Uganda yaahirisha uzinduzi wa mradi wa bomba la mafuta kuomboleza kifo cha Rais wa zamani wa Tanzania

Miss Zomboko

JF-Expert Member
May 18, 2014
4,492
9,265
Uganda imeahirisha uzinduzi wa mradi wa Bomba la Mafuta Ghafi la Afrika Mashariki (EACOP) ili kuomboleza kifo cha Rais wa zamani wa Tanzania hayati John Pombe Magufuli, ambaye alitoa mchango mkubwa katika mchakato wa mradi huo.

Mamlaka ya Petroli ya Uganda (PAU) jana ilitoa taarifa ikisema kuwa uzinduzi huo umeahirishwa hadi mwezi ujao.

Taarifa iliyotolewa na Mamlaka hiyo imesema, uongozi mahiri wa hayati Rais Magufuli uliweka msingi thabiti kwa mradi huo, ikiwemo makubaliano kati ya serikali ya nchi hizo mbili yaliyofikiwa mwaka 2017 na makubaliano ya Serikali ya Tanzania katika mwaka jana.
 
Uganda imeahirisha uzinduzi wa mradi wa Bomba la Mafuta Ghafi la Afrika Mashariki (EACOP) ili kuomboleza kifo cha Rais wa zamani wa Tanzania hayati John Pombe Magufuli, ambaye alitoa mchango mkubwa katika mchakato wa mradi huo.

Mamlaka ya Petroli ya Uganda (PAU) jana ilitoa taarifa ikisema kuwa uzinduzi huo umeahirishwa hadi mwezi ujao.

Taarifa iliyotolewa na Mamlaka hiyo imesema, uongozi mahiri wa hayati Rais Magufuli uliweka msingi thabiti kwa mradi huo, ikiwemo makubaliano kati ya serikali ya nchi hizo mbili yaliyofikiwa mwaka 2017 na makubaliano ya Serikali ya Tanzania katika mwaka jana.
sijaelewa, uzinduzi kwa maana gani. kama uzinduzi tulishauona kule tanga na uganda. hapa wanazindua nini
 
Back
Top Bottom