu juu
 
Hivi karibuni Uganda imeingia katika mgogoro wa kidiplomasia baada ya Uganda kukamata raia wa Rwanda kwa tuhuma za uspy/upelelezi katika nchi ya Uganda.Chanzo DW juzi.

Kwa taarifa hii imenifanya kutafakari nakuanza kuamini kuwa Rwanda imedhamiria kuwa Taifa lenye nguvu katika Afrika.

Pia nimekumbuka post moja hapa jf kuwa Rwanda inatumia wanawake zao wazuri katika kufanya upelelezi wao Tz

Pia nakumbuka post hapa jf kuwa wakati wa Bunge Dodoma huonekana wanawake wengi wakinyarwanda wakijiuza.

Pia nakumbuka juu ya post moja hapa Jf kuwa inawezekana Jeshi la Rwanda ndilo lililoshambulia wanajeshi wa Tanzania nchini Congo kwa mwamvuli wa waasi wa kongo.

Lakini pia nakumbuka kuwa Congo amewahi kuwashutumu Rwanda kuwa inafadhili waasi wa Congo kwaajili ya kuvuna rasilimali madini ya Congo

Lakini pia nakumbuka kuuwawa kwa mpinzani wa Kagame nchini Afrika kusini Hotelini jinsi mataifa mengine walivyoinyooshea mkono Rwanda kuwa imehusika.

Mwisho nchi hii imetangaza wazi kuwa wao ni rafiki wa Israel na wanashirikiana kwa karibu.Hii inaonyesha Rwanda ni nchi inayojizatiti sana katika maswala ya usalama na udukuzi

TANZANIA IKAE VIZURI
Usiwe mwepesi wa kutekwa na maigizo ya mashosti wawili. Museveni - Kagame - Kabila ni umoja imara usioyumba. Wenye ufahamu tunaelewa lengo la kiini macho hicho.
 
Kaa ukijua kila taifa lina mashushushu wake nchi nyingine kwa kazi maalumu iliyokusudiwa, kwa nchi zinazopakana ni kawaida, hata tz ina mashushushu wake nchi walizokusudia kupata taarifa kusudiwa,
Haya ndo maisha!!
Kweli Mkuu
 
Hahaha!! Kabisa mkuu.

Niliona clouds habari nikashangaa sana. Wakati ni watu walikuwa karibu sana
Hahah hao jamaa hata sijawahi kuelewa kama kweli ni washkaji au wanachorana tu.

Wao kugombana na kupatana ni sehemu yao ya maisha hahah.
 
Usiwe mwepesi wa kutekwa na maigizo ya mashosti wawili. Museveni - Kagame - Kabila ni umoja imara usioyumba. Wenye ufahamu tunaelewa lengo la kiini macho hicho.
Bila shaka hufahamu kama walishawahi kupigana kongo huyo Mseveni na Kagame mpk wakaenda kusuluhishwa na Malkia Elizabeth.
 
Back
Top Bottom