Ufugaji wa wadudu kama chakula cha mifugo na binadamu kilimo kilichokosa nafasi Tanzania

Victor Mlaki

JF-Expert Member
May 1, 2016
3,529
3,432
Licha ya Nchi ya Tanzania kuwa katika ukanda wenye hali ya hewa inayoruhusu uwepo na ukuaji wa viumbe wengi wakiwemo wadudu na mimea bado uwekezaji kwenye kilimo cha ufugaji wa wadudu lishe unaonekana kuwa wa chini sana ukilinganisha na nchi nyingine Duniani. Tanzania inaonekana kuwa nyuma sana katika uwekezaji kwenye kilimo cha ufugaji wa wadudu licha ya tafiti nyingi kuonesha uhitaji mkubwa wa wadudu lishe ambao wanaweza kuwa chanzo kikubwa cha protini.

Watanzania wengi leo wanachukulia kilimo cha ufugaji wa wadudu kwa ajili ya chakula cha binadamu na mifugo kama jambo la kustaajabisha na lenye nafasi ndogo sana katika sekta ya kiliimo licha ya Tafiti nyingi za Shirika la chakula Duniani kuonesha muelekeo wa dunia kwenda kwenye uhitaji wa protini na virutubisho vingine vinavyotokana na wadudu.

Wakulima wengi nchini wanawachukulia wadudu kama viumbe waharibifu na wasiweza kuwa sehemu ya fursa. Ni sehemu ndogo sana ya wakulima wanaoweza kuona thamani ya wadudu na kuwekeza katika kilimo hicho. Wakulima wanaowekeza kwenye kilimo cha ufugaji wa wadudu huonekana mara kadhaa kama watu wa kustaajabisha.

Ufugaji wa wadudu Tanzania unafanyika kwa kiasi kidogo sana na ni katika maeneo machache mfano katika vyuo kama Chuo cha kilimo cha Sokoine na vyuo vingine vya kilimo huku wakulima wengine wakibaki katika ombwe la kukosa maarifa na elimu pana juu ya kilimo cha ufugaji wa wadudu. Siyo jambo la kushangaza kuwakuta wanajamii wengi nchini wakielezea wadudu kama sehemu ya chakula walichotumia wazazi wao na siyo sehemu ya kilimo kinachohitaji uwekezaji kama kilimo cha ufugaji wa viumbe wengine na sehemu ndogo sana ya jamii nchini ndiyo inayoendeleza utamaduni wa kutumia wadudu lishe lakini haijawekeza kwa dhati katika kilimo hicho.

Ufugaji wa wadudu ni kilimo kinachoweza kuwa sehemu ya kupunguza wimbi la vijana wanaokosa ajira nchini na hivyo kuliongezea taifa pato. Hali halisi inaonesha kilimo ni uwanja mpana ambao Tanzania kama mchezaji bado inachezea nusu ya uwanja.
 
Kwanza ungejiuliza kwa nini wadudu na sio kuendelea kutumia dagaa na soya kama chanzo cha protini?

Je ni kweli kwamba kuzalisha wadudu kunapunguza gharama ya ufugaji?

Nini mtazamo wa jamii juu ya kuku kulishwa funza wanaotokana na kinyesi au mabaki ya uchafu, je walaji wakikuona au kujua unawalisha kuku wako funza, watanunua hao kuku?

Maoni yangu binafsi watu waachane na kuzalisha funza kama chakula cha kuku kwa sababu wanazalishwa katika mazingira ya uchafu sana kiasi kwamba kuna uwezekano wa kuzalisha magonjwa mengine. Kama tunatafuta source ya protini basi tutumie dagaa, uduvi, soya, damu au azolla.

Haya ni maoni yangu ili kuchangamsha mjadala isichukuliwe tofauti.
 
Kwanza ungejiuliza kwa nini wadudu na sio kuendelea kutumia dagaa na soya kama chanzo cha protini?

Je ni kweli kwamba kuzalisha wadudu kunapunguza gharama ya ufugaji...
Naam.... umetoa maoni mazuri sana ila wadudu siyo funza tu. Kuna Nyenje, mende n.k ...hata hao funza wanaweza kuzalishwa katika hali ya usafi mfano BSF larvae. Tafiti zinaonesha kuwa BSF hawasmbazi magonjwa mengi kama nzi wengine hivyo ni chanzo kizuri tu cha utunzaji wa mazingira.
 
Naam.... umetoa maoni mazuri sana ila wadudu siyo funza tu. Kuna Nyenje, mende n.k ...hata hao funza wanaweza kuzalishwa katika hali ya usafi mfano BSF larvae. Tafiti zinaonesha kuwa BSF hawasmbazi magonjwa mengi kama nzi wengine hivyo ni chanzo kizuri tu cha utunzaji wa mazingira.
Yawezezekana mhudhurishaji wa hii mada ukawa tayari ni mwenye elimu ya jambo hili, basi ni vyema nawe ukatoa mchango wako kwa kuielimisha jamii juu ya faida za kufuga wadudu kwa ajili ya chakula cha bin adam na mifugo pia.
 
Naam.... umetoa maoni mazuri sana ila wadudu siyo funza tu. Kuna Nyenje, mende n.k ...hata hao funza wanaweza kuzalishwa katika hali ya usafi mfano BSF larvae. Tafiti zinaonesha kuwa BSF hawasmbazi magonjwa mengi kama nzi wengine hivyo ni chanzo kizuri tu cha utunzaji wa mazingira.
Vizuri mkuu, je hawa BSF binadamu tunaweza kuwatumia kama mboga?
 
Licha ya mahitaji makubwa ya wadudu kama sehemu muhimu ya lishe kwa samaki pamoja na mifugo jamii ya ndege nchini ni idadi ndogo sana ya Watanzania waliowekeza kwenye kilimo hiki. Bei ya vyakula vya mifugo imezidi kuwa changamoto kubwa kwa wafugaji jambo linalohitaji kutafutiwa utatuzi.

Maeneo mengi ya nchi hii yanaruhusu kilimo cha ufugaji wa wadudu lishe lakini hitaji kubwa ni elimu kwa wanajamii. Mathalani kulingana na tafiti mbalimbali inaonekana kuwa wadudu lishe kama buu wa nzi chuma, mende na nyenje ni vyanzo vikubwa vya protini na vinaweza kuzidi protini ile inayopatikana kwenye ndege na wanyama.

Nyenje wamebainika kuwa na kiwango kikubwa zaidi cha protini pamoja na virutubisho vingine muhimu ikiwemo omega 3, pamoja na asidi muhimu kama vile follic acids. Wadudu hawa wanapatikana kwa wingi na wanafugika ila bado Watanzania wengi hatujatupia macho yetu huko.
 
Yawezezekana mhudhurishaji wa hii mada ukawa tayari ni mwenye elimu ya jambo hili, basi ni vyema nawe ukatoa mchango wako kwa kuielimisha jamii juu ya faida za kufuga wadudu kwa ajili ya chakula cha bin adam na mifugo pia.
naam... na hapa ndiyo mahali pa kuelimishana zaidi.
 
Licha ya mahitaji makubwa ya wadudu kama sehemu muhimu ya lishe kwa samaki pamoja na mifugo jamii ya ndege nchini ni idadi ndogo sana ya Watanzania waliowekeza kwenye kilimo hiki. Bei ya vyakula vya mifugo imezidi kuwa changamoto kubwa kwa wafugaji jambo linalohitaji kutafutiwa utatuzi.

Maeneo mengi ya nchi hii yanaruhusu kilimo cha ufugaji wa wadudu lishe lakini hitaji kubwa ni elimu kwa wanajamii. Mathalani kulingana na tafiti mbalimbali inaonekana kuwa wadudu lishe kama buu wa nzi chuma, mende na nyenje ni vyanzo vikubwa vya protini na vinaweza kuzidi protini ile inayopatikana kwenye ndege na wanyama.

Nyenje wamebainika kuwa na kiwango kikubwa zaidi cha protini pamoja na virutubisho vingine muhimu ikiwemo omega 3, pamoja na asidi muhimu kama vile follic acids. Wadudu hawa wanapatikana kwa wingi na wanafugika ila bado Watanzania wengi hatujatupia macho yetu huko.
Ombi langu...

Ufanye tafiti na soko hata kama Bongo hawaeleweki tukafanye michongo nje ya Nchi

Sent from my SM-A125F using JamiiForums mobile app
 
Kwanza ungejiuliza kwa nini wadudu na sio kuendelea kutumia dagaa na soya kama chanzo cha protini?

Je ni kweli kwamba kuzalisha wadudu kunapunguza gharama ya ufugaji?

Nini mtazamo wa jamii juu ya kuku kulishwa funza wanaotokana na kinyesi au mabaki ya uchafu, je walaji wakikuona au kujua unawalisha kuku wako funza, watanunua hao kuku?

Maoni yangu binafsi watu waachane na kuzalisha funza kama chakula cha kuku kwa sababu wanazalishwa katika mazingira ya uchafu sana kiasi kwamba kuna uwezekano wa kuzalisha magonjwa mengine. Kama tunatafuta source ya protini basi tutumie dagaa, uduvi, soya, damu au azolla.

Haya ni maoni yangu ili kuchangamsha mjadala isichukuliwe tofauti.
Vidonge unajua vinatengenezwa kwa kitumia nini? Usha goma kula vidonge? Ila ukolini ni mbaya sana, wazungu wametu Brain wash vibaya mno
 
Vidonge unajua vinatengenezwa kwa kitumia nini? Usha goma kula vidonge? Ila ukolini ni mbaya sana, wazungu wametu Brain wash vibaya mno
Be specific, unazungumzia vidonge gani?

Then andika ukiwa umetulia, kuna makosa mengi katika comment yako mpaka inanipa wasiwasi wa upeo wako.
 
Kwanza ungejiuliza kwa nini wadudu na sio kuendelea kutumia dagaa na soya kama chanzo cha protini?

Je ni kweli kwamba kuzalisha wadudu kunapunguza gharama ya ufugaji?

Nini mtazamo wa jamii juu ya kuku kulishwa funza wanaotokana na kinyesi au mabaki ya uchafu, je walaji wakikuona au kujua unawalisha kuku wako funza, watanunua hao kuku?

Maoni yangu binafsi watu waachane na kuzalisha funza kama chakula cha kuku kwa sababu wanazalishwa katika mazingira ya uchafu sana kiasi kwamba kuna uwezekano wa kuzalisha magonjwa mengine. Kama tunatafuta source ya protini basi tutumie dagaa, uduvi, soya, damu au azolla.

Haya ni maoni yangu ili kuchangamsha mjadala isichukuliwe tofauti.
Damu nadhani inatumika kwaajiri ya kupata madini ya chuma na sio protein.
 
Back
Top Bottom