Ufugaji wa ng'ombe wa maziwa; ushauri wa kitalaam, changamoto, mawazo na masoko

salmin siraj,

..ng'ombe aina ya Boran wanapatikana wapi hapa Tz?

..pia unaweza kutueleza bei yao kwa mfano dume wa boran aliyetayari kupanda ni bei gani?

..au jike wa boran mwenye mimba anauzwa bei gani?
 
Je, kama nahitaji Ng'ombe kwa ajili ya maziwa. Utanishauri kuchukua breed gani kati ya Friesian, Jersey na Ayshire?
Kama upo mkoa tofauti na dar es salaam zaid nakushauri uchukue breed aina ya friesian wanafnya vzr kwenye baridi baridi
 
Bei mara nyingi inategemea eneo unakochukulia na uzito /ukubwa wao ila wengi awana si system ya kuuza wenye mimba kama inavofanyika kwa ngombe wa kisasa
Ila ushauri wangu kwenye biashara hii ya ngombe wa nyama nunua waliokonda kwa bei ndogo minadani au kwa wafugaji nenepesha miezi mitatu baada ya hpo uza kwa bei nzuri
salmin siraj,

..ng'ombe aina ya Boran wanapatikana wapi hapa Tz?

..pia unaweza kutueleza bei yao kwa mfano dume wa boran aliyetayari kupanda ni bei gani?

..au jike wa boran mwenye mimba anauzwa bei gani?
 
Habari zenu ndugu zangu wajf leo nimeamua kuanzisha hii thread inayohusu ufugaji wa ng'ombe wa kisasa /maziwa kwa minajiri ya kujaribu kusolve changamoto mbalimbali zinazowakumba wafugaji wa sector hii kupitia uzoefu wangu mashambani na shuleni (SUA) hivo karibuni tusharee mawazo tupate kujifunza njia na namna tofauti ya kuzitatua hizi changamoto kitaalamuna kiasili ili ufugaji huu uweze kua yenye tija kwetu na jamii kiujumla.

Tuanze mwanzo kabisa kujua aina ya ng'ombe wa maziwa na sifa zake mbalimbali.

Friesian
Sifa
-Hawa ni wale wenye rangi meusi na nyeupe (rangi yeyote inaweza kutawala kuliko nyingine).
-Wana maumbo makubwa kuliko aina (breed) nyingine.
-Wanasifa ya kuwa na uwezo wa kutoa maziwa mengi kuliko aina nyingine zote za ng'mbe wa kisasa.
-Kutokana na kua na umbo kubwa wanafaa pia kutumika kama ngombe wa nyama.

Changamoto
-Sio wastahimilivu wa magonjwa hasa magonjwa ya kupe na ndorobo.
-Wanamahitaji makubwa ya chakula kutokana na kua na uzito mkubwa .
-Sio wastahimilivu kwenye mazingira ya joto sababu ni rangi nyeusi inaakisi joto zaid ya rangi nyingine.

Arshire
-Hawa wanamchanganyiko wa rangi nyekundu na nyeupe .
-Wanaumbo la wastani ukilinganisha na friesian (ni wakubwa kuliko aina ya jersey na guernsey.
-Ni wastahimilivu wa mazingira magumu mfano maeneo yenye joto.
-Kinga kwa maginjwa ipo juu ukilinganisha na fresian.
-Pia Wanatoa maziwa mengi yenye wastani asimilia 4% ya fatty(mafuta).

Changamoto
-Wanamatumizi makubwa ya chakula na maji.

Guernsey
-Hawa wanataka kufanana na arshire ila wao wanaumbo madogo na rangi zao ni kama njano hivi au red yenye brown ilochanganyika na rangi nyeupe

Sifa
  • Wanatoa maziwa ya wastani ukilinganisha na arshire na friesian
  • Maziwa yao yana asilimia ya fatty (mafuta ) 4.3%
  • Mahitaji ya chakula ni wastani

Changamoto
- Awatoa kiasi kikubwa cha maziwa kama friesian na arshire

Jersey
  • Sura zao ukiziangalia ni kama dish (sura kama imebonyea) na macho ya prominent (yametoka nje)
  • wanaumbo dogo zaid kuliko aina nyingine.
  • Wanatoa maziwa mazuri zaidi, mazito yenye kiasi kikubwa cha mafuta(fatty 4.8%)
  • wako very fertile (uwezo mkubwa wa kushika mimba na kuzaa kuliko aina nyingine .
  • Wanamature haraka sana (kupevuka).

Changamoto
-Wanatoa kiasi kidogo cha maziwa kuliko aina nyingine za ng'mbe wa waziwa

Aina nyingine zitumikazo ni
1. Brown swiss
2. Mpwapwa breed

Note
Ng'ombe wetu wengi Tanzania ni crossbreed yani ni mchanganyiko wa mbegu za kisasa na kitanzania sio pure breed.
Umetisha aisee tall mnyama
 
Hio ni friesian ndo katika zile picha nimeweka inamabaka muesi na meupe lakini ukwel kutokana na ngozi yao kua nyeusi na ngombe anaenekana zaidi na maadui kama kupe na ndorobo hivo wanatabia ya kupata magonjwa mara kwa mara hata hivo wanatoa maziwa mengi na ukipata friesian alochanganyika na ngombe wa asili kama boran unaweza kupata matokeo chanya kwenye kuzuia magonjwa na kupata maziwa ya kutosha.
Kuna breed moja wanaita Fleckvieh, inaonekana kufanya vizuri zaidi ya jamii nyingine kwenye utoaji wa maziwa na kuhilimi hali ngumu ya maisha ikiwa pamoja na kula chakula kichache pamoja na kuhimili vema baadhi ya magonjwa. Hii breed unaiongeleaje?
 
Hio ni friesian ndo katika zile picha nimeweka inamabaka muesi na meupe lakini ukwel kutokana na ngozi yao kua nyeusi na ngombe anaenekana zaidi na maadui kama kupe na ndorobo hivo wanatabia ya kupata magonjwa mara kwa mara hata hivo wanatoa maziwa mengi na ukipata friesian alochanganyika na ngombe wa asili kama boran unaweza kupata matokeo chanya kwenye kuzuia magonjwa na kupata maziwa ya kutosha.

..mbona sijakusikia ukimzungumzia ng'ombe wetu aliyeboreshwa aina ya KONGWA?

..hivi ng'ombe wa kongwa ana sifa na ubora gani kulinganisha na ng'ombe wa kienyeji, au wanaotokea nje kama Boran, Sahiwal, Ankole, etc?
 
Hio ni friesian ndo katika zile picha nimeweka inamabaka muesi na meupe lakini ukwel kutokana na ngozi yao kua nyeusi na ngombe anaenekana zaidi na maadui kama kupe na ndorobo hivo wanatabia ya kupata magonjwa mara kwa mara hata hivo wanatoa maziwa mengi na ukipata friesian alochanganyika na ngombe wa asili kama boran unaweza kupata matokeo chanya kwenye kuzuia magonjwa na kupata maziwa ya kutosha.
Mkuu Fleckvieh ni jamii ama breed inayojitegemea. Ni maarufu sana Australia na hata jirani zetu kenya wameanza kuifuga kwa miaka mingi tu. Jaribu Kuigoogle
 
Wow mkuu nmejaribu kufuatilia google kama ulivoniagiza nimeona iko kitu kiukwel hapo mwanzo sikufahamu nimesoma sana kuhusu hio breed na nimegundua inaweza kua breed bora zaidi ya nyingine zoote tunazofuga hapa bongo kwa jinsi ilivyongelewa kama utojari tuelezee humu ndani sifa zake zote na wengine wapate kufaidika na hili
Mkuu Fleckvieh ni jamii ama breed inayojitegemea. Ni maarufu sana Australia na hata jirani zetu kenya wameanza kuifuga kwa miaka mingi tu. Jaribu Kuigoogle
 
Mkuu swali zuri ila ni hivi hakuna breed inayoitwa kongwa bali kongwa beef ni brand ya kongwa ranch wao wanasifa ya kuzalisha nyama yenye ubora wake hapa tz na breed inayopatopatikana wa wingi kongwa ni boran hata pale ruvu ranch wanatumia brand kongwa beef ila breed zilizopo mule ni tofauti tofauti ila hasa borani wapo kwa wengi. Nyongeza pale dodoma mpwampwa kunakituo kituo cha utafiti wa mifugo wanabreed yao inaitwa mpwampwa breed yenye sifa zote za maziwa mengi na nyama ya ubora na ya kutosha
..mbona sijakusikia ukimzungumzia ng'ombe wetu aliyeboreshwa aina ya KONGWA?

..hivi ng'ombe wa kongwa ana sifa na ubora gani kulinganisha na ng'ombe wa kienyeji, au wanaotokea nje kama Boran, Sahiwal, Ankole, etc?
 
Mkuu swali zuri ila ni hivi hakuna breed inayoitwa kongwa bali kongwa beef ni brand ya kongwa ranch wao wanasifa ya kuzalisha nyama yenye ubora wake hapa tz na breed inayopatopatikana wa wingi kongwa ni boran hata pale ruvu ranch wanatumia brand kongwa beef ila breed zilizopo mule ni tofauti tofauti ila hasa borani wapo kwa wengi. Nyongeza pale dodoma mpwampwa kunakituo kituo cha utafiti wa mifugo wanabreed yao inaitwa mpwampwa breed yenye sifa zote za maziwa mengi na nyama ya ubora na ya kutosha

..nashukuru sana kwa elimu hii uliyonipa.

..MUNGU akuzidishie elimu na maarifa zaidi ili uendelee kutoa kwa wengine.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom