Mkuu Malila is it a fact wapo au ni tetesi ! Coz Mafia syo mbali !
Wapo,sio tetesi. Maboat ya kwenda kule ni yale ya matambala, kama mwoga, unaweza rudia njiani.
Mkuu Malila is it a fact wapo au ni tetesi ! Coz Mafia syo mbali !
Mkuu Malila kwanza nashukuru nashukuru kwa taarifa,pili nauliza kwani hakuna usafiri wa boat wa kufika kwenye hicho kisiwa?na kama unafahamu bei za hao kuchi original zipo vipi huko kisiwani?nashukuru!
Ngoja kesho nivute uzi kule ili nipate bei za pale kisiwani.
Nashukuru Mkuu,i am waiting
Mambo sio mabaya, nimempata mhusika mmoja ambaye katoka kisiwani Mafia, nimefika kwake na nimemkuta na jogoo original la kuchi. Ameniahidi kutusaidia ili mdogo wake awalete Mkuranga kupitia Nyamisati. Huyu jogoo aliyepo hapa kwake anamuuza Tsh 50,000/ na jogoo mwenyewe ni mkali sana, kauwa majogoo mawili ya majirani wa jamaa, hivyo lazima aondoshwe hapa.
Mkuu Malila nashukuru kwa taarifa!,mdogo wa huyo jamaa amesema anategemea kuleta Kuchi original wangapi?itakuwa baada ya muda gani?na bei yake itakuwaje?tufahamishane tafadhali
Nipo online nasubiri anipigie, jana nimeshindwa kuchukua jogoo mmoja niliyempata sbb ya kutokuwa na maandalizi huku shambani kwangu sababu ni mgomvi sana, na vijogoo vyangu ataua vyote, kwa hiyo nimemwacha ili nirudi nijenge kwanza uzio. Bei ilikuwa 50,000/ kwa huyo wa jana.
Mkuu Malila nashukuru kwa update!
Nami naomba kuuliza mwenye ujuzi,maana nami nimejitahidi kuwatafuta hapa Entebbe Uganda bila mafanikio, sijui nawezaje kupata mtu na jinsi ya kuwatuma huku
Nipo online nasubiri anipigie, jana nimeshindwa kuchukua jogoo mmoja niliyempata sbb ya kutokuwa na maandalizi huku shambani kwangu sababu ni mgomvi sana, na vijogoo vyangu ataua vyote, kwa hiyo nimemwacha ili nirudi nijenge kwanza uzio. Bei ilikuwa 50,000/ kwa huyo wa jana.
Mi natafuta jike
Nilinunua kifaranga kikubwakubwa nikujua ni jike, nikamweka na jogoo la kienyeji mwanzoy jogoo alikuwa akionyesha makeke lakini alivokuwa naona anawadunda wenzie kila muda ni kupigana nikashangaa
Nimehisi ni jogoo ingawa mpk sasa sijaprove
Naomba kupata jike nione
Huyo ni jogoo, jitahidi sana ununue mtetea. Jogoo la kuchi litaua kuku wengine hapo hasa majogoo ya kienyeji.