Ugali Kwa Mchuzi Wa Nyama, Mchicha, Maharage Na Chatini.

X-PASTER

JF-Expert Member
Feb 12, 2007
11,610
1,809
Ugali Kwa Mchuzi Wa Nyama, Mchicha, Maharage Na Chatini.

Vipimo Vya Mchuzi Wa Nyama

Nyama ya ng’ombe vipande vidogo............... 1kg

Nyanya............... 1

Kitunguu Kilichoktwa katwa............... 1

Mafuta............... 2 vijiko vya supu

Paprika (bizari ya masala ya rangi)............... ½ kijiko cha chai

Kidonge cha supu............... 1 (Royco au mchuzi mix)

Chumvi............... Kiasi

Ndimu............... Kiasi


Namna Ya Kutayarisha Na Kupika Nyama

1 Osha nyama kwa chungio ili itoke maji.

2 Kwenye sufuria, weka mafuta na ukaange vitunguu mpaka viwe rangi ya hudhurungi.

3 Kisha tia nyama na kidonge cha supu uwachie moto mdogo mpaka iwive.

4 Halafu tia nyanya na paprika ufunike sufuria na uiwache motoni mpaka ikauke, kamulia ndimu na itakuwa tayari.


Vipimo Vya Mboga

Mchicha ulio katwa katwa............... 400 gm

Nyanya............... 1

Kitunguu kilicho katwa............... 1

Nazi ya unga............... kiasi

Pilipili mbichi............... 2

Mafuta............... ½ kijiko cha supu

Chumvi............... kiasi


Namna Ya Kutayarisha na Kupika

1 Osha mboga vizuri mpaka iwe haina mchanga.

2 Katika sufuria, kaanga vitungu hadi viwe laini.

3 Tia nyanya, mboga, pilipili na chumvi ikisha toa maji utatia nazi na utaiwacha motoni mpaka ikauke kiasi na itakuwa tayari.


Vipimo Vya Maharage


Maharage............... 1 kopo

Kitunguu 1

Nazi............... 1 Kikombe cha robo lita

Nyanya (itowe maganda)............... 1 kiasi

Pilipili mbichi............... 2

Mafuta............... 1 kijiko cha supu

Chumvi............... kiasi


Namna Ya Kutayarisha Na kupika

1 Tia mafuta katika sufuria na ukaanga vitungu mpaka vilainike.

2 kisha tia nyanya na pilipili na ukaange kidogo.

3 Tia chumvi, maharage na nazi uwachie moto mdogo mpaka iwe nzito kiasi na itakuwa tayari.


Vipimo Vya chatini Ya Pilipili mbichi

Pilipili mbichi............... 5

Kotmiri (coriander)............... 1 Kijiko cha supu

Ndimu............... kiasi

Thomu............... 1 chembe

Mafuta ya zaituni............... 2 vijiko Vya supu

Chumvi............... kiasi


Namna Ya Kutayarisha


1 Kwenye blender, tia vipimo vyote na usage isipokuwa chumvi tia mwisho kwa juu kwenye bakuli na itakuwa tayari kwa kuliwa.


Vipimo Vya ugali

Maji............... 4 Vikombe kiasi inategemea na unga

Unga wa sembe............... 2 vikombe


Namna Ya Kutayarisha Na Kupika

Tia maji kiasi katika sufuria, weka motoni, yakipata moto korogea unga wa sembe kiasi na ufanye uji mzito uache uchemke vizuri huku ukikoroga.
Chota kibakuli kimoja cha uji huo weka pembeni kisha mimina unga wote uliobaki upigepige uchanganyike vizuri kwenye uji huo mpaka ushikamane.
Punguza moto anza kuusonga taratibu huku ukiongeza ule uji ulioweka pembeni kidogo kidogo mpaka uone sasa umeshikamana vizuri na hauna mabuja.

Endelea kusonga mpaka ulainike kisha mimina kwenye bakuli au sahani na itakuwa tayari kwa kuliwa na mchuzi wa nyama, maharage, mboga na chatini.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom