Elections 2010 Ufunguzi wa Kampeni ya Chadema Jangwani 2010

Hatimaye Shirika la Utangazaji la Tanzania (TBC) limeanza kurusha matangazo ya moja kwa moja ya uzinduzi wa kampeni ya CHADEMA kutoka viwanja vya Jangwani, leo, Jumamosi, Agosti 28, 2010, kuanzia takriban saa 9.30 alasiri.

Viongozi wote waandamizi wa CHADEMA, wakiwemo wagombea wote, wameonekana, na hivi sasa kuna utambulisho wa wagombea, baadhi yao wakiwa wamepangwa kuzungumza, kama vile Mpendazoe, Shibuda, Tundu Lissu, Halima Mdee, na wengineo, bila kumsahau mgombea Urais Dk. Wilbroad Peter Slaa na mgombea mwenza Mzee Ali Mzee.

Kumekucha!

-> Mwana wa Haki

P.S. Sugu ametambulishwa na "ana nafasi yake maalum".


Mheshimiwa Tundu Lissu amemwaga ugali na mboga. kumbe JK alihusika kusaini mkataba wa kuwafukia wachimbaji Bulyankulu? Hebu wadau tupeni uhondo huu.
 
Hata vigogo wa CCM wanajua yeye Sugu

(Haaa haa Seems Jamaaa ana usongo na utapeli aliofanyiwa wa "Malaria Haikubaliki" project)
 
Chadema ni kama Mvua Inanyesha nyesha
Hawewezi kukataaa kuitwa sugu kwa kuwa wao ni sugu
 
Sasa anafuata John Shibuda . . . Chapa ya Ng'ombe na Ugali

People's Power
Hakuna Kulala
Hatundanga - Nyiki
 
Anaanza kwa kusema atakayoyasema hayatawafurahisha.

Anajua hawatasema Shibuda kasema jambo la maana.

Du! Jamaa anashusha Kiswahili cha kindaaani
 
CCM kwa CCM hatutendeani haki . . . Kukua atazaa myai ya dhuluma au haki

CCM ndo inaleta mikataba mibovu

Tumpe likizo JK

Wana CCM wamkabidhi madaraka CHADEMA Kumuenzi baba wa Taifa

CCM imegeuza nchi yetu kwa walowezi ambao wanajifanya wawekezaji

CCM ukiwa mlokole hupwei uaskofu

Ukiwa mswalihina hupewi Uimamu wala ushehe

Ukitekeleza wajibu wako hutambuliki
 
Alnadaby na Nostradamus mna-share kitu kimoja: mawazo yenu hayaoni mbali ya pua zenu!!! CCM yenye sera na ''ilani ya maana na iliyokamilika'' imeipeleka wapi Tanzania na Watanzania? Mkiweza kujibu then kosoeni ilani za vyama vingine!

Mimi na Nostrademus ni watu makini na tunasoma na kuelewa mambo kwa upana zaidi.Mawazo yetu ni realistic na ndiyo mawazo ya watu wenye busara zao.Tunaelewa mstakabali wa taifa letu na wapi tunakoelekea.

Kwa kuwa tunaelewa basi hatutafanya makosa ya kuchagua watu wenye kutoa kauli za kejeli kama wewe.CCM itaendelea kutawala kama hamtaki basi shauri yenu.
 
Superman, you're good at typing man! Maana naona wewe uko post ya 6, wengine ndiyo wanadonyoa keyboard kuandika kile ulishaandika dakika 8 zilizopita!! lol :smile-big:
 
Tanzania Bila Malaria Inawezekana
lakini CCM Bila Rushwa haiwezekani . . .

Du, kamaliza

jamaaa anaongea kwa hamasa si mchezo.

Paa likivuja dawa ni kuliondoa na kuweka bati jipya
 
Nimekuwa nikikutafuta Superman, nimekupata. Sie tulioko mikoani hii ndo raha yetu pale tunapohabarishwa kwa namna hii!
Many thanks
 
Viongozi wa Serikali wanatambulishwa

Mkuu wa Wilaya ya Ilala, Kinondoni,
 
Mimi na Nostrademus ni watu makini na tunasoma na kuelewa mambo kwa upana zaidi.Mawazo yetu ni realistic na ndiyo mawazo ya watu wenye busara zao.Tunaelewa mstakabali wa taifa letu na wapi tunakoelekea.

Kwa kuwa tunaelewa basi hatutafanya makosa ya kuchagua watu wenye kutoa kauli za kejeli kama wewe.CCM itaendelea kutawala kama hamtaki basi shauri yenu.

wewe ni mwanachama wa chama cha mafisadi. Hakuna anayetegemea uchague chama kingine tofauti na ccm
 
Back
Top Bottom