Uganda kuidhinisha Kiswahili kama lugha ya pili baada ya Kingereza - Wakenya fursa hizooo

Angalia ulichoandika hapa, aisei mna matatizo sana ya kiufasaha, huzingatii alama za uakifishaji, Kiswahili chenyewe kibovu, mnatia huruma sana nyie, Kingereza kimewashinda, uandishi wenu wa Kiswahili unatia kinyaa, lugha za asili ndio hata hamjui salamu.
Lugha za asili wanazielewa Ila wanajifanya tu, ukitembea mikoani utasikia wakizungumza ,sasa Kiswahili ni janga kwao wapwani wapo Sawa lakini wabara hata usiseme wanatia huruma kweli.
 
Katiba ya Kenya imetamka wazi wazi kwamba lugha ya taifa Kenya ni Kiswahili, hakuna mahali popote katika katiba yenu panaposema lugha rasmi ya shughuli za serikali ni Kiingereza, acha uongo.

60% ya wakenya hawakifahamu kiingereza kwa ufasaha, sasa kama serikali lugha yake rasmi ni kiingereza, serika ya Kenya ni kwa ajili ya 40% pekee?
I will put it in English , official language in Kenya is English and national language is Swahili.
 
Hivi wakenya ni lugha gani wanaeza toka kifua mbele na kujidai wanajua kuizungumza bila kuchanganya labda lugha zao za asili.
Hawa majirani huwa wananishangaza sana. Wanajikutaga wajuaji sana wakati huwa ni mapoyoyo tu ambao mpaka leo bado yako chini ya ukoloni.

Mkenya anajivunia kuijua lugha ya kingereza kukiko hata muingereza mwenyewe.

Ukiskiliza maprofesa wao wakiwa wanaongea wanavyopachika misamiati migumu, mpaka mtu unajiuliza hivi huyu anatafuta sifa ama!? Maana hata akina Theresa May ambao ndio wenye lugha hii hawafanyagi huu upuuzi kwenye speech zao.

Cha ajabu zaidi hawa hawa wakenya wanaojinasibu kuwa wajuvi wa lugha hii ukiwakuta kwenye maongezi yao hawawezi kuongea sentensi tano bila kuchanganya neno la kiswahili(tena kibovu) halafu hapo hapo hawaishi kutunanga kwamba hatujui kiswahili wala kiingereza sababu tunaongea sana kiswangilish, wakati wao wenyewe ndio waongeaji wazuri wa hicho kiswanglish.

Halafu sasa hata hicho kingereza chenyewe wanavyoyatamka matamshi yake baadhi utatamani uombe subtitle yaani ni vituko vituko. Kiufupi hawa jamaa hawana lugha wanayopaswa kujivinia kati ya hizi mbili maana bado ni wagonjwa wa lugha zote mbili, afadhari hata Tanzania katika ya hizi ligha mbili ni moja tu ndio inayotupa shida.
 
Hata Kiswahili pia hawajui, "Kenya is a confused country as far as language is concern, the same for Uganda"
Ukija Kenya utapata kila Mkenya yaani takriban 95%, kwa kukisia, ya Wakenya wanaongea kiswahili lakini Wakenya wanaozungumza kingereza majumbani mwao hawajapita asilimia hamsini. Pengine useme kiswahili cha Kenya sio kizuri kama cha Tanzania, lakini usiseme kwamba Wakenya hawakipendi Kiswahili.
 
Katiba ya Kenya imetamka wazi wazi kwamba lugha ya taifa Kenya ni Kiswahili, hakuna mahali popote katika katiba yenu panaposema lugha rasmi ya shughuli za serikali ni Kiingereza, acha uongo.

60% ya wakenya hawakifahamu kiingereza kwa ufasaha, sasa kama serikali lugha yake rasmi ni kiingereza, serika ya Kenya ni kwa ajili ya 40% pekee?
Mwananchi akitaka huduma ya serikali na haelewi kingereza bila Shaka atatafsiriwa na yule anaemhudumia na ndio maana pia tuna habari za saa moja Kwa wale ambao hawaelewi kingereza na saa tatu Kwa wasomi.
 
I will put it in English , official language in Kenya is English and national language is Swahili.
Show me in this world, a country which uses official language in their daily government activities instead of its national language.

Kenyan national currency is Ksh. But $ is official language, why don't you use $ in your daily transaction instead of Ksh?.
 
Uandishi wa Kiswahili ni changamoto sana kwa Watanzania, ukizingatia huwa hamjui kuongea au kuandika kwa lugha nyingine yoyote, hata zenu za asili hamzijui, mnatia huruma.
Nina vijana wangu wanasoma Kampala shule Fulani,hapo pana mwalimu wa kiswahili kutoka Kenya,kama pana shida kubwa ya kiswahili ni hapo shuleni maana kiswahili kinachozungumzwa na kufundishwa na Huyo mwalimu ni majanga matupu hadi inatia huruma kwa wanafunzi hao wanaopenda kujua kiswahili kisha wafundishwe na mwl zuzu kiasi kile,mwl yule akafanya makosa ya wakati Fulani kuwapa kipindi vijana wale wa ki Tz kuwafundisha wenzao hapo ndipo alipozodoka maana wanafunzi wale hawakupenda tens wafundishwe na mwl yule. Kwa ujumla wenzetu wakenya kiswahili in lugha yenu imewafaa muitumie lakini hamuijui.Miaka hii ya karne tuliyomo kujisifia kujua lugha isiyo ya taifa lako (English) in uzuzu mwingine mkubwa kwa nini usijisifie kikaramajong! Waangalie Wajapan,Wachina,Wakorea, Wahindi no wachache kwa kutaja .Zama za ushamba zimepita wana EA tujenge chetu.
 
Ukija Kenya utapata kila Mkenya yaani takriban 95%, kwa kukisia, ya Wakenya wanaongea kiswahili lakini Wakenya wanaozungumza kingereza majumbani mwao hawajapita asilimia hamsini. Pengine useme kiswahili cha Kenya sio kizuri kama cha Tanzania, lakini usiseme kwamba Wakenya hawakipendi Kiswahili.
Kama wakenya wanaoelewa kiingereza ni chini ya 50%, vipi rais na viongozi wengine wa serikali wanapotoa hotuba kwa taifa zima wanatumia kiingereza, ina maana wanawatenga wakenya walio wengi na kuwathamini wachache wenye kujua kiingereza?. Tukisema Kenya haiwajali wananchi wa ngazi za chini tunakosea?
 
Kama wakenya wanaoelewa kiingereza ni chini ya 50%, vipi rais na viongozi wengine wa serikali wanapotoa hotuba kwa taifa zima wanatumia kiingereza, ina maana wanawatenga wakenya walio wengi na kuwathamini wachache wenye kujua kiingereza?. Tukisema Kenya haiwajali wananchi wa ngazi za chini tunakosea?
Ni kweli kwa kiwango fulani. Kumbuka sio kila Mkenya amesoma. Ili mtu aelewe kingereza lazima awe na masomo ya kutosha. Pengine hadi darasa la sita, kwa kukisia tu, ila sio kila Mkenya amefika kiwango hicho cha masomo. Kumbuka kuhusu kiswahili kila mtoto wa miaka miwili au mitatu anakiongea bila shida. Halafu siku hizi watoto wanaongea kiswahili na kingereza bila kuongea lugha ya mama. Kwa mfano watoto wa jamii za Kenya kwa mfano ya kikuyu, Luhya, na nyingine hawajui kuongea lugha hizo. Ina uzuri wake na ubaya wake. Uzuri ni kuwa inapunguza ukabila, ubaya ni kuwa inatenga hao watoto kutoka kwa watu wao ambao pengine hawajui lugha nyingine isipokuwa ya mama. Kwa mfano babu au nyanya anayezungumza lugha ya mama pekee anaweza kosa kuelewana na mtoto anayezungumza kiswahili na kingereza pekee. Lakini katika sherehe za kitaifa hotuba rasmi hutolewa kwa kingereza halafu baadaye rais anatafsiri kwa kiswahili .
 
Ukiongea kingereza kenya ndo utaonekana una IQ kubwa, intelligence nk
Lakini njaa haijui lugha.

Hawa majirani huwa wananishangaza sana. Wanajikutaga wajuaji sana wakati huwa ni mapoyoyo tu ambao mpaka leo bado yako chini ya ukoloni.

Mkenya anajivunia kuijua lugha ya kingereza kukiko hata muingereza mwenyewe.

Ukiskiliza maprofesa wao wakiwa wanaongea wanavyopachika misamiati migumu, mpaka mtu unajiuliza hivi huyu anatafuta sifa ama!? Maana hata akina Theresa May ambao ndio wenye lugha hii hawafanyagi huu upuuzi kwenye speech zao.

Cha ajabu zaidi hawa hawa wakenya wanaojinasibu kuwa wajuvi wa lugha hii ukiwakuta kwenye maongezi yao hawawezi kuongea sentensi tano bila kuchanganya neno la kiswahili(tena kibovu) halafu hapo hapo hawaishi kutunanga kwamba hatujui kiswahili wala kiingereza sababu tunaongea sana kiswangilish, wakati wao wenyewe ndio waongeaji wazuri wa hicho kiswanglish.

Halafu sasa hata hicho kingereza chenyewe wanavyoyatamka matamshi yake baadhi utatamani uombe subtitle yaani ni vituko vituko. Kiufupi hawa jamaa hawana lugha wanayopaswa kujivinia kati ya hizi mbili maana bado ni wagonjwa wa lugha zote mbili, afadhari hata Tanzania katika ya hizi ligha mbili ni moja tu ndio inayotupa shida.
 
Mwananchi akitaka huduma ya serikali na haelewi kingereza bila Shaka atatafsiriwa na yule anaemhudumia na ndio maana pia tuna habari za saa moja Kwa wale ambao hawaelewi kingereza na saa tatu Kwa wasomi.
Sasa kwanini msitumie lugha yenu ya taifa pekee ambayo ndio inayoeleweka na wengi, hii habari ya mtu kufafsiriwa ndani ya nchi yake inakuaje?
 
Sasa kwanini msitumie lugha yenu ya taifa pekee ambayo ndio inayoeleweka na wengi, hii habari ya mtu kufafsiriwa ndani ya nchi yake inakuaje?
Any Kenyan mwenye amepitia shule anaelewa English. Some may not be able to use it fluently in a conversation but trust moi, they understand. They get the message
 
Yaani umesema lugha ambayo wakenya wengi wanaielewa ni kiswahili alafu viongozi wenu wakiwa wanazungumza na wananchi Wanatumia kingereza alafu kuna watu wanatafsiri kwa kiswahili ili "hadhira" waelewe,
Naomba unijibu hapa, kwanini wasitumie lugha ya kiswahili ili wakenya wasiojua kingereza waelewa kwa ufasaha kuliko kutafsiriwa tena?
Note: Hadhira ni watu wanaotarajiwa kupokea Ujumbe.
Ni kweli kwa kiwango fulani. Kumbuka sio kila Mkenya amesoma. Ili mtu aelewe kingereza lazima awe na masomo ya kutosha. Pengine hadi darasa la sita, kwa kukisia tu, ila sio kila Mkenya amefika kiwango hicho cha masomo. Kumbuka kuhusu kiswahili kila mtoto wa miaka miwili au mitatu anakiongea bila shida. Halafu siku hizi watoto wanaongea kiswahili na kingereza bila kuongea lugha ya mama. Kwa mfano watoto wa jamii za Kenya kwa mfano ya kikuyu, Luhya, na nyingine hawajui kuongea lugha hizo. Ina uzuri wake na ubaya wake. Uzuri ni kuwa inapunguza ukabila, ubaya ni kuwa inatenga hao watoto kutoka kwa watu wao ambao pengine hawajui lugha nyingine isipokuwa ya mama. Kwa mfano babu au nyanya anayezungumza lugha ya mama pekee anaweza kosa kuelewana na mtoto anayezungumza kiswahili na kingereza pekee. Lakini katika sherehe za kitaifa hotuba rasmi hutolewa kwa kingereza halafu baadaye rais anatafsiri kwa kiswahili .
 
Kama wakenya wanaoelewa kiingereza ni chini ya 50%, vipi rais na viongozi wengine wa serikali wanapotoa hotuba kwa taifa zima wanatumia kiingereza, ina maana wanawatenga wakenya walio wengi na kuwathamini wachache wenye kujua kiingereza?. Tukisema Kenya haiwajali wananchi wa ngazi za chini tunakosea?
Kuna difference ya 'kuelewa' na 'kuzungumza'. Less that 50% ya kenyans are fluent but a huuuge number do understand English. They cannot speak but wanaelewa coz everything here is taught in English.
 
Hauwezi ukaijua lugha bila kuitumia, tena ukubwani, yaani unakumbana na Kingereza kuanzia kidato cha kwanza, halafu haukitumii kwenye mawasiliano, hicho kidogo unachofundishwa kinakutoka mara moja.
Lugha yoyote ile lazima uitumie mara kadhaa ndio uje kuimudu. Mpo ovyoo sana kingereza watu wa ze ze ze, na hata Kiswahili uandishi wenu ovyoo sana.
Hamna lugha hata moja mliyoimudu, hadi zenu za asili, asilimia kubwa kati yenu hamjui hata salamu kwa lugha zenu za asili.
Kwahiyo ndo unataka kusema nini?! Kwamba Wakenya Kiingereza ni your mothertongue language, au?! Angalia Kiingereza chenu kilivyo na strong accent... nini ile kama sio kuathiriwa na lugha zenu za asili halafu hapa unataka kufunga watu kamba kwamba mnaanza kuongea Kiingereza tangia mkiwa watoto wachanga?!

Kwamba kukitumia Kiingereza mara kwa mara... tutumie mara kwa mara kwa sababu zipi wakati tuna lugha yetu iliyounganisha Watanzania wote kuanzia mijini hadi vijijini??!! Kwetu sisi ni ushamba na ulimbukeni upo home au mtaani halafu unaongea Kiingereza!

Na kwa kukuthibitishia Watanzania hawana shobo na English, sasa wewe nenda zako mbele kisha kaa huko hata miaka 10 halafu ukirudi ujifanye ukifahamu Kiswahili uone! Kwa mfano wa haraka, hebu wasome wan-JF hapa walivyokuwa wanamkejeli Hasheem Thabeet:-
Hapa chini tunaona moja ya blogs maarufu Bongo ilikuwa inampa za uso mmoja wa Watanzania "asiyejua kuzungumza Kiswahili sawasawa"!
Wema.png


Lakini hapo hapo, anayekijua lazima atakijua no matter atakaa muda gani bila kuongea! Waganda ni wazuri sana kwa Kiingereza lakini hawana shobo na hiyo lugha kama mliyonayo nyie! Nyie ndo wale mtu anaenda UK au US, anakaa kule miaka mitano tu, akirudi East Africa anajifanya lugha yake ya zamani anaiongea kwa shida!!

Suala la kujua kilugha kwa Watanzania inategemea na asili yako, au umezaliwa wapi lakini sio sahihi kabisa kwamba eti Watanzania wengi hawajui lugha zao za asili!! Usahihi ni kwamba, wanaojua lugha zao za asili ni wengi maradufu kuliko wasiozijua!

Lakini kama ilivyo kwa Kiingereza, ukitaka kuwakera Watanzania basi ongea kilugha cha kwenu mahali ambako unafahamu kabisa waliopo sio wote ni wa kabila lenu!!!

Watanzania tunaunganishwa na Kiswahili, tofauti na nyie manake, pamoja na kuonea fahari Kiingereza, ukienda vijijini na miji midogo ya Kenya, ni Wakenya wachache sana wanaoongea Kiingereza vizuri na wengi wao wanaongea Kiswahili kibovu kilichoathiriwa na lugha zao za asili!

Suala la Wakenya wa vijijini na miji midogo kutokuwa wazuri kwenye Kiingereza ni ushahidi tosha kwamba Wakenya wengi wanaokijua Kiingereza ni wale walioenda shule!!
 
2 Reactions
Reply
Back
Top Bottom