Msengi Kiula
Senior Member
- Jan 10, 2008
- 167
- 63
Watawala wamewaondoa watu kwenye makazi ya wakulima Kisima, Changarawe/Mlyongima, kwa Magere/Butiama, kwa Rama, Pori kwa Pori # 2, Milima 3 nk kwa hila na kuumba tatizo la wakimbizi wa ndani(IDP's) kimya kimya.
Watu wamevunjiwa makazi yao, wameswagwa na kurundikwa Pori kwa pori #1 kwa nguvu za dola bila msaada ukiwa ni umbali wa takribani km 15 --25 kutoka walipokuwa wamelima na mazao kustawi.
Sasa hivi mashamba yao ni malisho ya wafugaji. Mtu kwenda kuhami shamba ni uadui.
Tunakwenda wapi? Ipo wapi hekima?
Kisima palikuwa na msikiti, nyumba ya mchungaji wa Anglikana, makazi ya kudumu na shule ilishaanza kujengwa!
Swali: Dar es salaam si ilianza kama kambi ya wavuvi?
Hoja: Nimeona kwenye taarifa za habari Mkuu amehalalisha wavamizi wa kiwanja cha serikali kule Kahama. Hawa tunaowazungumzia hapa siyo wavamizi, ni wachakarikaji- wakulima na mnyororo wa watoa huduma mbalimbali.
Tume ya Pinda iliyoongozwa na viongozi wa dini ilifanya kazi nzuri. Nini kimetokea ghafla kimya kimya na Lukuvi kupotoshwa?
Mbunge naona amezidiwa nguvu na aibu hii iliyotekea hakuna wa kuwasemea; ni ubabe ubabe tu!
Maendeleo yanaletwa na wananchi. Hali ya kulundikwa, imeleta matatizo mengine kabisaaa! Yepi hayo?
Kwa vile uwazi na ukweli unahitajika ,CCM liangalieni hili kwenye vikao vyenu muone serikali yenu ilivyofanya Kiteto. Mtagundua mengi! Kuna "ATM's" mahali zinazopotosha haki?
Jambo hili halijaripotiwa mahali popote kwenye vyombo vya habari hapa nchini. Amkeni! !
Watu wamevunjiwa makazi yao, wameswagwa na kurundikwa Pori kwa pori #1 kwa nguvu za dola bila msaada ukiwa ni umbali wa takribani km 15 --25 kutoka walipokuwa wamelima na mazao kustawi.
Sasa hivi mashamba yao ni malisho ya wafugaji. Mtu kwenda kuhami shamba ni uadui.
Tunakwenda wapi? Ipo wapi hekima?
Kisima palikuwa na msikiti, nyumba ya mchungaji wa Anglikana, makazi ya kudumu na shule ilishaanza kujengwa!
Swali: Dar es salaam si ilianza kama kambi ya wavuvi?
Hoja: Nimeona kwenye taarifa za habari Mkuu amehalalisha wavamizi wa kiwanja cha serikali kule Kahama. Hawa tunaowazungumzia hapa siyo wavamizi, ni wachakarikaji- wakulima na mnyororo wa watoa huduma mbalimbali.
Tume ya Pinda iliyoongozwa na viongozi wa dini ilifanya kazi nzuri. Nini kimetokea ghafla kimya kimya na Lukuvi kupotoshwa?
Mbunge naona amezidiwa nguvu na aibu hii iliyotekea hakuna wa kuwasemea; ni ubabe ubabe tu!
Maendeleo yanaletwa na wananchi. Hali ya kulundikwa, imeleta matatizo mengine kabisaaa! Yepi hayo?
Kwa vile uwazi na ukweli unahitajika ,CCM liangalieni hili kwenye vikao vyenu muone serikali yenu ilivyofanya Kiteto. Mtagundua mengi! Kuna "ATM's" mahali zinazopotosha haki?
Jambo hili halijaripotiwa mahali popote kwenye vyombo vya habari hapa nchini. Amkeni! !