Uganda kuidhinisha Kiswahili kama lugha ya pili baada ya Kingereza - Wakenya fursa hizooo

Huu ni ukweli mchungu ambao wakenya wengi washamba hawapendi kuusikia
Kwavile mnajidanganya Watanzania hawajui Kiingereza, bila kufahamu tofauti ya Watanzania na Wakenya, ni shobo kwenye lugha ya Kiingereza!!

Hivi kabisa unaamini mtu amesoma History, Swahili, and English kwa miaka 4, kisha akaenda A-Level akasoma History, Kiswahili, English (HKL),au (HGL) kwa miaka 2, kisha akaenda chuo akasoma ama Linguistic, BA, n.k, na kwa madogo wa siku hizi, wapo wengi sana waliosoma English Medium kuanzia shule ya msingi; lakini bado unaamini wote hao hawajui English?!

Unachekesha!! Unachekesha kwa sababu usichofahamu ni kwamba, wakati nyie mnaonea fahari kuongea Kiingereza hata pasipo na sababu za msingi, Watanzania wengi wanaamini kuongea Kiingereza pasipo na sababu za msingi ni ushamba na ulimbukeni!!

Kwa mfano, ukinikuta nimesimama kwenye kituo cha daladala ukaniongelesha Kiingereza, amini usiamini, ama sitakujibu, lakini nikikujibu basi nitakujibu kwa Kiswahili! Nitakujibu kwa hiyo lugha ya kigeni endapo tu utakuwa hufahamu Kiswahili!!

Halafu kingine usichokijua ni kwamba, Watanzania wengi tatizo lao ni kwenye Kiingereza cha kuongea lakini sio cha kuandika!!!

Kwenye kufundisha Kiswahili, Mfundishaji anahitajika kuwa na ufahamu wa kawaida wa lugha ya Kiingereza lakini anatakiwa kuwa na ufahamu wa juu wa Kiswahili, na sio ufahamu wa juu wa Kiingereza na ufahamu wa kawaida wa Kiswahili!!
 
Ushamba, chuki na ukoloni ndio tatizo kubwa kwako.
Au unataka kutuambia watu wa meru, kikuyu wanazungumza lugha ya kiswahili kwa ufasaha?
Au accent yao siijui eeh.
Hauwezi ukaijua lugha bila kuitumia, tena ukubwani, yaani unakumbana na Kingereza kuanzia kidato cha kwanza, halafu haukitumii kwenye mawasiliano, hicho kidogo unachofundishwa kinakutoka mara moja.
Lugha yoyote ile lazima uitumie mara kadhaa ndio uje kuimudu. Mpo ovyoo sana kingereza watu wa ze ze ze, na hata Kiswahili uandishi wenu ovyoo sana.
Hamna lugha hata moja mliyoimudu, hadi zenu za asili, asilimia kubwa kati yenu hamjui hata salamu kwa lugha zenu za asili.
 
Kenya mnachukulia Kiswahili kama dalili ya mtu ambaye hakusoma. Vipi shughuli zote za kiserikali ziendeshwe kwa kiingereza wakati lugha rasmi ya Taifa la Kenya ni kiswahili?.

Jambo la kusikitisha na kushangaza ni kwamba, viongozi wengi wa kisiasa na kiserikali hawajui kuzungumza kiswahili kabisa, ilhali mnajinasibu kwamba ni lugha ya taifa lenu, ninaihakika, zaidi ya 60% ya wabunge na mawaziri Kenya hawawezi kutoa hotuba ya Kiswahili kwa dakika 5.
Wakijibu kuhusu hii hoja unitag..
 
Wanaofundishwa Kiswahili lazima uongee kwanza lugha wanayoielewa ili muelewane, hapo ndio huwa mtihani kwa Watanzania wazee wa 'katalist' the the the
nchi zinazojivunia kuongea kiingereza ndani ya afrika zinakabiliwa na changamoto kubwa hasa kimatamshi wanamatamshi mabovu yanayotokana na lafudhi zao
Wakiongozwa na
Kenya
Nigeria
South Africa
 
  • Thanks
Reactions: Oii
nchi zinazojivunia kuongea kiingereza ndani ya afrika zinakabiliwa na changamoto kubwa hasa kimatamshi wanamatamshi mabovu yanayotokana na lafudhi zao
Wakiongozwa na
Kenya
Nigeria
South Africa

Angalia ulichoandika hapa, aisei mna matatizo sana ya kiufasaha, huzingatii alama za uakifishaji, Kiswahili chenyewe kibovu, mnatia huruma sana nyie, Kingereza kimewashinda, uandishi wenu wa Kiswahili unatia kinyaa, lugha za asili ndio hata hamjui salamu.
 
Angalia ulichoandika hapa, aisei mna matatizo sana ya kiufasaha, huzingatii alama za uakifishaji, Kiswahili chenyewe kibovu, mnatia huruma sana nyie, Kingereza kimewashinda, uandishi wenu wa Kiswahili unatia kinyaa, lugha za asili ndio hata hamjui salamu.
"aisei"nahisi kama kijaluo vile wakenya bwana 😂😂😂 alama za uandishi zingatia wewe ambae bado unajifunza humu jf .naona mmelishwa unga wa ndwele mnahisi kingereza kama lugha za babu zenu vile
 
"aisei"nahisi kama kijaluo vile wakenya bwana 😂😂😂 alama za uandishi zingatia wewe ambae bado unajifunza humu jf .naona mmelishwa unga wa ndwele mnahisi kingereza kama lugha za babu zenu vile

Hapa umejitahidi, ila bado sana, labda uhudhurie darasa tena.
 
Ushamba, chuki na ukoloni ndio tatizo kubwa kwako.
Au unataka kutuambia watu wa meru, kikuyu wanazungumza lugha ya kiswahili kwa ufasaha?
Au accent yao siijui eeh.
Language evolves bruh depending na many factors. Ndio maana languages zina diverge and create new languages
 
Kenya mnachukulia Kiswahili kama dalili ya mtu ambaye hakusoma. Vipi shughuli zote za kiserikali ziendeshwe kwa kiingereza wakati lugha rasmi ya Taifa la Kenya ni kiswahili?.

Jambo la kusikitisha na kushangaza ni kwamba, viongozi wengi wa kisiasa na kiserikali hawajui kuzungumza kiswahili kabisa, ilhali mnajinasibu kwamba ni lugha ya taifa lenu, ninaihakika, zaidi ya 60% ya wabunge na mawaziri Kenya hawawezi kutoa hotuba ya Kiswahili kwa dakika 5.
Hayo ni maoni yako, lugha rasmi Kwa shughuli za serikali ni kingereza lakini Kiswahili pia ni rasmi katika Bunge Ila mbunge yupo huru kutumia lugha yeyote Bora asichanganye maneno .hebu mtaje huyo mbunge ambaye hawezi akazungumza Kiswahili .
 
Hayo ni maoni yako, lugha rasmi Kwa shughuli za serikali ni kingereza lakini Kiswahili pia ni rasmi katika Bunge Ila mbunge yupo huru kutumia lugha yeyote Bora asichanganye maneno .hebu mtaje huyo mbunge ambaye hawezi akazungumza Kiswahili .
Katiba ya Kenya imetamka wazi wazi kwamba lugha ya taifa Kenya ni Kiswahili, hakuna mahali popote katika katiba yenu panaposema lugha rasmi ya shughuli za serikali ni Kiingereza, acha uongo.

60% ya wakenya hawakifahamu kiingereza kwa ufasaha, sasa kama serikali lugha yake rasmi ni kiingereza, serika ya Kenya ni kwa ajili ya 40% pekee?
 
Sio rahisi waganda kuacha kuongea lugha yao ya kiganda wanaipenda sana sio kwamba hawajui kiswahili wengi hususani kasikazini wengi wanakijua ila kuongea hawataki
Watu wa Uganda hawapendi hio lugha, inatumika tu Sana na watu wa kabila la waganda na jiji kuu la Kampala lakini ukienda Kwa wasoga wanatumia tu lugha Yao, ukienda Kwa watoro wanatumia tu kitoro vile vile wanyankole na wakonjo kule rwenzori .uziri wa Bantu za Uganda ni kwamba ukijua lugha moja utaelewa 90% ya lugha zingine za kibantu na inakua rahisi Sana Kwa ajili ya mawasiliano.
 
Hauwezi ukaijua lugha bila kuitumia, tena ukubwani, yaani unakumbana na Kingereza kuanzia kidato cha kwanza, halafu haukitumii kwenye mawasiliano, hicho kidogo unachofundishwa kinakutoka mara moja.
Lugha yoyote ile lazima uitumie mara kadhaa ndio uje kuimudu. Mpo ovyoo sana kingereza watu wa ze ze ze, na hata Kiswahili uandishi wenu ovyoo sana.
Hamna lugha hata moja mliyoimudu, hadi zenu za asili, asilimia kubwa kati yenu hamjui hata salamu kwa lugha zenu za asili.

Hujielewi wewe eti mtu hajui salam kwa lugha ya kikwao
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom