#COVID19 Uganda: Wawili wapigwa risasi kwa kukiuka amri ya Rais ya kutotumia usafiri wa umma

Luqman mohamedy

JF-Expert Member
Jul 24, 2016
892
1,226
Capture.PNG

Mmoja wa waliopigwa risasi, Alex Olyem. Picha na Jessica Sabano/Daily Monitor
Watu wawili wamelazwa hospitalini baada ya kupigwa risasi na maafisa wa polisi waliopelekwa kusimamia amri ya Rais Museveni ya kuzuiwa kwa usafiri wa umma kwa nia ya kukinga kuenea kwa ugonjwa wa COVID-19.

Alex Olyem na Kasim Ssebude ambao kwa sasa wamelazwa katika hospitali kuu ya Mukono, walipigwa risasi wakati wakiwa wanaendesha pikipiki katika eneo la Goma Manispaa ya Mukono.

Oryem alipigwa risasi mguu wakati Ssebude alipigwa risasi tumboni. Wawili hao ambao ni wajenzi walikuwa wakisafiri kutoka Seeta kwenda Namugongo wakati walipokumbana na polisi.

Polisi waliwatuhumu kwa kupuuza maagizo ya Rais, ingawa Bw. Oryem alisema kwamba hakujua maagizo ya rais kwa sababu hakuangalia habari Jumatano jioni wakati Rais Museveni akitangaza hatua mpya za kuzuia kuenea kwa coronavirus.

========

Two people are admitted to hospital after they were shot by police officers deployed to enforce President Museveni’s suspension of public transport in a bid to prevent the spread of coronavirus.

Alex Olyem and Kasim Ssebude who are currently admitted to Mukono general hospital were shot while riding on a motorcycle in Goma Division Mukono Municipality.

Oryem was shot in the leg while Ssebude was shot in the stomach. The two construction workers were travelling from Seeta to Namugongo when they were intercepted by police.

Police accused them of defying the presidential directives.

Oryem told Daily Monitor that he was unaware of the presidential directives because he did not watch news on Wednesday evening when President Museveni announced the new preventive measures against the spread of coronavirus.

The president said boda boda cyclists would not be allowed to transport passengers.

"As we were going to work, we met two officers who blocked us and blamed us for being two on a motorcycle. When we tried to ask the officers what offence we had committed, they just started shooting at us," Oryem said.

They said the police officers first shot two bullets in the air before shooting at them.

Kampala metropolitan police spokesperson, Mr Patrick Onyango, said the two were shot after they allegedly tried to attack a police officer.

“After police stopped them, they tried to attack our officers. He first fired warning shots in the air. People should not defy presidential directives aimed at preventing the spread of coronavirus in Uganda,” he said.

Uganda has so far confirmed 14 cases of coronavirus pandemic which has wreaked havoc in different parts of the world.


Source: Daily Monitor

=======

MAONI YANGU:

Nimeangalia video za India wakitumia fimbo ila Africa wanapiga cha moto.

Naeza kusema hii inatokana na kukosa stock ya chakula muda huo wa quarantine.

Niliwahi kusema njaa ni mbaya kuliko corona.Huwezi kumfungia mwenye njaa ndani akatulia.

Viongozi wa Africa ni tatizo zaidi ya Corona
 
Serikali za kipumbavu kama hizi ni tatizo kuliko corona!

Watu hawawezi kufa njaa kisa corona yenu hiyo! A manufactured disease from the factory!

Acha watu watafute riziki! Au wape wewe chakula wale!

Damn! Huyo museven anatakiwa atolewe kwa wananchi wamchane chane hiyo sura ili ajifunze kuwa na utu na awaachie waganda nchi yao!

Jitu zee lakini nalo limo tu! Age mate zake wote wanapunga upepo majumbani na wajukuu zao lakini lenyewe limo tu linang'ang'ana na dunia!
 
Wenzetu wakikukuta barabarani bila sababu za msingi wanakuchapa bakora au kukupiga virungu au wanakupeleka jela kwa muda wa miezi ila sisi Africa acha tuuane tu maana hakuna namna. Ndo akili zetu zilivyo na zinavyotutuma maana rai kwao si kitu.
 
Si unawaacha wafe kwani wataisha kwa corona?

Sent using Jamii Forums mobile app
Hapana mkuu.

Hao wote unaowaona hapo wakishaambukizana watarudi majumbani mwao. Wengi wana familia za watu wanne watano hadi kumi.

Wengine watoto walio na ndoto za kuishi baadae watawaambukiza na kuwaua.

Pili, huna haki ya kujiua jamii tunakuhitaji, kuna watu wanaishi kukutegemea wewe.
 
Two people are admitted to hospital after they were shot by police officers deployed to enforce President Museveni’s suspension of public transport in a bid to prevent the spread of coronavirus.

Alex Olyem and Kasim Ssebude who are currently admitted to Mukono general hospital were shot while riding on a motorcycle in Goma Division Mukono Municipality.

Oryem was shot in the leg while Ssebude was shot in the stomach. The two construction workers were travelling from Seeta to Namugongo when they were intercepted by police.

Police accused them of defying the presidential directives.

Oryem told Daily Monitor that he was unaware of the presidential directives because he did not watch news on Wednesday evening when President Museveni announced the new preventive measures against the spread of coronavirus.

The president said boda boda cyclists would not be allowed to transport passengers.

"As we were going to work, we met two officers who blocked us and blamed us for being two on a motorcycle. When we tried to ask the officers what offence we had committed, they just started shooting at us," Oryem said.

They said the police officers first shot two bullets in the air before shooting at them.

Kampala metropolitan police spokesperson, Mr Patrick Onyango, said the two were shot after they allegedly tried to attack a police officer.

“After police stopped them, they tried to attack our officers. He first fired warning shots in the air. People should not defy presidential directives aimed at preventing the spread of coronavirus in Uganda,” he said.

Uganda has so far confirmed 14 cases of coronavirus pandemic which has wreaked havoc in different parts of the world.
 
Mnasahau aliempiga risasi siyo M7 au kimbaombao wa Rwanda bali ni rai mwenzao ambaye kavaa mangwanda ya polisi.

Sipendi uongozi wa kimabavu wa huko Uganda na Rwanda lakini hata jamii inachangia sana kutengeneza Polisi na raia wenye akili za kupenda kutumia mabavu na kuvunja sheria.
 
Hapana mkuu.

Hao wote unaowaona hapo wakishaambukizana watarudi majumbani mwao. Wengi wana familia za watu wanne watano hadi kumi.

Wengine watoto walio na ndoto za kuishi baadae watawaambukiza na kuwaua.

Pili, huna haki ya kujiua jamii tunakuhitaji...kuna watu wanaishi kukutegemea wewe.
Sasa watu watakula nini wewe? Unafikiri watu wanatoka tu nje ili kufanya adventure!?

Nchi nyingi za kimasikini za Afrika wananchi wanaishi kwa kutafuta kama ndege! Hauwezi kumwambia mtu akae ndani atakula wapi?

Ndio maana magufuli anawapuuza tu ninyi wapiga kelele mitandaoni!

Watu wanahitaji kufanya kazi wale na maisha yaendelee!

Eti kaa ndani? ebo!
 
Sasa watu watakula nini wewe? Unafikiri watu wanatoka tu nje ili kufanya adventure!?

Nchi nyingi za kimasikini za Afrika wananchi wanaishi kwa kutafuta kama ndege! Hauwezi kumwambia mtu akae ndani atakula wapi?

Ndio maana magufuli anawapuuza tu ninyi wapiga kelele mitandaoni!

Watu wanahitaji kufanya kazi wale na maisha yaendelee!

Eti kaa ndani? ebo!
Hilo suala ni tata saana ila mwisho wa siku kukaa ndani ndiyo suluhisho pekee la kujikinga.

Halihitaji kujadiliwa kwa jazba na mbwembwe za matusi.

Kun mawili kuchagua ugonjwa ambao mwisho kifo ama kukaa ndani.

Taratibu zingine zinaweza kufanyika kupunguza adha ya njaa ila sio kukaidi amri.
 
Viongozi wa Africa ni mambulula wao hawaijui njaa pumbavu zao kazi kuiga iga tu sasa unaweka watu wasitoke ndani umetengeza mazingira ya watu wasiende kufanya kazi? Chakula utawapa wewe? Huo ugonjwa na na njaa kipi kibaya? Kama kweli mnaakili na mnajali watu wenu kwa nini msipitishe vyakula na maji watu watakaa ndani ata mwaka mkitaka. Pumbavu zenu mkishapata mishahara mnasahau kuna watu wana njaa kibao.

Hamtoi ajira rasmi wanapiga mishen town akipata elfu 5 anakuka analala kesho atatafta tena elfu tano hakuna cha akiba wala nini na hayo ndo maisha ya wananchi wenu karibu wote yaani haya majamaa wanadhania sijui kila mwananchi ana akiba ya mabilioni kama wao sitashangaa na huku kwetu wakiiga maana akili zao ni moja


Sent using Jamii Forums mobile app
 
7 Reactions
Reply
Back
Top Bottom