FaizaFoxy
Platinum Member
- Apr 13, 2011
- 92,870
- 109,164
Ufugaji wa mabwawa umepitwa na wakati,sasa ufugaji wa samaki ni AQUAPHONIC hii ndio mwisho miezi minne tu una sato wa nusu kilo.just google aquaphonic and learn for your self.kama kuna mtu inteRested PM me.
Kwa watakaopenda kuona how Aquaphonic work.siku nzuri ni weekend so Mtam na wengine wote interested tuwasiliane ijumaa ili tupange kama iwe jumamos au jumapili mje muone.
Bagamoyo Pale Chuoni wana mambwawa ya kawaida na wanauza Vitoto vya sato shillingi 50 kimoja. Kambale pia wapo. Kama kuna anayependa kwenda pale Bagamoyo Mbegani for study tour pia twaweza kupanga ila wao wanatembelewa working days tu.so inabidi iwe kati ya jumatatu to ijumaa working hrs.sisi vitoto vya kuanzia tulinunua Bagamoyo,lakini katika vitoto hivyo tutapata wazazi wa mbegu siku zijazo.
Katika ufugaji wa samaki kuna vitu muhimu vya kuzingatia.Samaki wanaokuwa kwa haraka ni Madume.Je utapataje Madume watoto? Ipo Dawa ambayo unaiweka katika chakula cha samaki watoto,baada ya muda 99% ya hawa watoto samaki wanageuka Madume.Kisha wewe unaendelea kuwalisha kama kawaida.
Samaki anaweza kula mchanganyiko wa chakula cha kuku lakini awezi pata virutubisho vyote kwani vingine vitapotea katika maji.
Hili pia ni tatizo kubwa hapa kwetu Tanzania juu ya ulishaji samaki ili wakue haraka. Samaki ili wakue haraka na kwa faida ya mfugaji chakula chake kinatakiwa kiwe katika mfumo wa pallets (kama vigololi vidogo size ya ulezi,mtama au zaidi) hii inamfanya samaki akila chakula katika mfumo wa pallets kumeza all food contents (minerals,protein,starch etc).
Mashine zipo za kutengeneza fish food,nikipata muda wakati nikiwa na PC ntaweza weka some docs za fish food,fish sex convention (how to do it),Aquaphonic and modern fish keeping ,nna docs nyingi sana za haya maswala but at this time nipo Mobile so siwezi attach kwa sasa
= Aquaponic