jerryempire
JF-Expert Member
- Jan 4, 2017
- 5,091
- 8,547
Habari wana jamvi,
Niende kwenye mada hasa nikibase kwenye historia ya Idd Amin aliyekuwa Rais wa Uganda.
Historia inamtafsiri Iddi Amin kama raisi katili kutokea katoka katika nchi ya Uganda ambae alitolewa kwa mapinduzi na majeshi ya Tanzania baada ya kuvamia mkoa wa Kagera na kudai kuwa ni sehemu ya Uganda, na kukimbilia uhamishoni Saudi Arabia hadi pale kifo kilipompata mwaka 2003. Vyombo vya kimataifa vilimtangaza Idd Amin kama Rais katili Africa kiasi cha kutungiwa mpaka filamu zenye kuonyesha ukatili wa kutisha wa Amin mpaka kufikia hatua ya kula nyama za watu.
Leo hii serikali ya Uganda inafanya maadhimisho ya kumkumbuka Rais Idd Amin kama Rais shujaa na mwanamapinduzi ambae na mwanaharakati ambae alipigania wananchi wake katika kupata maendeleo yao.
Shirika la BBC swahili limekutana na watu ambao walikuwa wakifanya kazi na kuishi ndani ya serikali ya Idd Amini na kumsifia kuwa alikuwa ni Rais mwenye huruma na wananchi wake isipokuwa kulikuwa na baadhi ya askari wake waliokuwa wanatumia vibaya madaraka waliyopewa na Idd Amini, hivyo serikali na umoja huo wa watu waliokuwepo kwenye utawala wa Idd Amin wamezindua maadhimisho/maonyesho yakiambatana na makumbusho ambayo itakuwa inatoa historia halisi ya Rais Idd Amin kama Rais shujaa wa nchi ya Uganda
Je historia ya Rais Idd Amin wa Uganda na kisa halisi cha vita ya Kagera vilipindishwa?
Niende kwenye mada hasa nikibase kwenye historia ya Idd Amin aliyekuwa Rais wa Uganda.
Historia inamtafsiri Iddi Amin kama raisi katili kutokea katoka katika nchi ya Uganda ambae alitolewa kwa mapinduzi na majeshi ya Tanzania baada ya kuvamia mkoa wa Kagera na kudai kuwa ni sehemu ya Uganda, na kukimbilia uhamishoni Saudi Arabia hadi pale kifo kilipompata mwaka 2003. Vyombo vya kimataifa vilimtangaza Idd Amin kama Rais katili Africa kiasi cha kutungiwa mpaka filamu zenye kuonyesha ukatili wa kutisha wa Amin mpaka kufikia hatua ya kula nyama za watu.
Leo hii serikali ya Uganda inafanya maadhimisho ya kumkumbuka Rais Idd Amin kama Rais shujaa na mwanamapinduzi ambae na mwanaharakati ambae alipigania wananchi wake katika kupata maendeleo yao.
Shirika la BBC swahili limekutana na watu ambao walikuwa wakifanya kazi na kuishi ndani ya serikali ya Idd Amini na kumsifia kuwa alikuwa ni Rais mwenye huruma na wananchi wake isipokuwa kulikuwa na baadhi ya askari wake waliokuwa wanatumia vibaya madaraka waliyopewa na Idd Amini, hivyo serikali na umoja huo wa watu waliokuwepo kwenye utawala wa Idd Amin wamezindua maadhimisho/maonyesho yakiambatana na makumbusho ambayo itakuwa inatoa historia halisi ya Rais Idd Amin kama Rais shujaa wa nchi ya Uganda
Je historia ya Rais Idd Amin wa Uganda na kisa halisi cha vita ya Kagera vilipindishwa?